< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
و حیرام، پادشاه صور، خادمان خود را نزدسلیمان فرستاد، چونکه شنیده بود که او رابه‌جای پدرش به پادشاهی مسح کرده‌اند، زیرا که حیرام همیشه دوست داود بود.۱
2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
و سلیمان نزد حیرام فرستاده، گفت۲
3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
که «تو پدر من داود رامی دانی که نتوانست خانه‌ای به اسم یهوه، خدای خود بنا نماید به‌سبب جنگهایی که او را احاطه می‌نمود تا خداوند ایشان را زیر کف پایهای اونهاد.۳
4 Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
اما الان یهوه، خدای من، مرا از هر طرف آرامی داده است که هیچ دشمنی و هیچ واقعه بدی وجود ندارد.۴
5 Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
و اینک مراد من این است که خانه‌ای به اسم یهوه، خدای خود، بنا نمایم چنانکه خداوند به پدرم داود وعده داد و گفت که پسرت که او را به‌جای تو بر کرسی خواهم نشانید، خانه را به اسم من بنا خواهد کرد.۵
6 “Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
و حال امر فرما که سروهای آزاد از لبنان برای من قطع نمایند و خادمان من همراه خادمان تو خواهندبود، و مزد خادمانت را موافق هرآنچه بفرمایی به تو خواهم داد، زیرا تو می‌دانی که در میان ما کسی نیست که مثل صیدونیان در قطع نمودن درختان ماهر باشد.»۶
7 Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
پس چون حیرام سخنان سلیمان را شنید، به غایت شادمان شده، گفت: «امروز خداوند متبارک باد که به داود پسری حکیم بر این قوم عظیم عطانموده است.»۷
8 Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
و حیرام نزد سلیمان فرستاده، گفت: «پیغامی که نزد من فرستادی اجابت نمودم و من خواهش تو را درباره چوب سرو آزاد وچوب صنوبر بجا خواهم آورد.۸
9 Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
خادمان من آنهارا از لبنان به دریا فرود خواهند‌آورد و من آنها رابستنه خواهم ساخت در دریا، تا مکانی که برای من معین کنی و آنها را در آنجا از هم باز خواهم کرد تا آنها را ببری و اما تو درباره دادن آذوقه به خانه من اراده مرا به‌جا خواهی آورد.»۹
10 Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
پس حیرام چوبهای سرو آزاد و چوبهای صنوبر را موافق تمامی اراده‌اش به سلیمان داد.۱۰
11 naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
وسلیمان بیست هزار کر گندم و بیست هزار کرروغن صاف به حیرام به جهت قوت خانه‌اش داد، و سلیمان هرساله اینقدر به حیرام می‌داد.۱۱
12 Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
وخداوند سلیمان را به نوعی که به او وعده داده بود، حکمت بخشید و در میان حیرام و سلیمان صلح بود و با یکدیگر عهد بستند.۱۲
13 Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
و سلیمان پادشاه از تمامی اسرائیل سخره گرفت و آن سخره سی هزار نفر بود.۱۳
14 Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
و از ایشان ده هزار نفر، هر ماهی به نوبت به لبنان می‌فرستاد. یک ماه در لبنان و دو ماه در خانه خویش می‌ماندند. و ادونیرام رئیس سخره بود.۱۴
15 Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
وسلیمان را هفتاد هزار مرد باربردار و هشتاد هزارنفر چوب بر در کوه بود.۱۵
16 pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
سوای سروران گماشتگان سلیمان که ناظر کار بود، یعنی سه هزارو سیصد نفر که بر عاملان کار ضابط بودند.۱۶
17 Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
وپادشاه امر فرمود تا سنگهای بزرگ و سنگهای گرانبها و سنگهای تراشیده شده به جهت بنای خانه کندند.۱۷
18 Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.
و بنایان سلیمان و بنایان حیرام وجبلیان آنها را تراشیدند، پس چوبها و سنگها را به جهت بنای خانه مهیا ساختند.۱۸

< 1 Wafalme 5 >