< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
and to send: depart Hiram king Tyre [obj] servant/slave his to(wards) Solomon for to hear: hear for [obj] him to anoint to/for king underneath: instead father his for to love: lover to be Hiram to/for David all [the] day: always
2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
and to send: depart Solomon to(wards) Hiram to/for to say
3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
you(m. s.) to know [obj] David father my for not be able to/for to build house: home to/for name LORD God his from face: because [the] battle which to turn: surround him till to give: put LORD [obj] them underneath: under palm: sole (foot my *Q(K)*)
4 Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
and now to rest LORD God my to/for me from around: side nothing Satan and nothing chance bad: evil
5 Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
and look! I to say to/for to build house: home to/for name LORD God my like/as as which to speak: speak LORD to(wards) David father my to/for to say son: child your which to give: put underneath: instead you upon throne your he/she/it to build [the] house: home to/for name my
6 “Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
and now to command and to cut: cut to/for me cedar from [the] Lebanon and servant/slave my to be with servant/slave your and wages servant/slave your to give: pay to/for you like/as all which to say for you(m. s.) to know for nothing in/on/with us man: anyone to know to/for to cut: cut tree: wood like/as Sidonian
7 Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
and to be like/as to hear: hear Hiram [obj] word Solomon and to rejoice much and to say to bless LORD [the] day: today which to give: give to/for David son: child wise upon [the] people [the] many [the] this
8 Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
and to send: depart Hiram to(wards) Solomon to/for to say to hear: hear [obj] which to send: depart to(wards) me I to make: do [obj] all pleasure your in/on/with tree: wood cedar and in/on/with tree: wood cypress
9 Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
servant/slave my to go down from [the] Lebanon sea [to] and I to set: make them raft in/on/with sea till [the] place which to send: depart to(wards) me and to shatter them there and you(m. s.) to lift: raise and you(m. s.) to make: do [obj] pleasure my to/for to give: give food house: household my
10 Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
and to be Hiram to give: give to/for Solomon tree: wood cedar and tree: wood cypress all pleasure his
11 naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
and Solomon to give: give to/for Hiram twenty thousand kor wheat food to/for house: household his and twenty kor oil beaten thus to give: give Solomon to/for Hiram year in/on/with year
12 Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
and LORD to give: give wisdom to/for Solomon like/as as which to speak: promise to/for him and to be peace between Hiram and between Solomon and to cut: make(covenant) covenant two their
13 Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
and to ascend: establish [the] king Solomon taskworker from all Israel and to be [the] taskworker thirty thousand man
14 Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
and to send: depart them Lebanon [to] ten thousand in/on/with month change month to be in/on/with Lebanon two month in/on/with house: home his and Adoniram upon [the] taskworker
15 Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
and to be to/for Solomon seventy thousand to lift: bearing(armour) burden and eighty thousand to hew in/on/with mountain: hill country
16 pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
to/for alone from ruler [the] to stand to/for Solomon which upon [the] work three thousand and three hundred [the] to rule in/on/with people [the] to make: do in/on/with work
17 Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
and to command [the] king and to set out stone great: large stone precious to/for to found [the] house: home stone cutting
18 Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.
and to hew to build Solomon and to build Hiram and [the] Gebalite and to establish: prepare [the] tree: wood and [the] stone to/for to build [the] house: home

< 1 Wafalme 5 >