< 1 Wafalme 22 >

1 Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
Nebylo pak za tři léta války mezi Syrskými a Izraelskými.
2 Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
I stalo se léta třetího, přijel Jozafat král Judský k králi Izraelskému.
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
Mluvil pak byl král Izraelský služebníkům svým: Víte-li, že naše bylo Rámot Galád, a my zanedbáváme vzíti ho zase z moci krále Syrského?
4 Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
Pročež řekl Jozafatovi: Potáhneš-li se mnou na vojnu proti Rámot Galád? Odpověděl Jozafat králi Izraelskému: Jako jsem já, tak jsi ty, jako lid můj, tak lid tvůj, jako koni moji, tak koni tvoji.
5 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
Řekl také Jozafat králi Izraelskému: Vzeptej se dnes medle na slovo Hospodinovo.
6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
I shromáždil král Izraelský proroků okolo čtyř set mužů a řekl jim: Mám-li táhnouti na vojnu proti Rámot Galád, či tak nechati? I řekli: Táhni, nebo dá je Pán v ruku krále.
7 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
Tedy řekl Jozafat: Což není zde již žádného proroka Hospodinova, abychom se ho zeptali?
8 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
Na to řekl král Izraelský Jozafatovi: Ještěť jest muž jeden, skrze něhož bychom se mohli poraditi s Hospodinem, ale já ho nenávidím, proto že mi dobrého neprorokuje, než zlé, Micheáš syn Jemlův. Ale Jozafat řekl: Nechť tak nemluví král.
9 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
Protož povolav král Izraelský komorníka jednoho, řekl: Přiveď sem rychle Micheáše syna Jemlova.
10 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
(Mezi tím král Izraelský a Jozafat král Judský, jeden každý na stolici své, odění jsouce rouchem, seděli v placu u vrat brány Samařské, a všickni proroci prorokovali před nimi.
11 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
Sedechiáš pak syn Kenanův udělal sobě byl rohy železné a řekl: Takto praví Hospodin: Těmito trkati budeš Syrské, dokudž nepohubíš jich.
12 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
Takž podobně i jiní všickni proroci prorokovali, řkouce: Jeď do Rámot Galád, a šťastněť se povede; nebo dá je Hospodin v ruku královu.)
13 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
V tom posel ten, kterýž šel, aby zavolal Micheáše, mluvil jemu, řka: Aj, nyní slova proroků jedněmi ústy předpovídají dobré věci králi. Medle, buď řeč tvá jako řeč kterého z nich, a mluv dobré věci.
14 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
Tedy řekl Micheáš: Živť jest Hospodin, že což mi koli řekne Hospodin, to mluviti budu.
15 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
A když přišel k králi, řekl jemu král: Micheáši, máme-li jeti na vojnu proti Rámot Galád, či tak nechati? Kterýž řekl jemu: Jeď a šťastněť se povede, nebo dá je Hospodin v ruku krále.
16 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
I řekl jemu král: I kolikrátž tě mám přísahou zavazovati, abys mi nemluvil než pravdu ve jménu Hospodinovu?
17 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
Protož řekl: Viděl jsem všecken lid Izraelský rozptýlený po horách jako ovce, kteréž nemají pastýře; nebo řekl Hospodin: Nemají pána tito, navrať se jeden každý do domu svého v pokoji.
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
I řekl král Izraelský Jozafatovi: Zdaližť jsem neřekl, že mi nebude prorokovati dobrého, ale zlé?
19 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
Řekl dále: Z té příčiny slyš slovo Hospodinovo: Viděl jsem Hospodina sedícího na stolici své, a všecko vojsko nebeské stojící po pravici jeho i po levici jeho.
20 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
I řekl Hospodin: Kdo oklamá Achaba, aby vytáhl a padl u Rámot Galád? A když pravil ten toto, a jiný pravil jiné,
21 Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
Tožť vyšel jakýsi duch, a postaviv se před Hospodinem, řekl: Já ho oklamám. Hospodin pak řekl jemu: Jakým způsobem?
22 “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
Odpověděl: Vyjdu a budu duchem lživým v ústech všech proroků jeho. Kterýžto řekl: Oklamáš a dovedeš toho; vyjdiž a učiň tak.
23 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
Protož, aj, jižtě dal Hospodin ducha lživého v ústa všech proroků tvých těchto, ješto však Hospodin mluvil zlé proti tobě.
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
Tedy přistoupiv Sedechiáš syn Kenanův, dal Micheášovi poliček a řekl: Kudyže odšel duch Hospodinův ode mne, aby mluvil tobě?
25 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
Odpověděl Micheáš: Aj, uzříš v ten den, když vejdeš do nejtajnějšího pokoje, abys se skryl.
26 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
I řekl král Izraelský: Jmi Micheáše, a doveď ho k Amonovi knížeti města, a k Joasovi synu královu.
27 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
A řekneš: Takto praví král: Dejte tohoto do žaláře, a dávejte mu jísti maličko chleba a maličko vody, dokudž se nenavrátím v pokoji.
28 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
Ale Micheáš řekl: Jestliže ty se navrátíš v pokoji, tedyť nemluvil skrze mne Hospodin. Přes to řekl: Slyštež to všickni lidé!
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
A tak táhl král Izraelský, a Jozafat král Judský proti Rámot Galád.
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
I řekl král Izraelský Jozafatovi: Změním já se, když půjdu k bitvě, ale ty oblec se v roucho své. I změnil se král Izraelský a jel k bitvě.
31 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
Král pak Syrský přikázal třidcíti dvěma svým hejtmanům nad vozy, a řekl: Nebojujte proti malému ani proti velikému, než proti samému králi Izraelskému.
32 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
I stalo se, když uzřeli hejtmané nad vozy Jozafata, řekli: Jistě král Izraelský jest. I obrátili se proti němu, aby bojovali. Tedy zkřikl Jozafat.
33 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
V tom když uzřeli hejtmané nad vozy, že on není král Izraelský, obrátili se od něho.
34 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
Muž pak jeden střelil z lučiště náhodou, a postřelil krále Izraelského, kdež se pancíř spojuje. Pročež řekl vozkovi svému: Obrať se a vyvez mne z vojska, nebo jsem nemocen.
35 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
I rozmohla se bitva v ten den. Král pak stál na voze proti Syrským; potom umřel u večer, a tekla krev z rány do vozu.
36 Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
I volal biřic po vojště, když již slunce zapadlo, řka: Jeden každý do města svého, a jeden každý do země své navrať se.
37 Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
Umřel tedy král a dovezen jest do Samaří, i pochovali ho v Samaří.
38 Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
A když pohřížen byl vůz v rybníku Samařském, střebali psi krev jeho, též když umývali zbroj jeho, vedlé řeči Hospodinovy, kterouž byl mluvil.
39 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Jiné pak věci Achabovy, a cožkoli činil, i jaký dům z kostí slonových vystavěl, i všecka města, kteráž vzdělal, o tom zapsáno jest v knize o králích Izraelských.
40 Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
A tak usnul Achab s otci svými, a kraloval Ochoziáš syn jeho místo něho.
41 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
Jozafat pak syn Azy počal kralovati nad Judou léta čtvrtého Achaba, krále Izraelského.
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
A byl Jozafat ve třidcíti pěti letech, když počal kralovati, a dvadceti pět let kraloval nad Jeruzalémem, jehož matky jméno bylo Azuba, dcera Silchi.
43 Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
I chodil po vší cestě Azy otce svého, aniž se od ní uchýlil, čině, což dobrého bylo před oblíčejem Hospodinovým. Toliko poněvadž výsostí nezkazili, ještě lid obětoval a kadil na těch výsostech.
44 Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
Všel také v pokoj král Jozafat s králem Izraelským.
45 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Jiné pak věci Jozafatovy, i síla jeho, kterouž prokazoval a kterouž bojoval, zapsány jsou v knize o králích Judských.
46 Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
Ten ostatky ohyzdných sodomářů, kteříž ještě pozůstali za dnů Azy otce jeho, vyplénil z země.
47 Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
Tehdáž nebylo žádného krále v zemi Idumejské, hejtmana měli místo krále.
48 Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
I nadělal Jozafat lodí mořských, aby jeli do Ofir pro zlato. Ale nejeli, nebo polámaly se lodí v Aziongaber.
49 Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
Řekl byl také Ochoziáš syn Achabův Jozafatovi: Nechť jedou služebníci moji s služebníky tvými na lodech. Ale Jozafat nechtěl.
50 Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
I usnul Jozafat s otci svými, a pochován jest s otci svými v městě Davida otce svého; kraloval pak Joram syn jeho místo něho.
51 Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
Ochoziáš syn Achabův počal kralovati nad Izraelem v Samaří, léta sedmnáctého Jozafata krále Judského, a kraloval nad Izraelem dvě létě.
52 Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
Nebo činil zlé věci před oblíčejem Hospodinovým, a chodil po cestě otce svého a po cestě matky své, i po cestě Jeroboáma syna Nebatova, kterýž přivodil k hřešení lid Izraelský.
53 Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
Sloužil také Bálovi a klaněl se jemu, čímž popudil k hněvu Hospodina Boha Izraelského vedlé toho všeho, což činil otec jeho.

< 1 Wafalme 22 >