< 1 Wafalme 4 >

1 Basi Mfalme Solomoni akatawala Israeli yote.
Kong Salomo var Konge over hele Israel
2 Hawa ndio waliokuwa maafisa wake wakuu: Kuhani: Azaria mwana wa Sadoki;
Hans øverste Embedsmænd var følgende: Azarja, Zadoks Søn, var Ypperstepræst;
3 Elihorefu na Ahiya, wana wa Shisha: waandishi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi: karani;
Elihoref og Ahija, Sjisjas Sønner, var Statsskrivere; Josjafat, Ahiluds Søn, var Kansler;
4 Benaya mwana wa Yehoyada: jemadari mkuu wa jeshi; Sadoki na Abiathari: makuhani;
Benaja, Jojadas Søn, stod i Spidsen for Hæren; Zadok og Ebjatar var Præster;
5 Azaria mwana wa Nathani: kiongozi wa maafisa wa wilaya; Zabudi mwana wa Nathani: kuhani na mshauri binafsi wa mfalme;
Azarja, Natans Søn, var Overfoged; Præsten Zabud, Natans Søn, var Kongens Ven;
6 Ahishari: msimamizi wa jumba la kifalme; Adoniramu mwana wa Abda: msimamizi wa kazi za kulazimisha.
Ahisjar var Slotshøvedsmand; Adoniram, Abdas Søn, havde Tilsyn med Hoveriarbejdet.
7 Pia Solomoni alikuwa na watawala kumi na wawili wa wilaya katika Israeli yote, walioleta mahitaji kwa mfalme na kwa watu wa nyumbani kwa mfalme. Kila mmoja alitoa chakula kwa mwezi mmoja katika mwaka.
Fremdeles havde Salomno tolv Fogeder over hele Israel, som skulde sørge for Kongens og Hoffets Underhold, hver af dem en Måned om Året.
8 Majina yao ni haya: Ben-Huri: katika nchi ya vilima ya Efraimu;
Deres Navne var: Hurs Søn i Efraims Bjerge;
9 Ben-Dekeri: katika Makasi, Shaalbimu, Beth-Shemeshi na Elon-Bethhanani;
Dekers Søn i Makaz-Sja'albim, Bet-Sjemesj og Elon indtil Bet-Hanan;
10 Ben-Hesedi: katika Arubothi (Soko na nchi yote ya Heferi zilikuwa zake);
Heseds Søn i Arubbot; han havde Soko og hele Hefers Land;
11 Ben-Abinadabu: katika Nafoth-Dori (alimwoa Tafathi binti Solomoni);
Abinadabs Søn havde hele Dors Højland; han var gift med Salomos Datter Tafat;
12 Baana mwana wa Ahiludi: katika Taanaki na Megido, na katika Beth-Shani yote karibu na Sarethani chini ya Yezreeli, kuanzia Beth-Shani hadi Abel-Mehola kupita hadi Yokmeamu;
Ba'ana, Ahiluds Søn, havde Ta'anak, Megiddo og hele Bet- Sjean op til Zaretan, neden for Jizre'el fra Bet-Sjean til Abel-Mehola ud over Jokmeam;
13 Ben-Geberi: katika Ramoth-Gileadi (makao ya Yairi mwana wa Manase katika Gileadi ilikuwa miji yake, pamoja na wilaya ya Argobu katika Bashani na miji yake mikubwa sitini yenye kuzungukwa na kuta zenye makomeo ya shaba);
Gebers Søn i Ramot i Gilead; han havde Manasses Søn Ja'irs Teltbyer i Gilead, og han havde Argoblandet i Basan, tresindstyve store Byer med Mure og Kobberportstænger;
14 Ahinadabu mwana wa Ido: katika Mahanaimu;
Ahinadab, Iddos Søn, havde Mahanajim;
15 Ahimaasi: katika Naftali (alikuwa amemwoa Basemathi binti Solomoni);
Ahima'az i Naftali; han var ligeledes gift med en Datter af Salomo, Basemat;
16 Baana mwana wa Hushai: katika Asheri na katika Bealothi;
Ba'ana, Husjajs Søn, i Aser og Bealot;
17 Yehoshafati mwana wa Parua: katika Isakari;
Josjafat, Paruas Søn, i Issakar;
18 Shimei mwana wa Ela: katika Benyamini;
Sjim'i, Elas Søn, i Benjamin;
19 Geberi mwana wa Uri: katika Gileadi (nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani). Naye alikuwa ndiye mtawala pekee katika eneo hilo.
Geber, Uris Søn, i Gads Land, det Land, der havde tilhørt Amoriiterkongen Sihon og Kong Og af Basan; der var kun een Foged i det Land.
20 Watu wa Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani; walikula, wakanywa na kufurahi.
Juda og Israel var talrige, så talrige som Sandet ved Havet, og de spiste og drak og var glade.
21 Mfalme Solomoni akatawala katika falme zote kuanzia Mto Frati hadi nchi ya Wafilisti, hadi kwenye mpaka wa Misri. Nchi hizi zilileta ushuru na zilikuwa chini ya Solomoni, siku zote za maisha yake.
Og Salomo herskede over alle Rigerne fra Floden til Filisternes Land og Ægyptens Grænse og de bragte Gaver og tjente Salomo, så længe han levede.
22 Mahitaji ya Solomoni ya kila siku yalikuwa kori thelathini za unga laini, kori sitini za unga wa kawaida.
Salomos daglige Bebov af Levnedsmidler var tredive Kor fint Hvedemel og tresindstyve Kor almindeligt Mel,
23 Ngʼombe kumi wa zizini, ngʼombe ishirini wa malisho, kondoo na mbuzi mia moja, pamoja na ayala, paa, kulungu na kuku wazuri sana.
ti Stykker Fedekvæg, tyve Stykker Græskvæg og hundrede Stykker Småkvæg foruden Hjorte, Gazeller, Antiloper og fede Gæs.
24 Kwa kuwa Solomoni alitawala falme zote magharibi ya mto, kuanzia Tifsa hadi Gaza, naye akawa na amani pande zote.
Thi han herskede over hele Landet hinsides Floden, fra Tifsa til Gaza, over alle Kongerne hinsides Floden, og han håvde Fred rundt om til alle Sider;
25 Wakati wa maisha ya Solomoni Yuda na Israeli, kuanzia Dani mpaka Beer-Sheba, wakaishi salama kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake.
og Juda og Israel boede trygt, så længe Salomo levede, hver Mand under sin Vinstok og sit Figentræ, fra ban til Be'ersjeba.
26 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 ya magari ya vita, na farasi 12,000.
Og Salomo havde 40 000 Spand Heste til sit Vognhold og 12 000 Ryttere.
27 Maafisa wa eneo hilo, kila mmoja katika mwezi wake, walileta mahitaji kwa ajili ya Mfalme Solomoni na wote waliokula mezani mwa mfalme. Walihakikisha kuwa hakuna chochote kilichopungua.
Og de nævnte Fogeder sørgede for Underhold til Kong Salomo og alle, der havde Adgang til hans Bord, hver i sin Måned, og de lod det ikke skorte på noget;
28 Pia walileta sehemu walizopangiwa za shayiri na majani kwa ajili ya farasi wavutao magari na farasi wengine mahali palipostahili.
og Byggen og Strået til Hestene og Forspandene bragte de til det Sted, hvor han var, efter som Turen kom til hver enkelt.
29 Mungu akampa Solomoni hekima na akili kubwa, pia ufahamu mpana usiopimika kama mchanga ulioko pwani ya bahari.
Gud skænkede Salomo Visdom og Kløgt i såre rigt Mål og en omfattende Forstand, som Sandet ved Havets Bred,
30 Hekima ya Solomoni ilikuwa kubwa kuliko hekima ya watu wote wa Mashariki na kubwa kuliko hekima yote ya Misri.
så at Salomos Visdom var større end alle Østerlændingenes og alle Ægypternes Visdom.
31 Alikuwa na hekima kuliko kila mwandishi, akiwemo Ethani Mwezrahi: kuliko Hemani, Kalkoli na Darda, wana wa Maholi. Umaarufu wake ukaenea kwa mataifa yote yaliyomzunguka.
Han var visere end alle andre, ja visere end Ezraiten Etan og visere end Heman, Kalkol og Darda, Mabols Sønner, og hans Ry nåede ud til alle Folkeslag rundt om.
32 Akanena mithali 3,000 na nyimbo zake zilikuwa 1,005.
Han fremsagde 3000 Tanke sprog, og Tallet på hans Sange var 1 005"
33 Akaelezea maisha ya mimea kuanzia mwerezi wa Lebanoni hadi hisopo iotayo ukutani. Pia akafundisha kuhusu wanyama na ndege, wanyama wenye damu baridi, wakiwemo samaki.
Han talte om Træerne lige fra Cederen på Libanon til Ysopen, der vokser frem af Muren; og han talte om Dyrene, Fuglene, Krybdyrene og Fiskene.
34 Watu wa mataifa yote wakaja kusikiliza hekima ya Solomoni, waliotumwa na wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamesikia juu ya hekima yake.
Fra alle Folkeslag kom man for at lytte til Salomos Visdom, fra alle Jordens Konger, der hørte om hans Visdom.

< 1 Wafalme 4 >