< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
Sur Kralı Hiram, Süleyman'ın babası Davut'un yerine kral olarak meshedildiğini duyunca, elçilerini Süleyman'a gönderdi. Çünkü Davut'la hep dostça geçinmişti.
2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
Süleyman Hiram'a şu haberi gönderdi:
3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
“Bildiğin gibi, babam Davut çevresindeki savaşlar yüzünden Tanrısı RAB'bin adına bir tapınak yapamadı. Bu savaşlarda RAB, Davut'un düşmanlarını onun ayakları altına serdi.
4 Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
Oysa şimdi Tanrım RAB her yönden bana rahatlık verdi. Ne bir düşmanım var, ne de kötü bir olay.
5 Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
RAB, babam Davut'a, ‘Tahtına oturtacağım oğlun benim adıma bir tapınak yapacak’ diye söz verdi. Ben de Tanrım RAB'bin adına bir tapınak yapmaya karar verdim.
6 “Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
“Şimdi bana Lübnan'dan sedir ağaçları kesmeleri için adamlarına buyruk ver. Benim adamlarım da seninkilerle birlikte çalışsın. Adamların için istediğin ücreti vereceğim. Aramızda Saydalılar kadar ağaç kesmede usta adamlar olmadığını biliyorsun.”
7 Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
Hiram, Süleyman'dan bu haberi alınca çok sevindi ve, “Bugün, o büyük ulusu yönetmek üzere Davut'a bilge bir oğul veren RAB'be övgüler olsun!” dedi.
8 Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
Sonra Hiram Süleyman'a şu haberi gönderdi: “Gönderdiğin haberi aldım. Sedir ve çam ağaçlarıyla ilgili bütün dileklerini yerine getireceğim.
9 Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
Adamlarım tomrukları Lübnan'dan denize indirecekler, ben de onları sallar halinde bağlatıp belirteceğin yere kadar yüzdüreceğim. Orada adamlarım onları çözer, sen de alıp götürürsün. Sarayımın yiyecek gereksinimini karşılamakla, sen de benim dileğimi yerine getirmiş olursun.”
10 Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
Hiram Süleyman'a istediği kadar sedir ve çam tomruğu sağladı.
11 naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
Süleyman her yıl Hiram'a sarayının yiyecek gereksinimi olarak yirmi bin kor buğday, yirmi kor saf zeytinyağı verirdi.
12 Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
RAB, verdiği söz uyarınca, Süleyman'a bilgelik verdi. Süleyman'la Hiram arasında barış vardı. Aralarında bir antlaşma yaptılar.
13 Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
Kral Süleyman angaryasına çalıştırmak üzere bütün İsrail'den otuz bin adam topladı.
14 Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
Sırayla her ay on binini Lübnan'a gönderiyordu. Bir ay Lübnan'da, iki ay evlerinde kalıyorlardı. Angaryasına çalışan adamların başında Adoniram vardı.
15 Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
Süleyman'ın yük taşıyan 70 000, dağlarda taş kesen 80 000 adamı vardı.
16 pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
Ayrıca, işin yürümesini sağlayan ve işçileri yöneten 3 300 görevlisi vardı.
17 Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
İşçiler, kralın buyruğu uyarınca, tapınağın temelini yontma taşlarla atmak üzere ocaktan büyük ve kaliteli taşlar kesip çıkardılar.
18 Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.
Süleyman'ın ve Hiram'ın yapıcılarıyla Gevallılar, tapınağın yapımı için taşlarla keresteleri kesip hazırladılar.

< 1 Wafalme 5 >