< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
Tirski kralj Hirám je svoje služabnike poslal k Salomonu, kajti slišal je, da so ga mazilili [za] kralja namesto njegovega očeta, kajti Hirám je bil vedno Davidov oboževalec.
2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
Salomon je poslal k Hirámu, rekoč:
3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
»Ti veš, da moj oče David ni mogel zgraditi hiše imenu Gospoda, svojega Boga, zaradi vojn, ki so bile okoli njega na vsaki strani, dokler jih ni Gospod položil pod podplate njegovih stopal.
4 Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
Toda sedaj mi je Gospod, moj Bog, dal počitek na vsaki strani, tako da ni niti nasprotnika niti zlih dogodkov.
5 Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
Glej, namenil sem se zgraditi hišo imenu Gospoda, svojega Boga, kakor je Gospod spregovoril mojemu očetu Davidu, rekoč: ›Tvoj sin, ki ga bom namesto tebe postavil na tvoj prestol, on bo zgradil hišo mojemu imenu.
6 “Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
Zdaj torej zapovej, da mi iz Libanona posekajo cedrova drevesa in moji služabniki bodo s tvojimi služabniki in dal ti bom plačilo za tvoje služabnike, glede na vse, kar mi boš določil; kajti veš, da med nami ni nobenega, ki tako vešče seka les kot Sidónci.‹«
7 Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
Ko je Hirám slišal Salomonove besede, se je pripetilo, da se je silno razveselil in rekel: »Blagoslovljen bodi ta dan Gospod, ki je Davidu dal modrega sina nad tem velikim ljudstvom.«
8 Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
In Hirám je poslal k Salomonu, rekoč: »Preudaril sem stvari, zaradi katerih pošiljaš k meni in izpolnil bom vso tvojo željo glede cedrovega lesa in glede cipresovega lesa.
9 Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
Moji služabniki ga bodo spravljali dol iz Libanona do morja in po morju ga bom spravljal v splavih na mesto, ki mi ga boš določil in povzročim jim, da bodo tam razvezani in jih boš sprejel, ti pa boš izpolnil mojo željo, da mi daješ hrano za mojo družino.«
10 Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
Tako je Hirám dajal Salomonu cedrov les in cipresov les glede na vse njegove želje.
11 naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
Salomon je dajal Hirámu dvajset tisoč mer pšenice za hrano njegovi družini in dvajset mer čistega olja. Tako je Salomon dajal Hirámu leto za letom.
12 Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
Gospod je dal Salomonu modrost, kakor mu je obljubil in bil je mir med Hirámom in Salomonom in onadva sta sklenila zavezo.
13 Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
Kralj Salomon je zbral dajatev obveznega dela iz vsega Izraela, in dajatev obveznega dela je bila trideset tisoč mož.
14 Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
Pošiljal jih je k Libanonu, deset tisoč na mesec, v izmenah. En mesec so bili na Libanonu in dva meseca doma. Adonirám pa je bil nad dajatvijo obveznega dela.
15 Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
Salomon jih je imel sedemdeset tisoč, ki so nosili bremena in osemdeset tisoč sekalcev v gorah,
16 pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
poleg glavnih Salomonovih častnikov, ki so bili nad delom, tri tisoč tristo, ki so vladali nad ljudstvom, ki je opravljalo delo.
17 Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
Kralj je zapovedal in prinesli so velike kamne, drage kamne, klesane kamne, da hiši položijo temelj.
18 Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.
Salomonovi graditelji, Hirámovi graditelji in kamnoseki so jih klesali. Tako so pripravili les in kamne, da zgradijo hišo.

< 1 Wafalme 5 >