< 1 Wafalme 22 >
1 Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
A nie było przez trzy lata wojny między Syryjczykami i między Izraelczykami.
2 Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
I stało się roku trzeciego, że przyjechał Jozafat król Judzki, do króla Izraelskiego.
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
Tedy rzekł król Izraelski do sług swoich: Nie wiecież, iż nasze jest Ramot Galaad? A my zaniedbywamy odebrać go z ręki króla Syryjskiego.
4 Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
Przetoż rzekł do Jozafata: Pociągnieszże ze mną na wojnę przeciwko Ramot Galaad? I rzekł Jozafat do króla Izraelskiego: Jakom ja, tak i ty; jako lud mój, tak lud twój; jako konie moje, tak konie twoje.
5 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
Nadto rzekł Jozafat do króla Izraelskiego: Spytaj się proszę dziś słowa Pańskiego.
6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
A tak zebrał król Izraelski proroków około czterech set mężów, i rzekł do nich: Mamże ciągnąć na wojnę przeciwko Ramot Galaad? czy zaniechać? I odpowiedzieli mu: Ciągnij; bo je Pan da w ręce królewskie.
7 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
Ale Jozafat rzekł: Nie maszże tu którego proroka Pańskiego, żebyśmy się go pytali?
8 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
I rzekł król Izraelski do Jozafata: Jest jeszcze mąż jeden, przez któregobyśmy się mogli radzić Pana; ale go ja nienawidzę, bo mi nic dobrego nie prorokuje, jedno złe, Micheasz, syn Jemla. I rzekł Jozafat: Niech tak nie mówi król.
9 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
A tak zawołał król Izraelski komornika niektórego, i rzekł: Przywiedź tu rychło Micheasza, syna Jemlowego.
10 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
Między tem król Izraelski, i Jozafat, król Judzki, siedzieli na stolicach swoich, ubrani w szaty królewskie, na placu u wrót bramy Samaryjskiej, a wszyscy prorocy prorokowali przed nimi.
11 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
A Sedechyjasz, syn Chenaana, sprawił sobie rogi żelazne, i rzekł: Tak mówi Pan: Temi będziesz bódł Syryjczyki, aż je wyniszczysz.
12 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
Także wszyscy prorocy prorokowali, mówiąc: Ciągnij do Ramot Galaad, a będzieć się szczęściło; albowiem je poda Pan w ręce królewskie.
13 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
Tedy poseł, który chodził, aby przyzwał Micheasza, rzekł do niego, mówiąc: Oto teraz słowa proroków jednemi usty dobrze tuszą królowi; niechże będzie proszę słowo twoje, jako słowo jednego z nich, a mów dobre rzeczy.
14 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
I rzekł Micheasz: Jako żywy Pan, że co mi kolwiek rzecze Pan, to mówić będę.
15 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
A gdy przyszedł do króla, rzekł król do niego: Micheaszu, mamyż ciągnąć na wojnę przeciw Ramot Galaad, czyli zaniechać? A on mu rzekł: Ciągnij, a będzieć się szczęściło; albowiem je poda Pan w ręce królewskie.
16 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
I rzekł do niego król: A wieleż cię razy mam przysięgą obowiązać, abyś mi nie mówił jedno prawdę w imieniu Pańskiem?
17 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
Przetoż rzekł: Widziałem wszystek lud Izraelski rozproszony po górach jako owce, które nie mają pasterza; bo rzekł Pan: Nie mają ci pana; niech się wróci każdy do domu swego w pokoju.
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
I rzekł król Izraelski do Jozafata: Izażem ci nie powiadał, że mi nie miał prorokować dobrego, ale złe?
19 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
A Micheasz rzekł: Słuchajże tedy słowa Pańskiego: Widziałem Pana siedzącego na stolicy swojej, i wszystko wojsko niebieskie stojące po prawicy jego, i po lewicy jego.
20 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
I rzekł Pan: Kto zwiedzie Achaba, aby szedł a upadł w Ramot Galaad? A gdy mówił jeden tak, a drugi inaczej;
21 Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
Tedy wystąpił duch, i stanął przed Panem, mówiąc: Ja go zwiodę. A Pan mu rzekł: Przez cóż?
22 “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
Odpowiedział: Wynijdę, a będę duchem kłamliwym w ustach wszystkich proroków jego. I rzekł mu Pan: Zwiedziesz, i pewnie przemożesz. Idźże, a czyń tak.
23 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
Przetoż teraz oto dał Pan ducha kłamliwego w usta tych wszystkich proroków twoich, gdyż Pan wyrzekł przeciwko tobie złe.
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
Tedy przystąpiwszy Sedechyjasz, syn Chenaana, uderzył Micheasza w policzek, mówiąc: Kiedyż odszedł Duch Pański odemnie, aby z tobą mówił?
25 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
I odpowiedział Micheasz: Oto ty ujrzysz dnia onego, kiedy wnijdziesz do najskrytszej komory, abyś się skrył.
26 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
I rzekł król Izraelski: Weźmij Micheasza, a wiedź go do Amona, starosty miejskiego, i do Joasa, syna królewskiego.
27 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
I rzeczesz: Tak mówi król: Wsadźcie tego męża do więzienia; a dawajcie mu jeść chleb utrapienia i wodę ucisku, aż się wrócę w pokoju.
28 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
Ale odpowiedział Micheasz: Jeźliże się wrócisz w pokoju, tedyć nie mówił Pan przez mię. Nadto rzekł: Słuchajcież wszyscy ludzie.
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
A tak ciągnął król Izraelski i Jozafat, król Judzki, do Ramot Galaad.
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
I rzekł król Izraelski do Jozafata: Odmienię się, gdy pójdę do bitwy; ale ty ubierz się w szaty twoje. I odmienił się król Izraelski, a szedł ku bitwie.
31 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
A król Syryjski rozkazał był hetmanom, których było trzydzieści i dwa nad wozami jego, mówiąc: Nie potykajcie się ani z małym, ani z wielkim, tylko z samym królem Izraelskim.
32 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
I stało się, gdy ujrzeli Jozafata hetmani, co byli nad wozami, rzekli: Zaprawdę to król Izraelski; i obrócili się przeciwko niemu, chcąc się z nim potykać; ale Jozafat zawołał.
33 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
Wtem obaczywszy hetmani, co byli nad wozami, że nie ten był król Izraelski, odwrócili się od niego.
34 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
Lecz mąż niektóry strzelił z łuku na niepewne, i postrzelił króla Izraelskiego między nity i między pancerz; który rzekł woźnicy swemu: Nawróć, a wywieź mię z wojska; bom jest raniony.
35 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
I wzmogła się bitwa dnia onego, a król stał na wozie przeciw Syryjczykom: potem umarł w wieczór, a krew ciekła z rany jego na wóz.
36 Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
Tedy wołał woźny w wojsku, gdy już słońce zachodziło, mówiąc: Wróć się każdy do miasta swego i każdy do ziemi swojej.
37 Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
A tak umarł król, a odwiezion jest do Samaryi, i pochowano go w Samaryi.
38 Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
A gdy umywano wóz w sadzawce Samaryjskiej, lizali psy krew jego, także gdy umywano zbroję jego: według słowa Pańskiego, które był powiedział.
39 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
A inne sprawy Achabowe i wszystko, co czynił, i dom z kości słoniowych, który zbudował, wszystkie też miasta, które pobudował, azaż to nie jest spisane w kronikach o królach Izraelskich?
40 Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
I zasnął Achab z ojcami swymi, a królował Ochozyjasz, syn jego, miasto niego.
41 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
A Jozafat, syn Azy, począł królować nad Judą czwartego roku za panowania Achaba, króla Izraelskiego.
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
A Jozafat miał trzydzieści i pięć lat, gdy królować począł, a dwadzieścia i pięć lat królował w Jeruzalemie; a imię matki jego było Azuba, córka Salajowa.
43 Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
I chodził po wszystkiej drodze Azy, ojca swego, a nie odchylał się od niej, czyniąc to, co było dobrego przed oczyma Pańskiemi. Wszakże iż wyżyn nie poburzyli, jeszcze lud ofiarował i kadził po wyżynach.
44 Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
Uczynił też pokój Jozafat z królem Izraelskim.
45 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
A inne sprawy Jozafatowe, i moc jego, której dokazywał, i jako walczył, azaż to nie jest napisane w kronikach królów Judzkich?
46 Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
Ten wyplenił z ziemi ostatek Sodomczyków, którzy byli pozostali za dni Azy, ojca jego.
47 Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
Na ten czas nie było króla w Edomskiej ziemi; tylko starosta był miasto króla.
48 Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
I nasprawiał Jozafat okrętów na morze, aby chodziły do Ofir po złoto. Ale nie doszły; bo się rozbiły one okręty w Asyjon Gaber.
49 Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
Rzekł także był Ochozyjasz, syn Achaba, do Jozafata: Niech jadą słudzy moi z sługami twymi w okrętach. Ale niechciał Jozafat.
50 Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
Zasnął tedy Jozafat z ojcami swymi, i pochowany jest z ojcami swymi w mieście Dawida, ojca swego; a królował Joram, syn jego, miasto niego.
51 Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
Ochozyjasz, syn Achaba, począł królować nad Izraelem w Samaryi roku siedmnastego Jozafata, króla Judzkiego, i królował nad Izraelem dwa lata.
52 Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
I czynił złe przed oczyma Pańskiemi, chodząc drogą ojca swego, i drogą matki swej, i drogą Jeroboama, syna Nabatowego, który przywiódł do grzechów Izraela.
53 Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
Służył także Baalowi, a kłaniał mu się, i pobudzał do gniewu Pana, Boga Izraelskiego, według wszystkiego, co czynił ojciec jego.