< 1 Wafalme 6 >

1 Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.
Forsothe it was doon in the fourthe hundrid and fourescore yeer of the goynge out of the sones of Israel fro the lond of Egipt, in the fourthe yeer, in the monethe Zio; thilke is the secounde monethe of the rewme of Salomon on Israel; he bigan to bilde an hows to the Lord.
2 Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa dhiraa ishirini na kimo cha dhiraa thelathini kwenda juu.
Forsothe the hows which kyng Salomon bildide to the Lord, hadde sexti cubitis in lengthe, and twenti cubitis in breede, and thretti cubitis in heiythe.
3 Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu.
And a porche was bifor the temple of twenti cubitis of lengthe, by the mesure of the breed of the temple; and the porche hadde ten cubitis of breede, bifor the face of the temple.
4 Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu.
And Salomon made in the temple `wyndows streyte withoutforth, and large with ynne.
5 Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu.
And he bildide on the wal of the temple bildyngis of tablis bi cumpas, in the wallis of the hows, `bi cumpas of the temple, and of Goddis answeryng place; and he made sidis in the cumpas.
6 Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano, ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.
The bildyng of tablis, that was vndur, hadde fyue cubitis of breede; and the myddil bildyng of tablis was of sixe cubits of breede; and the thridde bildyng of tablis was hauynge seuene cubitis of breede. Sotheli he puttide beemys in the hous bi cumpas with outforth, that tho cleuiden not to the wallis of the temple.
7 Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.
Forsothe whanne the hows was bildid, it was bildid of `stoonys hewid and perfit; and an hamer, and ax, and al thing maad of yrun, weren not herd in the hows, while it was in bildyng.
8 Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu.
The dore of the myddil side was in the wal of the riythalf hows; and bi a vijs thei stieden in to the myddil soler, and fro the myddil soler in to the thridde soler.
9 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi.
And Salomon bildide the hows, and endide it. Also Salomon hilide the hows with couplis of cedre,
10 Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.
and bildide a bildyng of tablis ouer al the hows, bi fyue cubitis of heiythe, and hilide the hows with `trees of cedre.
11 Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema:
And the word of the Lord was maad to Salomon, and seide,
12 “Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako.
This is the hows, which thou bildist; if thou gost in myn heestis, and dost my domes, and kepist alle my comaundementis, and goist bi tho, Y schal make stidefast my word to thee, `which word Y spak to Dauid, thi fadir;
13 Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”
and Y schal dwelle in the myddis of the sones of Israel, and Y schal not forsake my puple Israel.
14 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha.
Therfor Salomon bildide the hows, and endide it;
15 Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari.
and he bildide the wallis of the hows with ynne with tablis of cedre, fro the pawment of the hows `til to the heiynesse of the wal, and `til to the couplis; and hilide with trees of cedre with ynne; and he hilide the pawment of the hows with tablis of beeche.
16 Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu.
And he bildide a wal of tablis of cedre of twenti cubitis at the hyndrere part of the temple, fro the pawment `til to the hiyere partis; and he made the ynnere hows of Goddis answeryng place, in to the hooli of hooli thingis.
17 Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.
Sotheli thilke temple bifor the doris of Goddis answering place was of fourti cubitis.
18 Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.
And al the hows with ynne was clothid with cedre, and hadde hise smethenessis, and hise ioynyngis maad suteli, and grauyngis apperynge aboue; alle thingis weren clothid with tablis of cedre, and outirli a stoon miyte not appere in the wal.
19 Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana.
Forsothe Salomon made Goddis answeryng place in the myddis of the hows, in the ynnere part, that he schulde sette there the arke of boond of pees of the Lord.
20 Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo.
Sotheli Goddis answeryng place hadde twenti cubitis of lengthe, and twenti cubitis of breede, and twenti cubitis of hiyte; and he hilide, and clothide it with pureste gold; but also he clothide the auter with cedre.
21 Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu.
Also he hilide with pureste gold the hows bifor `Goddis answeryng place, and fastnyde platis with goldun nailis.
22 Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.
No thing was in the temple, `which thing was not hilid with gold; but also he hilid with gold al the auter of Goddis answeryng place.
23 Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi kwenda juu.
And he made in `Goddis answeryng place twey cherubyns of the trees of olyues, of ten cubits of heiyte;
24 Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi.
o wynge of cherub was of fyue cubitis, and the tother wynge of cherub was of fyue cubitis, that is, hauynge ten cubitis, fro the heiynesse of `the o wynge `til to the hiynesse of the tother wynge.
25 Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo.
And the secunde cherub was of ten cubitis in euene mesure; and o werk was in the twey cherubyns,
26 Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi.
that is, o cherub hadde the hiythe of ten cubitis, and in lijk maner the tother cherub.
27 Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba.
And he settide cherubyns in the myddis of the ynnere temple; forsothe the cherubyns helden forth her wyngis, and o wenge touchide the wal, and the wynge of the secunde cherub touchide the tother wal; forsothe the othere wyngis in the middil part of the temple touchiden hem silf togidere.
28 Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.
And he hilide the cherubyns with gold,
29 Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua.
and alle the wallis of the temple `bi cumpas; and grauyde with dyuerse grauyngis and smethenesse; and he made in tho wallys cherubyns, and palmes, and dyuerse peynturis, as stondinge forth and goynge out of the wal.
30 Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.
But also he hilide with gold the pawment of the hows, withynne and with outforthe.
31 Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano.
And in the entryng of `Goddis answering place he made twei litil doris of the trees of olyues; and he made postis of fyue corneris,
32 Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa.
and twei doris of the trees of olyues; and grauyde in tho the peynture of cherubyns, and the licnessis of palmes, and grauyngis aboue stondynge forth gretli; and he hilide tho with gold; and he hilide as wel the cherubyns, as palmes, and othere thingis with gold.
33 Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa.
And in the entring of the temple he made postis foure cornerid of the trees of olyues;
34 Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine.
and he made twei doris of the trees of beech, ech ayens other; and euer either dore was double, and it was openyd holdynge it silf togidere.
35 Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.
And he grauyde cherubyns, and palmes, and grauyngis apperynge greetli; and he hilide alle thingis with goldun platis, bi square werk at reule.
36 Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.
And he bildide a large street with ynne, bi thre ordris of stoonys maad fair, and bi oon ordre of trees of cedre.
37 Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano.
The hows of the Lord was foundid in the fourthe yeer, in the monethe Zio;
38 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.
and the hows was maad perfit in al his werk, and in alle vessels, ether `purtenauncis, in the eleuenthe yeer, in the monethe Zebul; thilke is the eiythe monethe; and he bildide that hows in seuene yeer.

< 1 Wafalme 6 >