< 1 Wafalme 2 >

1 Siku zilipokaribia za Daudi kufa, akampa mwanawe Solomoni agizo.
and to present: come day David to/for to die and to command [obj] Solomon son: child his to/for to say
2 Akasema, “Mimi ninakaribia kwenda njia ya dunia yote. Hivyo uwe hodari, jionyeshe kuwa mwanaume,
I to go: went in/on/with way: journey all [the] land: country/planet and to strengthen: strengthen and to be to/for man
3 shika lile Bwana Mungu wako analokuagiza: Enenda katika njia zake, ushike maagizo na amri zake, sheria zake na kanuni zake, kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, ili upate kustawi katika yote ufanyayo na popote uendako,
and to keep: obey [obj] charge LORD God your to/for to go: walk in/on/with way: conduct his to/for to keep: obey statute his commandment his and justice: judgement his and testimony his like/as to write in/on/with instruction Moses because be prudent [obj] all which to make: do and [obj] all which to turn there
4 ili kwamba Bwana aweze kunitimizia ahadi yake: ‘Kama wazao wako wakiangalia sana wanavyoishi, na kama wakienenda kwa uaminifu mbele zangu kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote, kamwe hutakosa kuwa na mtu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’
because to arise: establish LORD [obj] word his which to speak: speak upon me to/for to say if to keep: look at son: descendant/people your [obj] way: conduct their to/for to go: walk to/for face: before my in/on/with truth: faithful in/on/with all heart their and in/on/with all soul their to/for to say not to cut: lack to/for you man from upon throne Israel
5 “Sasa wewe mwenyewe unafahamu lile Yoabu mwana wa Seruya alilonitendea, lile alilofanya kwa majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yetheri. Aliwaua, akimwaga damu yao wakati wa amani kama vile ni kwenye vita, tena akaipaka damu ile kwenye mkanda uliokuwa kiunoni mwake na viatu alivyovaa miguuni mwake.
and also you(m. s.) to know [obj] which to make: do to/for me Joab son: child Zeruiah which to make: do to/for two ruler army Israel to/for Abner son: child Ner and to/for Amasa son: child Jether and to kill them and to set: put blood battle in/on/with peace and to give: put blood battle in/on/with belt his which in/on/with loin his and in/on/with sandal his which in/on/with foot his
6 Shughulika naye kwa kadiri ya hekima yako, lakini usiache kichwa chake chenye mvi kishukie kaburi kwa amani. (Sheol h7585)
and to make: do like/as wisdom your and not to go down greyheaded his in/on/with peace hell: Sheol (Sheol h7585)
7 “Lakini uwaonyeshe wema wana wa Barzilai wa Gileadi na uwaruhusu wawe miongoni mwa wale walao mezani pako. Walisimama nami nilipomkimbia ndugu yako Absalomu.
and to/for son: child Barzillai [the] Gileadite to make: do kindness and to be in/on/with to eat table your for so to present: come to(wards) me in/on/with to flee I from face: before Absalom brother: male-sibling your
8 “Ukumbuke, unaye Shimei mwana wa Gera, Mbenyamini kutoka Bahurimu, ambaye alinilaani kwa laana kali siku niliyokwenda Mahanaimu. Aliposhuka kunilaki huko Yordani, nilimwapia kwa Bwana: ‘Sitakuua kwa upanga!’
and behold with you Shimei son: child Gera Benjaminite [the] Benjaminite from Bahurim and he/she/it to lighten me curse be sick in/on/with day to go: went I Mahanaim and he/she/it to go down to/for to encounter: meet me [the] Jordan and to swear to/for him in/on/with LORD to/for to say if: surely no to die you in/on/with sword
9 Lakini sasa, usidhani kwamba hana hatia. Wewe ni mtu wa hekima, utajua la kumtendea. Zishushe mvi zake kaburini kwa damu.” (Sheol h7585)
and now not to clear him for man wise you(m. s.) and to know [obj] which to make: do to/for him and to go down [obj] greyheaded his in/on/with blood hell: Sheol (Sheol h7585)
10 Kisha Daudi akapumzika pamoja na baba zake naye akazikwa katika Mji wa Daudi.
and to lie down: be dead David with father his and to bury in/on/with city David
11 Daudi alikuwa ametawala juu ya Israeli miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
and [the] day which to reign David upon Israel forty year in/on/with Hebron to reign seven year and in/on/with Jerusalem to reign thirty and three year
12 Kwa hiyo Solomoni akaketi katika kiti cha ufalme cha baba yake Daudi, nao utawala wake ukaimarika sana.
and Solomon to dwell upon throne David father his and to establish: establish royalty his much
13 Basi Adoniya, mwana wa Hagithi, akaenda kwa Bathsheba, mama yake Solomoni. Bathsheba akamuuliza, “Je, umekuja kwa amani?” Akajibu, “Ndiyo, kwa amani.”
and to come (in): come Adonijah son: child Haggith to(wards) Bathsheba Bathsheba mother Solomon and to say peace to come (in): come you and to say peace
14 Kisha akaongeza, “Ninalo jambo la kukuambia.” Akajibu, “Waweza kulisema.”
and to say word: speaking to/for me to(wards) you and to say to speak: speak
15 Akasema, “Kama unavyojua, ufalme ulikuwa wangu. Israeli wote waliniangalia mimi kama mfalme wao. Lakini mambo yalibadilika, ufalme umekwenda kwa ndugu yangu, kwa maana umemjia kutoka kwa Bwana.
and to say you(f. s.) to know for to/for me to be [the] kingship and upon me to set: consider all Israel face their to/for to reign and to turn: turn [the] kingship and to be to/for brother: male-sibling my for from LORD to be to/for him
16 Sasa ninalo ombi moja ninalokuomba. Usinikatalie.” Bathsheba akasema, “Waweza kuliomba.”
and now petition one I to ask from with you not to return: refuse [obj] face: before my and to say to(wards) him to speak: speak
17 Kwa hiyo akaendelea kusema, “Tafadhali mwombe Mfalme Solomoni, anipatie Abishagi, Mshunami, awe mke wangu; hatakukatalia wewe.”
and to say to say please to/for Solomon [the] king for not to return: refuse [obj] face: before your and to give: give to/for me [obj] Abishag [the] Shunammites to/for woman: wife
18 Bathsheba akamjibu, “Vema sana, nitazungumza na mfalme kwa ajili yako.”
and to say Bathsheba Bathsheba pleasant I to speak: speak upon you to(wards) [the] king
19 Bathsheba alipokwenda kwa Mfalme Solomoni kuzungumza naye kwa ajili ya Adoniya, mfalme alisimama kumlaki mama yake, akamwinamia na kuketi kwenye kiti chake cha ufalme. Akaamuru kiti cha ufalme kuletwa kwa ajili ya mama yake mfalme, naye akaketi mkono wake wa kuume.
and to come (in): come Bathsheba Bathsheba to(wards) [the] king Solomon to/for to speak: speak to/for him upon Adonijah and to arise: rise [the] king to/for to encounter: meet her and to bow to/for her and to dwell upon throne his and to set: put throne to/for mother [the] king and to dwell to/for right his
20 Bathsheba akamwambia mfalme, “Ninalo ombi moja dogo la kukuomba; usinikatalie.” Mfalme akajibu, “Omba, mama yangu; sitakukatalia.”
and to say petition one small I to ask from with you not to return: refuse [obj] face: before my and to say to/for her [the] king to ask mother my for not to return: refuse [obj] face: before your
21 Akasema, “Mruhusu Abishagi, Mshunami, aolewe na ndugu yako Adoniya.”
and to say to give: give(marriage) [obj] Abishag [the] Shunammites to/for Adonijah brother: male-sibling your to/for woman: wife
22 Mfalme Solomoni akamjibu mama yake, “Kwa nini uombe Abishagi, Mshunami, kwa ajili ya Adoniya? Ungeweza pia kuomba ufalme kwa ajili yake, kwani yeye ni ndugu yangu mkubwa: naam, kwa ajili yake, na kwa kuhani Abiathari na Yoabu mwana wa Seruya!”
and to answer [the] king Solomon and to say to/for mother his and to/for what? you(f. s.) to ask [obj] Abishag [the] Shunammites to/for Adonijah and to ask to/for him [obj] [the] kingship for he/she/it brother: male-sibling my [the] great: old from me and to/for him and to/for Abiathar [the] priest and to/for Joab son: child Zeruiah
23 Mfalme Solomoni akaapa kwa Bwana, akasema: “Mungu na aniulie mbali, tena bila huruma, ikiwa Adoniya hatalipa kwa uhai wake kwa ajili ya ombi hili!
and to swear [the] king Solomon in/on/with LORD to/for to say thus to make: do to/for me God and thus to add for in/on/with soul: life his to speak: speak Adonijah [obj] [the] word [the] this
24 Basi sasa, hakika kama Bwana aishivyo, yeye ambaye ameniimarisha salama kwenye kiti cha ufalme cha Daudi baba yangu, naye amenipa ufalme wa kudumu kama alivyoahidi, Adoniya atauawa leo!”
and now alive LORD which to establish: establish me (and to dwell me *Q(k)*) upon throne David father my and which to make to/for me house: home like/as as which to speak: promise for [the] day to die Adonijah
25 Hivyo Mfalme Solomoni akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akampiga Adoniya akafa.
and to send: depart [the] king Solomon in/on/with hand: by Benaiah son: child Jehoiada and to fall on in/on/with him and to die
26 Mfalme akamwambia kuhani Abiathari, “Nenda huko Anathothi katika mashamba yako. Wewe unastahili kufa, lakini sitakuua sasa, kwa sababu ulilichukua Sanduku la Bwana Mwenyezi mbele ya Daudi baba yangu na ulishiriki taabu zote za baba yangu.”
and to/for Abiathar [the] priest to say [the] king Anathoth to go: went upon land: country your for man death you(m. s.) and in/on/with day: today [the] this not to die you for to lift: bear [obj] ark Lord YHWH/God to/for face: before David father my and for to afflict in/on/with all which to afflict father my
27 Hivyo Solomoni akamwondoa Abiathari kwenye ukuhani wa Bwana, akilitimiza neno la Bwana alilokuwa amenena huko Shilo kuhusu nyumba ya Eli.
and to drive out: drive out Solomon [obj] Abiathar from to be priest to/for LORD to/for to fill [obj] word LORD which to speak: speak upon house: household Eli in/on/with Shiloh
28 Habari zilipomfikia Yoabu, ambaye alikuwa amefanya shauri baya na Adoniya, lakini sio na Absalomu, alikimbilia kwenye hema la Bwana na kushika pembe za madhabahu.
and [the] tidings to come (in): come till Joab for Joab to stretch after Adonijah and after Absalom not to stretch and to flee Joab to(wards) tent LORD and to strengthen: hold in/on/with horn [the] altar
29 Mfalme Solomoni akaambiwa kuwa Yoabu amekimbilia kwenye hema la Bwana naye alikuwa kando ya madhabahu. Basi Solomoni akamwagiza Benaya mwana wa Yehoyada: “Nenda ukamuue!”
and to tell to/for king Solomon for to flee Joab to(wards) tent LORD and behold beside [the] altar and to send: depart Solomon [obj] Benaiah son: child Jehoiada to/for to say to go: went to fall on in/on/with him
30 Ndipo Benaya akaingia kwenye hema la Bwana na kumwambia Yoabu, “Mfalme anasema, ‘Toka nje!’” Lakini akajibu, “La! Nitafia hapa hapa.” Benaya akamwarifu mfalme, “Hivi ndivyo Yoabu alivyonijibu.”
and to come (in): come Benaiah to(wards) tent LORD and to say to(wards) him thus to say [the] king to come out: come and to say not for here to die and to return: return Benaiah [obj] [the] king word to/for to say thus to speak: speak Joab and thus to answer me
31 Kisha mfalme akamwamuru Benaya, “Fanya kama asemavyo. Muue na kumzika, ili uniondolee mimi na nyumba ya baba yangu dhambi ya damu isiyokuwa na hatia ile Yoabu aliyoimwaga.
and to say to/for him [the] king to make: do like/as as which to speak: speak and to fall on in/on/with him and to bury him and to turn aside: remove blood for nothing which to pour: kill Joab from upon me and from upon house: household father my
32 Bwana atamlipiza kwa ajili ya damu aliyoimwaga, kwa sababu pasipo Daudi baba yangu kujua, aliwashambulia watu wawili na kuwaua kwa upanga. Wote wawili, Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Israeli, na Amasa mwana wa Yetheri, jemadari wa jeshi la Yuda, walikuwa watu wazuri na wanyofu kuliko yeye.
and to return: return LORD [obj] blood his upon head his which to fall on in/on/with two human righteous and pleasant from him and to kill them in/on/with sword and father my David not to know [obj] Abner son: child Ner ruler army Israel and [obj] Amasa son: child Jether ruler army Judah
33 Hatia ya damu yao na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na wazao wake milele. Lakini kwa Daudi na uzao wake, nyumba yake na kiti chake cha ufalme, iwepo amani ya Bwana milele.”
and to return: return blood their in/on/with head Joab and in/on/with head seed: children his to/for forever: enduring and to/for David and to/for seed: children his and to/for house: household his and to/for throne his to be peace till forever: enduring from from with LORD
34 Basi Benaya mwana wa Yehoyada akakwea, akampiga na kumuua Yoabu, naye akazikwa katika nchi yake mwenyewe katika jangwa.
and to ascend: rise Benaiah son: child Jehoiada and to fall on in/on/with him and to die him and to bury in/on/with house: home his in/on/with wilderness
35 Mfalme akamweka Benaya mwana wa Yehoyada juu ya jeshi kwenye nafasi ya Yoabu na kumweka kuhani Sadoki badala ya Abiathari.
and to give: put [the] king [obj] Benaiah son: child Jehoiada underneath: instead him upon [the] army and [obj] Zadok [the] priest to give: put [the] king underneath: instead Abiathar
36 Kisha mfalme akatuma ujumbe kwa Shimei na kumwambia, “Ujijengee nyumba huko Yerusalemu uishi huko, lakini usiende mahali pengine popote.
and to send: depart [the] king and to call: call to to/for Shimei and to say to/for him to build to/for you house: home in/on/with Jerusalem and to dwell there and not to come out: come from there where? and where?
37 Siku utakayoondoka kuvuka Bonde la Kidroni, uwe na hakika utakufa; damu yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.”
and to be in/on/with day to come out: come you and to pass [obj] torrent: valley Kidron to know to know for to die to die blood your to be in/on/with head your
38 Shimei akamjibu mfalme, “Ulilolisema ni jema. Mtumishi wako atatenda kama bwana wangu mfalme alivyosema.” Naye Shimei akakaa Yerusalemu kwa muda mrefu.
and to say Shimei to/for king pleasant [the] word: speaking like/as as which to speak: speak lord my [the] king so to make: do servant/slave your and to dwell Shimei in/on/with Jerusalem day many
39 Lakini baada ya miaka mitatu, watumwa wawili wa Shimei wakatoroka kwenda kwa Akishi mwana wa Maaka, mfalme wa Gathi, naye Shimei akaambiwa, “Watumwa wako wako Gathi.”
and to be from end three year and to flee two servant/slave to/for Shimei to(wards) Achish son: child Maacah king Gath and to tell to/for Shimei to/for to say behold servant/slave your in/on/with Gath
40 Kwa ajili ya hili, Shimei akatandika punda wake, akaenda kwa Akishi huko Gathi kuwatafuta watumwa wake. Basi Shimei akaondoka na kuwarudisha watumwa wake kutoka Gathi.
and to arise: rise Shimei and to saddle/tie [obj] donkey his and to go: went Gath [to] to(wards) Achish to/for to seek [obj] servant/slave his and to go: went Shimei and to come (in): bring [obj] servant/slave his from Gath
41 Solomoni alipoambiwa kuwa Shimei ametoka Yerusalemu na kwenda Gathi na amekwisha kurudi,
and to tell to/for Solomon for to go: went Shimei from Jerusalem Gath and to return: return
42 mfalme akamwita Shimei na kumwambia, “Je, sikukuapiza kwa Bwana na kukuonya kuwa, ‘Siku utakayoondoka kwenda mahali pengine popote, uwe na hakika utakufa?’ Wakati ule uliniambia, ‘Ulilolisema ni jema. Nitatii!’
and to send: depart [the] king and to call: call to to/for Shimei and to say to(wards) him not to swear you in/on/with LORD and to testify in/on/with you to/for to say in/on/with day to come out: come you and to go: went where? and where? to know to know for to die to die and to say to(wards) me pleasant [the] word: speaking to hear: obey
43 Kwa nini basi hukutunza kiapo chako kwa Bwana na kutii amri niliyokupa?”
and why? not to keep: obey [obj] oath LORD and [obj] [the] commandment which to command upon you
44 Pia mfalme akamwambia Shimei, “Unajua katika moyo wako makosa uliyomtendea baba yangu Daudi. Sasa Bwana atakulipiza kwa ajili ya mabaya yako uliyotenda.
and to say [the] king to(wards) Shimei you(m. s.) to know [obj] all [the] distress: harm which to know heart your which to make: do to/for David father my and to return: return LORD [obj] distress: harm your in/on/with head your
45 Lakini Mfalme Solomoni atabarikiwa, na kiti cha ufalme cha Daudi kitakuwa imara mbele za Bwana milele.”
and [the] king Solomon to bless and throne David to be to establish: establish to/for face: before LORD till forever: enduring
46 Kisha mfalme akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akatoka nje, akampiga Shimei na kumuua. Sasa ufalme ukawa umeimarika kikamilifu mikononi mwa Solomoni.
and to command [the] king [obj] Benaiah son: child Jehoiada and to come out: come and to fall on in/on/with him and to die and [the] kingdom to establish: establish in/on/with hand: power Solomon

< 1 Wafalme 2 >