< 1 Wafalme 18 >
1 Baada ya muda mrefu, katika mwaka wa tatu, neno la Bwana likamjia Eliya kusema, “Nenda ukajionyeshe kwa Ahabu na mimi nitanyesha mvua juu ya nchi.”
Après beaucoup de jours, la parole de Yahweh fut adressée à Élie, dans la troisième année, en ces termes: « Va, parais devant Achab, et je ferai tomber de la pluie sur la face du sol. »
2 Kwa hiyo Eliya akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huu njaa ilikuwa kali sana katika Samaria,
Et Élie partit, pour se présenter devant Achab. La famine était devenue grande à Samarie,
3 naye Ahabu alikuwa amemwita Obadia ambaye alikuwa msimamizi wa jumba lake la kifalme. (Obadia alimcha Bwana sana.
Achab fit appeler Abdias, chef de sa maison. — Or Abdias craignait beaucoup Yahweh,
4 Wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Bwana, Obadia alikuwa amewachukua manabii mia moja na kuwaficha katika mapango mawili, hamsini kwenye kila moja na akawa akiwapa chakula na maji.)
car, lorsque Jézabel massacra les prophètes de Yahweh, Abdias prit cent prophètes et les cacha cinquante par cinquante dans des cavernes, où il les nourrit de pain et d’eau. —
5 Ahabu alikuwa amemwambia Obadia, “Nenda katika nchi yote kwenye vijito vyote na mabonde. Huenda tunaweza kupata majani ya kuwalisha farasi na nyumbu wapate kuishi ili tusilazimike kuwaua hata mmoja wa wanyama wetu.”
Achab dit à Abdias: « Va par le pays vers toutes les sources d’eau et vers tous les torrents; peut-être se trouvera-t-il de l’herbe, et nous conserverons la vie aux chevaux et aux mulets, et nous n’aurons pas à abattre de bétail. »
6 Kwa hiyo wakagawanya nchi waliyokusudia kutafuta majani, Ahabu akaenda upande mmoja na Obadia upande mwingine.
Ils se partagèrent le pays pour le parcourir; Achab alla seul par un chemin, et Abdias alla seul par un autre chemin.
7 Wakati Obadia alipokuwa akitembea njiani, Eliya akakutana naye. Obadia akamtambua, akamsujudia hadi nchi na kusema, “Je, hivi kweli ni wewe, bwana wangu Eliya?”
Comme Abdias était en route, voici qu’Élie le rencontra. Abdias, l’ayant reconnu, tomba sur son visage et dit: « Est-ce toi, mon seigneur Élie? »
8 Eliya akamjibu, “Ndiyo, nenda ukamwambie bwana wako Ahabu, ‘Eliya yuko hapa.’”
Il lui répondit: « C’est moi; va dire à ton maître: Voici Élie! »
9 Obadia akamuuliza, “Ni kosa gani nimefanya, hata ukaamua kumkabidhi mtumishi wako mkononi mwa Ahabu ili aniue?
Et Abdias dit: « Quel péché ai-je commis, que tu livres ton serviteur entre les mains d’Achab, pour qu’il me fasse mourir?
10 Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, hakuna taifa hata moja au ufalme ambapo bwana wangu hajamtuma mtu kukutafuta. Kila wakati taifa au ufalme walipodai kwamba haupo huko, aliwafanya waape kwamba hawakuweza kukupata.
Yahweh, ton Dieu, est vivant! Il n’y a ni nation ni royaume où mon maître n’ait envoyé pour te chercher; et quand on disait: Élie n’est pas ici, il faisait jurer le royaume et la nation qu’on ne t’avait pas trouvé.
11 Lakini sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kusema, ‘Eliya yuko hapa.’
Et maintenant tu me dis: Va dire à ton maître: Voici Élie!
12 Sijui ni wapi Roho wa Bwana ataamua kukupeleka wakati nitakapokuacha. Kama nikienda kumwambia Ahabu na asikupate, ataniua. Hata hivyo mimi mtumishi wako nimemwabudu Bwana tangu ujana wangu.
Et lorsque je t’aurai quitté, l’Esprit de Yahweh te transportera je ne sais où; et j’irai informer Achab, qui ne te trouvera pas et me tuera. Cependant ton serviteur craint Yahweh dès sa jeunesse.
13 Je, hukusikia, bwana wangu, nilifanya nini wakati Yezebeli alipokuwa akiua manabii wa Bwana? Niliwaficha manabii wa Bwana mia moja katika mapango mawili, hamsini katika kila moja, nami nikawapatia chakula na maji.
N’a-t-on pas dit à mon seigneur ce que j’ai fait quand Jézabel a massacré les prophètes de Yahweh? J’ai caché cent des prophètes de Yahweh, cinquante par cinquante, dans des cavernes, et je les ai nourris de pain et d’eau.
14 Nawe sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kumwambia, ‘Eliya yuko hapa.’ Yeye ataniua!”
Et maintenant tu dis: Va dire à ton maître: Voici Élie! Il me tuera. »
15 Eliya akasema, “Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo, yeye ninayemtumikia, hakika nitajionyesha kwa Ahabu leo.”
Mais Élie dit: « Yahweh des armées, devant qui je me tiens, est vivant! Aujourd’hui je me présenterai devant Achab. »
16 Basi Obadia akaenda kukutana na Ahabu na kumwambia, naye Ahabu akaenda kukutana na Eliya.
Abdias alla à la rencontre d’Achab et lui apprit la nouvelle; et Achab se rendit au-devant d’Élie.
17 Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe, mtaabishaji wa Israeli?”
Dès qu’Achab aperçut Élie, Achab lui dit: « Toi ici, le perturbateur d’Israël? »
18 Eliya akamjibu, “Mimi sijaitaabisha Israeli. Lakini wewe na jamaa ya baba yako ndio mnaofanya hivyo. Mmeziacha amri za Bwana na mkafuata Mabaali.
Élie répondit: « Je ne trouble point Israël; c’est toi, au contraire, et la maison de ton père, en ce que vous avez abandonné les commandements de Yahweh et que tu es allé après les Baals.
19 Sasa waite watu kutoka Israeli yote tukutane nao juu ya Mlima Karmeli. Nawe uwalete hao manabii wa Baali mia nne na hamsini na hao manabii mia nne wa Ashera, walao chakula mezani mwa Yezebeli.”
Maintenant, envoie rassembler tout Israël auprès de moi, à la montagne du Carmel, ainsi que les quatre cent cinquante prophètes de Baal et les quatre cents prophètes d’Astarté, qui mangent de la table de Jézabel. »
20 Ndipo Ahabu akatuma ujumbe katika Israeli yote na kuwakusanya manabii hao juu ya mlima Karmeli.
Achab envoya des messagers vers tous les enfants d’Israël, et rassembla les prophètes à la montagne du Carmel.
21 Eliya akasimama mbele ya watu na kusema, “Mtasitasita katika mawazo mawili hadi lini? Ikiwa Bwana ndiye Mungu, mfuateni yeye; lakini ikiwa Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye.” Lakini watu hawakusema kitu.
Alors Élie s’approcha de tout le peuple et dit: « Jusques à quand clocherez-vous des deux côtés? Si Yahweh est Dieu, allez après lui; si c’est Baal, allez après lui! » Le peuple ne lui répondit rien.
22 Kisha Eliya akawaambia, “Ni mimi peke yangu nabii wa Bwana aliyebaki, lakini Baali ana manabii mia nne na hamsini.
Et Élie dit au peuple: « Je suis resté seul des prophètes de Yahweh, et il y a quatre cent cinquante prophètes de Baal.
23 Leteni mafahali wawili. Wao na wajichagulie mmoja, wamkate vipande vipande na waweke juu ya kuni lakini wasiiwashie moto. Nitamwandaa huyo fahali mwingine na kumweka juu ya kuni lakini sitawasha moto.
Que l’on nous donne deux taureaux; qu’ils choisissent pour eux l’un des taureaux, qu’ils le coupent par morceaux et qu’ils le placent sur le bois, sans y mettre le feu; et moi je préparerai l’autre taureau, et je le placerai sur le bois, sans y mettre le feu.
24 Kisha mliitie jina la mungu wenu, nami nitaliitia jina la Bwana Mungu yule ambaye atajibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.” Kisha watu wote wakasema, “Hilo unalosema ni jema.”
Puis invoquez le nom de votre dieu, et moi j’invoquerai le nom de Yahweh. Le dieu qui répondra par le feu, celui-là est Dieu. » Tout le peuple répondit en disant: « C’est bien! »
25 Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni mmoja kati ya hawa mafahali na mwe wa kwanza kumwandaa, kwa kuwa ninyi mko wengi sana. Liitieni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
Élie dit aux prophètes de Baal: « Choisissez pour vous l’un des taureaux, préparez-le d’abord, car vous êtes les plus nombreux, et invoquez le nom de votre dieu, mais ne mettez pas le feu. »
26 Kwa hiyo wakamchukua yule fahali waliyepewa, nao wakamwandaa. Kisha wakaliitia jina la Baali kutoka asubuhi hadi adhuhuri, wakapiga kelele, “Ee Baali, utujibu!” Lakini hapakuwa na jibu; hakuna aliyejibu. Nao wakacheza kuizunguka madhabahu waliyoijenga.
Ils prirent le taureau qu’on leur donna et le préparèrent; et ils invoquèrent le nom de Baal depuis le matin jusqu’à midi, en disant: « Baal, réponds-nous! » Mais il n’y eut ni voix ni réponse. Et ils sautaient devant l’autel qu’ils avaient fait.
27 Wakati wa adhuhuri, Eliya akaanza kuwadhihaki, akisema, “Pigeni kelele zaidi! Hakika yeye ni mungu! Labda amezama katika mawazo mazito, au ana shughuli nyingi, au amesafiri. Labda amelala usingizi mzito, naye ni lazima aamshwe.”
À midi, Élie se moqua d’eux et dit: « Criez à haute voix, car il est dieu; il est en méditation, ou il est occupé, ou il est en voyage; peut-être qu’il dort, et il se réveillera. »
28 Kwa hiyo wakapiga kelele zaidi na kama ilivyokuwa desturi yao wakajichanja wenyewe kwa visu na vyembe, mpaka damu ikachuruzika.
Et ils crièrent à haute voix, et ils se firent, selon leur coutume, des incisions avec des épées et avec des lances, jusqu’à ce que le sang coulât sur eux.
29 Adhuhuri ikapita, nao wakaendelea na utabiri wao wa kiwazimu mpaka wakati wa dhabihu ya jioni. Lakini hapakuwa na jibu, hakuna aliyejibu, hakuna aliyeangalia.
Lorsque midi fut passé, ils prophétisèrent jusqu’ au moment où l’on présente l’oblation. Mais il n’y eut ni voix, ni réponse, ni signe d’attention.
30 Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Sogeeni karibu nami.” Watu wote wakamkaribia, naye akakarabati madhabahu ya Bwana, ambayo ilikuwa imevunjwa.
Élie dit à tout le peuple: « Approchez-vous de moi. » Tout le peuple s’étant approché de lui, Élie rétablit l’autel de Yahweh, qui avait été renversé.
31 Eliya akachukua mawe kumi na mawili, moja kwa ajili ya kila kabila la wana wa Yakobo, ambaye neno la Bwana lilimjia, likisema, “Jina lako litakuwa Israeli.”
Élie prit douze pierres, d’après le nombre des tribus des fils de Jacob, auquel la parole de Yahweh avait été adressée en ces termes: « Israël sera ton nom. »
32 Kwa mawe hayo, akajenga madhabahu katika jina la Bwana, na akachimba handaki kuizunguka, ukubwa wa kutosha vipimo viwili vya mbegu.
Il bâtit avec ces pierres un autel au nom de Yahweh; puis, ayant fait autour de l’autel un fossé de la capacité de deux mesures de semence,
33 Akapanga kuni, akamkata yule fahali vipande vipande na kuvipanga juu ya kuni. Kisha akawaambia, “Jazeni mapipa manne maji na kuyamwaga juu ya sadaka ya kuteketezwa na juu ya kuni.”
il arrangea le bois, coupa le taureau par morceaux et le plaça sur le bois.
34 Akawaambia, “Fanyeni hivyo tena.” Nao wakafanya hivyo tena. Akaagiza, “Fanyeni kwa mara ya tatu.” Nao wakafanya hivyo kwa mara ya tatu.
Et il dit: « Remplissez d’eau quatre cruches, et versez- les sur l’holocauste et sur le bois. » Il dit: « Faites-le une seconde fois »; et ils le firent une seconde fois. Il dit: « Faites le une troisième fois »; et ils le firent une troisième fois.
35 Maji yakatiririka kuizunguka madhabahu na hata kujaza lile handaki.
L’eau coula autour de l’autel, et il fit remplir aussi d’eau le fossé.
36 Wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea mbele na kuomba, akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Abrahamu, na Isaki na Israeli, ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu katika Israeli na ya kwamba mimi ni mtumishi wako na nimefanya mambo haya yote kwa neno lako.
À l’heure où l’on offre l’oblation du soir, Élie, le prophète, s’avança et dit: « Yahweh, Dieu d’Abraham, d’Isaac et d’Israël, que l’on sache aujourd’hui que vous êtes Dieu en Israël, que je suis votre serviteur et que j’ai fait toutes ces choses sur votre parole.
37 Unijibu mimi, Ee Bwana, nijibu mimi, ili watu hawa wajue kwamba wewe, Ee Bwana, ndiwe Mungu, na kwamba unaigeuza mioyo yao ikurudie tena.”
Exaucez-moi, Yahweh, exaucez-moi! Afin que ce peuple reconnaisse que vous, Yahweh, êtes Dieu, et que c’est vous qui ramenez leur cœur en arrière. »
38 Kisha moto wa Bwana ukashuka na kuiteketeza ile dhabihu, zile kuni, yale mawe, ule udongo, na pia kuramba yale maji yaliyokuwa ndani ya handaki.
Alors le feu de Yahweh tomba, et il consuma l’holocauste, le bois, les pierres et la terre, et absorba l’eau qui était dans le fossé.
39 Wakati watu wote walipoona hili, wakaanguka kifudifudi na kulia, “Bwana: yeye ndiye Mungu! Bwana: yeye ndiye Mungu!”
Quand tout le peuple vit cela, ils tombèrent sur leur visage et ils dirent: C’est Yahweh qui est Dieu! C’est Yahweh qui est Dieu! »
40 Kisha Eliya akawaamuru, “Wakamateni hao manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja atoroke!” Wakawakamata, naye Eliya akawaleta mpaka Bonde la Kishoni na kuwachinja huko.
Et Élie leur dit: Saisissez les prophètes de Baal; que pas un d’eux n’échappe! » Ils les saisirent, et Élie les fit descendre au torrent de Cison, où il les tua.
41 Eliya akamwambia Ahabu, “Nenda, ukale na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.”
Élie dit à Achab: « Monte, mange et bois; car j’entends le bruissement de la pluie. »
42 Hivyo Ahabu akaondoka ili kula na kunywa. Lakini Eliya akapanda kileleni mwa Karmeli, akasujudu na akaweka kichwa chake katikati ya magoti yake.
Achab monta pour manger et pour boire; mais Élie monta au sommet du Carmel et, se penchant vers la terre, il mit son visage entre ses genoux,
43 Akamwambia mtumishi wake, “Nenda ukatazame kuelekea bahari.” Akaenda na kutazama. Akasema, “Hakuna kitu chochote huko.” Mara saba Eliya akasema, “Nenda tena.”
et il dit à son serviteur: « Monte, regarde du côté de la mer. » Le serviteur monta et, ayant regardé, il dit: « Il n’y a rien. » Et Élie dit: « Retourne sept fois. »
44 Mara ya saba, mtumishi akaleta taarifa, “Wingu dogo kama mkono wa mwanadamu linainuka kutoka baharini.” Hivyo Eliya akasema, “Nenda ukamwambie Ahabu, ‘Tandika gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.’”
À la septième fois, il dit: « Voici un petit nuage, comme la paume de la main d’un homme, qui s’élève de la mer. » Et Élie dit: « Va dire à Achab: Attelle et descends, afin que la pluie ne te surprenne pas. »
45 Wakati ule ule anga likawa jeusi kwa mawingu, upepo ukainuka na mvua kubwa ikanyesha, naye Ahabu akaenda zake Yezreeli.
En peu de temps, le ciel fut assombri par les nuages et le vent, et il tomba une forte pluie; et Achab, monté sur son char, s’en retourna à Jezrahel.
46 Nguvu za Bwana zikamjia Eliya, naye akajikaza viuno, akakimbia mbele ya Ahabu njia yote hadi maingilio ya Yezreeli.
Et la main de Yahweh fut sur Élie; il se ceignit les reins et courut devant Achab, jusqu’à l’entrée de Jezrahel.