< 1 Wafalme 5 >
1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
Hiram, roi de Tyr, envoya aussi ses serviteurs vers Salomon; car il apprit qu’on l’avait oint roi, en la place de son père, parce qu’Hiram avait toujours été l’ami de David.
2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
Or Salomon envoya vers Hiram, disant:
3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
Vous savez le désir de David mon père, et qu’il n’a pu bâtir une maison au nom du Seigneur son Dieu, à cause des guerres qui le menaçaient de toutes parts, jusqu’à ce que le Seigneur eût mis ses ennemis sous la plante de ses pieds.
4 Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
Mais maintenant le Seigneur mon Dieu m’a donné la paix alentour; et il n’y a ni adversaire, ni obstacle fâcheux.
5 Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
C’est pourquoi je pense à bâtir un temple au nom du Seigneur mon Dieu, comme a parlé le Seigneur à David, mon père, disant: Ton fils, que je mettrai en ta place sur ton trône, sera celui qui bâtira une maison à mon nom.
6 “Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
Ordonnez donc que vos serviteurs coupent pour moi des cèdres du Liban, et que mes serviteurs soient avec les vôtres; quant à la récompense de vos serviteurs, je vous la donnerai telle que vous la demanderez; car vous savez que parmi mon peuple, il n’est pas d’homme qui sache couper le bois comme les Sidoniens.
7 Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
Lors donc qu’Hiram eut entendu les paroles de Salomon, il se réjouit beaucoup, et dit: Béni aujourd’hui le Seigneur Dieu, qui a donné à David un fils très sage pour gouverner ce très grand peuple!
8 Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
Et Hiram envoya vers Salomon, disant: J’ai entendu tout ce que vous m’avez mandé; je ferai tout ce que vous désirez pour les bois de cèdre et de sapin.
9 Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
Mes serviteurs les porteront du Liban à la mer, et moi je les ferai mettre en radeaux sur la mer, jusqu’au lieu que vous m’aurez marqué; je les y ferai aborder; vous les enlèverez, et vous me fournirez tout ce qui me sera nécessaire pour nourrir ma maison.
10 Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
C’est pourquoi Hiram donnait à Salomon des bois de cèdre et de sapin, selon tous ses désirs.
11 naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
Et Salomon fournissait à Hiram, pour nourrir sa maison, vingt mille cors de froment et vingt cors d’huile très pure: voilà ce que Salomon livrait chaque année à Hiram.
12 Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
Le Seigneur donna aussi la sagesse à Salomon, comme il le lui avait dit: et il y avait paix entre Hiram et Salomon, et ils firent tous deux alliance.
13 Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
Et le roi Salomon choisit des ouvriers de tout Israël, et la taxation était de trente mille hommes.
14 Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
Et il les envoyait au Liban tour à tour, dix mille chaque mois, de sorte qu’ils étaient deux mois dans leurs maisons; et Adoniram était préposé à cette taxation.
15 Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
Salomon avait soixante-dix mille hommes qui portaient des fardeaux, et quatre-vingt mille qui taillaient des pierres sur la montagne,
16 pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
Sans les préposés qui présidaient à chaque ouvrage, au nombre de trois mille trois cents, et qui donnaient les ordres au peuple et à ceux qui faisaient l’ouvrage.
17 Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
Et le roi leur ordonna de prendre de grandes pierres, des pierres de prix, pour les fondements du temple, et de les équarrir;
18 Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.
Et les maçons de Salomon et les maçons d’Hiram les taillèrent; or ceux de Giblos préparèrent les bois et les pierres pour bâtir la maison du Seigneur.