< 1 Wafalme 22 >

1 Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
Tallo a tawen ti naglabas nga awan ti gubat iti nagbaetan ti Aram ken Israel.
2 Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
Ket napasamak nga iti maikatlo a tawen, napan ni Jehosafat nga ari ti Juda iti ari ti Israel.
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
Ita, kinuna ti ari ti Israel kadagiti adipenna, “Ammoyo kadi a ti Ramot Galaad ket kukuatayo, ngem awan ti ar-aramidentayo tapno maalatayo daytoy manipud iti ima ti ari ti Aram?”
4 Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
Isu a kinunana kenni Jehosafat, “Kaduaannak kadi a maki-gubat idiay Ramot Galaad?” Simmungbat ni Jehosafat iti ari ti Israel, “Agserbiak kenka, agbalin dagiti tattaok a tattaom, ken dagiti kabaliok a kabaliom.”
5 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
Kinuna ni Jehosafat iti ari ti Israel, “Pangaasim ta kiddawem ti panangidalan manipud iti sao ni Yahweh no ania ti rumbeng nga aramidem nga umuna.”
6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
Ket inummong ti ari ti Israel dagiti amin a profeta, nga uppat a gasut a lallaki, ket kinunana kadakuada, “Mapanak kadi makigubat idiay Ramot Galaad, wenno saan?” Kinunada, “Rautem, ta iyawatto ti Apo daytoy iti ari.”
7 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
Ngem kinuna ni Jehosafat, “Awan kadin ditoy ti sabali pay a profeta ni Yahweh a mabalintayo a pagkiddawan iti balakad?”
8 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
Kinuna ti ari ti Israel kenni Jehosafat, “Adda pay maysa a tao a mabalintayo a pagkiddawan iti balakad manipud kenni Yahweh a tumulong, ni Micaias nga anak ni Imla, ngem kagurak isuna ta saan a mangipadpadto iti aniaman a nasayaat a banag maipanggep kaniak, pasig a kinarigat laeng.” Ngem kinuna ni Jehosafat, “Saan koma nga ibaga ti ari dayta.”
9 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
Ket nangayab ti ari ti Israel iti opisial ket binilinna, “Iyegyo a dagus ni Micaias nga anak ni Imla.”
10 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
Ita, nakatugaw ni Ahab nga ari ti Israel ken ni Jehosafat nga ari ti Juda kadagiti tronoda, nakakawesda kadagiti kawes ti ari, iti nawaya a lugar iti pagserekan iti ruangan ti Samaria, ket nangipadto amin dagiti profeta, iti sangoananda.
11 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
Nangaramid ni Zedekia nga anak ni Kenaana kadagiti landok a sinan sara ket kinunana, “Kastoy ti imbaga ni Yahweh: 'Babaen kadagitoy ket sangdoenyonto dagiti taga-Aram agingga a maibusda.”
12 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
Kasta met laeng ti impadto dagiti amin a profeta, a kunada, “Darupenyo ti Ramot Galaad ket agballigikayo, ta iyawat ni Yahweh daytoy iti ari.”
13 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
Nagsao kenkuana ti mensahero a napan nangayab kenni Micaias, a kunana, “Ita dumngegka, pasig a nasayaat a banbanag dagiti sasao nga imbaga dagiti profeta ti ari. Pangngaasim ta kasta met koma ti sawem ket nasayaat a banbanag ti ibagam.”
14 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
Simmungbat ni Micaias, “Iti nagan ni Yahweh nga adda iti agnanayon, ti ibaga ni Yahweh kaniak ti sawek.”
15 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
Idi napan isuna iti ayan ti ari, kinuna ti ari kenkuana, “Micaias, mapankami kadi makigubat idiay Ramot Galaad, wenno saan?” Simmungbat ni Micaias, “Rautem ket parmekem. Iyawatto ni Yaweh daytoy iti ima ti ari.”
16 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
Ket kinuna ti ari kenkuana, “Namin-ano a daras nga imbagak kenka nga ikarim nga ibagam laeng kaniak ti kinapudno iti nagan ni Yahweh?”
17 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
Isu a kinuna ni Micaias, “Nakitak ti entero nga Israel a nawarawara kadagiti banbantay, kasla da la karnero nga awan iti mangipaspastor, ket kinuna ni Yahweh, 'Awan ti mangipaspastor kadagitoy. Agsubli koma ti tunggal tao iti balayna a sitatalged.”’
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
Isu a kinuna ti ari ti Israel kenni Jehosafat, “Saan kadi nga imbagak kenka a saan isuna nga agipadto iti nasayaat maipanggep kaniak, ngem didigra laeng?”
19 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
Ket kinuna ni Micaias, “Denggem ngarud ti sao ni Yahweh: Nakitak ni Yahweh a nakatugaw iti tronona, ken dagiti amin a buybuyot ti langit ket agtaktakder iti makannawan ken iti makannigidna.
20 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
Kinuna ni Yahweh, 'Siasino ti mangallilaw kenni Ahab, tapno mapan isuna ken maparmek idiay Ramot Galaad?' Ket nagduduma ti insungbat ti tunggal maysa.
21 Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
Ket adda maysa nga espiritu a nagpasango, nagtakder iti sangoanan ni Yahweh, ket kinunana, 'Siak ti mangallilaw kenkuana.' Kinuna ni Yahweh kenkuana, 'Kasano?'
22 “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
Simmungbat ti espiritu, 'Mapanak ken agbalinak nga agul-ulbod nga espiritu iti ngiwat dagiti amin a profetana.' Simmungbat ni Yahweh, 'Allilawem isuna, ket agballigikanto. Mapanka ket aramiden ti imbagam.'
23 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
Ita kitaem, nangikabil ni Yahweh iti agul-ulbod nga espiritu iti ngiwat dagiti amin a profetam, ket nangituyang ni Yahweh ti didigra para kenka.”
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
Kalpasanna immasideg ni Zedekaia nga anak ni Kenaana, tinungpana ni Micaias, ket kinunana, “Kasano a rimmuar kaniak ti Espiritu ni Yahweh tapno makitungtong kenka?”
25 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
Kinuna ni Micaias, “Kitaem, maammoamto dayta, iti dayta nga aldaw, inton agtarayka nga aglemmeng iti akin uneg a siled.
26 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
Kinuna ti ari ti Israel iti adipena, “Tiliwem ni Micaias ket iyapanmo kenni Amon, a gobernador ti siudad, kenni Joas, nga anakko.
27 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
Ibagam kenkuana, 'Kuna ti ari, Ibaludyo daytoy a tao ket bassit a tinapay ti ipakanyo ken ikkanyo ti laeng ti bassit a danum, agingga a makasangpetak a sitatalged.”’
28 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
Ket kinuna ni Micaias, “No makasublika a sitatalged, saan ngarud a nagsao ni Yahweh kaniak.” Ket kinunana pay, “Denggenyo daytoy, dakayo amin a tattao.”
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
Napan ngarud ni Ahab nga ari ti Israel, ken ni Jehosafat nga ari ti Juda idiay Ramot Galaad.
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
Kinuna ti ari ti Israel kenni Jehosafat, “Manglimlimoak ket mapanak iti paggugubatan, ngem ikawesmo dagiti pagan-anaymo a kas ari.” Isu a nanglimlimo ngarud ti ari ti Israel ket napan iti paggugubatan.
31 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
Ita, binilin ti ari ti Aram dagiti tallo pulo ket dua a kapitan ti karwahena, a kunana, “Saanyo a darupen uray siasinoman kadagiti soldado. Ketdi, darupenyo laeng ti ari ti Israel.”
32 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
Ket idi nakita dagiti kapitan dagiti karwahe ni Jehosafat kinunada, “Sigurado a dayta ti ari ti Israel.” Dinarupda isuna, ket nagriaw ni Jehosafat.
33 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
Ket idi nakita dagiti mangidadaulo kadagiti karwahe a saan nga isu ti ari ti Israel, saandan nga intuloy iti panangkamatda kenkuana.
34 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
Ngem adda maysa a lalaki a nangipasaksak lattan iti panana ket natamaan ti ari ti Israel iti nagsaipan ti kabalna. Ket kinuna ni Ahab iti mangiturturong iti karwahena, “Agsublita ken ipanawnak ditoy paggugubatan, ta nasugatanak iti nakaro.”
35 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
Kimarkaro ti gubat iti dayta nga aldaw, ket sisasadag ti ari iti karwahena a nakasango kadagiti taga-Aram. Natay isuna iti karabianna. Nagsayasay ti darana manipud iti sugatna iti datar iti karwahe.
36 Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
Ket idi lumlumneken ti init, impukkaw dagiti armada, a kunada, “Agsubli ti tunggal maysa iti siudadna, ken tunggal maysa iti rehionna!”
37 Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
Natay ngarud ni Ahab ket impanda idiay Samaria, ket impunponda isuna idiay Samaria.
38 Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
Binugwanda ti karwahe iti pagdigosan idiay Samaria, ket dinilpatan dagiti aso ti darana (ditoy ti pagdigdigusan dagiti balangkantis), kas iti sao nga imbaga ni Yahweh.
39 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Maipapan kadagiti dadduma a banbanag maipanggep kenni Ahab, amin nga inaramidna, ti impatakderna a marfil a balay, ken amin a siudad nga imbangonna saan kadi a naisurat dagitoy iti Libro dagiti Pakasaritaan dagiti Ar-ari ti Israel?
40 Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
Pimmusay ngarud ni Ahab, ket ni Ahazias nga anakna a lalaki ti nagbalin nga ari a simmukat kenkuana.
41 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
Ket nangrugi a nagturay idiay Juda ni Jehosafat nga anak ni Asa idi maikapat a tawen a panagturay ni Ahab nga ari ti Israel.
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Tallopulo ket lima ti tawen ni Jehosafat idi nagturay isuna, ket nagturay isuna iti duapulo ket lima a tawen idiay Jerusalem. Ti nagan ti inana ket Azuba, nga anak a babai ni Silhi.
43 Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Nagbiag isuna iti wagas ni Asa nga amana; saanna a tinallikudan dagitoy; inaramidna no ania ti nasayaat iti imatang ni Yahweh. Nupay kasta, saan pay a naikkat dagiti disso a pagdaydayawan. Agidatdaton ken agpupuor latta iti insenso dagiti tattao kadagiti disso a pagdaydayawan.
44 Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
Nakipagkapia ni Jehosafat iti ari ti Israel.
45 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Maipapan kadagiti dadduma a banbanag maipangep kenni Jehosafat, ken ti kinabileg nga impakitana ken no kasano a nangabak isuna iti gubat, saan kadi a naisurat dagitoy iti Libro dagiti Pakasaritaan dagiti Ar-ari ti Juda?
46 Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
Pinapanawna manipud iti daga dagiti nabatbati a balangkantis a natda kadagiti al-aldaw ti amana a ni Asa.
47 Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
Awan ti ari idiay Edom, ngem nagturay ti pannakabagi ti ari sadiay.
48 Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
Nangaramid ni Jehosafat kadagiti barko a paglayag a mapan idiay Ofir gapu iti balitok, ngem saanda a nakadanon gapu ta nadadael dagiti barko idiay Ezion Geber.
49 Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
Ket kinuna ni Ahazias nga anak ni Ahab kenni Jehosafat, “Ipalubosmo koma a makilayag dagiti adipenko kadagiti adipenmo kadagiti barko.” Ngem saan nga immannugot ni Jehosafat.
50 Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
Pimmusay ni Jehosafat ket naitabon a kaduada iti siudad ni David, a kapuonanna; ni Jehoram nga anakna ti nagbalin nga ari a simmukat kenkuana.
51 Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
Nagturay ni Ahazias nga anak ni Ahab iti Israel idiay Samaria idi maikasangapulo ket pito a tawen a panagturay ni Jehoshafat nga ari ti Juda, ket nagturay isuna iti dua a tawen iti Israel.
52 Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
Dakes ti inaramidna iti imatang ni Yahweh ken nagbiag iti wagas ti amana, ken iti wagas ti inana, ken iti wagas ni Jeroboam nga anak ni Nabat, ket iti kasta insungsongna ti Israel nga agbasol.
53 Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
Nagserbi isuna kenni Baal ken dinayawna isuna, isu a pinagpungtotna ni Yahweh, a Dios ti Israel, a kas iti inaramid ti amana.

< 1 Wafalme 22 >