< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
Now Hiram, king of Tyre, hearing that Solomon had been made king in place of his father, sent his servants to him; for Hiram had ever been a friend to David.
2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
And Solomon sent back word to Hiram, saying,
3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
You have knowledge that David my father was not able to make a house for the name of the Lord his God, because of the wars which were round him on every side, till the Lord put all those who were against him under his feet.
4 Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
But now the Lord my God has given me rest on every side; no one is making trouble, and no evil is taking place.
5 Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
And so it is my purpose to make a house for the name of the Lord my God, as he said to David my father, Your son, whom I will make king in your place, will be the builder of a house for my name.
6 “Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
So now, will you have cedar-trees from Lebanon cut down for me, and my servants will be with your servants; and I will give you payment for your servants at whatever rate you say; for it is common knowledge that we have no such wood-cutters among us as the men of Zidon.
7 Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
And these words of Solomon made Hiram glad, and he said, Now may the Lord be praised who has given to David a wise son to be king over this great people.
8 Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
Then Hiram sent to Solomon, saying; The words you sent have been given to me: I will do all your desire in the question of cedar-wood and cypress-wood.
9 Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
My men will take them down from Lebanon to the sea, where I will have them corded together to go by sea to whatever place you say, and I will have them cut up there so that you may take them away; as for payment, it will be enough if you give me food for my people.
10 Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
So Hiram gave Solomon all the cedar-wood and cypress-wood he had need of;
11 naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
And Solomon gave Hiram twenty thousand measures of grain, as food for his people, and twenty measures of clear oil; this he did every year.
12 Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
Now the Lord had given Solomon wisdom, as he had said to him; and there was peace between Hiram and Solomon, and they made an agreement together.
13 Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
Then King Solomon got together men for the forced work through all Israel, thirty thousand men in number;
14 Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
And sent them to Lebanon in bands of ten thousand every month: for a month they were working in Lebanon and for two months in their country, and Adoniram was in control of them.
15 Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
Then he had seventy thousand for the work of transport, and eighty thousand stone-cutters in the mountains;
16 pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
In addition to the chiefs of the responsible men put by Solomon to oversee the work, three thousand and three hundred in authority over the workmen.
17 Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
By the king's orders great stones, stones of high price, were cut out, so that the base of the house might be made of squared stone.
18 Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.
Solomon's builders and Hiram's builders did the work of cutting them, and put edges on them, and got the wood and the stone ready for the building of the house.

< 1 Wafalme 5 >