< 1 Wafalme 2 >

1 Siku zilipokaribia za Daudi kufa, akampa mwanawe Solomoni agizo.
Les jours de David approchaient où il devait mourir, et il donna cet ordre à Salomon, son fils:
2 Akasema, “Mimi ninakaribia kwenda njia ya dunia yote. Hivyo uwe hodari, jionyeshe kuwa mwanaume,
« Je m'en vais par le chemin de toute la terre. Sois donc fort, et montre-toi un homme;
3 shika lile Bwana Mungu wako analokuagiza: Enenda katika njia zake, ushike maagizo na amri zake, sheria zake na kanuni zake, kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, ili upate kustawi katika yote ufanyayo na popote uendako,
et garde les instructions de l'Éternel, ton Dieu, pour marcher dans ses voies, pour observer ses lois, ses commandements, ses ordonnances et ses témoignages, selon ce qui est écrit dans la loi de Moïse, afin que tu prospères dans tout ce que tu fais et partout où tu te tournes.
4 ili kwamba Bwana aweze kunitimizia ahadi yake: ‘Kama wazao wako wakiangalia sana wanavyoishi, na kama wakienenda kwa uaminifu mbele zangu kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote, kamwe hutakosa kuwa na mtu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’
Alors Yahvé accomplira la parole qu'il a prononcée à mon sujet, en disant: « Si tes enfants prennent garde à leur voie, pour marcher devant moi dans la vérité, de tout leur cœur et de toute leur âme, tu ne manqueras pas, dit-il, d'un homme sur le trône d'Israël ».
5 “Sasa wewe mwenyewe unafahamu lile Yoabu mwana wa Seruya alilonitendea, lile alilofanya kwa majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yetheri. Aliwaua, akimwaga damu yao wakati wa amani kama vile ni kwenye vita, tena akaipaka damu ile kwenye mkanda uliokuwa kiunoni mwake na viatu alivyovaa miguuni mwake.
Vous savez d'ailleurs ce que m'a fait Joab, fils de Tseruja, ce qu'il a fait aux deux chefs des armées d'Israël, à Abner, fils de Ner, et à Amasa, fils de Jéther, qu'il a tués, et qu'il a fait couler en paix le sang de la guerre, en mettant le sang de la guerre sur la ceinture qu'il avait à la taille et sur les sandales qu'il avait aux pieds.
6 Shughulika naye kwa kadiri ya hekima yako, lakini usiache kichwa chake chenye mvi kishukie kaburi kwa amani. (Sheol h7585)
Fais donc selon ta sagesse, et ne laisse pas sa tête grise descendre en paix au séjour des morts. (Sheol h7585)
7 “Lakini uwaonyeshe wema wana wa Barzilai wa Gileadi na uwaruhusu wawe miongoni mwa wale walao mezani pako. Walisimama nami nilipomkimbia ndugu yako Absalomu.
Mais fais preuve de bonté envers les fils de Barzillai, le Galaadite, et qu'ils soient du nombre de ceux qui mangent à ta table, car c'est ainsi qu'ils sont venus à moi lorsque j'ai fui Absalom, ton frère.
8 “Ukumbuke, unaye Shimei mwana wa Gera, Mbenyamini kutoka Bahurimu, ambaye alinilaani kwa laana kali siku niliyokwenda Mahanaimu. Aliposhuka kunilaki huko Yordani, nilimwapia kwa Bwana: ‘Sitakuua kwa upanga!’
« Voici qu'il y a avec toi Shimei, fils de Gera, Benjamite de Bahurim, qui m'a maudit d'une manière redoutable le jour où je suis allé à Mahanaïm; mais il est descendu à ma rencontre au Jourdain, et je lui ai juré par Yahvé: 'Je ne te ferai pas mourir par l'épée'.
9 Lakini sasa, usidhani kwamba hana hatia. Wewe ni mtu wa hekima, utajua la kumtendea. Zishushe mvi zake kaburini kwa damu.” (Sheol h7585)
Maintenant donc, ne le tiens pas pour innocent, car tu es un homme sage; tu sauras ce que tu dois lui faire, et tu feras descendre au séjour des morts sa tête grise dans le sang. » (Sheol h7585)
10 Kisha Daudi akapumzika pamoja na baba zake naye akazikwa katika Mji wa Daudi.
David se coucha avec ses pères, et il fut enterré dans la ville de David.
11 Daudi alikuwa ametawala juu ya Israeli miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
Les jours où David régna sur Israël furent de quarante ans; il régna sept ans à Hébron, et il régna trente-trois ans à Jérusalem.
12 Kwa hiyo Solomoni akaketi katika kiti cha ufalme cha baba yake Daudi, nao utawala wake ukaimarika sana.
Salomon s'assit sur le trône de David, son père, et son royaume fut solidement établi.
13 Basi Adoniya, mwana wa Hagithi, akaenda kwa Bathsheba, mama yake Solomoni. Bathsheba akamuuliza, “Je, umekuja kwa amani?” Akajibu, “Ndiyo, kwa amani.”
Alors Adonija, fils de Haggith, vint auprès de Bethsabée, mère de Salomon. Elle dit: « Viens-tu paisiblement? » Il a dit: « pacifiquement ».
14 Kisha akaongeza, “Ninalo jambo la kukuambia.” Akajibu, “Waweza kulisema.”
Il dit en outre: « J'ai quelque chose à vous dire. » Elle a dit: « Dis-le. »
15 Akasema, “Kama unavyojua, ufalme ulikuwa wangu. Israeli wote waliniangalia mimi kama mfalme wao. Lakini mambo yalibadilika, ufalme umekwenda kwa ndugu yangu, kwa maana umemjia kutoka kwa Bwana.
Il dit: « Vous savez que le royaume était à moi, et que tout Israël s'est tourné vers moi pour que je règne. Mais le royaume s'est retourné et est devenu celui de mon frère, car il lui a été donné par Yahvé.
16 Sasa ninalo ombi moja ninalokuomba. Usinikatalie.” Bathsheba akasema, “Waweza kuliomba.”
Maintenant, je te demande une chose. Ne me renie pas. » Elle lui a dit: « Dis-le. »
17 Kwa hiyo akaendelea kusema, “Tafadhali mwombe Mfalme Solomoni, anipatie Abishagi, Mshunami, awe mke wangu; hatakukatalia wewe.”
Il dit: « Parle au roi Salomon, car il ne te dira pas non, pour qu'il me donne pour femme Abishag, la Sunamite. »
18 Bathsheba akamjibu, “Vema sana, nitazungumza na mfalme kwa ajili yako.”
Bethsabée dit: « Très bien. Je parlerai en ton nom au roi. »
19 Bathsheba alipokwenda kwa Mfalme Solomoni kuzungumza naye kwa ajili ya Adoniya, mfalme alisimama kumlaki mama yake, akamwinamia na kuketi kwenye kiti chake cha ufalme. Akaamuru kiti cha ufalme kuletwa kwa ajili ya mama yake mfalme, naye akaketi mkono wake wa kuume.
Bethsabée alla donc vers le roi Salomon, pour lui parler en faveur d'Adonija. Le roi se leva à sa rencontre, se prosterna devant elle, s'assit sur son trône et fit placer un trône pour la mère du roi, et elle s'assit à sa droite.
20 Bathsheba akamwambia mfalme, “Ninalo ombi moja dogo la kukuomba; usinikatalie.” Mfalme akajibu, “Omba, mama yangu; sitakukatalia.”
Elle dit alors: « Je te demande une petite requête; ne me refuse pas. » Le roi lui dit: « Demande, ma mère, car je ne te refuserai pas. »
21 Akasema, “Mruhusu Abishagi, Mshunami, aolewe na ndugu yako Adoniya.”
Elle dit: « Qu'Abishag, la Sunamite, soit donnée pour femme à Adonija, ton frère. »
22 Mfalme Solomoni akamjibu mama yake, “Kwa nini uombe Abishagi, Mshunami, kwa ajili ya Adoniya? Ungeweza pia kuomba ufalme kwa ajili yake, kwani yeye ni ndugu yangu mkubwa: naam, kwa ajili yake, na kwa kuhani Abiathari na Yoabu mwana wa Seruya!”
Le roi Salomon répondit à sa mère: « Pourquoi demandes-tu à Abischag, la Sunamite, pour Adonija? Demande pour lui aussi le royaume, car il est mon frère aîné; pour lui aussi, pour le prêtre Abiathar, et pour Joab, fils de Tseruja. »
23 Mfalme Solomoni akaapa kwa Bwana, akasema: “Mungu na aniulie mbali, tena bila huruma, ikiwa Adoniya hatalipa kwa uhai wake kwa ajili ya ombi hili!
Alors le roi Salomon jura par Yahvé, en disant: « Que Dieu me fasse ainsi, et plus encore, si Adonija n'a pas prononcé cette parole contre sa propre vie.
24 Basi sasa, hakika kama Bwana aishivyo, yeye ambaye ameniimarisha salama kwenye kiti cha ufalme cha Daudi baba yangu, naye amenipa ufalme wa kudumu kama alivyoahidi, Adoniya atauawa leo!”
Maintenant que Yahvé est vivant, lui qui m'a affermi et m'a mis sur le trône de mon père David, et qui m'a fait une maison comme il l'avait promis, Adonija sera mis à mort aujourd'hui. »
25 Hivyo Mfalme Solomoni akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akampiga Adoniya akafa.
Le roi Salomon envoya Benaja, fils de Jehojada, qui tomba sur lui, de sorte qu'il mourut.
26 Mfalme akamwambia kuhani Abiathari, “Nenda huko Anathothi katika mashamba yako. Wewe unastahili kufa, lakini sitakuua sasa, kwa sababu ulilichukua Sanduku la Bwana Mwenyezi mbele ya Daudi baba yangu na ulishiriki taabu zote za baba yangu.”
Le roi dit au prêtre Abiathar: « Va à Anathoth, dans tes champs, car tu es digne de mourir. Mais je ne te ferai pas mourir maintenant, parce que tu as porté l'arche du Seigneur Yahvé devant David, mon père, et parce que tu as été affligé dans tout ce que mon père a été affligé. »
27 Hivyo Solomoni akamwondoa Abiathari kwenye ukuhani wa Bwana, akilitimiza neno la Bwana alilokuwa amenena huko Shilo kuhusu nyumba ya Eli.
Salomon chassa donc Abiathar de la fonction de prêtre de l'Éternel, afin d'accomplir la parole de l'Éternel qu'il avait prononcée au sujet de la maison d'Éli à Silo.
28 Habari zilipomfikia Yoabu, ambaye alikuwa amefanya shauri baya na Adoniya, lakini sio na Absalomu, alikimbilia kwenye hema la Bwana na kushika pembe za madhabahu.
Cette nouvelle parvint à Joab, car Joab avait suivi Adonija, bien qu'il n'eût pas suivi Absalom. Joab s'enfuit vers la tente de l'Éternel et s'accrocha aux cornes de l'autel.
29 Mfalme Solomoni akaambiwa kuwa Yoabu amekimbilia kwenye hema la Bwana naye alikuwa kando ya madhabahu. Basi Solomoni akamwagiza Benaya mwana wa Yehoyada: “Nenda ukamuue!”
On dit au roi Salomon: « Joab s'est enfui vers la tente de l'Éternel, et voici qu'il est près de l'autel. » Alors Salomon envoya Benaja, fils de Jehoiada, en disant: « Va, tombe sur lui. »
30 Ndipo Benaya akaingia kwenye hema la Bwana na kumwambia Yoabu, “Mfalme anasema, ‘Toka nje!’” Lakini akajibu, “La! Nitafia hapa hapa.” Benaya akamwarifu mfalme, “Hivi ndivyo Yoabu alivyonijibu.”
Benaja vint à la tente de Yahvé et lui dit: « Le roi dit: « Sors! »" Il a dit: « Non; mais je mourrai ici. » Benaiah rapporta de nouveau la parole au roi, en disant: « Voici ce que Joab a dit, et voici comment il m'a répondu. »
31 Kisha mfalme akamwamuru Benaya, “Fanya kama asemavyo. Muue na kumzika, ili uniondolee mimi na nyumba ya baba yangu dhambi ya damu isiyokuwa na hatia ile Yoabu aliyoimwaga.
Le roi lui dit: « Fais ce qu'il a dit, tombe sur lui et enterre-le, afin d'ôter de moi et de la maison de mon père le sang que Joab a versé sans raison.
32 Bwana atamlipiza kwa ajili ya damu aliyoimwaga, kwa sababu pasipo Daudi baba yangu kujua, aliwashambulia watu wawili na kuwaua kwa upanga. Wote wawili, Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Israeli, na Amasa mwana wa Yetheri, jemadari wa jeshi la Yuda, walikuwa watu wazuri na wanyofu kuliko yeye.
Yahvé fera retomber son sang sur sa propre tête, car il est tombé sur deux hommes plus justes et meilleurs que lui, et les a tués par l'épée, sans que mon père David le sache: Abner, fils de Ner, chef de l'armée d'Israël, et Amasa, fils de Jether, chef de l'armée de Juda.
33 Hatia ya damu yao na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na wazao wake milele. Lakini kwa Daudi na uzao wake, nyumba yake na kiti chake cha ufalme, iwepo amani ya Bwana milele.”
Ainsi leur sang retombera sur la tête de Joab et sur la tête de sa descendance pour toujours. Mais pour David, pour sa descendance, pour sa maison et pour son trône, il y aura une paix éternelle de la part de Yahvé. »
34 Basi Benaya mwana wa Yehoyada akakwea, akampiga na kumuua Yoabu, naye akazikwa katika nchi yake mwenyewe katika jangwa.
Alors Benaja, fils de Jehojada, monta, se jeta sur lui et le tua; et il fut enterré dans sa maison, dans le désert.
35 Mfalme akamweka Benaya mwana wa Yehoyada juu ya jeshi kwenye nafasi ya Yoabu na kumweka kuhani Sadoki badala ya Abiathari.
Le roi remit Benaja, fils de Jehojada, à sa place dans l'armée, et le roi mit le sacrificateur Tsadok à la place d'Abiathar.
36 Kisha mfalme akatuma ujumbe kwa Shimei na kumwambia, “Ujijengee nyumba huko Yerusalemu uishi huko, lakini usiende mahali pengine popote.
Le roi fit appeler Shimei et lui dit: « Construis-toi une maison à Jérusalem, et habite là, et ne va pas ailleurs.
37 Siku utakayoondoka kuvuka Bonde la Kidroni, uwe na hakika utakufa; damu yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.”
Car le jour où tu sortiras et passeras le torrent de Cédron, sache que tu mourras certainement. Ton sang sera sur ta tête. »
38 Shimei akamjibu mfalme, “Ulilolisema ni jema. Mtumishi wako atatenda kama bwana wangu mfalme alivyosema.” Naye Shimei akakaa Yerusalemu kwa muda mrefu.
Shimei dit au roi: « Ce que tu dis est bien. Ce que mon seigneur le roi a dit, ton serviteur le fera aussi. » Shimei vécut de nombreux jours à Jérusalem.
39 Lakini baada ya miaka mitatu, watumwa wawili wa Shimei wakatoroka kwenda kwa Akishi mwana wa Maaka, mfalme wa Gathi, naye Shimei akaambiwa, “Watumwa wako wako Gathi.”
Au bout de trois ans, deux des esclaves de Shimei s'enfuirent chez Akish, fils de Maaca, roi de Gath. Ils en informèrent Shimei en disant: « Voici tes esclaves à Gath. »
40 Kwa ajili ya hili, Shimei akatandika punda wake, akaenda kwa Akishi huko Gathi kuwatafuta watumwa wake. Basi Shimei akaondoka na kuwarudisha watumwa wake kutoka Gathi.
Shimei se leva, sella son âne et alla à Gath, chez Akish, pour chercher ses esclaves; et Shimei alla chercher ses esclaves à Gath.
41 Solomoni alipoambiwa kuwa Shimei ametoka Yerusalemu na kwenda Gathi na amekwisha kurudi,
On raconta à Salomon que Shimei était allé de Jérusalem à Gath, et qu'il était revenu.
42 mfalme akamwita Shimei na kumwambia, “Je, sikukuapiza kwa Bwana na kukuonya kuwa, ‘Siku utakayoondoka kwenda mahali pengine popote, uwe na hakika utakufa?’ Wakati ule uliniambia, ‘Ulilolisema ni jema. Nitatii!’
Le roi fit appeler Shimei et lui dit: « Ne t'ai-je pas adjuré par l'Éternel et ne t'ai-je pas averti en disant: « Sache bien que le jour où tu sortiras et marcheras ailleurs, tu mourras certainement? » Tu m'as répondu: « La parole que j'ai entendue est bonne. »
43 Kwa nini basi hukutunza kiapo chako kwa Bwana na kutii amri niliyokupa?”
Pourquoi donc n'as-tu pas respecté le serment de l'Éternel et le commandement dont je t'ai instruit? »
44 Pia mfalme akamwambia Shimei, “Unajua katika moyo wako makosa uliyomtendea baba yangu Daudi. Sasa Bwana atakulipiza kwa ajili ya mabaya yako uliyotenda.
Le roi dit encore à Shimei: « Tu sais dans ton cœur toute la méchanceté que tu as commise envers David, mon père. C'est pourquoi Yahvé fera retomber ta méchanceté sur ta propre tête.
45 Lakini Mfalme Solomoni atabarikiwa, na kiti cha ufalme cha Daudi kitakuwa imara mbele za Bwana milele.”
Mais le roi Salomon sera béni, et le trône de David sera affermi devant Yahvé pour toujours. »
46 Kisha mfalme akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akatoka nje, akampiga Shimei na kumuua. Sasa ufalme ukawa umeimarika kikamilifu mikononi mwa Solomoni.
Le roi donna des ordres à Benaja, fils de Jehoïada, qui sortit et tomba sur lui, de sorte qu'il mourut. Le royaume fut établi entre les mains de Salomon.

< 1 Wafalme 2 >