< 1 Wafalme 21 >

1 Baada ya hayo, Nabothi, Myezreeli, alikuwa na shamba la mizabibu jirani na jumba la kifalme la Ahabu mfalme wa Samaria.
Or après ces événements, en ce même temps, Naboth, le Jezrahélite, avait une vigne qui était dans Jezrahel, près du palais d’Achab, roi de Samarie.
2 Ahabu akamwambia Nabothi, “Nipe shamba lako la mizabibu nilitumie kwa bustani ya mboga, kwa kuwa liko karibu na jumba langu la kifalme. Badala yake, nitakupa shamba jingine la mizabibu zuri zaidi au, kama utapenda, nitakulipa kiasi chochote unachoona ni thamani yake.”
Achab parla à Naboth, disant: Donne-moi ta vigne, afin que je me fasse un jardin potager, parce qu’elle est voisine, et je te donnerai en sa place une vigne meilleure, ou, si ta juges plus commode pour toi, le prix en argent, selon ce qu’elle vaut.
3 Lakini Nabothi akamjibu, “Bwana na apishe mbali kukupa wewe urithi wa baba zangu.”
Naboth lui répondit: Que le Seigneur me soit propice, pour que je ne vous donne point l’héritage de mes pères!
4 Basi Ahabu akaenda nyumbani, mwenye huzuni na hasira kwa sababu ya yale ambayo Nabothi, Myezreeli, alikuwa amesema, “Sitakupa urithi wa baba zangu.” Akajinyoosha juu ya kitanda akisononeka, na akakataa kula.
Achab vint donc en sa maison, indigné et frémissant, à cause de la parole que lui avait répondue Naboth, le Jezrahélite, disant: Je ne vous donnerai point l’héritage de mes pères. Et, se jetant sur son lit, il tourna sa face vers la muraille, et ne mangea point du pain.
5 Yezebeli mke wake akaingia na akamuuliza, “Kwa nini unahuzunika hivi? Kwa nini huli chakula?”
Mais Jézabel, sa femme, entra auprès de lui, et lui dit: Qu’est-ce que cela? Pourquoi votre âme est-elle contristée? et pourquoi ne mangez-vous point du pain?
6 Akamjibu, “Kwa sababu nilimwambia Nabothi, Myezreeli, ‘Niuzie shamba lako la mizabibu, au kama ukipenda, nitakupa shamba jingine la mizabibu badala yake.’ Lakini akasema, ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’”
Il lui répondit: J’ai parlé à Naboth, le Jezrahélite, et je lui ai dit: Donne-moi ta vigne, en acceptant de l’argent, ou si cela te plaît, je te donnerai une vigne meilleure en sa place. Et lui m’a répondu: Je ne vous donnerai point ma vigne.
7 Yezebeli mke wake akasema, “Hivi ndivyo unavyofanya, nawe ni mfalme katika Israeli yote? Inuka na ule! Changamka. Nitakupatia shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli.”
Jézabel, sa femme, lui dit donc: Vous avez une grande autorité et vous gouvernez bien le royaume d’Israël. Levez-vous et mangez du pain, et ayez l’esprit calme; c’est moi qui vous donnerai la vigne de Naboth, le Jezrahélite.
8 Kwa hiyo akaandika barua kwa jina la Ahabu akaweka muhuri wake juu ya hizo barua, akazipeleka kwa wazee na kwa watu wenye cheo walioishi katika mji pamoja na Nabothi.
C’est pourquoi elle écrivit des lettres au nom d’Achab, et les scella de l’anneau du roi, et elle les envoya aux anciens et aux grands qui étaient dans la ville de Naboth, et habitaient avec lui.
9 Katika barua hizo aliandika: “Tangazeni siku ya watu kufunga na mkamketishe Nabothi mahali pa wazi miongoni mwa watu.
Or le sens de ces lettres était celui-ci: Publiez un jeûne, et faites asseoir Naboth entre les premiers du peuple,
10 Lakini waketisheni watu wawili wabaya kabisa mkabala naye, nao washuhudie kuwa yeye amemlaani Mungu na mfalme. Kisha mtoeni nje na kumpiga kwa mawe hadi afe.”
Et subornez contre lui deux hommes, fils de Bélial, et qu’ils disent ce faux témoignage: Il a blasphémé Dieu et le roi; ensuite menez-le hors de la ville, lapidez-le, et qu’ainsi il meure.
11 Hivyo wazee na watu wenye cheo walioishi katika mji wa Nabothi wakafanya kama Yezebeli alivyoelekeza katika barua aliyowaandikia.
Ses concitoyens donc, les anciens et les grands qui habitaient avec lui dans la ville, firent comme leur avait ordonné Jézabel, et comme il était écrit dans la lettre qu’elle leur avait envoyée:
12 Wakatangaza mfungo na kumketisha Nabothi mahali pa wazi miongoni mwa watu.
Ils publièrent un jeûne, et firent asseoir Naboth entre les premiers du peuple.
13 Kisha watu wawili wabaya kabisa wakaja wakaketi mkabala naye, nao wakaleta mashtaka dhidi ya Nabothi mbele ya watu, wakisema, “Nabothi amemlaani Mungu na mfalme.” Kwa hiyo wakamtoa nje na kumpiga kwa mawe hadi akafa.
Et deux hommes, fils du diable, ayant été amenés, ils les firent asseoir en face de lui; mais ceux-ci, comme hommes diaboliques, rendirent contre lui ce témoignage devant la multitude: Naboth a blasphémé Dieu et le roi. C’est pourquoi on l’amena hors de la ville, et on le lapida.
14 Kisha wakatuma ujumbe kwa Yezebeli, kusema, “Nabothi amepigwa mawe na amekufa.”
Et ils envoyèrent à Jézabel, disant: Naboth a été lapidé, et il est mort.
15 Mara tu Yezebeli aliposikia kwamba Nabothi amepigwa mawe na amekufa, akamwambia Ahabu, “Amka na uchukue lile shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli, ambalo alikataa kukuuzia. Hayuko hai tena, bali amekufa.”
Or il arriva que, lorsque Jézabel eut appris que Naboth avait été lapidé et qu’il était mort, elle dit à Achab: Levez-vous, et prenez possession de la vigne de Naboth, le Jezrahélite, qui n’a pas voulu se rendre à votre désir, ni vous la donner en acceptant de l’argent; car Naboth ne vit plus, mais il est mort.
16 Ahabu aliposikia Nabothi amekufa, akainuka na kushuka ili kulichukua shamba la mizabibu la Nabothi.
Lorsque Achab eut appris cela, c’est-à-dire que Naboth était mort, il se leva, et il descendait dans la vigne de Naboth, le Jezrahélite, pour en prendre possession.
17 Kisha neno la Bwana likamjia Eliya, Mtishbi:
La parole du Seigneur fut donc adressée à Elle, le Thesbite, disant:
18 “Shuka ukakutane na Ahabu mfalme wa Israeli, anayetawala Samaria. Sasa yuko katika shamba la mizabibu la Nabothi, ambapo amekwenda alimiliki.
Lève-toi, et descends à la rencontre d’Achab, roi d’Israël, qui est dans Samarie: car voilà qu’il descend dans la vigne de Naboth pour en prendre possession.
19 Umwambie, ‘Hivi ndivyo Bwana asemavyo: Je, hujamuua mtu na kuitwaa mali yake?’ Kisha umwambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Mahali ambapo mbwa waliramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba damu yako, naam, yako wewe!’”
Et tu lui parleras, disant: Voici ce que dit le Seigneur: Tu as tué, et de plus tu as pris possession. Et après cela, tu ajouteras: Voici ce que dit le Seigneur: En ce même lieu dans lequel les chiens ont léché le sang de Naboth, ils lécheront aussi ton sang.
20 Ahabu akamwambia Eliya, “Kwa hiyo umenipata, wewe adui yangu!” Akajibu, “Ndiyo, nimekupata. Kwa sababu umejiuza mwenyewe kufanya uovu mbele ya macho ya Bwana.
Et Achab dit à Elie: Est-ce que tu m’as trouvé ton ennemi? Elie lui répondit: Je vous ai trouvé tel, parce que vous vous êtes vendu pour faire le mal en la présence du Seigneur.
21 ‘Nitaleta maafa juu yako. Nitaangamiza uzao wako na kukatilia mbali kutoka kwa Ahabu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, wa mtumwa au wa mtu huru.
Voilà que j’amènerai des maux sur toi; je moissonnerai ta postérité, et je tuerai d’Achab celui qui urine contre une muraille, celui qui est renfermé, et celui qui est le dernier dans Israël.
22 Nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwana wa Nebati na ile ya Baasha mwana wa Ahiya, kwa sababu umenighadhibisha kwa kuwa umesababisha Israeli kutenda dhambi.’
Et je rendrai ta maison comme la maison de Jéroboam, fils de Nabath, et comme la maison de Baasa, fils d’Ahia, parce que tu as agi de manière à provoquer mon courroux, et que tu as fait pécher Israël.
23 “Pia kwa habari ya Yezebeli Bwana anasema, ‘Mbwa watamla Yezebeli karibu na ukuta wa Yezreeli.’
Mais le Seigneur a parlé aussi de Jézabel, disant: Les chiens mangeront Jézabel dans la campagne de Jezrahel.
24 “Mbwa watawala wale wa nyumba ya Ahabu watakaofia mjini, nao wale watakaofia mashambani wataliwa na ndege wa angani.”
Si Achab meurt dans la ville, les chiens mangeront sa chair; et s’il meurt dans la campagne, les oiseaux du ciel le mangeront.
25 (Hapajapata kamwe kuwa na mtu kama Ahabu, aliyejiuza mwenyewe kutenda uovu machoni mwa Bwana, akiwa anachochewa na Yezebeli mkewe.
Ainsi, il n’y eut point un autre semblable à Achab, qui se vendit pour faire le mal en la présence du Seigneur; car Jézabel, sa femme, l’excita,
26 Alitenda kwa uovu sana katika kuabudu sanamu, kama wale Waamori ambao Bwana aliowafukuza mbele ya Israeli.)
Et il devint tellement abominable, qu’il suivait les idoles qu’avaient faites les Amorrhéens, que le Seigneur extermina à la face des enfants d’Israël.
27 Ahabu aliposikia maneno haya, akararua nguo zake, akavaa nguo za gunia na kufunga. Akalala na kujifunika nguo za gunia na kwenda kwa unyenyekevu.
C’est pourquoi, lorsque Achab eut entendu ces paroles, il déchira ses vêtements, couvrit sa chair d’un cilice, jeûna et dormit avec le sac, et marcha la tête baissée.
28 Ndipo neno la Bwana lilipomjia Eliya Mtishbi kusema,
Et la parole du Seigneur fut adressée à Elie, le Thesbite, disant:
29 “Umeona jinsi Ahabu alivyojinyenyekeza mbele zangu? Kwa kuwa amejishusha mwenyewe, sitaleta maafa haya wakati akiwa hai, lakini nitayaleta juu ya nyumba yake katika siku za mwanawe.”
N’as-tu pas vu Achab humilié devant moi? Puis donc qu’il s’est humilié à cause de moi, je n’amènerai pas le malheur en ses jours, mais pendant les jours de son fils, je porterai le malheur dans sa maison.

< 1 Wafalme 21 >