< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
А Тирският цар Хирам, като чу, че помазали Соломона за цар вместо баща му, прати слугите си до него; защото Хирам бе всякога приятел на Давида.
2 Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
И Соломон прати на Хирама да кажат:
3 “Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
Ти знаеш, че баща ми Давид не можа да построи дом за името на Господа своя Бог по причина на боевете, които го обикаляха от всякъде, докато Господ не положи неприятелите му под стъпалата на нозете му.
4 Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
Но сега, Господ моят Бог, ми даде спокойствие навред; нямам противник нито злополука.
5 Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
И, ето, аз възнамерявам да построя дом за името на Господа моя Бог според както Господ говори на баща ми Давида, като рече: Стани ти, когото ще поставя вместо тебе на престола ти, той ще построи дом за името Ми.
6 “Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
Сега, прочее, заповядай да ми насекат кедри от Ливан; моите слуги ще бъдат с твоите слуги; и ще ти дам заплата за слугите ти напълно според както ще речеш; защото ти знаеш, че между нас няма човек, който знае да сече дървета, толкова изкусно, колкото сидонците.
7 Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
Тогава Хирам, като чу Соломоновите думи, много се зарадва и рече: Благословен да бъда днес Господ, Който даде на Давида мъдър син да царува над тоя велик народ.
8 Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
И Хирам прати до Соломона да кажат: Чух известието, което ти ми прати; аз ще сторя все що искаш за кедровите дървета и за елховите дървета.
9 Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
Моите слуги ще ги снемат от Ливан до морето; и аз ще ги свържа на салове, за да се превозват по море до мястото, което би ми посочил, и там да се развържат и ти да ги прибереш. Също и ти ще сториш каквото искам, да продоволствуваш моя дом.
10 Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
И тъй, Хирам даваше на Соломона кедрови дървета и елхови дървета, колкото той искаше.
11 naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
А Соломон даде на Хирама двадесет хиляди кора пшеница за храна на дома му, и двадесет кора първоток дървено масло; така даваше Соломон на Хирама всяка година.
12 Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
И Господ даде на Соломона мъдрост, според както му беше обещал; и имаше мир между Хирама и Соломона, и те двамата направиха договор помежду си.
13 Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
И цар Соломон събра набор от целия Израил, и събраните мъже бяха тридесет хиляди души.
14 Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
И изпращаше ги в Ливан на смени, по десет хиляди души на месец; един месец бяха в Ливан и два месеца у домовете си; а над набора беше Адонирам.
15 Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
Соломон имаше и седемдесет хиляди бременосци и осемдесет хиляди каменоделци в планините,
16 pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
освен три хиляди и триста Соломонови настойници, които бяха над работите, надзираващи людете, които работеха тая работа.
17 Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
И по царската заповед изкараха големи камъни, камъни с голяма стойност, за да положат основите на дома с дялани камъни.
18 Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.
И Соломоновите зидари, и Хирамовите зидари, и гевалците ги издялаха, и приготвиха дърветата и камъните, за да построят дома.

< 1 Wafalme 5 >