< 1 Wafalme 2 >

1 Siku zilipokaribia za Daudi kufa, akampa mwanawe Solomoni agizo.
Now the days of David had drawn near, so that he would die, and he instructed his son Solomon, saying:
2 Akasema, “Mimi ninakaribia kwenda njia ya dunia yote. Hivyo uwe hodari, jionyeshe kuwa mwanaume,
“I am entering the way of all the earth. Be strengthened and be a good man.
3 shika lile Bwana Mungu wako analokuagiza: Enenda katika njia zake, ushike maagizo na amri zake, sheria zake na kanuni zake, kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, ili upate kustawi katika yote ufanyayo na popote uendako,
And observe the care of the Lord your God, so that you walk in his ways, so that you care for his ceremonies, and his precepts, and judgments, and testimonies, just as it is written in the law of Moses. So may you understand everything that you do, in any direction that you may turn yourself.
4 ili kwamba Bwana aweze kunitimizia ahadi yake: ‘Kama wazao wako wakiangalia sana wanavyoishi, na kama wakienenda kwa uaminifu mbele zangu kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote, kamwe hutakosa kuwa na mtu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’
So may the Lord confirm his words, which he has spoken about me, saying: ‘If your sons will guard their ways, and if they will walk before me in truth, with all their heart and with all their soul, there shall not be taken away from you a man on the throne of Israel.’
5 “Sasa wewe mwenyewe unafahamu lile Yoabu mwana wa Seruya alilonitendea, lile alilofanya kwa majemadari wawili wa majeshi ya Israeli, Abneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yetheri. Aliwaua, akimwaga damu yao wakati wa amani kama vile ni kwenye vita, tena akaipaka damu ile kwenye mkanda uliokuwa kiunoni mwake na viatu alivyovaa miguuni mwake.
Also, you know what Joab, the son of Zeruiah, has done to me, what he did to the two leaders of the army of Israel, to Abner, the son of Ner, and to Amasa, the son of Jether. He killed them, and so he shed the blood of war in peace time, and he set the bloodshed of battle on his belt, which was around his waist, and in his shoes, which were on his feet.
6 Shughulika naye kwa kadiri ya hekima yako, lakini usiache kichwa chake chenye mvi kishukie kaburi kwa amani. (Sheol h7585)
Therefore, act according to your wisdom. And you shall not allow his gray head to be led away to death in peace. (Sheol h7585)
7 “Lakini uwaonyeshe wema wana wa Barzilai wa Gileadi na uwaruhusu wawe miongoni mwa wale walao mezani pako. Walisimama nami nilipomkimbia ndugu yako Absalomu.
Then, too, repay grace to the sons of Barzillai the Gileadite. And you shall allow them to eat at your table. For they met me when I fled from the face of Absalom, your brother.
8 “Ukumbuke, unaye Shimei mwana wa Gera, Mbenyamini kutoka Bahurimu, ambaye alinilaani kwa laana kali siku niliyokwenda Mahanaimu. Aliposhuka kunilaki huko Yordani, nilimwapia kwa Bwana: ‘Sitakuua kwa upanga!’
Also, you have with you Shimei, the son of Gera, the son of Benjamin, from Bahurim, who cursed me with a grievous curse, when I went away to the camp. And he descended to meet me when I crossed over the Jordan, and I swore to him by the Lord, saying, ‘I will not put you to death by the sword,’
9 Lakini sasa, usidhani kwamba hana hatia. Wewe ni mtu wa hekima, utajua la kumtendea. Zishushe mvi zake kaburini kwa damu.” (Sheol h7585)
yet do not choose to treat him as if he were innocent. Since you are a wise man, you will know what to do with him. And you shall lead away his grey hair to death with blood.” (Sheol h7585)
10 Kisha Daudi akapumzika pamoja na baba zake naye akazikwa katika Mji wa Daudi.
And so, David slept with his fathers, and he was buried in the city of David.
11 Daudi alikuwa ametawala juu ya Israeli miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
Now the days during which David reigned over Israel are forty years: he reigned seven years in Hebron, thirty-three in Jerusalem.
12 Kwa hiyo Solomoni akaketi katika kiti cha ufalme cha baba yake Daudi, nao utawala wake ukaimarika sana.
Then Solomon sat upon the throne of his father David, and his kingdom was strengthened exceedingly.
13 Basi Adoniya, mwana wa Hagithi, akaenda kwa Bathsheba, mama yake Solomoni. Bathsheba akamuuliza, “Je, umekuja kwa amani?” Akajibu, “Ndiyo, kwa amani.”
And Adonijah, the son of Haggith, entered to Bathsheba, the mother of Solomon. And she said to him, “Is your entrance peaceful?” He responded, “It is peaceful.”
14 Kisha akaongeza, “Ninalo jambo la kukuambia.” Akajibu, “Waweza kulisema.”
And he added, “My word is for you.” She said to him, “Speak.” And he said:
15 Akasema, “Kama unavyojua, ufalme ulikuwa wangu. Israeli wote waliniangalia mimi kama mfalme wao. Lakini mambo yalibadilika, ufalme umekwenda kwa ndugu yangu, kwa maana umemjia kutoka kwa Bwana.
“You know that the kingdom was mine, and that all of Israel had preferred me for themselves as king. But the kingdom was transferred, and has become my brother’s. For it was appointed to him by the Lord.
16 Sasa ninalo ombi moja ninalokuomba. Usinikatalie.” Bathsheba akasema, “Waweza kuliomba.”
Now therefore, I beg of you one petition. May you not confound my face.” And she said to him, “Speak.”
17 Kwa hiyo akaendelea kusema, “Tafadhali mwombe Mfalme Solomoni, anipatie Abishagi, Mshunami, awe mke wangu; hatakukatalia wewe.”
And he said: “I beg that you may speak to king Solomon, for he is not able to refuse anything to you, so that he may give Abishag the Shunammite to me as wife.”
18 Bathsheba akamjibu, “Vema sana, nitazungumza na mfalme kwa ajili yako.”
And Bathsheba said: “It is well. I will speak to the king on your behalf.”
19 Bathsheba alipokwenda kwa Mfalme Solomoni kuzungumza naye kwa ajili ya Adoniya, mfalme alisimama kumlaki mama yake, akamwinamia na kuketi kwenye kiti chake cha ufalme. Akaamuru kiti cha ufalme kuletwa kwa ajili ya mama yake mfalme, naye akaketi mkono wake wa kuume.
Then Bathsheba went to king Solomon, so that she might speak to him on behalf of Adonijah. And the king rose up to meet her, and he reverenced her, and he sat down upon his throne. And a throne was stationed for the mother of the king, and she sat at his right hand.
20 Bathsheba akamwambia mfalme, “Ninalo ombi moja dogo la kukuomba; usinikatalie.” Mfalme akajibu, “Omba, mama yangu; sitakukatalia.”
And she said to him: “I petition one small request from you. May you not confound my face.” And the king said to her: “Ask, my mother. For it is not right that I turn away your face.”
21 Akasema, “Mruhusu Abishagi, Mshunami, aolewe na ndugu yako Adoniya.”
And she said, “Let Abishag the Shunammite be given to Adonijah, your brother, as wife.”
22 Mfalme Solomoni akamjibu mama yake, “Kwa nini uombe Abishagi, Mshunami, kwa ajili ya Adoniya? Ungeweza pia kuomba ufalme kwa ajili yake, kwani yeye ni ndugu yangu mkubwa: naam, kwa ajili yake, na kwa kuhani Abiathari na Yoabu mwana wa Seruya!”
And king Solomon responded, and he said to his mother: “Why do you request Abishag the Shunammite for Adonijah? Why not request the kingdom for him! For he is my older brother, and he has Abiathar, the priest, and Joab, the son of Zeruiah.”
23 Mfalme Solomoni akaapa kwa Bwana, akasema: “Mungu na aniulie mbali, tena bila huruma, ikiwa Adoniya hatalipa kwa uhai wake kwa ajili ya ombi hili!
And so king Solomon swore by the Lord, saying: “May God do these things to me, and may he add these other things! For Adonijah has spoken this word against his own life.
24 Basi sasa, hakika kama Bwana aishivyo, yeye ambaye ameniimarisha salama kwenye kiti cha ufalme cha Daudi baba yangu, naye amenipa ufalme wa kudumu kama alivyoahidi, Adoniya atauawa leo!”
And now, as the Lord lives, who has confirmed me and placed me upon the throne of my father David, and who, just as he said, has made a house for me: Adonijah shall be put to death this day.”
25 Hivyo Mfalme Solomoni akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akampiga Adoniya akafa.
And king Solomon sent by the hand of Benaiah, the son of Jehoiada, who put him to death, and so he died.
26 Mfalme akamwambia kuhani Abiathari, “Nenda huko Anathothi katika mashamba yako. Wewe unastahili kufa, lakini sitakuua sasa, kwa sababu ulilichukua Sanduku la Bwana Mwenyezi mbele ya Daudi baba yangu na ulishiriki taabu zote za baba yangu.”
Also, the king said to Abiathar, the priest: “Go into Anathoth, to your own land, for you are a man worthy of death. But I will not put you to death this day, since you carried the ark of the Lord God before David, my father, and since you have endured hardship in all the things, for which my father labored.”
27 Hivyo Solomoni akamwondoa Abiathari kwenye ukuhani wa Bwana, akilitimiza neno la Bwana alilokuwa amenena huko Shilo kuhusu nyumba ya Eli.
Therefore, Solomon cast out Abiathar, so that he would not be the priest of the Lord, so that the word of the Lord might be fulfilled, which he spoke over the house of Eli at Shiloh.
28 Habari zilipomfikia Yoabu, ambaye alikuwa amefanya shauri baya na Adoniya, lakini sio na Absalomu, alikimbilia kwenye hema la Bwana na kushika pembe za madhabahu.
And the news came to Joab, for Joab had turned aside after Adonijah, and he had not turned aside after Solomon. And so, Joab fled into the tabernacle of the Lord, and he took hold of the horn of the altar.
29 Mfalme Solomoni akaambiwa kuwa Yoabu amekimbilia kwenye hema la Bwana naye alikuwa kando ya madhabahu. Basi Solomoni akamwagiza Benaya mwana wa Yehoyada: “Nenda ukamuue!”
And it was reported to king Solomon that Joab had fled into the tabernacle of the Lord, and that he was beside the altar. And Solomon sent Benaiah, the son of Jehoiada, saying, “Go, put him to death.”
30 Ndipo Benaya akaingia kwenye hema la Bwana na kumwambia Yoabu, “Mfalme anasema, ‘Toka nje!’” Lakini akajibu, “La! Nitafia hapa hapa.” Benaya akamwarifu mfalme, “Hivi ndivyo Yoabu alivyonijibu.”
And Benaiah went to the tabernacle of the Lord, and he said to him: “The king says this: ‘Come out.’” But he said: “I will not come out. Instead, I will die here.” Benaiah sent word back to the king, saying, “Joab said this, and he responded to me in this way.”
31 Kisha mfalme akamwamuru Benaya, “Fanya kama asemavyo. Muue na kumzika, ili uniondolee mimi na nyumba ya baba yangu dhambi ya damu isiyokuwa na hatia ile Yoabu aliyoimwaga.
And the king said to him, “Do just as he has said. And put him to death, and bury him. And so shall you take away the innocent blood, which was shed by Joab, from me and from my father’s house.
32 Bwana atamlipiza kwa ajili ya damu aliyoimwaga, kwa sababu pasipo Daudi baba yangu kujua, aliwashambulia watu wawili na kuwaua kwa upanga. Wote wawili, Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Israeli, na Amasa mwana wa Yetheri, jemadari wa jeshi la Yuda, walikuwa watu wazuri na wanyofu kuliko yeye.
And the Lord shall repay his blood upon his own head. For he killed two men, just and better than himself, and he killed them with the sword, while my father, David, did not know it: Abner, the son of Ner, leader of the military of Israel, and Amasa, the son of Jether, leader of the army of Judah.
33 Hatia ya damu yao na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na wazao wake milele. Lakini kwa Daudi na uzao wake, nyumba yake na kiti chake cha ufalme, iwepo amani ya Bwana milele.”
And their blood shall be turned back upon the head of Joab, and upon the head of his offspring forever. But as for David, and his offspring and house, and his throne, may there be peace from the Lord, even unto eternity.”
34 Basi Benaya mwana wa Yehoyada akakwea, akampiga na kumuua Yoabu, naye akazikwa katika nchi yake mwenyewe katika jangwa.
And so Benaiah, the son of Jehoiada, went up and, attacking him, put him to death. And he was buried in his own house in the desert.
35 Mfalme akamweka Benaya mwana wa Yehoyada juu ya jeshi kwenye nafasi ya Yoabu na kumweka kuhani Sadoki badala ya Abiathari.
And the king appointed Benaiah, the son of Jehoiada, in his place over the army. And he appointed Zadok, the priest, in place of Abiathar.
36 Kisha mfalme akatuma ujumbe kwa Shimei na kumwambia, “Ujijengee nyumba huko Yerusalemu uishi huko, lakini usiende mahali pengine popote.
Also, the king sent for and summoned Shimei, and he said to him: “Build a house for yourself in Jerusalem, and live there. And do not depart from that place to here or to there.
37 Siku utakayoondoka kuvuka Bonde la Kidroni, uwe na hakika utakufa; damu yako itakuwa juu ya kichwa chako mwenyewe.”
For on whatever day you will have departed and crossed the torrent Kidron, know that you shall be put to death. Your blood will be upon your own head.”
38 Shimei akamjibu mfalme, “Ulilolisema ni jema. Mtumishi wako atatenda kama bwana wangu mfalme alivyosema.” Naye Shimei akakaa Yerusalemu kwa muda mrefu.
And Shimei said to the king: “The word is good. Just as my lord the king has said, so will your servant do.” And so Shimei lived in Jerusalem for many days.
39 Lakini baada ya miaka mitatu, watumwa wawili wa Shimei wakatoroka kwenda kwa Akishi mwana wa Maaka, mfalme wa Gathi, naye Shimei akaambiwa, “Watumwa wako wako Gathi.”
But it happened that, after three years, the servants of Shimei fled to Achish, the son of Maacah, the king of Gath. And it was reported to Shimei that his servants had gone away to Gath.
40 Kwa ajili ya hili, Shimei akatandika punda wake, akaenda kwa Akishi huko Gathi kuwatafuta watumwa wake. Basi Shimei akaondoka na kuwarudisha watumwa wake kutoka Gathi.
And Shimei rose up, and he saddled his donkey. And went away to Achish in Gath, in order to seek his servants. And he led them away from Gath.
41 Solomoni alipoambiwa kuwa Shimei ametoka Yerusalemu na kwenda Gathi na amekwisha kurudi,
And it was reported to Solomon that Shimei had gone away from Jerusalem to Gath, and had returned.
42 mfalme akamwita Shimei na kumwambia, “Je, sikukuapiza kwa Bwana na kukuonya kuwa, ‘Siku utakayoondoka kwenda mahali pengine popote, uwe na hakika utakufa?’ Wakati ule uliniambia, ‘Ulilolisema ni jema. Nitatii!’
And sending, he summoned him, and he said to him: “Did I not testify to you by the Lord, and warn you in advance, ‘On whatever day, having departed, you go forth to here or to there, know that you shall die?’ And you responded to me, ‘The word that I have heard is good.’
43 Kwa nini basi hukutunza kiapo chako kwa Bwana na kutii amri niliyokupa?”
Then why have you not kept the oath to the Lord, and the commandment which I instructed to you?”
44 Pia mfalme akamwambia Shimei, “Unajua katika moyo wako makosa uliyomtendea baba yangu Daudi. Sasa Bwana atakulipiza kwa ajili ya mabaya yako uliyotenda.
And the king said to Shimei: “You know all the evil, of which your heart is conscious, which you did to David, my father. The Lord has repaid your wickedness upon your own head.”
45 Lakini Mfalme Solomoni atabarikiwa, na kiti cha ufalme cha Daudi kitakuwa imara mbele za Bwana milele.”
And king Solomon shall be blessed, and the throne of David shall be established before the Lord, even forever.
46 Kisha mfalme akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada, naye akatoka nje, akampiga Shimei na kumuua. Sasa ufalme ukawa umeimarika kikamilifu mikononi mwa Solomoni.
And so the king commanded Benaiah, the son of Jehoiada. And going out, he struck him down, and he died.

< 1 Wafalme 2 >