< 1 Wafalme 3 >
1 Solomoni akafanya urafiki na Mfalme Farao wa Misri na kumwoa binti yake. Akamleta huyo binti katika Mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga jumba lake la kifalme na Hekalu la Bwana, pamoja na ukuta kuzunguka Yerusalemu.
А Соломон се сроди с египетския цар Фараона, като взе Фараоновата дъщеря; и доведе я да живее в Давидовия град догде да свърши съграждането на своя дом, и на Господния дом и не стената около Ерусалим.
2 Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitoa dhabihu huko kwenye vilima, kwa sababu Hekalu lilikuwa bado halijajengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.
Но людете жертвуваха по високите места, понеже до онова време нямаше дом съграден за Господното име.
3 Solomoni akaonyesha upendo wake kwa Bwana kwa kuenenda sawasawa na amri za Daudi baba yake, ila yeye alitoa dhabihu na kufukiza uvumba huko mahali pa juu.
И Соломон възлюби Господа, и ходеше в повеленията на баща си Давида; само че жертвуваше и кадеше по високите места.
4 Mfalme akaenda Gibeoni kutoa dhabihu, kwa maana ndipo palipokuwa mahali pa juu pa kuabudia, naye Solomoni akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya hayo madhabahu.
И царят отиде в Гаваон, за да принесе там жертва, защото това бе главното високо място; хиляда всеизгаряния принесе Соломон на оня олтар.
5 Bwana akamtokea Solomoni huko Gibeoni wakati wa usiku katika ndoto, naye Mungu akasema, “Omba lolote utakalo nikupe.”
А в Гаваон Господ се яви на Соломона на сън през нощта; и рече Бог: Искай какво да ти дам.
6 Solomoni akajibu, “Umemfanyia mtumishi wako, baba yangu Daudi, fadhili nyingi, kwa kuwa alikuwa mwaminifu kwako na mwenye haki, tena mnyofu wa moyo. Nawe umemzidishia fadhili hii kuu kwani umempa mwana wa kuketi kwenye kiti chake cha ufalme, kama ilivyo leo.
А Соломон каза: Ти показа голяма милост към слугата Си баща ми Давида, понеже той ходи пред Тебе във вярност, в правда и в сърдечна правота с Тебе; и Ти си запазил за него тая голяма милост, че си му дал син да седи на престола му, както е днес.
7 “Sasa, Ee Bwana Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako mfalme badala ya baba yangu Daudi. Lakini mimi ni mtoto mdogo tu, wala sijui jinsi ya kutekeleza wajibu wangu.
И сега, Господи Боже мой, Ти си направил слугата Си цар вместо баща ми Давида; а аз съм малко момче; на зная как да се обхождам.
8 Mtumishi wako yuko hapa miongoni mwa watu uliowachagua: taifa kubwa, watu wengi wasioweza kuhesabika wala kutoa idadi yao.
И слугата Ти е всред Твоите люде които Ти си избрал, люде много, които поради множеството си не могат да се изброят, нито да се пресметнат.
9 Hivyo mpe mtumishi wako moyo wa ufahamu ili kutawala watu wako na kupambanua kati ya mema na mabaya. Kwa maana, ni nani awezaye kutawala watu wako hawa walio wengi hivi?”
Дай, прочее, на слугата Си разумно сърце, за да съди людете Ти, за да различава между добро и зло; защото кой може да съди тоя Твой голям народ;
10 Bwana akapendezwa kwamba Solomoni ameliomba jambo hili.
И тия думи бяха угодни Господу, понеже Соломон поиска това нещо.
11 Basi Mungu akamwambia, “Kwa kuwa umeomba neno hili na hukuomba maisha marefu au upate utajiri kwa nafsi yako, wala adui zako wafe, bali umeomba ufahamu katika kutoa haki,
И Бог му каза: Понеже ти поиска това нещо, и не поиска за себе си дълъг живот, нито поиска за себе си богатство, нито поиска смъртта на неприятелите си, но поиска за себе си разум за да разбираш правосъдие,
12 nitafanya lile uliloomba. Nitakupa moyo wa hekima na wa ufahamu, kiasi kwamba hajakuwepo mtu mwingine kama wewe, wala kamwe hatakuwepo baada yako.
ето, сторих според както си казал; ето, дадох ти мъдро и разумно сърце, така щото преди тебе не е имало подобен на тебе, нито подир тебе ще се издигне подобен на тебе.
13 Zaidi ya hayo, nitakupa yale ambayo hukuomba, yaani utajiri na heshima, ili kwamba maisha yako yote hapatakuwa na mtu kama wewe miongoni mwa wafalme.
А при това ти дадох каквото не си поискал - и богатство и слава, така щото между царете не ще има подобен на тебе през всичките ти дни.
14 Nawe kama ukienenda katika njia zangu na kutii sheria na amri zangu kama baba yako Daudi alivyofanya, nitakupa maisha marefu.”
И ако ходиш в Моите пътища, и пазиш повеленията Ми и заповедите Ми, както ходи баща ти Давид, тогава ще продължа дните ти.
15 Ndipo Solomoni akaamka, akatambua kuwa ilikuwa ndoto. Akarudi Yerusalemu, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Bwana, naye akatoa dhabihu za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha akawafanyia watumishi wake wote karamu.
И събуди се Соломон; и, ето, бе сън. След това, дойде в Ерусалим и като застана пред ковчега на Господния завет, пожертвува всеизгаряния и принесе примирителни приноси; направи и угощение на всичките си слуги.
16 Basi wanawake wawili makahaba walikuja kwa mfalme na kusimama mbele yake.
Тогава дойдоха при царя две блудници та застанаха пред него.
17 Mmojawapo akasema, “Bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunaishi kwenye nyumba moja. Nilikuwa nimezaa alipokuwa pamoja nami.
И едната жена рече: О, господарю мой! аз и тая жена живеем в една къща; и аз родих като живеех с нея в къщата.
18 Siku ya tatu baada ya mtoto wangu kuzaliwa, mwanamke huyu pia naye akazaa mtoto. Tulikuwa peke yetu, hapakuwa na mtu mwingine yeyote katika nyumba isipokuwa sisi wawili.
И на третия ден, откак родих аз, роди и тая жена; и ние бяхме сами заедно, нямаше външен човек с нас в къщата, само ние двете бяхме в къщата.
19 “Wakati wa usiku mwana wa huyu mwanamke akafa kwa sababu alimlalia.
И през нощта умря синът на тая жена, понеже го налегнала.
20 Hivyo akaondoka katikati ya usiku na kumchukua mwanangu kutoka ubavuni pangu wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa nimelala. Akamweka kifuani mwake na kumweka mwanawe aliyekufa kifuani mwangu.
А тя, като станала посред нощ, взела сина ми от при мене, когато слугинята ти спеше, та го турила на своята пазуха, а своя мъртъв син турила на моята пазуха.
21 Asubuhi yake, nikaamka ili kumnyonyesha mwanangu, naye alikuwa amekufa! Lakini nilipomwangalia sana katika nuru ya asubuhi, niliona kuwa hakuwa yule mwana niliyekuwa nimemzaa.”
И в зори, като станах, за да накърмя сина си, ето, той бе мъртъв; но на утринта, като го разгледах, ето, не бе моят син, когото бях родила.
22 Huyo mwanamke mwingine akasema, “Hapana! Mwana aliye hai ndiye wangu, aliyekufa ni wako.” Lakini yule wa kwanza akasisitiza, “Hapana! Mwana aliyekufa ni wako, aliye hai ni wangu.” Hivi ndivyo walivyobishana mbele ya mfalme.
А другата жена рече: Не, но живият е моят син, и мъртвият е твоят син. А тая рече: Не, но мъртвият е твоят син, а живият е моят син. Така говориха пред царя.
23 Mfalme akasema, “Huyu anasema, ‘Mwanangu ndiye aliye hai, na aliyekufa ndiye mwanao,’ maadamu yule anasema, ‘Hapana! Aliyekufa ni wako, na aliye hai ni wangu.’”
Тогава царят рече: Едната казва: Тоя живият е моят син, а мъртвият е твоят син; а другата казва: Не, но мъртвият е твоят син, а живият е моят син.
24 Kisha mfalme akasema, “Nileteeni upanga.” Basi wakamletea mfalme upanga.
И царят рече: Донесете ми нож. И донесоха нож пред царя.
25 Ndipo mfalme akatoa amri: “Mkate mtoto aliye hai vipande viwili; mpe huyu nusu na mwingine nusu.”
И царят рече: Разделете на две живото дете, и дайте половината на едната и половината на другата.
26 Mwanamke ambaye mwanawe alikuwa hai akajawa na huruma kwa ajili ya mwanawe na kumwambia mfalme, “Tafadhali, bwana wangu, mpe yeye mtoto aliye hai! Usimuue!” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Mkate vipande viwili. Asiwe wangu au wake!”
Тогава оная жена, чието беше живото дете, говори на царя (защото сърцето й я заболя за сина й), казвайки: О господарю мой! дай й живото дете, и недей го убива. А другата рече: Нито мое да е, нито твое; разделете го.
27 Kisha mfalme akatoa uamuzi wake: “Mpeni mama wa kwanza mtoto aliye hai. Msimuue; ndiye mama yake.”
Тогава царят в отговор рече: Дайте на тая живото дете, и недейте го убива; тая е майка му.
28 Wakati Israeli yote iliposikia hukumu aliyotoa mfalme, wakamwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa alikuwa na hekima kutoka kwa Mungu kwa kutoa haki.
И целият Израил чу за съда който царят отсъди; и бояха се от царя, защото видяха, че Божия мъдрост имаше в него, за да раздава правосъдие.