< 1 Wafalme 22 >

1 Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
And they continued three yeere without warre betweene Aram and Israel.
2 Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
And in the third yeere did Iehoshaphat the King of Iudah come downe to ye King of Israel.
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
(Then the King of Israel saide vnto his seruants, Knowe yee not that Ramoth Gilead was ours? and wee stay, and take it not out of ye hand of the King of Aram?)
4 Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
And he sayde vnto Iehoshaphat, Wilt thou goe with mee to battel against Ramoth Gilead? And Iehoshaphat saide vnto the King of Israel, I am as thou art, my people as thy people, and mine horses as thine horses.
5 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
Then Iehoshaphat saide vnto the King of Israel, Aske counsaile, I pray thee, of the Lord to day.
6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
Then the King of Israel gathered the prophets vpon a foure hundreth men, and said vnto them, Shal I go against Ramoth Gilead to battel, or shall I let it alone? And they said, Go vp: for ye Lord shall deliuer it into the hands of the King.
7 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
And Iehoshaphat said, Is there here neuer a Prophet of the Lord more, that we might inquire of him?
8 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
And the King of Israel said vnto Iehoshaphat, There is yet one man (Michaiah the sonne of Imlah) by whom we may aske counsel of the Lord, but I hate him: for he doeth not prophecie good vnto me, but euill. And Iehoshaphat sayd, Let not the King say so.
9 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
Then the King of Israel called an Eunuche, and sayde, Call quickely Michaiah the sonne of Imlah.
10 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
And the King of Israel and Iehoshaphat the King of Iudah sate either of them on his throne in their apparell in the voyde place at the entring in of the gate of Samaria, and all the prophets prophecied before them.
11 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
And Zidkiiah the sonne of Chenaanah made him hornes of yron, and sayd, Thus sayth the Lord, With these shalt thou push the Aramites, vntill thou hast consumed them.
12 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
And all the prophets prophecied so, saying, Goe vp to Ramoth Gilead, and prosper: for the Lord shall deliuer it into the Kings hand.
13 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
And the messenger that was gone to call Michaiah spake vnto him, saying, Beholde now, the wordes of the prophets declare good vnto the King with one accorde: let thy word therefore, I pray thee, be like the worde of one of them, and speake thou good.
14 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
And Michaiah saide, As the Lord liueth, whatsoeuer the Lord sayth vnto me, that will I speake.
15 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
So he came to the King, and the King said vnto him, Michaiah, shall we go against Ramoth Gilead to battel, or shall we leaue off? And he answered him, Goe vp, and prosper: and the Lord shall deliuer it into the hand of the King.
16 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
And the King said vnto him, How oft shall I charge thee, that thou tell me nothing but that which is true in the Name of the Lord?
17 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
Then he said, I sawe all Israel scattered vpon the mountaines, as sheepe that had no shepheard. And the Lord sayde, These haue no master, let euery man returne vnto his house in peace.
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
(And the King of Israel saide vnto Iehoshaphat, Did I not tell thee, that he would prophecie no good vnto me, but euill?)
19 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
Againe he said, Heare thou therefore the worde of the Lord. I sawe the Lord sit on his throne, and all the hoste of heauen stood about him on his right hand and on his left hand.
20 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
And the Lord sayd, Who shall entise Ahab that he may go and fall at Ramoth Gilead? And one said on this maner, and another sayd on that maner.
21 Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
Then there came forth a spirit, and stoode before the Lord, and sayd, I wil entise him. And the Lord sayd vnto him, Wherewith?
22 “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
And he sayd, I will goe out, and be a false spirit in the mouth of all his prophets. Then he sayd, Thou shalt entise him, and shalt also preuayle: goe forth, and doe so.
23 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
Now therefore behold, the Lord hath put a lying spirite in the mouth of all these thy prophets, and the Lord hath appoynted euill against thee.
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
Then Zidkiiah the sonne of Chenaanah came neere, and smote Michaiah on the cheeke and sayd, When went the Spirite of the Lord from me, to speake vnto thee?
25 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
And Michaiah saide, Behold, thou shalt see in that day, when thou shalt goe from chamber to chamber to hide thee.
26 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
And the King of Israel sayd, Take Michaiah, and cary him vnto Amon the gouernour of the citie, and vnto Ioash the Kings sonne,
27 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
And say, Thus saith the King, Put this man in the prison house, and feede him with bread of affliction, and with water of affliction, vntill I returne in peace.
28 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
And Michaiah sayde, If thou returne in peace, the Lord hath not spoken by me. And he sayd, Hearken all ye people.
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
So the King of Israel and Iehoshaphat the King of Iudah went vp to Ramoth Gilead.
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
And the King of Israel sayde to Iehoshaphat, I will change mine apparell, and will enter into the battell, but put thou on thine apparell. And the King of Israel changed himselfe, and went into the battel.
31 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
And the King of Aram commanded his two and thirtie captaines ouer his charets, saying, Fight neither with small, nor great, saue onely against the King of Israel.
32 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
And when the captaines of the charets saw Iehoshaphat, they sayd, Surely it is the King of Israel, and they turned to fight against him: and Iehoshaphat cryed.
33 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
And when the captaines of the charets saw that he was not the King of Israel, they turned backe from him.
34 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
Then a certaine man drewe a bow mightily and smote the King of Israel betweene the ioyntes of his brigandine. Wherefore he sayde vnto his charet man, Turne thine hand and cary me out of the hoste: for I am hurt.
35 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
And the battel encreased that day, and the King stoode still in his charet against the Aramites, and dyed at euen: and the blood ran out of the wound into the middes of the charet.
36 Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
And there went a proclamation thorowout the hoste about the going downe of the sunne, saying, Euery man to his citie, and euery man to his owne countrey.
37 Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
So the King died, and was brought to Samaria, and they buried the King in Samaria.
38 Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
And one washed the charet in the poole of Samaria, and the dogs licked vp his blood (and they washed his armour) according vnto the word of the Lord which he spake.
39 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Concerning the rest of the actes of Ahab and all that he did, and the yuorie house which he built, and all the cities that he built, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Israel?
40 Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
So Ahab slept with his fathers, and Ahaziah his sonne reigned in his stead.
41 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
And Iehoshaphat the sonne of Asa began to reigne vpon Iudah in the fourth yeere of Ahab King of Israel.
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Iehoshaphat was fiue and thirty yere olde, when he began to reigne, and reigned fiue and twentie yeere in Ierusalem. And his mothers name was Azubah the daughter of Shilhi.
43 Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
And he walked in all the wayes of Asa his father, and declined not therefrom, but did that which was right in the eyes of the Lord. Neuerthelesse the hie places were not taken away: for the people offred still and burnt incense in the hie places.
44 Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
And Iehoshaphat made peace with the King of Israel.
45 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Concerning the rest of the actes of Iehoshaphat, and his worthy deedes that he did, and his battels which he fought, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Iudah?
46 Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
And the Sodomites, which remayned in the dayes of his father Asa, he put cleane out of the land.
47 Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
There was then no King in Edom: the deputie was King.
48 Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
Iehoshaphat made shippes of Tharshish to sayle to Ophir for golde, but they went not, for the shippes were broken at Ezion Gaber.
49 Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
Then sayde Ahaziah the sonne of Ahab vnto Iehoshaphat, Let my seruants goe with thy seruants in the ships, But Iehoshaphat would not.
50 Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
And Iehoshaphat did sleepe with his fathers, and was buried with his fathers in the citie of Dauid his father, and Iehoram his sonne reigned in his stead.
51 Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
Ahaziah the sonne of Ahab began to reigne ouer Israel in Samaria, the seuenteenth yeere of Iehoshaphat King of Iudah, and reigned two yeeres ouer Israel.
52 Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
But he did euill in the sight of the Lord, and walked in the way of his father, and in the way of his mother, and in the way of Ieroboam the sonne of Nebat, which made Israel to sinne.
53 Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
For he serued Baal and worshipped him, and prouoked the Lord God of Israel vnto wrath, according vnto all that his father had done.

< 1 Wafalme 22 >