< 1 Wafalme 22 >

1 Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
and to dwell three year nothing battle between Syria and between Israel
2 Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
and to be in/on/with year [the] third and to go down Jehoshaphat king Judah to(wards) king Israel
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
and to say king Israel to(wards) servant/slave his to know for to/for us Ramoth (Ramoth)-gilead and we be silent from to take: take [obj] her from hand: power king Syria
4 Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
and to say to(wards) Jehoshaphat to go: went with me to/for battle Ramoth Gilead and to say Jehoshaphat to(wards) king Israel like me like you like/as people my like/as people your like/as horse my like/as horse your
5 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
and to say Jehoshaphat to(wards) king Israel to seek please like/as day: today [obj] word LORD
6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
and to gather king Israel [obj] [the] prophet like/as four hundred man and to say to(wards) them to go: went upon Ramoth (Ramoth)-gilead to/for battle if to cease and to say to ascend: rise and to give: give Lord in/on/with hand: power [the] king
7 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
and to say Jehoshaphat nothing here prophet to/for LORD still and to seek from [obj] him
8 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
and to say king Israel to(wards) Jehoshaphat still man one to/for to seek [obj] LORD from [obj] him and I to hate him for not to prophesy upon me pleasant that if: except if: except bad: evil Micaiah son: child Imlah and to say Jehoshaphat not to say [the] king so
9 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
and to call: call to king Israel to(wards) eunuch one and to say to hasten [emph?] Micaiah son: child Imlah
10 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
and king Israel and Jehoshaphat king Judah to dwell man: anyone upon throne his to clothe garment in/on/with threshing floor entrance gate Samaria and all [the] prophet to prophesy to/for face: before their
11 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
and to make to/for him Zedekiah son: child Chenaanah horn iron and to say thus to say LORD in/on/with these to gore [obj] Syria till to end: destroy them
12 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
and all [the] prophet to prophesy so to/for to say to ascend: rise Ramoth (Ramoth)-gilead and to prosper and to give: give LORD in/on/with hand: power [the] king
13 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
and [the] messenger which to go: went to/for to call: call to Micaiah to speak: speak to(wards) him to/for to say behold please word [the] prophet lip: according one pleasant to(wards) [the] king to be please (word your *Q(K)*) like/as word one from them and to speak: speak pleasant
14 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
and to say Micaiah alive LORD for [obj] which to say LORD to(wards) me [obj] him to speak: speak
15 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
and to come (in): come to(wards) [the] king and to say [the] king to(wards) him Micaiah to go: went to(wards) Ramoth (Ramoth)-gilead to/for battle if to cease and to say to(wards) him to ascend: rise and to prosper and to give: give LORD in/on/with hand: power [the] king
16 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
and to say to(wards) him [the] king till like/as what? beat I to swear you which not to speak: speak to(wards) me except truth: true in/on/with name LORD
17 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
and to say to see: see [obj] all Israel to scatter to(wards) [the] mountain: mount like/as flock which nothing to/for them to pasture and to say LORD not lord to/for these to return: return man: anyone to/for house: home his in/on/with peace
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
and to say king Israel to(wards) Jehoshaphat not to say to(wards) you not to prophesy upon me pleasant that if: except if: except bad: evil
19 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
and to say to/for so to hear: hear word LORD to see: see [obj] LORD to dwell upon throne his and all army [the] heaven to stand: stand upon him from right his and from left his
20 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
and to say LORD who? to entice [obj] Ahab and to ascend: rise and to fall: kill in/on/with Ramoth Gilead and to say this in/on/with thus and this to say in/on/with thus
21 Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
and to come out: come [the] spirit and to stand: stand to/for face: before LORD and to say I to entice him
22 “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
and to say LORD to(wards) him in/on/with what? and to say to come out: come and to be spirit deception in/on/with lip all prophet his and to say to entice and also be able to come out: come and to make: do so
23 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
and now behold to give: put LORD spirit deception in/on/with lip all prophet your these and LORD to speak: promise upon you distress: harm
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
and to approach: approach Zedekiah son: child Chenaanah and to smite [obj] Micaiah upon [the] jaw and to say where? this to pass spirit LORD from with me to/for to speak: speak with you
25 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
and to say Micaiah look! you to see: see in/on/with day [the] he/she/it which to come (in): come chamber in/on/with chamber to/for to hide
26 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
and to say king Israel to take: take [obj] Micaiah and to return: return him to(wards) Amon ruler [the] city and to(wards) Joash son: child [the] king
27 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
and to say thus to say [the] king to set: put [obj] this house: home [the] prison and to eat him food: bread oppression and water oppression till to come (in): come I in/on/with peace
28 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
and to say Micaiah if to return: return to return: return in/on/with peace not to speak: speak LORD in/on/with me and to say to hear: hear people all their
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
and to ascend: rise king Israel and Jehoshaphat king Judah Ramoth (Ramoth)-gilead
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
and to say king Israel to(wards) Jehoshaphat to search and to come (in): come in/on/with battle and you(m. s.) to clothe garment your and to search king Israel and to come (in): come in/on/with battle
31 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
and king Syria to command [obj] ruler [the] chariot which to/for him thirty and two to/for to say not to fight with small and with great: large that if: except if: except with king Israel to/for alone him
32 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
and to be like/as to see: see ruler [the] chariot [obj] Jehoshaphat and they(masc.) to say surely king Israel he/she/it and to turn aside: turn aside upon him to/for to fight and to cry out Jehoshaphat
33 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
and to be like/as to see: see ruler [the] chariot for not king Israel he/she/it and to return: return from after him
34 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
and man: anyone to draw in/on/with bow to/for integrity his and to smite [obj] king Israel between [the] joint and between [the] armor and to say to/for charioteer his to overturn hand: themselves your and to come out: send me from [the] camp for be weak: ill
35 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
and to ascend: rise [the] battle in/on/with day [the] he/she/it and [the] king to be to stand: stand in/on/with chariot before Syria and to die in/on/with evening and to pour: pour blood [the] wound to(wards) bosom: lap [the] chariot
36 Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
and to pass [the] cry in/on/with camp like/as to come (in): (sun)set [the] sun to/for to say man: anyone to(wards) city his and man: anyone to(wards) land: country/planet his
37 Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
and to die [the] king and to come (in): come Samaria and to bury [obj] [the] king in/on/with Samaria
38 Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
and to overflow [obj] [the] chariot upon pool Samaria and to lick [the] dog [obj] blood his and [the] to fornicate to wash: wash like/as word LORD which to speak: speak
39 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
and remainder word: deed Ahab and all which to make: do and house: home [the] tooth: ivory which to build and all [the] city which to build not they(masc.) to write upon scroll: book Chronicles [the] day to/for king Israel
40 Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
and to lie down: be dead Ahab with father his and to reign Ahaziah son: child his underneath: instead him
41 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
and Jehoshaphat son: child Asa to reign upon Judah in/on/with year four to/for Ahab king Israel
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Jehoshaphat son: aged thirty and five year in/on/with to reign he and twenty and five year to reign in/on/with Jerusalem and name mother his Azubah daughter Shilhi
43 Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
and to go: walk in/on/with all way: conduct Asa father his not to turn aside: turn aside from him to/for to make: do [the] upright in/on/with eye: seeing LORD surely [the] high place not to turn aside: remove still [the] people to sacrifice and to offer: offer in/on/with high place
44 Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
and to ally Jehoshaphat with king Israel
45 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
and remainder word: deed Jehoshaphat and might his which to make: do and which to fight not they(masc.) to write upon scroll: book word: deed [the] day to/for king Judah
46 Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
and remainder [the] male cult prostitute which to remain in/on/with day Asa father his to burn: burn from [the] land: country/planet
47 Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
and king nothing in/on/with Edom to stand king
48 Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
Jehoshaphat (to make: do *Q(K)*) fleet Tarshish to/for to go: went Ophir [to] to/for gold and not to go: went for (to break *Q(K)*) fleet in/on/with Ezion-geber Ezion-geber
49 Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
then to say Ahaziah son: child Ahab to(wards) Jehoshaphat to go: went servant/slave my with servant/slave your in/on/with fleet and not be willing Jehoshaphat
50 Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
and to lie down: be dead Jehoshaphat with father his and to bury with father his in/on/with city David father his and to reign Jehoram son: child his underneath: instead him
51 Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
Ahaziah son: child Ahab to reign upon Israel in/on/with Samaria in/on/with year seven ten to/for Jehoshaphat king Judah and to reign upon Israel year
52 Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
and to make: do [the] bad: evil in/on/with eye: seeing LORD and to go: walk in/on/with way: conduct father his and in/on/with way: conduct mother his and in/on/with way: conduct Jeroboam son: child Nebat which to sin [obj] Israel
53 Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
and to serve: minister [obj] [the] Baal and to bow to/for him and to provoke [obj] LORD God Israel like/as all which to make: do father his

< 1 Wafalme 22 >