< 1 Wafalme 22 >

1 Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
Un trīs gadus tiem bija miers un kara nebija starp Sīriešiem un Israēli.
2 Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
Bet trešā gadā Jehošafats, Jūda ķēniņš, nogāja pie Israēla ķēniņa.
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
Un Israēla ķēniņš sacīja uz saviem kalpiem: vai jūs nezināt, ka Rāmota Gileādā pieder mums, un mēs esam klusu un viņu neņemam no Sīriešu ķēniņa rokas?
4 Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
Un viņš sacīja uz Jehošafatu: vai tu ar mani gribi iet karā pret Rāmotu Gileādā? Un Jehošafats sacīja uz Israēla ķēniņu: es būšu kā tu, un mani ļaudis kā tavi ļaudis, un mani zirgi kā tavi zirgi.
5 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
Un Jehošafats sacīja uz Israēla ķēniņu: vaicā jel šodien Tā Kunga vārdu.
6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
Un Israēla ķēniņš sapulcināja tos praviešus, četrsimt vīrus, un sacīja uz tiem: vai man būs iet karā uz Rāmotu Gileādā, jeb vai man no tam būs atstāties? Un tie sacīja: celies, jo Tas Kungs viņu dos ķēniņa rokā.
7 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
Bet Jehošafats sacīja: vai še nav vēl kāds no Tā Kunga praviešiem, ka mēs to varētu vaicāt?
8 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
Un Israēla ķēniņš sacīja uz Jehošafatu: vēl ir gan viens vīrs, caur ko To Kungu var vaicāt, bet es viņu ienīstu, jo tas man nesludina labu, bet ļaunu vien, Miha, Jemlas dēls. Un Jehošafats sacīja: lai ķēniņš tā nerunā.
9 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
Tad Israēla ķēniņš aicināja vienu sulaini un sacīja: atved drīz Mihu, Jemlas dēlu.
10 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
Un Israēla ķēniņš un Jehošafats, Jūda ķēniņš, sēdēja ikkatrs savā krēslā savās drēbēs ģērbušies tai pagalmā, kur ieiet pa Samarijas vārtiem, un visi pravieši sludināja viņu priekšā.
11 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
Un Cedeķija, Kenaānas dēls, taisīja sev dzelzs ragus un sacīja: tā saka Tas Kungs: ar šiem tu badīsi Sīriešus, kamēr tos izdeldēsi.
12 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
Un visi pravieši sludināja tā sacīdami: celies pret Rāmotu Gileādā, jums būs laba laime, jo Tas Kungs viņu dos ķēniņa rokā.
13 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
Un tas vēstnesis, kas bija gājis pēc Miha, uz to runāja un sacīja: redzi jel, tie pravieši runā vienā mutē labu ķēniņam, lai jel tavs vārds tāpat ir kā viņu vārds, un runā labu.
14 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
Bet Miha sacīja: tik tiešām kā Tas Kungs dzīvs, ko Tas Kungs uz mani sacīs, to es runāšu.
15 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
Un kad viņš nāca ķēniņa priekšā, tad ķēniņš uz viņu sacīja: Miha, vai mums būs iet karā pret Rāmotu Gileādā, jeb vai mums no tam būs atstāties? Un tas uz viņu sacīja: celies, tev izdosies, jo Tas Kungs viņu dos ķēniņa rokā.
16 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
Tad ķēniņš uz viņu sacīja: cik reiz man tev būs piekodināt, cita nekā man nesacīt kā taisnību Tā Kunga Vārdā?
17 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
Un viņš sacīja: es redzēju visu Israēli izklīdinātu pa kalniem, itin kā avis, kam gana nav. Un Tas Kungs sacīja: šiem kunga nav, lai ikviens ar mieru iet savā namā.
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
Tad Israēla ķēniņš sacīja uz Jehošafatu: vai es tev neesmu sacījis, ka viņš par mani labu nesludina, bet ļaunu?
19 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
Un (Miha) sacīja: “Tādēļ klausi Tā Kunga vārdu: es redzēju To Kungu sēžam uz Sava goda krēsla un visu debess spēku ap Viņu stāvam pa labai un pa kreisai rokai.
20 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
Un Tas Kungs sacīja: “Kurš pierunās Ahabu, lai tas ceļas un krīt Rāmotā Gileādā?” Un viens runāja šā, otrs tā.
21 Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
Tad viens gars izgāja un nostājās Tā Kunga priekšā un sacīja: “Es viņu pierunāšu.” Tad Tas Kungs uz to sacīja: “Caur ko?”
22 “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
Un viņš sacīja: “Es iziešu un būšu melu gars visu viņa praviešu mutē.” Un Viņš sacīja: “Tu viņu pierunāsi un arī pārspēsi; ej un dari tā.”
23 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
Un nu redzi, Tas Kungs melu garu devis visu šo tavu praviešu mutē, un Tas Kungs par tevi ļaunu runājis.”
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
Tad Cedeķija, Kenaānas dēls, piegāja un deva Miham pliķi un sacīja: kā tad Tā Kunga Gars būtu no manis atstājies, ar tevi runāt?
25 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
Un Miha sacīja: redzi, to tu redzēsi tai dienā, kad tu no vienas istabas otrā iesi paslēpties.
26 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
Un Israēla ķēniņš sacīja: ņem Mihu un ved to atpakaļ pie Amona, pilsētas virsnieka, un pie Joasa, ķēniņa dēla,
27 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
Un saki: tā saka ķēniņš: liekat to cietumā un ēdinājiet to ar bēdu maizi un ar bēdu ūdeni, kamēr es atkal laimīgs pārnākšu.
28 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
Un Miha sacīja: ja tu atkal laimīgs pārnāksi, tad Tas Kungs caur mani nav runājis. Un viņš sacīja: klausāties, visi ļaudis!
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
Tā Israēla ķēniņš un Jehošafats, Jūda ķēniņš, cēlās pret Rāmotu Gileādā.
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
Un Israēla ķēniņš sacīja uz Jehošafatu: es pārģērbies iešu kaujā, bet tu ģērbies savās drēbēs. Un Israēla ķēniņš pārģērbās un gāja kaujā.
31 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
Un Sīriešu ķēniņš saviem ratu virsniekiem (to bija trīsdesmit un divi) bija pavēlējis un sacījis: nelaužaties ne uz mazu ne uz lielu, bet uz Israēla ķēniņu vien.
32 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
Kad nu tie ratu virsnieki Jehošafatu redzēja, tad tie sacīja: tiešām tas ir Israēla ķēniņš, un tie griezās un lauzās uz viņu, bet Jehošafats brēca.
33 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
Kad nu tie ratu virsnieki redzēja, ka šis nebija Israēla ķēniņš, tad tie no viņa griezās nost.
34 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
Un viens vīrs uzvilka savu stopu no nejauši un iešāva Israēla ķēniņam starp sprādzēm un krūšu bruņām. Tad viņš sacīja uz savu ratu vadītāju: griez savu roku un izved mani no kaujas, jo es esmu ievainots.
35 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
Un kaušanās palika karsta tai dienā, un ķēniņš stāvēja savos ratos Sīriešiem pretī un nomira vakarā; un asinis tecēja no vainas uz ratu grīdu.
36 Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
Tad pa visu karapulku saulei noejot sauca un sacīja: ikviens uz savu pilsētu, ikviens uz savu zemi!
37 Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
Tā ķēniņš nomira un tapa novests uz Samariju, un ķēniņu apraka Samarijā.
38 Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
Kad nu tos ratus mazgāja Samarijas dīķī, tad maukām mazgājoties suņi laizīja viņa asinis pēc Tā Kunga vārda, ko viņš bija runājis.
39 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Kas nu vēl par Ahabu stāstāms, un viss, ko viņš darījis, un tas ziloņkaulu nams, ko viņš taisījis, un visas pilsētas, ko viņš cēlis, tas viss rakstīts Israēla ķēniņu laiku grāmatā.
40 Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Tā Ahabs aizmiga saviem tēviem pakaļ, un Ahazija, viņa dēls, palika par ķēniņu viņa vietā.
41 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
Un Jehošafats, Asas dēls, palika par ķēniņu pār Jūdu Ahaba, Israēla ķēniņa, ceturtā gadā.
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Un Jehošafats bija trīsdesmit un piecus gadus vecs, kad viņš palika par ķēniņu un valdīja divdesmit un piecus gadus Jeruzālemē. Un viņa mātei bija vārds Azuba, Šilkus meita.
43 Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Un viņš staigāja visos sava tēva Asas ceļos, viņš no tiem neatstājās un darīja, kas Tam Kungam patika. Tik tie kalnu altāri netapa nopostīti, un tie ļaudis upurēja un kvēpināja vēl pa tiem kalniem.
44 Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
Un Jehošafatam bija miers ar Israēla ķēniņu.
45 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Un kas vēl stāstāms par Jehošafatu un viņa spēks, ko viņš parādījis, un kā viņš karojis, tas viss ir rakstīts Jūda ķēniņu laiku grāmatā,
46 Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
Viņš arī izdzina no zemes tos atlikušos mauciniekus, kas Asas, viņa tēva, laikā bija atlikuši.
47 Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
To brīdi neviena ķēniņa nebija Edomā, bet ķēniņa vietnieks valdīja.
48 Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
Un Jehošafats lika taisīt lielus kuģus, braukt uz Ofiru pēc zelta. Bet tie nenogāja, jo EceonĢeberā tie kuģi tapa sadragāti.
49 Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
Tad Ahazija, Ahaba dēls, sacīja uz Jehošafatu: lai mani kalpi iet ar taviem kalpiem līdzi uz laivām. Bet Jehošafats negribēja.
50 Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
Un Jehošafats aizmiga saviem tēviem pakaļ un tapa aprakts pie saviem tēviem Dāvida pilsētā. Un viņa dēls Jehorams palika par ķēniņu viņa vietā.
51 Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
Un Ahazija, Ahaba dēls, palika par ķēniņu pār Israēli Samarijā Jehošafata, Jūda ķēniņa, septiņpadsmitā gadā, un valdīja divus gadus pār Israēli.
52 Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
Un viņš darīja, kas Tam Kungam nepatika, un staigāja sava tēva ceļā un savas mātes ceļā un Jerobeama, Nebata dēla, ceļā, kas Israēli paveda uz grēkiem.
53 Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
Un viņš kalpoja Baālam un metās zemē priekš tā un apkaitināja To Kungu, Israēla Dievu, tā kā viņa tēvs bija darījis.

< 1 Wafalme 22 >