< 1 Wafalme 22 >
1 Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
And they remained three years there not [was] war between Aram and between Israel.
2 Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
And it was in the year third and he went down Jehoshaphat [the] king of Judah to [the] king of Israel.
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
And he said [the] king of Israel to servants his ¿ do you know that [belongs] to us Ramoth Gilead and we [are] inactive from taking it from [the] hand of [the] king of Aram.
4 Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
And he said to Jehoshaphat ¿ will you go with me for battle Ramoth Gilead and he said Jehoshaphat to [the] king of Israel as me as you as people my as people your as horses my as horses your.
5 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
And he said Jehoshaphat to [the] king of Israel seek please as the day [the] word of Yahweh.
6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
And he gathered [the] king of Israel the prophets about four hundred man and he said to them ¿ will I go on Ramoth Gilead for battle or? will I refrain and they said go up so he may give [it] [the] Lord in [the] hand of the king.
7 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
And he said Jehoshaphat ¿ [is] there not here a prophet of Yahweh still so we may enquire from him.
8 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
And he said [the] king of Israel - to Jehoshaphat still a man one to consult Yahweh from him and I I hate him for not he prophesies on me good that except evil Micaiah [the] son of Imlah and he said Jehoshaphat may not he speak the king thus.
9 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
And he summoned [the] king of Israel a court-official one and he said bring quickly! Micaiah [the] son of Imlah.
10 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
And [the] king of Israel and Jehoshaphat [the] king of Judah [were] sitting each on throne his clothed garments at [the] threshing floor [the] entrance of [the] gate of Samaria and all the prophets [were] prophesying before them.
11 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
And he made for himself Zedekiah [the] son of Kenaanah horns of iron and he said thus he says Yahweh with these you will gore Aram until destroy them.
12 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
And all the prophets [were] prophesying thus saying go up Ramoth Gilead and succeed and he will give [it] Yahweh in [the] hand of the king.
13 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
And the messenger who he had gone - to summon Micaiah he spoke to him saying here! please [the] words of the prophets a mouth one [is] good to the king let it be please (word your *Q(K)*) like [the] word of one from them and you will speak good.
14 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
And he said Micaiah [by] [the] life of Yahweh for [that] which he will say Yahweh to me it I will speak.
15 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
And he came to the king and he said the king to him O Micaiah ¿ will we go against Ramoth Gilead for battle or? will we refrain and he said to him go up and succeed and he will give [it] Yahweh in [the] hand of the king.
16 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
And he said to him the king until how many? times [will] I make swear you that not you must speak to me only truth in [the] name of Yahweh.
17 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
And he said I saw all Israel scattered to the mountains like flock which not [belongs] to them a shepherd and he said Yahweh not masters [belong] to these let them return each to house his in peace.
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
And he said [the] king of Israel to Jehoshaphat ¿ not did I say to you not he prophesies on me good that except evil.
19 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
And he said therefore hear [the] word of Yahweh I saw Yahweh sitting on throne his and all [the] host of the heavens [was] standing at him from right his and from left his.
20 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
And he said Yahweh who? will he deceive Ahab so he may go up and he may fall at Ramoth Gilead and it said this [one] by thus and this [one] [was] saying by thus.
21 Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
And it came forth the spirit and it stood before Yahweh and it said I I will deceive him
22 “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
and he said Yahweh to it how? And it said I will go out and I will be a spirit of falsehood in [the] mouth of all prophets his and he said you will deceive and also you will prevail go out and do thus.
23 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
And therefore here! he has put Yahweh a spirit of falsehood in [the] mouth of all prophets your these and Yahweh he has spoken on you evil.
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
And he drew near Zedekiah [the] son of Kenaanah and he struck Micaiah on the cheek and he said where? this did it pass on [the] spirit of Yahweh from with me to speak with you.
25 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
And he said Micaiah there you [are] about to see on the day that when you will go a room in a room to hide yourself.
26 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
And he said [the] king of Israel take Micaiah and take back him to Amon [the] official of the city and to Joash [the] son of the king.
27 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
And you will say thus he says the king put this [one] [the] house of imprisonment and feed him bread oppression and water oppression until come I in peace.
28 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
And he said Micaiah certainly [if] you will return in peace not he has spoken Yahweh by me and he said listen O peoples all of them.
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
And he went up [the] king of Israel and Jehoshaphat [the] king of Judah Ramoth Gilead.
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
And he said [the] king of Israel to Jehoshaphat I will disguise myself and I will go in the battle and you wear own clothes your and he disguised himself [the] king of Israel and he went in the battle.
31 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
And king of Aram he had commanded [the] commanders of the chariotry which [belonged] to him thirty and two saying not you must do battle with [the] small and with [the] great that except with [the] king of Israel to only him.
32 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
And it was when saw [the] commanders of the chariotry Jehoshaphat and they they said surely [is] [the] king of Israel he and they turned aside on him to do battle and he cried out Jehoshaphat.
33 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
And it was when saw [the] commanders of the chariotry that not [was] [the] king of Israel he and they turned back from after him.
34 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
And someone he drew on the bow to innocence his and he struck [the] king of Israel between the joints and between the body armor and he said to charioteer his turn around hand your and take out me from the camp for I have been wounded.
35 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
And it went up the battle on the day that and the king he was placed in the chariot opposite to Aram and he died in the evening and it flowed [the] blood of the wound into [the] bottom of the chariot.
36 Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
And it passed the cry in the camp when went the sun saying everyone to city his and everyone to land his.
37 Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
And he died the king and he came Samaria and people buried the king in Samaria.
38 Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
And someone washed off the chariot at - [the] pool of Samaria and they licked up the dogs blood his and the prostitutes they bathed according to [the] word of Yahweh which he had spoken.
39 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
And [the] rest of [the] matters of Ahab and all that he did and [the] house of ivory which he built and all the cities which he built ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Israel.
40 Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
And he lay down Ahab with ancestors his and he became king Ahaziah son his in place of him.
41 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
And Jehoshaphat [the] son of Asa he became king over Judah in year four of Ahab [the] king of Israel.
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Jehoshaphat [was] a son of thirty and five year[s] when became king he and twenty and five year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Azubah [the] daughter of Shilhi.
43 Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
And he walked in all [the] way of Asa father his not he turned aside from it to do the right in [the] eyes of Yahweh. Only the high places not they were removed still the people [were] sacrificing and making smoke at the high places.
44 Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
And he made peace Jehoshaphat with [the] king of Israel.
45 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Jehoshaphat and might his which he did and which he waged war ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
46 Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
And [the] rest of the cult prostitute[s] which it remained in [the] days of Asa father his he destroyed from the land.
47 Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
And [was] a king there not in Edom a deputy [was] king.
48 Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
Jehoshaphat (he made *Q(K)*) ships of Tarshish to go Ophir towards for gold and not it went for (they were broken *Q(K)*) [the] ships at Ezion Geber.
49 Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
Then he said Ahaziah [the] son of Ahab to Jehoshaphat let them go servants my with servants your in [the] ships and not he was willing Jehoshaphat.
50 Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
And he lay down Jehoshaphat with ancestors his and he was buried with ancestors his in [the] city of David ancestor his and he became king Jehoram son his in place of him.
51 Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
Ahaziah [the] son of Ahab he became king over Israel in Samaria in year seven-teen of Jehoshaphat [the] king of Judah and he reigned over Israel two years.
52 Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
And he did the evil in [the] eyes of Yahweh and he walked in [the] way of father his and in [the] way of mother his and in [the] way of Jeroboam [the] son of Nebat who he caused to sin Israel.
53 Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
And he served Baal and he bowed down to it and he provoked to anger Yahweh [the] God of Israel according to all that he had done father his.