< 1 Wafalme 19 >

1 Ahabu akamwambia Yezebeli kila kitu Eliya alichokuwa amefanya na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
And he told Ahab to Jezebel all that he had done Elijah and all that he had killed all the prophets with the sword.
2 Hivyo Yezebeli akamtuma mjumbe kwa Eliya, kusema, “Hao miungu initendee hivyo na kuzidi, kama kufikia kesho wakati kama huu sitaifanya roho yako kama mmojawapo wa hao manabii.”
And she sent Jezebel a messenger to Elijah saying thus may they do! [the] gods and thus may they add! if about this time tomorrow I will make life your like [the] life of one from them.
3 Eliya aliogopa, na akakimbia kuokoa maisha yake. Alipofika Beer-Sheba katika Yuda, akamwacha mtumishi wake huko,
And he saw and he arose and he went to life his and he came Beer Sheba which [belongs] to Judah and he left servant his there.
4 lakini yeye mwenyewe akatembea mwendo wa kutwa nzima katika jangwa. Akafika kwenye mti wa mretemu, akakaa chini yake na kuomba ili afe. Akasema, “Yatosha sasa, Bwana, ondoa roho yangu, kwani mimi si bora kuliko baba zangu.”
And he he went in the wilderness a journey of a day and he came and he sat under a broom plant (one *Q(k)*) and he asked self his to die and he said - enough now O Yahweh take life my for not [am] good I more than ancestors my.
5 Kisha akajinyoosha chini ya mti, akalala usingizi. Mara malaika akamgusa na akamwambia, “Inuka na ule.”
And he lay down and he slept under a broom plant one and there! this an angel [was] touching him and he said to him arise eat.
6 Akatazama pande zote, napo hapo karibu na kichwa chake palikuwepo mkate uliookwa kwenye makaa ya moto na gudulia la maji. Akala na kunywa, kisha akajinyoosha tena.
And he looked and there! [was] [the] place of head his a bread cake of hot coals and a jug of water and he ate and he drank and he returned and he lay down.
7 Yule malaika wa Bwana akaja tena mara ya pili, akamgusa akamwambia, “Inuka na ule, kwa kuwa safari ni ndefu kwako.”
And he returned [the] angel of Yahweh - a second [time] and he touched him and he said arise eat for [is too] great for you the journey.
8 Kwa hiyo akainuka, akala na kunywa. Akiwa ametiwa nguvu na kile chakula, akasafiri siku arobaini usiku na mchana mpaka akafika Horebu, mlima wa Mungu.
And he arose and he ate and he drank and he went in [the] strength of - the food that forty day[s] and forty night[s] to [the] mountain of God Horeb.
9 Huko akaingia katika pango, akalala humo usiku ule. Nalo neno la Bwana likamjia, kusema, “Unafanya nini hapa, Eliya?”
And he went there into the cave and he spent [the] night there and there! [the] word of Yahweh [was] to him and he said to him what? [is] to you here O Elijah.
10 Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
And he said certainly I have been zealous for Yahweh - [the] God of hosts for they have forsaken covenant your [the] people of Israel altars your they have torn down and prophets your they have killed with the sword and I am left I to alone me and they have sought life my to take away it.
11 Bwana akasema, “Toka nje ukasimame juu ya mlima mbele za Bwana, kwa kuwa Bwana yu karibu kupita hapo.” Kisha upepo mwingi na wenye nguvu ukapasua milima ile na kuvunjavunja miamba mbele za Bwana, lakini Bwana hakuwamo katika ule upepo. Baada ya upepo palikuwa na tetemeko la nchi, lakini Bwana hakuwamo kwenye lile tetemeko.
And he said go out and you will stand on the mountain before Yahweh and there! Yahweh [was] passing by and a wind great and strong [was] tearing mountains and breaking rocks before Yahweh not [was] in the wind Yahweh and [was] after the wind an earthquake not [was] in the earthquake Yahweh.
12 Baada ya tetemeko la nchi ukaja moto, lakini Bwana hakuwamo katika ule moto. Baada ya moto ikaja sauti ya utulivu ya kunongʼona.
And [was] after the earthquake a fire not [was] in the fire Yahweh and [was] after the fire a sound of a whisper soft.
13 Eliya alipoisikia, akafunika uso kwa vazi lake, akatoka na kusimama kwenye mdomo wa pango. Kisha ile sauti ikamwambia, “Eliya, unafanya nini hapa?”
And it was - when heard Elijah and he wrapped face his in cloak his and he went out and he stood [the] entrance of the cave and there! [was] to him a voice and it said what? [is] to you here O Elijah.
14 Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
And he said certainly I have been zealous for Yahweh - [the] God of hosts for they have forsaken covenant your [the] people of Israel altars your they have torn down and prophets your they have killed with the sword and I am left I to alone me and they have sought life my to take away it.
15 Bwana akamwambia, “Rudi kwa njia uliyoijia, uende kwenye Jangwa la Dameski. Wakati utakapofika huko, mtie Hazaeli mafuta awe mfalme wa Aramu
And he said Yahweh to him go go back to way your [the] wilderness of towards Damascus and you will go and you will anoint Hazael to king over Aram.
16 Pia mtie mafuta Yehu mwana wa Nimshi awe mfalme wa Israeli, na umtie Elisha mwana wa Shafati kutoka Abel-Mehola mafuta awe nabii badala yako.
And Jehu [the] son of Nimshi you will anoint to king over Israel and Elisha [the] son of Shaphat from Abel Meholah you will anoint to prophet in place of you.
17 Yehu atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Hazaeli, naye Elisha atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Yehu.
And it will be the [one who] escapes from [the] sword of Hazael he will put to death Jehu and the [one who] escapes from [the] sword of Jehu he will put to death Elisha.
18 Hata sasa nimeweka akiba watu elfu saba katika Israeli, wote ambao hawajampigia Baali magoti, na wote ambao midomo yao haijambusu.”
And I will leave among Israel seven thousand all the knees which not they have bowed down to Baal and every mouth which not it has kissed it.
19 Hivyo Eliya akaondoka kutoka huko na kumkuta Elisha mwana wa Shafati. Alikuwa akilima kwa jozi kumi na mbili za maksai, na yeye mwenyewe aliongoza ile jozi ya kumi na mbili. Eliya akapita karibu naye, akamrushia vazi lake.
And he went from there and he found Elisha [the] son of Shaphat and he [was] plowing two [plus] ten pairs [were] before him and he [was] with two [plus] the ten and he passed on Elijah to him and he threw cloak his to him.
20 Kisha Elisha akawaacha maksai wake, akamkimbilia Eliya, akamwambia, “Niruhusu nikawabusu baba yangu na mama yangu, halafu nitafuatana nawe.” Eliya akajibu, “Rudi zako, kwani nimekutendea nini?”
And he left the ox[en] and he ran after Elijah and he said I want to kiss please father my and mother my and I will go after you and he said to him go turn back for what? have I done to you.
21 Basi Elisha akamwacha Eliya, naye akarudi. Akachukua ile jozi yake ya maksai na kuwachinja. Akaipika ile nyama kwa kutumia miti ya nira kama kuni na kuwapa watu, nao wakala. Kisha akaondoka, akamfuata Eliya, akamtumikia.
And he turned back from after him and he took [the] pair of the ox[en] and he sacrificed it and with [the] equipment of the ox[en] he cooked them the flesh and he gave [it] to the people and they ate and he arose and he went after Elijah and he served him.

< 1 Wafalme 19 >