< 1 Wafalme 3 >

1 Solomoni akafanya urafiki na Mfalme Farao wa Misri na kumwoa binti yake. Akamleta huyo binti katika Mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga jumba lake la kifalme na Hekalu la Bwana, pamoja na ukuta kuzunguka Yerusalemu.
and be related Solomon with Pharaoh king Egypt and to take: marry [obj] daughter Pharaoh and to come (in): bring her to(wards) city David till to end: finish he to/for to build [obj] house: home his and [obj] house: temple LORD and [obj] wall Jerusalem around
2 Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitoa dhabihu huko kwenye vilima, kwa sababu Hekalu lilikuwa bado halijajengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.
except [the] people to sacrifice in/on/with high place for not to build house: home to/for name LORD till [the] day [the] they(masc.)
3 Solomoni akaonyesha upendo wake kwa Bwana kwa kuenenda sawasawa na amri za Daudi baba yake, ila yeye alitoa dhabihu na kufukiza uvumba huko mahali pa juu.
and to love: lover Solomon [obj] LORD to/for to go: walk in/on/with statute David father his except in/on/with high place he/she/it to sacrifice and to offer: offer
4 Mfalme akaenda Gibeoni kutoa dhabihu, kwa maana ndipo palipokuwa mahali pa juu pa kuabudia, naye Solomoni akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya hayo madhabahu.
and to go: went [the] king Gibeon [to] to/for to sacrifice there for he/she/it [the] high place [the] great: large thousand burnt offering to ascend: offer up Solomon upon [the] altar [the] he/she/it
5 Bwana akamtokea Solomoni huko Gibeoni wakati wa usiku katika ndoto, naye Mungu akasema, “Omba lolote utakalo nikupe.”
in/on/with Gibeon to see: see LORD to(wards) Solomon in/on/with dream [the] night and to say God to ask what? to give: give to/for you
6 Solomoni akajibu, “Umemfanyia mtumishi wako, baba yangu Daudi, fadhili nyingi, kwa kuwa alikuwa mwaminifu kwako na mwenye haki, tena mnyofu wa moyo. Nawe umemzidishia fadhili hii kuu kwani umempa mwana wa kuketi kwenye kiti chake cha ufalme, kama ilivyo leo.
and to say Solomon you(m. s.) to make: do with servant/slave your David father my kindness great: large like/as as which to go: walk to/for face: before your in/on/with truth: faithful and in/on/with righteousness and in/on/with uprightness heart with you and to keep: obey to/for him [obj] [the] kindness [the] great: large [the] this and to give: give to/for him son: child to dwell upon throne his like/as day: today [the] this
7 “Sasa, Ee Bwana Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako mfalme badala ya baba yangu Daudi. Lakini mimi ni mtoto mdogo tu, wala sijui jinsi ya kutekeleza wajibu wangu.
and now LORD God my you(m. s.) to reign [obj] servant/slave your underneath: instead David father my and I youth small not to know to come out: come and to come (in): come
8 Mtumishi wako yuko hapa miongoni mwa watu uliowachagua: taifa kubwa, watu wengi wasioweza kuhesabika wala kutoa idadi yao.
and servant/slave your in/on/with midst people your which to choose people many which not to count and not to recount from abundance
9 Hivyo mpe mtumishi wako moyo wa ufahamu ili kutawala watu wako na kupambanua kati ya mema na mabaya. Kwa maana, ni nani awezaye kutawala watu wako hawa walio wengi hivi?”
and to give: give to/for servant/slave your heart to hear: understand to/for to judge [obj] people your to/for to understand between good to/for bad: evil for who? be able to/for to judge [obj] people your [the] heavy [the] this
10 Bwana akapendezwa kwamba Solomoni ameliomba jambo hili.
and be good [the] word: thing in/on/with eye: appearance Lord for to ask Solomon [obj] [the] word: thing [the] this
11 Basi Mungu akamwambia, “Kwa kuwa umeomba neno hili na hukuomba maisha marefu au upate utajiri kwa nafsi yako, wala adui zako wafe, bali umeomba ufahamu katika kutoa haki,
and to say God to(wards) him because which to ask [obj] [the] word: thing [the] this and not to ask to/for you day many and not to ask to/for you riches and not to ask soul: life enemy your and to ask to/for you to understand to/for to hear: judge justice
12 nitafanya lile uliloomba. Nitakupa moyo wa hekima na wa ufahamu, kiasi kwamba hajakuwepo mtu mwingine kama wewe, wala kamwe hatakuwepo baada yako.
behold to make: do like/as word your behold to give: give to/for you heart wise and to understand which like you not to be to/for face: before your and after you not to arise: rise like you
13 Zaidi ya hayo, nitakupa yale ambayo hukuomba, yaani utajiri na heshima, ili kwamba maisha yako yote hapatakuwa na mtu kama wewe miongoni mwa wafalme.
and also which not to ask to give: give to/for you also riches also glory which not to be like you man: anyone in/on/with king all day your
14 Nawe kama ukienenda katika njia zangu na kutii sheria na amri zangu kama baba yako Daudi alivyofanya, nitakupa maisha marefu.”
and if to go: walk in/on/with way: conduct my to/for to keep: obey statute: decree my and commandment my like/as as which to go: walk David father your and to prolong [obj] day your
15 Ndipo Solomoni akaamka, akatambua kuwa ilikuwa ndoto. Akarudi Yerusalemu, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Bwana, naye akatoa dhabihu za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha akawafanyia watumishi wake wote karamu.
and to awake Solomon and behold dream and to come (in): come Jerusalem and to stand: stand to/for face: before ark covenant Lord and to ascend: offer up burnt offering and to make: offer peace offering and to make feast to/for all servant/slave his
16 Basi wanawake wawili makahaba walikuja kwa mfalme na kusimama mbele yake.
then to come (in): come two woman to fornicate to(wards) [the] king and to stand: stand to/for face: before his
17 Mmojawapo akasema, “Bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunaishi kwenye nyumba moja. Nilikuwa nimezaa alipokuwa pamoja nami.
and to say [the] woman [the] one please lord my I and [the] woman [the] this to dwell in/on/with house: home one and to beget with her in/on/with house: home
18 Siku ya tatu baada ya mtoto wangu kuzaliwa, mwanamke huyu pia naye akazaa mtoto. Tulikuwa peke yetu, hapakuwa na mtu mwingine yeyote katika nyumba isipokuwa sisi wawili.
and to be in/on/with day [the] third to/for to beget me and to beget also [the] woman [the] this and we together nothing be a stranger with us in/on/with house: home exception two we in/on/with house: home
19 “Wakati wa usiku mwana wa huyu mwanamke akafa kwa sababu alimlalia.
and to die son: child [the] woman [the] this night which to lie down: lay down upon him
20 Hivyo akaondoka katikati ya usiku na kumchukua mwanangu kutoka ubavuni pangu wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa nimelala. Akamweka kifuani mwake na kumweka mwanawe aliyekufa kifuani mwangu.
and to arise: rise in/on/with midst [the] night and to take: take [obj] son: child my from beside me and maidservant your sleeping and to lie down: lay down him in/on/with bosom: embrace her and [obj] son: child her [the] to die to lie down: lay down in/on/with bosom: embrace my
21 Asubuhi yake, nikaamka ili kumnyonyesha mwanangu, naye alikuwa amekufa! Lakini nilipomwangalia sana katika nuru ya asubuhi, niliona kuwa hakuwa yule mwana niliyekuwa nimemzaa.”
and to arise: rise in/on/with morning to/for to suckle [obj] son: child my and behold to die and to understand to(wards) him in/on/with morning and behold not to be son: child my which to beget
22 Huyo mwanamke mwingine akasema, “Hapana! Mwana aliye hai ndiye wangu, aliyekufa ni wako.” Lakini yule wa kwanza akasisitiza, “Hapana! Mwana aliyekufa ni wako, aliye hai ni wangu.” Hivi ndivyo walivyobishana mbele ya mfalme.
and to say [the] woman [the] another not for son: child my [the] alive and son: child your [the] to die and this to say not for son: child your [the] to die and son: child my [the] alive and to speak: speak to/for face: before [the] king
23 Mfalme akasema, “Huyu anasema, ‘Mwanangu ndiye aliye hai, na aliyekufa ndiye mwanao,’ maadamu yule anasema, ‘Hapana! Aliyekufa ni wako, na aliye hai ni wangu.’”
and to say [the] king this to say this son: child my [the] alive and son: child your [the] to die and this to say not for son: child your [the] to die and son: child my [the] alive
24 Kisha mfalme akasema, “Nileteeni upanga.” Basi wakamletea mfalme upanga.
and to say [the] king to take: bring to/for me sword and to come (in): bring [the] sword to/for face: before [the] king
25 Ndipo mfalme akatoa amri: “Mkate mtoto aliye hai vipande viwili; mpe huyu nusu na mwingine nusu.”
and to say [the] king to cut [obj] [the] youth [the] alive to/for two and to give: give [obj] [the] half to/for one and [obj] [the] half to/for one
26 Mwanamke ambaye mwanawe alikuwa hai akajawa na huruma kwa ajili ya mwanawe na kumwambia mfalme, “Tafadhali, bwana wangu, mpe yeye mtoto aliye hai! Usimuue!” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Mkate vipande viwili. Asiwe wangu au wake!”
and to say [the] woman which son: child her [the] alive to(wards) [the] king for to grow warm compassion her upon son: child her and to say please lord my to give: give to/for her [obj] [the] to beget [the] alive and to die not to die him and this to say also to/for me also to/for you not to be to cut
27 Kisha mfalme akatoa uamuzi wake: “Mpeni mama wa kwanza mtoto aliye hai. Msimuue; ndiye mama yake.”
and to answer [the] king and to say to give: give to/for her [obj] [the] to beget [the] alive and to die not to die him he/she/it mother his
28 Wakati Israeli yote iliposikia hukumu aliyotoa mfalme, wakamwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa alikuwa na hekima kutoka kwa Mungu kwa kutoa haki.
and to hear: hear all Israel [obj] [the] justice: judgement which to judge [the] king and to fear: revere from face of [the] king for to see: examine for wisdom God in/on/with entrails: among his to/for to make: do justice

< 1 Wafalme 3 >