< 1 Wafalme 21 >

1 Baada ya hayo, Nabothi, Myezreeli, alikuwa na shamba la mizabibu jirani na jumba la kifalme la Ahabu mfalme wa Samaria.
and to be after [the] word: thing [the] these vineyard to be to/for Naboth [the] Jezreelite which in/on/with Jezreel beside temple: palace Ahab king Samaria
2 Ahabu akamwambia Nabothi, “Nipe shamba lako la mizabibu nilitumie kwa bustani ya mboga, kwa kuwa liko karibu na jumba langu la kifalme. Badala yake, nitakupa shamba jingine la mizabibu zuri zaidi au, kama utapenda, nitakulipa kiasi chochote unachoona ni thamani yake.”
and to speak: speak Ahab to(wards) Naboth to/for to say to give: give [emph?] to/for me [obj] vineyard your and to be to/for me to/for garden herb for he/she/it near beside house: palace my and to give: give to/for you underneath: instead him vineyard pleasant from him if be pleasing in/on/with eye: appearance your to give: give to/for you silver: money price this
3 Lakini Nabothi akamjibu, “Bwana na apishe mbali kukupa wewe urithi wa baba zangu.”
and to say Naboth to(wards) Ahab forbid to/for me from LORD from to give: give I [obj] inheritance father my to/for you
4 Basi Ahabu akaenda nyumbani, mwenye huzuni na hasira kwa sababu ya yale ambayo Nabothi, Myezreeli, alikuwa amesema, “Sitakupa urithi wa baba zangu.” Akajinyoosha juu ya kitanda akisononeka, na akakataa kula.
and to come (in): come Ahab to(wards) house: home his stubborn and vexed upon [the] word which to speak: speak to(wards) him Naboth [the] Jezreelite and to say not to give: give to/for you [obj] inheritance father my and to lie down: lay down upon bed his and to turn: turn [obj] face his and not to eat food
5 Yezebeli mke wake akaingia na akamuuliza, “Kwa nini unahuzunika hivi? Kwa nini huli chakula?”
and to come (in): come to(wards) him Jezebel woman: wife his and to speak: speak to(wards) him what? this spirit your stubborn and nothing you to eat food
6 Akamjibu, “Kwa sababu nilimwambia Nabothi, Myezreeli, ‘Niuzie shamba lako la mizabibu, au kama ukipenda, nitakupa shamba jingine la mizabibu badala yake.’ Lakini akasema, ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’”
and to speak: speak to(wards) her for to speak: speak to(wards) Naboth [the] Jezreelite and to say to/for him to give: give [emph?] to/for me [obj] vineyard your in/on/with silver: money or if delighting you(m. s.) to give: give to/for you vineyard underneath: instead him and to say not to give: give to/for you [obj] vineyard my
7 Yezebeli mke wake akasema, “Hivi ndivyo unavyofanya, nawe ni mfalme katika Israeli yote? Inuka na ule! Changamka. Nitakupatia shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli.”
and to say to(wards) him Jezebel woman: wife his you(m. s.) now to make: [do] kingship upon Israel to arise: rise to eat food: bread and be good heart your I to give: give to/for you [obj] vineyard Naboth [the] Jezreelite
8 Kwa hiyo akaandika barua kwa jina la Ahabu akaweka muhuri wake juu ya hizo barua, akazipeleka kwa wazee na kwa watu wenye cheo walioishi katika mji pamoja na Nabothi.
and to write scroll: document in/on/with name Ahab and to seal in/on/with signet his and to send: depart (scroll: document *Q(K)*) to(wards) [the] old: elder and to(wards) [the] noble which in/on/with city his [the] to dwell with Naboth
9 Katika barua hizo aliandika: “Tangazeni siku ya watu kufunga na mkamketishe Nabothi mahali pa wazi miongoni mwa watu.
and to write in/on/with scroll: document to/for to say to call: call out fast and to dwell [obj] Naboth in/on/with head: leader [the] people
10 Lakini waketisheni watu wawili wabaya kabisa mkabala naye, nao washuhudie kuwa yeye amemlaani Mungu na mfalme. Kisha mtoeni nje na kumpiga kwa mawe hadi afe.”
and to dwell two human son: young animal Belial before him and to testify him to/for to say to bless God and king and to come out: send him and to stone him and to die
11 Hivyo wazee na watu wenye cheo walioishi katika mji wa Nabothi wakafanya kama Yezebeli alivyoelekeza katika barua aliyowaandikia.
and to make: do human city his [the] old: elder and [the] noble which [the] to dwell in/on/with city his like/as as which to send: depart to(wards) them Jezebel like/as as which to write in/on/with scroll: document which to send: depart to(wards) them
12 Wakatangaza mfungo na kumketisha Nabothi mahali pa wazi miongoni mwa watu.
to call: call out fast and to dwell [obj] Naboth in/on/with head [the] people
13 Kisha watu wawili wabaya kabisa wakaja wakaketi mkabala naye, nao wakaleta mashtaka dhidi ya Nabothi mbele ya watu, wakisema, “Nabothi amemlaani Mungu na mfalme.” Kwa hiyo wakamtoa nje na kumpiga kwa mawe hadi akafa.
and to come (in): come two [the] human son: young animal Belial and to dwell before him and to testify him human [the] Belial [obj] Naboth before [the] people to/for to say to bless Naboth God and king and to come out: send him from outside to/for city and to stone him in/on/with stone and to die
14 Kisha wakatuma ujumbe kwa Yezebeli, kusema, “Nabothi amepigwa mawe na amekufa.”
and to send: depart to(wards) Jezebel to/for to say to stone Naboth and to die
15 Mara tu Yezebeli aliposikia kwamba Nabothi amepigwa mawe na amekufa, akamwambia Ahabu, “Amka na uchukue lile shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli, ambalo alikataa kukuuzia. Hayuko hai tena, bali amekufa.”
and to be like/as to hear: hear Jezebel for to stone Naboth and to die and to say Jezebel to(wards) Ahab to arise: rise to possess: take [obj] vineyard Naboth [the] Jezreelite which to refuse to/for to give: give to/for you in/on/with silver: money for nothing Naboth alive for to die
16 Ahabu aliposikia Nabothi amekufa, akainuka na kushuka ili kulichukua shamba la mizabibu la Nabothi.
and to be like/as to hear: hear Ahab for to die Naboth and to arise: rise Ahab to/for to go down to(wards) vineyard Naboth [the] Jezreelite to/for to possess: take him
17 Kisha neno la Bwana likamjia Eliya, Mtishbi:
and to be word LORD to(wards) Elijah [the] Tishbite to/for to say
18 “Shuka ukakutane na Ahabu mfalme wa Israeli, anayetawala Samaria. Sasa yuko katika shamba la mizabibu la Nabothi, ambapo amekwenda alimiliki.
to arise: rise to go down to/for to encounter: meet Ahab king Israel which in/on/with Samaria behold in/on/with vineyard Naboth which to go down there to/for to possess: take him
19 Umwambie, ‘Hivi ndivyo Bwana asemavyo: Je, hujamuua mtu na kuitwaa mali yake?’ Kisha umwambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Mahali ambapo mbwa waliramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba damu yako, naam, yako wewe!’”
and to speak: speak to(wards) him to/for to say thus to say LORD to murder and also to possess: take and to speak: speak to(wards) him to/for to say thus to say LORD in/on/with place which to lick [the] dog [obj] blood Naboth to lick [the] dog [obj] blood your also you(m. s.)
20 Ahabu akamwambia Eliya, “Kwa hiyo umenipata, wewe adui yangu!” Akajibu, “Ndiyo, nimekupata. Kwa sababu umejiuza mwenyewe kufanya uovu mbele ya macho ya Bwana.
and to say Ahab to(wards) Elijah to find me enemy my and to say to find because to sell you to/for to make: do [the] bad: evil in/on/with eye: seeing LORD
21 ‘Nitaleta maafa juu yako. Nitaangamiza uzao wako na kukatilia mbali kutoka kwa Ahabu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, wa mtumwa au wa mtu huru.
look! I (to come (in): bring *Q(k)*) to(wards) you distress: harm and to burn: burn after you and to cut: eliminate to/for Ahab to urinate in/on/with wall and to restrain and to leave: release in/on/with Israel
22 Nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwana wa Nebati na ile ya Baasha mwana wa Ahiya, kwa sababu umenighadhibisha kwa kuwa umesababisha Israeli kutenda dhambi.’
and to give: make [obj] house: household your like/as house: household Jeroboam son: child Nebat and like/as house: household Baasha son: child Ahijah to(wards) [the] vexation which to provoke and to sin [obj] Israel
23 “Pia kwa habari ya Yezebeli Bwana anasema, ‘Mbwa watamla Yezebeli karibu na ukuta wa Yezreeli.’
and also to/for Jezebel to speak: speak LORD to/for to say [the] dog to eat [obj] Jezebel in/on/with rampart Jezreel
24 “Mbwa watawala wale wa nyumba ya Ahabu watakaofia mjini, nao wale watakaofia mashambani wataliwa na ndege wa angani.”
[the] to die to/for Ahab in/on/with city to eat [the] dog and [the] to die in/on/with land: country to eat bird [the] heaven
25 (Hapajapata kamwe kuwa na mtu kama Ahabu, aliyejiuza mwenyewe kutenda uovu machoni mwa Bwana, akiwa anachochewa na Yezebeli mkewe.
except not to be like/as Ahab which to sell to/for to make: do [the] bad: evil in/on/with eye: seeing LORD which to incite [obj] him Jezebel woman: wife his
26 Alitenda kwa uovu sana katika kuabudu sanamu, kama wale Waamori ambao Bwana aliowafukuza mbele ya Israeli.)
and to abhor much to/for to go: follow after [the] idol like/as all which to make: do [the] Amorite which to possess: take LORD from face: before son: descendant/people Israel
27 Ahabu aliposikia maneno haya, akararua nguo zake, akavaa nguo za gunia na kufunga. Akalala na kujifunika nguo za gunia na kwenda kwa unyenyekevu.
and to be like/as to hear: hear Ahab [obj] [the] word [the] these and to tear garment his and to set: put sackcloth upon flesh his and to fast and to lie down: lay down in/on/with sackcloth and to go: went softly
28 Ndipo neno la Bwana lilipomjia Eliya Mtishbi kusema,
and to be word LORD to(wards) Elijah [the] Tishbite to/for to say
29 “Umeona jinsi Ahabu alivyojinyenyekeza mbele zangu? Kwa kuwa amejishusha mwenyewe, sitaleta maafa haya wakati akiwa hai, lakini nitayaleta juu ya nyumba yake katika siku za mwanawe.”
to see: see for be humble Ahab from to/for face: before my because for be humble from face: before my not (to come (in): bring *Q(k)*) [the] distress: harm in/on/with day his in/on/with day son: child his to come (in): bring [the] distress: harm upon house: household his

< 1 Wafalme 21 >