< 1 Wafalme 21 >

1 Baada ya hayo, Nabothi, Myezreeli, alikuwa na shamba la mizabibu jirani na jumba la kifalme la Ahabu mfalme wa Samaria.
Après ces choses, Naboth, de Jizreel, possédait une vigne qui était à Jizreel, près du palais d'Achab, roi de Samarie.
2 Ahabu akamwambia Nabothi, “Nipe shamba lako la mizabibu nilitumie kwa bustani ya mboga, kwa kuwa liko karibu na jumba langu la kifalme. Badala yake, nitakupa shamba jingine la mizabibu zuri zaidi au, kama utapenda, nitakulipa kiasi chochote unachoona ni thamani yake.”
Achab parla à Naboth, et dit: « Donne-moi ta vigne, pour que j'en fasse un jardin d'herbes aromatiques, car elle est près de ma maison; et je te donnerai pour cela une vigne meilleure que celle-ci. Ou, si cela te semble bon, je te donnerai sa valeur en argent. »
3 Lakini Nabothi akamjibu, “Bwana na apishe mbali kukupa wewe urithi wa baba zangu.”
Naboth dit à Achab: « Que Yahvé me défende de te donner l'héritage de mes pères! »
4 Basi Ahabu akaenda nyumbani, mwenye huzuni na hasira kwa sababu ya yale ambayo Nabothi, Myezreeli, alikuwa amesema, “Sitakupa urithi wa baba zangu.” Akajinyoosha juu ya kitanda akisononeka, na akakataa kula.
Achab entra dans sa maison, maussade et furieux, à cause de la parole que lui avait adressée Naboth de Jizreel, qui avait dit: « Je ne te donnerai pas l'héritage de mes pères. » Il se coucha sur son lit, détourna son visage, et ne voulut pas manger de pain.
5 Yezebeli mke wake akaingia na akamuuliza, “Kwa nini unahuzunika hivi? Kwa nini huli chakula?”
Mais Jézabel, sa femme, vint le trouver et lui dit: « Pourquoi ton esprit est-il si triste que tu ne manges pas de pain? »
6 Akamjibu, “Kwa sababu nilimwambia Nabothi, Myezreeli, ‘Niuzie shamba lako la mizabibu, au kama ukipenda, nitakupa shamba jingine la mizabibu badala yake.’ Lakini akasema, ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’”
Il lui dit: « Parce que j'ai parlé à Naboth, le Jizreélite, et que je lui ai dit: « Donne-moi ta vigne pour de l'argent; ou bien, si cela te plaît, je te donnerai une autre vigne en échange. Il répondit: 'Je ne te donnerai pas ma vigne'. »
7 Yezebeli mke wake akasema, “Hivi ndivyo unavyofanya, nawe ni mfalme katika Israeli yote? Inuka na ule! Changamka. Nitakupatia shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli.”
Jézabel, sa femme, lui dit: Est-ce toi qui gouvernes maintenant le royaume d'Israël? Lève-toi, mange du pain, et que ton cœur s'égaye. Je te donnerai la vigne de Naboth, le Jizreélite. »
8 Kwa hiyo akaandika barua kwa jina la Ahabu akaweka muhuri wake juu ya hizo barua, akazipeleka kwa wazee na kwa watu wenye cheo walioishi katika mji pamoja na Nabothi.
Elle écrivit donc des lettres au nom d'Achab et les scella de son sceau, puis elle envoya les lettres aux anciens et aux nobles qui étaient dans sa ville et qui habitaient avec Naboth.
9 Katika barua hizo aliandika: “Tangazeni siku ya watu kufunga na mkamketishe Nabothi mahali pa wazi miongoni mwa watu.
Elle écrivit dans les lettres: « Proclamez un jeûne, et élevez Naboth au milieu du peuple.
10 Lakini waketisheni watu wawili wabaya kabisa mkabala naye, nao washuhudie kuwa yeye amemlaani Mungu na mfalme. Kisha mtoeni nje na kumpiga kwa mawe hadi afe.”
Placez devant lui deux hommes, des méchants, et qu'ils témoignent contre lui en disant: « Tu as maudit Dieu et le roi ». Puis on l'emmènera et on le lapidera jusqu'à ce que mort s'ensuive. »
11 Hivyo wazee na watu wenye cheo walioishi katika mji wa Nabothi wakafanya kama Yezebeli alivyoelekeza katika barua aliyowaandikia.
Les hommes de sa ville, les anciens et les nobles qui y habitaient, firent ce que Jézabel leur avait ordonné dans les lettres qu'elle avait écrites et envoyées.
12 Wakatangaza mfungo na kumketisha Nabothi mahali pa wazi miongoni mwa watu.
Ils proclamèrent un jeûne et mirent Naboth en vedette parmi le peuple.
13 Kisha watu wawili wabaya kabisa wakaja wakaketi mkabala naye, nao wakaleta mashtaka dhidi ya Nabothi mbele ya watu, wakisema, “Nabothi amemlaani Mungu na mfalme.” Kwa hiyo wakamtoa nje na kumpiga kwa mawe hadi akafa.
Les deux hommes, les méchants, entrèrent et s'assirent devant lui. Les méchants témoignèrent contre lui, contre Naboth même, en présence du peuple, en disant: « Naboth a maudit Dieu et le roi! » Puis ils le transportèrent hors de la ville et le lapidèrent à mort.
14 Kisha wakatuma ujumbe kwa Yezebeli, kusema, “Nabothi amepigwa mawe na amekufa.”
Puis ils envoyèrent dire à Jézabel: « Naboth a été lapidé et il est mort. »
15 Mara tu Yezebeli aliposikia kwamba Nabothi amepigwa mawe na amekufa, akamwambia Ahabu, “Amka na uchukue lile shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli, ambalo alikataa kukuuzia. Hayuko hai tena, bali amekufa.”
Lorsque Jézabel apprit que Naboth avait été lapidé et qu'il était mort, elle dit à Achab: « Lève-toi, prends possession de la vigne de Naboth, le Jizreélite, qu'il a refusé de te donner à prix d'argent; car Naboth n'est pas vivant, mais mort. »
16 Ahabu aliposikia Nabothi amekufa, akainuka na kushuka ili kulichukua shamba la mizabibu la Nabothi.
Lorsqu'Achab apprit que Naboth était mort, il se leva pour descendre à la vigne de Naboth, le Jizreélite, afin d'en prendre possession.
17 Kisha neno la Bwana likamjia Eliya, Mtishbi:
La parole de Yahvé fut adressée à Élie, le Tishbite, en ces termes:
18 “Shuka ukakutane na Ahabu mfalme wa Israeli, anayetawala Samaria. Sasa yuko katika shamba la mizabibu la Nabothi, ambapo amekwenda alimiliki.
« Lève-toi, descends à la rencontre d'Achab, roi d'Israël, qui habite à Samarie. Voici qu'il est dans la vigne de Naboth, où il est descendu pour en prendre possession.
19 Umwambie, ‘Hivi ndivyo Bwana asemavyo: Je, hujamuua mtu na kuitwaa mali yake?’ Kisha umwambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Mahali ambapo mbwa waliramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba damu yako, naam, yako wewe!’”
Tu lui parleras en disant: « L'Éternel dit: « As-tu tué et pris possession? » Tu lui parleras en disant: « Yahvé dit: « A l'endroit où les chiens ont léché le sang de Naboth, les chiens lécheront ton sang, même le tien ». »"
20 Ahabu akamwambia Eliya, “Kwa hiyo umenipata, wewe adui yangu!” Akajibu, “Ndiyo, nimekupata. Kwa sababu umejiuza mwenyewe kufanya uovu mbele ya macho ya Bwana.
Achab dit à Élie: « Tu m'as trouvé, mon ennemi? » Il répondit: « Je t'ai trouvé, car tu t'es vendu pour faire ce qui est mal aux yeux de l'Éternel.
21 ‘Nitaleta maafa juu yako. Nitaangamiza uzao wako na kukatilia mbali kutoka kwa Ahabu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, wa mtumwa au wa mtu huru.
Voici, je vais faire venir le malheur sur toi, je te balaierai et j'exterminerai d'Achab tous ceux qui urinent contre un mur, ceux qui sont enfermés et ceux qui sont en liberté en Israël.
22 Nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwana wa Nebati na ile ya Baasha mwana wa Ahiya, kwa sababu umenighadhibisha kwa kuwa umesababisha Israeli kutenda dhambi.’
Je rendrai ta maison semblable à la maison de Jéroboam, fils de Nebat, et à la maison de Baescha, fils d'Achille, à cause de la provocation par laquelle tu m'as irrité et tu as fait pécher Israël. »
23 “Pia kwa habari ya Yezebeli Bwana anasema, ‘Mbwa watamla Yezebeli karibu na ukuta wa Yezreeli.’
Yahvé parla aussi de Jézabel, et dit: « Les chiens mangeront Jézabel près du rempart de Jizreel.
24 “Mbwa watawala wale wa nyumba ya Ahabu watakaofia mjini, nao wale watakaofia mashambani wataliwa na ndege wa angani.”
Les chiens mangeront celui qui mourra d'Achab dans la ville, et les oiseaux du ciel mangeront celui qui mourra dans les champs. »
25 (Hapajapata kamwe kuwa na mtu kama Ahabu, aliyejiuza mwenyewe kutenda uovu machoni mwa Bwana, akiwa anachochewa na Yezebeli mkewe.
Mais il n'y eut personne comme Achab, qui se vendit pour faire ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, et que Jézabel, sa femme, excita.
26 Alitenda kwa uovu sana katika kuabudu sanamu, kama wale Waamori ambao Bwana aliowafukuza mbele ya Israeli.)
Il a fait des choses très abominables en suivant les idoles, selon tout ce qu'ont fait les Amoréens, que l'Éternel a chassés devant les enfants d'Israël.
27 Ahabu aliposikia maneno haya, akararua nguo zake, akavaa nguo za gunia na kufunga. Akalala na kujifunika nguo za gunia na kwenda kwa unyenyekevu.
Lorsqu'Achab entendit ces paroles, il déchira ses vêtements, mit un sac sur son corps, jeûna, se coucha dans un sac et se mit à errer avec découragement.
28 Ndipo neno la Bwana lilipomjia Eliya Mtishbi kusema,
La parole de Yahvé fut adressée à Élie, le Tishbite, en ces termes:
29 “Umeona jinsi Ahabu alivyojinyenyekeza mbele zangu? Kwa kuwa amejishusha mwenyewe, sitaleta maafa haya wakati akiwa hai, lakini nitayaleta juu ya nyumba yake katika siku za mwanawe.”
« Vois-tu comment Achab s'humilie devant moi? Parce qu'il s'humilie devant moi, je ne ferai pas venir le malheur de son vivant, mais je ferai venir le malheur sur sa maison au jour de son fils. »

< 1 Wafalme 21 >