< 1 Wafalme 4 >

1 Basi Mfalme Solomoni akatawala Israeli yote.
سلیمان پادشاه بر تمام اسرائیل حکومت می‌کرد
2 Hawa ndio waliokuwa maafisa wake wakuu: Kuhani: Azaria mwana wa Sadoki;
و مقامات دربار او عبارت بودند از: عزریا (پسر صادوق)، رئیس کاهنان؛ الیحورف و اخیا (پسران شیشه)، کاتب؛ یهوشافاط (پسر اخیلود)، وقایع‌نگار؛ بنایا (پسر یهویاداع)، فرماندهٔ سپاه؛ صادوق و اَبیّاتار، کاهن؛ عزریا (پسر ناتان)، سرپرست حاکمان؛ زابود (پسر ناتان)، کاهن و مشاور پادشاه؛ اخیشار، سرپرست امور دربار؛ ادونیرام (پسر عبدا) سرپرست کارهای اجباری.
3 Elihorefu na Ahiya, wana wa Shisha: waandishi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi: karani;
4 Benaya mwana wa Yehoyada: jemadari mkuu wa jeshi; Sadoki na Abiathari: makuhani;
5 Azaria mwana wa Nathani: kiongozi wa maafisa wa wilaya; Zabudi mwana wa Nathani: kuhani na mshauri binafsi wa mfalme;
6 Ahishari: msimamizi wa jumba la kifalme; Adoniramu mwana wa Abda: msimamizi wa kazi za kulazimisha.
7 Pia Solomoni alikuwa na watawala kumi na wawili wa wilaya katika Israeli yote, walioleta mahitaji kwa mfalme na kwa watu wa nyumbani kwa mfalme. Kila mmoja alitoa chakula kwa mwezi mmoja katika mwaka.
سلیمان در تمام اسرائیل دوازده حاکم گماشته بود و آنها وظیفه داشتند خوراک دربار را تهیه کنند. هر یک از ایشان، یک ماه در سال مسئول تدارکات دربار بودند.
8 Majina yao ni haya: Ben-Huri: katika nchi ya vilima ya Efraimu;
این است اسامی دوازده حاکم و حوزه‌های فعالیت آنها: بن هور، در کوهستان افرایم؛ بن دقر، در ماقص، شعلبیم، بیت‌شمس، ایلون و بیت حانان؛ بن حسد، در اربوت، سوکوه و تمامی قلمرو حافر؛ بن ابیناداب، (که با تافَت دختر سلیمان ازدواج کرده بود) در تمام منطقهٔ دُر؛ بعنا (پسر اخیلود)، در تعنک، مجدو، تمام سرزمین نزدیک بیت‌شان و صرتان، جنوب شهر یزرعیل، و تا شهر آبل مهوله و شهر یقمعام؛ بن جابر، در راموت جلعاد که شامل دهکده‌های یاعیر (پسر منسی) در جلعاد و ناحیه ارجوب در باشان می‌شد با شصت شهر حصاردار دیگر که دروازه‌هایشان پشت‌بندهای مفرغین داشت؛ اخیناداب (پسر عدو)، در محنایم؛ اخیمعص (که با باسمت دختر دیگر سلیمان ازدواج کرده بود)، در نفتالی؛ بعنا (پسر حوشای)، در اشیر و بعلوت؛ یهوشافاط (پسر فاروح)، در سرزمین یساکار؛ شمعی (پسر ایلا)، در سرزمین بنیامین؛ جابر (پسر اوری)، در جلعاد که شامل سرزمینهای سیحون، پادشاه اموری‌ها و عوج، پادشاه باشان می‌شد. این دوازده حاکم زیر نظر حاکم کل قرار داشتند.
9 Ben-Dekeri: katika Makasi, Shaalbimu, Beth-Shemeshi na Elon-Bethhanani;
10 Ben-Hesedi: katika Arubothi (Soko na nchi yote ya Heferi zilikuwa zake);
11 Ben-Abinadabu: katika Nafoth-Dori (alimwoa Tafathi binti Solomoni);
12 Baana mwana wa Ahiludi: katika Taanaki na Megido, na katika Beth-Shani yote karibu na Sarethani chini ya Yezreeli, kuanzia Beth-Shani hadi Abel-Mehola kupita hadi Yokmeamu;
13 Ben-Geberi: katika Ramoth-Gileadi (makao ya Yairi mwana wa Manase katika Gileadi ilikuwa miji yake, pamoja na wilaya ya Argobu katika Bashani na miji yake mikubwa sitini yenye kuzungukwa na kuta zenye makomeo ya shaba);
14 Ahinadabu mwana wa Ido: katika Mahanaimu;
15 Ahimaasi: katika Naftali (alikuwa amemwoa Basemathi binti Solomoni);
16 Baana mwana wa Hushai: katika Asheri na katika Bealothi;
17 Yehoshafati mwana wa Parua: katika Isakari;
18 Shimei mwana wa Ela: katika Benyamini;
19 Geberi mwana wa Uri: katika Gileadi (nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani). Naye alikuwa ndiye mtawala pekee katika eneo hilo.
20 Watu wa Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani; walikula, wakanywa na kufurahi.
در آن زمان اسرائیل و یهودا مانند شنهای کنار دریا بی‌شمار بودند. آنها از زندگی مرفه و شادی برخوردار بودند.
21 Mfalme Solomoni akatawala katika falme zote kuanzia Mto Frati hadi nchi ya Wafilisti, hadi kwenye mpaka wa Misri. Nchi hizi zilileta ushuru na zilikuwa chini ya Solomoni, siku zote za maisha yake.
سلیمان بر تمام سرزمینهای واقع در بین رود فرات و فلسطین که تا سرحد مصر نیز می‌رسیدند سلطنت می‌کرد. اقوام این سرزمینها به او باج و خراج می‌دادند و در تمام مدت عمرش تابع او بودند.
22 Mahitaji ya Solomoni ya kila siku yalikuwa kori thelathini za unga laini, kori sitini za unga wa kawaida.
آذوقهٔ روزانهٔ دربار عبارت بود از: حدود پنج تن آرد و ده تن بلغور،
23 Ngʼombe kumi wa zizini, ngʼombe ishirini wa malisho, kondoo na mbuzi mia moja, pamoja na ayala, paa, kulungu na kuku wazuri sana.
ده گاو از طویله، بیست گاو از چراگاه، صد گوسفند و نیز غزال، آهو، گوزن و انواع مرغان.
24 Kwa kuwa Solomoni alitawala falme zote magharibi ya mto, kuanzia Tifsa hadi Gaza, naye akawa na amani pande zote.
قلمرو سلطنت سلیمان از تفصح تا غزه می‌رسید و تمام ممالک غرب رود فرات را در بر می‌گرفت. تمام پادشاهان غرب رود فرات تابع او بودند و او با سرزمینهای همسایه در صلح بود.
25 Wakati wa maisha ya Solomoni Yuda na Israeli, kuanzia Dani mpaka Beer-Sheba, wakaishi salama kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake.
مردم یهودا و اسرائیل در طول سلطنت سلیمان در کمال آرامش بودند و هر خانواده، از دان تا بئرشبع، زیر درختان مو و انجیر خود آسوده می‌نشستند.
26 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 ya magari ya vita, na farasi 12,000.
سلیمان دوازده هزار اسب و چهار هزار اصطبل برای اسبان ارابه‌های خود داشت.
27 Maafisa wa eneo hilo, kila mmoja katika mwezi wake, walileta mahitaji kwa ajili ya Mfalme Solomoni na wote waliokula mezani mwa mfalme. Walihakikisha kuwa hakuna chochote kilichopungua.
حاکمان، هر یک در ماه تعیین شده، خوراک سلیمان و مهمانان او را بدون کم و کسر تهیه می‌کردند.
28 Pia walileta sehemu walizopangiwa za shayiri na majani kwa ajili ya farasi wavutao magari na farasi wengine mahali palipostahili.
در ضمن هر یک به سهم خود برای اسبان ارابه و سایر اسبان کاه و جو فراهم می‌ساختند.
29 Mungu akampa Solomoni hekima na akili kubwa, pia ufahamu mpana usiopimika kama mchanga ulioko pwani ya bahari.
خدا به سلیمان فهم و حکمت بی‌نظیری بخشید و بصیرت او مانند شنهای کنار دریا بی‌حد و حصر بود.
30 Hekima ya Solomoni ilikuwa kubwa kuliko hekima ya watu wote wa Mashariki na kubwa kuliko hekima yote ya Misri.
حکمت سلیمان از حکمت دانشمندان مشرق‌زمین و علمای مصر هم زیادتر بود.
31 Alikuwa na hekima kuliko kila mwandishi, akiwemo Ethani Mwezrahi: kuliko Hemani, Kalkoli na Darda, wana wa Maholi. Umaarufu wake ukaenea kwa mataifa yote yaliyomzunguka.
او حتی از حکمای معروفی چون ایتان ازراحی و پسران ماحول یعنی حیمان و کلکول و دَردَع حکیمتر بود. سلیمان در میان تمام ممالک دنیای زمان خود معروف شد.
32 Akanena mithali 3,000 na nyimbo zake zilikuwa 1,005.
سه هزار مثل گفت و هزار و پنج سرود نوشت.
33 Akaelezea maisha ya mimea kuanzia mwerezi wa Lebanoni hadi hisopo iotayo ukutani. Pia akafundisha kuhusu wanyama na ndege, wanyama wenye damu baridi, wakiwemo samaki.
سلیمان دربارهٔ حیوانات و پرندگان و خزندگان و ماهیان اطلاع کافی داشت، او همچنین تمام گیاهان را از درختان سرو لبنان گرفته تا بوته‌های کوچک زوفا که در شکاف دیوارها می‌رویند، می‌شناخت و دربارهٔ آنها سخن می‌گفت.
34 Watu wa mataifa yote wakaja kusikiliza hekima ya Solomoni, waliotumwa na wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamesikia juu ya hekima yake.
پادشاهان سراسر جهان که آوازهٔ حکمت او را شنیده بودند نمایندگانی به دربار او می‌فرستادند تا از حکمتش برخوردار شوند.

< 1 Wafalme 4 >