< 1 Wafalme 19 >
1 Ahabu akamwambia Yezebeli kila kitu Eliya alichokuwa amefanya na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
И возвести Ахаав Иезавели жене своей вся, елика сотвори Илиа, и яко изби пророки оружием.
2 Hivyo Yezebeli akamtuma mjumbe kwa Eliya, kusema, “Hao miungu initendee hivyo na kuzidi, kama kufikia kesho wakati kama huu sitaifanya roho yako kama mmojawapo wa hao manabii.”
И посла Иезавель ко Илии и рече: аще ты еси Илиа, аз же Иезавель: сия да сотворят ми бози и сия да приложат ми, яко в сей же час утро положу душу твою, якоже душу единаго от них.
3 Eliya aliogopa, na akakimbia kuokoa maisha yake. Alipofika Beer-Sheba katika Yuda, akamwacha mtumishi wake huko,
И убояся Илиа, и воста, и отиде души ради своея, и прииде в Вирсавию землю Иудину, и остави отрочище свое тамо,
4 lakini yeye mwenyewe akatembea mwendo wa kutwa nzima katika jangwa. Akafika kwenye mti wa mretemu, akakaa chini yake na kuomba ili afe. Akasema, “Yatosha sasa, Bwana, ondoa roho yangu, kwani mimi si bora kuliko baba zangu.”
сам же иде в пустыню дне путь, и прииде, и седе под смерчием, и проси души своей смерти, и рече: довлеет ныне (ми), возми убо от мене душу мою, Господи, яко несмь аз лучший отец моих.
5 Kisha akajinyoosha chini ya mti, akalala usingizi. Mara malaika akamgusa na akamwambia, “Inuka na ule.”
И ляже, и успе под садом: и се, Ангел Господень коснуся ему и рече ему: востани, яждь и пий.
6 Akatazama pande zote, napo hapo karibu na kichwa chake palikuwepo mkate uliookwa kwenye makaa ya moto na gudulia la maji. Akala na kunywa, kisha akajinyoosha tena.
И воззре Илиа: и се, у возглавия его опреснок ячменный и чванец воды. И воста, и яде и пи, и возвратився успе.
7 Yule malaika wa Bwana akaja tena mara ya pili, akamgusa akamwambia, “Inuka na ule, kwa kuwa safari ni ndefu kwako.”
И обратися Ангел Господень вторицею, и коснуся ему, и рече ему: востани, яждь и пий, яко мног от тебе путь.
8 Kwa hiyo akainuka, akala na kunywa. Akiwa ametiwa nguvu na kile chakula, akasafiri siku arobaini usiku na mchana mpaka akafika Horebu, mlima wa Mungu.
И воста, и яде и пи: и иде в крепости яди тоя четыредесять дний и четыредесять нощей до горы Божия Хорив.
9 Huko akaingia katika pango, akalala humo usiku ule. Nalo neno la Bwana likamjia, kusema, “Unafanya nini hapa, Eliya?”
И вниде тамо в пещеру, и вселися в ней. И се, глагол Господень к нему и рече: что ты зде, Илие?
10 Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
И рече Илиа: ревнуя поревновах по Господе (Бозе) Вседержители, яко оставиша Тя сынове Израилевы: олтари Твоя раскопаша, и пророки Твоя избиша оружием, и остах аз един, и ищут души моея изяти ю.
11 Bwana akasema, “Toka nje ukasimame juu ya mlima mbele za Bwana, kwa kuwa Bwana yu karibu kupita hapo.” Kisha upepo mwingi na wenye nguvu ukapasua milima ile na kuvunjavunja miamba mbele za Bwana, lakini Bwana hakuwamo katika ule upepo. Baada ya upepo palikuwa na tetemeko la nchi, lakini Bwana hakuwamo kwenye lile tetemeko.
И рече: изыди утро и стани пред Господем в горе: и се, мимо пойдет Господь, и дух велик и крепок разоряя горы и сокрушая камение в горе пред Господем, (но) не в дусе Господь: и по дусе трус, и не в трусе Господь:
12 Baada ya tetemeko la nchi ukaja moto, lakini Bwana hakuwamo katika ule moto. Baada ya moto ikaja sauti ya utulivu ya kunongʼona.
и по трусе огнь, и не во огни Господь: и по огни глас хлада тонка, и тамо Господь.
13 Eliya alipoisikia, akafunika uso kwa vazi lake, akatoka na kusimama kwenye mdomo wa pango. Kisha ile sauti ikamwambia, “Eliya, unafanya nini hapa?”
И бысть яко услыша Илиа, покры лице свое милотию своею, и изыде и ста пред вертепом. И се, к нему бысть глас и рече: что ты зде, Илие?
14 Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
И рече Илиа: ревнуя поревновах по Господе Бозе Вседержители, яко оставиша завет Твой сынове Израилевы, и олтари Твоя раскопаша, и пророки Твоя избиша оружием, и остах аз един, и ищут души моея изяти ю.
15 Bwana akamwambia, “Rudi kwa njia uliyoijia, uende kwenye Jangwa la Dameski. Wakati utakapofika huko, mtie Hazaeli mafuta awe mfalme wa Aramu
И рече Господь к нему: иди, возвратися путем своим, и изыдеши на путь пустыни Дамасковы, и помажеши Азаила на царство Сирийское,
16 Pia mtie mafuta Yehu mwana wa Nimshi awe mfalme wa Israeli, na umtie Elisha mwana wa Shafati kutoka Abel-Mehola mafuta awe nabii badala yako.
и Ииуа сына Намессиина помажеши на царство над Израилем, и Елиссеа сына Сафатова от Авелмаула помажеши вместо себе пророка:
17 Yehu atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Hazaeli, naye Elisha atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Yehu.
и будет спасаемаго от оружия Азаилева убиет Ииуй, и спасаемаго от оружия Ииуина убиет Елиссей:
18 Hata sasa nimeweka akiba watu elfu saba katika Israeli, wote ambao hawajampigia Baali magoti, na wote ambao midomo yao haijambusu.”
и оставиши во Израили седмь тысящ мужей, вся колена, яже не преклониша колена Ваалу, и всяка уста, яже не молишася ему.
19 Hivyo Eliya akaondoka kutoka huko na kumkuta Elisha mwana wa Shafati. Alikuwa akilima kwa jozi kumi na mbili za maksai, na yeye mwenyewe aliongoza ile jozi ya kumi na mbili. Eliya akapita karibu naye, akamrushia vazi lake.
И иде оттуду, и обрете Елиссеа сына Сафатова, и сей оряше двеманадесятьма супругома волов пред ним, и той сам по двоюнадесяти супруг. И прииде Илиа к нему, и поверже милоть свою на него.
20 Kisha Elisha akawaacha maksai wake, akamkimbilia Eliya, akamwambia, “Niruhusu nikawabusu baba yangu na mama yangu, halafu nitafuatana nawe.” Eliya akajibu, “Rudi zako, kwani nimekutendea nini?”
И остави Елиссей волы, и тече вслед Илии, и рече: (молю тя, ) да облобыжу отца моего и матерь мою, и иду вслед тебе. И рече ему Илиа: иди, возвратися, яко сотворих тебе.
21 Basi Elisha akamwacha Eliya, naye akarudi. Akachukua ile jozi yake ya maksai na kuwachinja. Akaipika ile nyama kwa kutumia miti ya nira kama kuni na kuwapa watu, nao wakala. Kisha akaondoka, akamfuata Eliya, akamtumikia.
И возвратися от него: и взя супруги волов, и закла, и испече я в сосудех воловных, и даде людем, и ядоша. И воста, и иде вслед Илии, и служаше ему.