< 1 Wafalme 2 >

1 Siku zilipokaribia za Daudi kufa, akampa mwanawe Solomoni agizo.
Forsothe the daies of Dauid neiyiden, that he schulde die; and he comaundide to Salomon, his sone, and seide, Lo!
2 Akasema, “Mimi ninakaribia kwenda njia ya dunia yote. Hivyo uwe hodari, jionyeshe kuwa mwanaume,
Y entre in to the weie of al erthe; be thou coumfortid, and be thou a strong man.
3 shika lile Bwana Mungu wako analokuagiza: Enenda katika njia zake, ushike maagizo na amri zake, sheria zake na kanuni zake, kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, ili upate kustawi katika yote ufanyayo na popote uendako,
And kepe thou the kepyngis and heestis of thi Lord God, that thou go in hise weies, and kepe hise cerymonyes, and hise heestis, and hise domes, and witnessyngis, as it is writun in the lawe of Moises; that thou vndurstonde alle thingis whiche thou doist, and whidur euer thou schalt turne thee.
4 ili kwamba Bwana aweze kunitimizia ahadi yake: ‘Kama wazao wako wakiangalia sana wanavyoishi, na kama wakienenda kwa uaminifu mbele zangu kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote, kamwe hutakosa kuwa na mtu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’
That the Lord conferme hise wordis, whiche the Lord spak of me, and seide, If thi sones kepen my weies, and goen bifor me in treuthe, in al her herte, and in al her soule, a man schal not be takun awei of thee fro the trone of Israel.
5 “Sasa wewe mwenyewe unafahamu lile Yoabu mwana wa Seruya alilonitendea, lile alilofanya kwa majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yetheri. Aliwaua, akimwaga damu yao wakati wa amani kama vile ni kwenye vita, tena akaipaka damu ile kwenye mkanda uliokuwa kiunoni mwake na viatu alivyovaa miguuni mwake.
Also thou knowist what thingis Joab, the sone of Saruye, dide to me; what thingis he dide to twey princis of the oost of Israel, to Abner, sone of Ner, and to Amasa, sone of Jether, whiche he killide, and schedde the blood of batel in pees; and puttide the blood of batel in his girdil, that was aboute hise leendis, and in his scho, that was in hise feet.
6 Shughulika naye kwa kadiri ya hekima yako, lakini usiache kichwa chake chenye mvi kishukie kaburi kwa amani. (Sheol h7585)
Therfor thou schalt do by thi wisdom, and thou schalt not lede forth his hoornesse pesibli to hellis. (Sheol h7585)
7 “Lakini uwaonyeshe wema wana wa Barzilai wa Gileadi na uwaruhusu wawe miongoni mwa wale walao mezani pako. Walisimama nami nilipomkimbia ndugu yako Absalomu.
But also thou schalt yelde grace to the sones of Bersellai of Galaad, and thei schulen be eetynge in thi boord; for thei metten me, whanne Y fledde fro the face of Absolon, thi brother.
8 “Ukumbuke, unaye Shimei mwana wa Gera, Mbenyamini kutoka Bahurimu, ambaye alinilaani kwa laana kali siku niliyokwenda Mahanaimu. Aliposhuka kunilaki huko Yordani, nilimwapia kwa Bwana: ‘Sitakuua kwa upanga!’
Also thou hast anentis thee Semey, sone of Gera, sone of Gemyny, of Bahurym, which Semei curside me bi the worste cursyng, whanne Y yede to `the castels; but for he cam doun to me in to metyng, whanne Y passide Jordan, and Y swoor to him bi the Lord, and seide, Y schal not slee thee bi swerd,
9 Lakini sasa, usidhani kwamba hana hatia. Wewe ni mtu wa hekima, utajua la kumtendea. Zishushe mvi zake kaburini kwa damu.” (Sheol h7585)
nyle thou suffre hym to be vnpunyschid; forsothe thou art a wise man, and thou schalt wite what thou schalt do to hym, and thou schalt lede forth hise hoor heeris with blood to hellis. (Sheol h7585)
10 Kisha Daudi akapumzika pamoja na baba zake naye akazikwa katika Mji wa Daudi.
Sotheli Dauid slepte with hise fadris, and was biriede in the citee of Dauid.
11 Daudi alikuwa ametawala juu ya Israeli miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
Forsothe the daies, in whiche Dauid regnede on Israel, ben fourti yeer; in Ebron he regned seuene yeer, in Jerusalem thre and thretti yeer.
12 Kwa hiyo Solomoni akaketi katika kiti cha ufalme cha baba yake Daudi, nao utawala wake ukaimarika sana.
Forsothe Salomon sat on the trone of Dauid, his fadir, and his rewme was maad stidfast greetli.
13 Basi Adoniya, mwana wa Hagithi, akaenda kwa Bathsheba, mama yake Solomoni. Bathsheba akamuuliza, “Je, umekuja kwa amani?” Akajibu, “Ndiyo, kwa amani.”
And Adonye, sone of Agith, entride to Bersabee, modir of Salomon; and sche seide to hym, Whether thin entryng is pesible? And he answeride, It is pesible.
14 Kisha akaongeza, “Ninalo jambo la kukuambia.” Akajibu, “Waweza kulisema.”
And he addide, A word of me is to thee. `To whom sche seide, Speke thou.
15 Akasema, “Kama unavyojua, ufalme ulikuwa wangu. Israeli wote waliniangalia mimi kama mfalme wao. Lakini mambo yalibadilika, ufalme umekwenda kwa ndugu yangu, kwa maana umemjia kutoka kwa Bwana.
And he seide, Thou knowist that the rewme was myn, and al Israel purposide to make me in to king to hem; but the rewme is translatid, and is maad my brotheris; for of the Lord it is ordeyned to hym.
16 Sasa ninalo ombi moja ninalokuomba. Usinikatalie.” Bathsheba akasema, “Waweza kuliomba.”
Now therfor Y preye of the oon axyng; schende thou not my face. And sche seide to hym, Speke thou. And he seide, Y preie,
17 Kwa hiyo akaendelea kusema, “Tafadhali mwombe Mfalme Solomoni, anipatie Abishagi, Mshunami, awe mke wangu; hatakukatalia wewe.”
that thou seie to Salomon the king; for he may not denye ony thing to thee; that he yyue to me Abisag of Sunam wijf.
18 Bathsheba akamjibu, “Vema sana, nitazungumza na mfalme kwa ajili yako.”
And Bersabee seide, Wel, Y schal speke for thee to the kyng.
19 Bathsheba alipokwenda kwa Mfalme Solomoni kuzungumza naye kwa ajili ya Adoniya, mfalme alisimama kumlaki mama yake, akamwinamia na kuketi kwenye kiti chake cha ufalme. Akaamuru kiti cha ufalme kuletwa kwa ajili ya mama yake mfalme, naye akaketi mkono wake wa kuume.
Therfor Bersabee cam to kyng Salomon, to speke to hym for Adonye; and the kyng roos ayens the comyng of hir, and worschipide hir, and `sat on his trone; and a trone was set to the modir of the kyng, and sche sat at his riyt side.
20 Bathsheba akamwambia mfalme, “Ninalo ombi moja dogo la kukuomba; usinikatalie.” Mfalme akajibu, “Omba, mama yangu; sitakukatalia.”
And sche seide to hym, Y preie of thee o litil axyng; schende thou not my face. And the kyng seide to hir, My modir, axe thou; for it is not leueful that Y turne awei thi face.
21 Akasema, “Mruhusu Abishagi, Mshunami, aolewe na ndugu yako Adoniya.”
And sche seide, Abisag of Sunam be youun wijf to Adonye, thi brother.
22 Mfalme Solomoni akamjibu mama yake, “Kwa nini uombe Abishagi, Mshunami, kwa ajili ya Adoniya? Ungeweza pia kuomba ufalme kwa ajili yake, kwani yeye ni ndugu yangu mkubwa: naam, kwa ajili yake, na kwa kuhani Abiathari na Yoabu mwana wa Seruya!”
And kyng Salomon answeride, and seide to his modir, Whi axist thou Abisag of Sunam to Adonye? Axe thou to hym also the rewme; for he is `my gretter brothir, and he hath Abiathar, preest, and Joab, sone of Saruye.
23 Mfalme Solomoni akaapa kwa Bwana, akasema: “Mungu na aniulie mbali, tena bila huruma, ikiwa Adoniya hatalipa kwa uhai wake kwa ajili ya ombi hili!
Therfor kyng Salomon swoor bi the Lord, and seide, God do to me these thingis, and adde these thinges, for Adonie spak this word ayens his lijf.
24 Basi sasa, hakika kama Bwana aishivyo, yeye ambaye ameniimarisha salama kwenye kiti cha ufalme cha Daudi baba yangu, naye amenipa ufalme wa kudumu kama alivyoahidi, Adoniya atauawa leo!”
And now the Lord lyueth, that confermede me, and hath set me on the trone of my fadir, and that hath maad to me an hows, as he spak, for Adonye schal be slayn to dai.
25 Hivyo Mfalme Solomoni akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akampiga Adoniya akafa.
And kyng Salomon sente bi the hond of Banaie, sone of Joiada; which Banaie killide Adonye, and he was deed.
26 Mfalme akamwambia kuhani Abiathari, “Nenda huko Anathothi katika mashamba yako. Wewe unastahili kufa, lakini sitakuua sasa, kwa sababu ulilichukua Sanduku la Bwana Mwenyezi mbele ya Daudi baba yangu na ulishiriki taabu zote za baba yangu.”
Also the kyng seide to Abiathar, preest, Go thou in to Anatot, to thi feeld; and sotheli thou art a man of deeth, `that is, worthi the deeth, for conspiryng ayens me, and the ordynaunce of God, and of my fadir; but to dai Y schal not sle thee, for thou barist the arke of the Lord God bifor Dauid, my fadir, and thou suffridist trauele in alle thingis, in whiche my fadir trauelide.
27 Hivyo Solomoni akamwondoa Abiathari kwenye ukuhani wa Bwana, akilitimiza neno la Bwana alilokuwa amenena huko Shilo kuhusu nyumba ya Eli.
Therfor Salomon puttide out Abiathar, that he schulde not be preest of the Lord, that the word of the Lord were fillid, which he spak on the hows of Heli, in Silo.
28 Habari zilipomfikia Yoabu, ambaye alikuwa amefanya shauri baya na Adoniya, lakini sio na Absalomu, alikimbilia kwenye hema la Bwana na kushika pembe za madhabahu.
Forsothe a messager cam to Salomon, that Joab hadde bowid aftir Adonye, and that he hadde not bowid after Salomon. Therfor Joab fledde in to the tabernacle of the Lord, and took the horn of the auter.
29 Mfalme Solomoni akaambiwa kuwa Yoabu amekimbilia kwenye hema la Bwana naye alikuwa kando ya madhabahu. Basi Solomoni akamwagiza Benaya mwana wa Yehoyada: “Nenda ukamuue!”
And it was teld to kyng Salomon, that Joab hadde fledde in to the tabernacle of the Lord, and was bisidis the auter; and Salomon sente Banaie, sone of Joiada, and seide, Go thou, and sle hym.
30 Ndipo Benaya akaingia kwenye hema la Bwana na kumwambia Yoabu, “Mfalme anasema, ‘Toka nje!’” Lakini akajibu, “La! Nitafia hapa hapa.” Benaya akamwarifu mfalme, “Hivi ndivyo Yoabu alivyonijibu.”
And Banaie cam to the tabernacle of the Lord, and seide to Joab, The kyng seith these thingis, Go thou out. And he seide, Y schal not go out, but Y schal die here. Banaie telde the word to the kyng, and seide, Joab spak thes thingis, and answeride these thingis to me.
31 Kisha mfalme akamwamuru Benaya, “Fanya kama asemavyo. Muue na kumzika, ili uniondolee mimi na nyumba ya baba yangu dhambi ya damu isiyokuwa na hatia ile Yoabu aliyoimwaga.
And the kyng seide to Banaie, Do thou as he spak, and sle thou hym, and birie him; and thou schalt remoue the innocent blood, that was sched out of Joab, fro me, and fro the hows of my fadir.
32 Bwana atamlipiza kwa ajili ya damu aliyoimwaga, kwa sababu pasipo Daudi baba yangu kujua, aliwashambulia watu wawili na kuwaua kwa upanga. Wote wawili, Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Israeli, na Amasa mwana wa Yetheri, jemadari wa jeshi la Yuda, walikuwa watu wazuri na wanyofu kuliko yeye.
And the Lord yelde on his heed his blood, for he killide twei iust men, and betere than hym silf, and he killide hem bi swerd, while Dauid, my fadir, `wiste not, Abner, the sone of Ner, the prince of the chyualrie of Israel, and Amasa, sone of Jether, the prince of the oost of Juda.
33 Hatia ya damu yao na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na wazao wake milele. Lakini kwa Daudi na uzao wake, nyumba yake na kiti chake cha ufalme, iwepo amani ya Bwana milele.”
And the blood of hem schal turne ayen in to the heed of Joab, and in to the heed of his seed with outen ende; forsothe pees be of the Lord til in to with outen ende to Dauid, and to his seed, and to the hous and trone of hym.
34 Basi Benaya mwana wa Yehoyada akakwea, akampiga na kumuua Yoabu, naye akazikwa katika nchi yake mwenyewe katika jangwa.
Therfor Banaie, sone of Joiada, stiede, and asailide, and killide Joab; and Joab was biried in his hows in deseert.
35 Mfalme akamweka Benaya mwana wa Yehoyada juu ya jeshi kwenye nafasi ya Yoabu na kumweka kuhani Sadoki badala ya Abiathari.
And the kyng ordeynede Banaie, sone of Joiada, on the oost for hym; and the kyng puttide Sadoch preest for Abiathar.
36 Kisha mfalme akatuma ujumbe kwa Shimei na kumwambia, “Ujijengee nyumba huko Yerusalemu uishi huko, lakini usiende mahali pengine popote.
Also the kyng sente, and clepide Semey, and seide to hym, Bilde to thee an hows in Jerusalem, and dwelle thou there, and thou schalt not go out fro thennus hidur and thidur;
37 Siku utakayoondoka kuvuka Bonde la Kidroni, uwe na hakika utakufa; damu yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.”
sotheli in what euer dai thou goist out, and passist the stronde of Cedron, wite thou thee worthi to be slayn; thi blood schal be on thin heed.
38 Shimei akamjibu mfalme, “Ulilolisema ni jema. Mtumishi wako atatenda kama bwana wangu mfalme alivyosema.” Naye Shimei akakaa Yerusalemu kwa muda mrefu.
And Semei seide to the kyng, The word of the kyng is good; as my lord the kyng spak, so thi seruaunt schal do. Therfor Semey dwellide in Jerusalem in many daies.
39 Lakini baada ya miaka mitatu, watumwa wawili wa Shimei wakatoroka kwenda kwa Akishi mwana wa Maaka, mfalme wa Gathi, naye Shimei akaambiwa, “Watumwa wako wako Gathi.”
Forsothe it was doon after thre yeer, that the seruauntis of Semei fledden to Achis, sone of Maacha, the kyng of Geth; and it was teld to Semey, that hise seruauntis hadden go in to Geth.
40 Kwa ajili ya hili, Shimei akatandika punda wake, akaenda kwa Akishi huko Gathi kuwatafuta watumwa wake. Basi Shimei akaondoka na kuwarudisha watumwa wake kutoka Gathi.
And Semey roos, and sadlide his asse, and yede to Achis, in to Geth, to seke hise seruauntis; and brouyte hem ayen fro Geth.
41 Solomoni alipoambiwa kuwa Shimei ametoka Yerusalemu na kwenda Gathi na amekwisha kurudi,
Forsothe it was teld to kyng Salomon, that Semey hadde go to Geth fro Jerusalem, and hadde come ayen.
42 mfalme akamwita Shimei na kumwambia, “Je, sikukuapiza kwa Bwana na kukuonya kuwa, ‘Siku utakayoondoka kwenda mahali pengine popote, uwe na hakika utakufa?’ Wakati ule uliniambia, ‘Ulilolisema ni jema. Nitatii!’
And Salomon sente, and clepide hym, and seide to hym, Whether Y witnessede not to thee bi the Lord, and bifor seide to thee, In what euer dai thou schalt go out hidur and thidur, wite thou that thou schalt die; and thou answeridist to me, The word is good, which Y herde?
43 Kwa nini basi hukutunza kiapo chako kwa Bwana na kutii amri niliyokupa?”
Whi therfor keptist thou not the ooth of the Lord, and the comaundement which Y comaundide to thee?
44 Pia mfalme akamwambia Shimei, “Unajua katika moyo wako makosa uliyomtendea baba yangu Daudi. Sasa Bwana atakulipiza kwa ajili ya mabaya yako uliyotenda.
And the kyng seide to Semei, Thou knowist al the yuel, of which thin herte is gilti to thee, which yuel thou didist to my fadir; the Lord hath yolde thi malice in to thin heed.
45 Lakini Mfalme Solomoni atabarikiwa, na kiti cha ufalme cha Daudi kitakuwa imara mbele za Bwana milele.”
And kyng Salomon schal be blessid; and the trone of Dauid schal be stable bifor the Lord til in to with outen ende.
46 Kisha mfalme akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akatoka nje, akampiga Shimei na kumuua. Sasa ufalme ukawa umeimarika kikamilifu mikononi mwa Solomoni.
Therfor the kyng comaundide to Banaie, sone of Joiada; and he assailide, and smoot Semey, and he was deed.

< 1 Wafalme 2 >