< 1 Wafalme 18 >

1 Baada ya muda mrefu, katika mwaka wa tatu, neno la Bwana likamjia Eliya kusema, “Nenda ukajionyeshe kwa Ahabu na mimi nitanyesha mvua juu ya nchi.”
Après bien des jours, la parole de Yahvé fut adressée à Élie, la troisième année, en ces termes: « Va, montre-toi à Achab, et je ferai tomber la pluie sur la terre. »
2 Kwa hiyo Eliya akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huu njaa ilikuwa kali sana katika Samaria,
Élie alla se montrer à Achab. La famine était grave à Samarie.
3 naye Ahabu alikuwa amemwita Obadia ambaye alikuwa msimamizi wa jumba lake la kifalme. (Obadia alimcha Bwana sana.
Achab appela Abdias, qui avait la charge de la maison. (Or Abdias craignait beaucoup Yahvé;
4 Wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Bwana, Obadia alikuwa amewachukua manabii mia moja na kuwaficha katika mapango mawili, hamsini kwenye kila moja na akawa akiwapa chakula na maji.)
car lorsque Jézabel avait exterminé les prophètes de Yahvé, Abdias avait pris cent prophètes, en avait caché cinquante dans une caverne, et les avait nourris de pain et d'eau).
5 Ahabu alikuwa amemwambia Obadia, “Nenda katika nchi yote kwenye vijito vyote na mabonde. Huenda tunaweza kupata majani ya kuwalisha farasi na nyumbu wapate kuishi ili tusilazimike kuwaua hata mmoja wa wanyama wetu.”
Achab dit à Abdias: « Parcourez le pays, allez à toutes les sources d'eau et à tous les ruisseaux. Peut-être trouverons-nous de l'herbe et sauverons-nous les chevaux et les mules en vie, afin de ne pas perdre tous les animaux. »
6 Kwa hiyo wakagawanya nchi waliyokusudia kutafuta majani, Ahabu akaenda upande mmoja na Obadia upande mwingine.
Et ils se partagèrent le pays pour le parcourir. Achab prit un chemin à part, et Abdias prit un autre chemin à part.
7 Wakati Obadia alipokuwa akitembea njiani, Eliya akakutana naye. Obadia akamtambua, akamsujudia hadi nchi na kusema, “Je, hivi kweli ni wewe, bwana wangu Eliya?”
Comme Abdias était en chemin, voici qu'Élie le rencontra. Il le reconnut, tomba sur sa face et dit: « Est-ce toi, mon seigneur Élie? »
8 Eliya akamjibu, “Ndiyo, nenda ukamwambie bwana wako Ahabu, ‘Eliya yuko hapa.’”
Il lui répondit: « C'est moi. Va dire à ton maître: « Voici Élie, il est là! ».
9 Obadia akamuuliza, “Ni kosa gani nimefanya, hata ukaamua kumkabidhi mtumishi wako mkononi mwa Ahabu ili aniue?
Il dit: « Comment ai-je péché, pour que tu livres ton serviteur entre les mains d'Achab, afin qu'il me tue?
10 Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, hakuna taifa hata moja au ufalme ambapo bwana wangu hajamtuma mtu kukutafuta. Kila wakati taifa au ufalme walipodai kwamba haupo huko, aliwafanya waape kwamba hawakuweza kukupata.
L'Éternel, ton Dieu, est vivant! Il n'y a ni nation ni royaume où mon seigneur n'ait envoyé pour te chercher. Quand on a dit: « Il n'est pas ici », il a juré par le royaume et la nation qu'on ne te trouverait pas.
11 Lakini sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kusema, ‘Eliya yuko hapa.’
Maintenant, vous dites: « Va dire à ton maître: « Voici Élie qui est ici ».
12 Sijui ni wapi Roho wa Bwana ataamua kukupeleka wakati nitakapokuacha. Kama nikienda kumwambia Ahabu na asikupate, ataniua. Hata hivyo mimi mtumishi wako nimemwabudu Bwana tangu ujana wangu.
Il arrivera, dès que je te quitterai, que l'Esprit de Yahvé te portera je ne sais où; aussi, quand je viendrai prévenir Achab, et qu'il ne te trouvera pas, il me tuera. Mais moi, ton serviteur, j'ai craint Yahvé dès ma jeunesse.
13 Je, hukusikia, bwana wangu, nilifanya nini wakati Yezebeli alipokuwa akiua manabii wa Bwana? Niliwaficha manabii wa Bwana mia moja katika mapango mawili, hamsini katika kila moja, nami nikawapatia chakula na maji.
N'a-t-on pas raconté à mon seigneur ce que j'ai fait quand Jézabel a tué les prophètes de l'Éternel, comment j'ai caché cent hommes des prophètes de l'Éternel avec cinquante dans une caverne, et comment je les ai nourris de pain et d'eau?
14 Nawe sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kumwambia, ‘Eliya yuko hapa.’ Yeye ataniua!”
Et maintenant, tu dis: « Va dire à ton maître: « Voici Élie », et il me tuera. Il me tuera. »
15 Eliya akasema, “Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo, yeye ninayemtumikia, hakika nitajionyesha kwa Ahabu leo.”
Élie dit: « L'Éternel des armées est vivant, devant qui je me tiens, et je me montrerai à lui aujourd'hui. »
16 Basi Obadia akaenda kukutana na Ahabu na kumwambia, naye Ahabu akaenda kukutana na Eliya.
Abdias alla à la rencontre d'Achab et le lui dit, et Achab alla à la rencontre d'Élie.
17 Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe, mtaabishaji wa Israeli?”
Lorsqu'Achab vit Élie, il lui dit: « Est-ce toi, le trouble-fête d'Israël? »
18 Eliya akamjibu, “Mimi sijaitaabisha Israeli. Lakini wewe na jamaa ya baba yako ndio mnaofanya hivyo. Mmeziacha amri za Bwana na mkafuata Mabaali.
Il répondit: « Ce n'est pas Israël que j'ai troublé, mais toi et la maison de ton père, parce que vous avez abandonné les commandements de l'Éternel et que vous avez suivi les Baals.
19 Sasa waite watu kutoka Israeli yote tukutane nao juu ya Mlima Karmeli. Nawe uwalete hao manabii wa Baali mia nne na hamsini na hao manabii mia nne wa Ashera, walao chakula mezani mwa Yezebeli.”
Maintenant, envoie et rassemble vers moi tout Israël sur la montagne du Carmel, ainsi que quatre cent cinquante des prophètes de Baal et quatre cents des prophètes d'Ashéra, qui mangent à la table de Jézabel. »
20 Ndipo Ahabu akatuma ujumbe katika Israeli yote na kuwakusanya manabii hao juu ya mlima Karmeli.
Achab envoya donc chercher tous les enfants d'Israël et rassembla les prophètes sur le mont Carmel.
21 Eliya akasimama mbele ya watu na kusema, “Mtasitasita katika mawazo mawili hadi lini? Ikiwa Bwana ndiye Mungu, mfuateni yeye; lakini ikiwa Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye.” Lakini watu hawakusema kitu.
Élie s'approcha de tout le peuple et dit: « Jusques à quand hésiterez-vous entre les deux camps? Si Yahvé est Dieu, suivez-le; mais si c'est Baal, suivez-le. » Les gens n'ont pas dit un mot.
22 Kisha Eliya akawaambia, “Ni mimi peke yangu nabii wa Bwana aliyebaki, lakini Baali ana manabii mia nne na hamsini.
Et Élie dit au peuple: « Moi, et moi seul, je suis resté comme prophète de l'Éternel; mais les prophètes de Baal sont quatre cent cinquante hommes.
23 Leteni mafahali wawili. Wao na wajichagulie mmoja, wamkate vipande vipande na waweke juu ya kuni lakini wasiiwashie moto. Nitamwandaa huyo fahali mwingine na kumweka juu ya kuni lakini sitawasha moto.
Qu'ils nous donnent donc deux taureaux; qu'ils en choisissent un pour eux, qu'ils le coupent en morceaux, qu'ils le posent sur le bois et qu'ils n'y mettent pas le feu; et moi, je préparerai l'autre taureau, je le poserai sur le bois et je n'y mettrai pas le feu.
24 Kisha mliitie jina la mungu wenu, nami nitaliitia jina la Bwana Mungu yule ambaye atajibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.” Kisha watu wote wakasema, “Hilo unalosema ni jema.”
Tu invoqueras le nom de ton dieu, et moi j'invoquerai le nom de Yahvé. Le Dieu qui répond par le feu, qu'il soit Dieu. » Tout le peuple répondit: « Ce que tu dis est bien. »
25 Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni mmoja kati ya hawa mafahali na mwe wa kwanza kumwandaa, kwa kuwa ninyi mko wengi sana. Liitieni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
Élie dit aux prophètes de Baal: « Choisissez pour vous un taureau, et habillez-le le premier, car vous êtes nombreux; invoquez le nom de votre dieu, mais n'y mettez pas le feu. »
26 Kwa hiyo wakamchukua yule fahali waliyepewa, nao wakamwandaa. Kisha wakaliitia jina la Baali kutoka asubuhi hadi adhuhuri, wakapiga kelele, “Ee Baali, utujibu!” Lakini hapakuwa na jibu; hakuna aliyejibu. Nao wakacheza kuizunguka madhabahu waliyoijenga.
Ils prirent le taureau qu'on leur avait donné, l'habillèrent et invoquèrent le nom de Baal depuis le matin jusqu'à midi, en disant: « Baal, écoute-nous! ». Mais il n'y avait pas de voix, et personne ne répondait. Ils sautèrent autour de l'autel qui avait été construit.
27 Wakati wa adhuhuri, Eliya akaanza kuwadhihaki, akisema, “Pigeni kelele zaidi! Hakika yeye ni mungu! Labda amezama katika mawazo mazito, au ana shughuli nyingi, au amesafiri. Labda amelala usingizi mzito, naye ni lazima aamshwe.”
À midi, Élie se moqua d'eux et dit: « Criez à haute voix, car c'est un dieu. Ou bien il est plongé dans ses pensées, ou bien il est parti quelque part, ou bien il est en voyage, ou bien il dort et il faut le réveiller. »
28 Kwa hiyo wakapiga kelele zaidi na kama ilivyokuwa desturi yao wakajichanja wenyewe kwa visu na vyembe, mpaka damu ikachuruzika.
Ils criaient à haute voix et se coupaient sur leur chemin avec des couteaux et des lances jusqu'à ce que le sang jaillisse sur eux.
29 Adhuhuri ikapita, nao wakaendelea na utabiri wao wa kiwazimu mpaka wakati wa dhabihu ya jioni. Lakini hapakuwa na jibu, hakuna aliyejibu, hakuna aliyeangalia.
Quand midi fut passé, ils prophétisèrent jusqu'au moment de l'offrande du soir; mais il n'y eut ni voix, ni réponse, et personne ne fit attention.
30 Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Sogeeni karibu nami.” Watu wote wakamkaribia, naye akakarabati madhabahu ya Bwana, ambayo ilikuwa imevunjwa.
Elie dit à tout le peuple: « Approchez-vous de moi! »; et tout le peuple s'approcha de lui. Il répara l'autel de Yahvé qui avait été renversé.
31 Eliya akachukua mawe kumi na mawili, moja kwa ajili ya kila kabila la wana wa Yakobo, ambaye neno la Bwana lilimjia, likisema, “Jina lako litakuwa Israeli.”
Elie prit douze pierres, selon le nombre des tribus des fils de Jacob, à qui la parole de Yahvé avait été adressée en disant: « Israël sera ton nom. »
32 Kwa mawe hayo, akajenga madhabahu katika jina la Bwana, na akachimba handaki kuizunguka, ukubwa wa kutosha vipimo viwili vya mbegu.
Avec les pierres, il construisit un autel au nom de Yahvé. Il fit autour de l'autel une tranchée assez grande pour contenir deux seahs de semences.
33 Akapanga kuni, akamkata yule fahali vipande vipande na kuvipanga juu ya kuni. Kisha akawaambia, “Jazeni mapipa manne maji na kuyamwaga juu ya sadaka ya kuteketezwa na juu ya kuni.”
Il rangea le bois, coupa le taureau en morceaux et le posa sur le bois. Il dit: « Remplissez d'eau quatre jarres, et versez-la sur l'holocauste et sur le bois. »
34 Akawaambia, “Fanyeni hivyo tena.” Nao wakafanya hivyo tena. Akaagiza, “Fanyeni kwa mara ya tatu.” Nao wakafanya hivyo kwa mara ya tatu.
Il dit: « Faites-le une seconde fois. » Et ils le firent une seconde fois. Il dit: « Faites-le une troisième fois. » Et ils le firent une troisième fois.
35 Maji yakatiririka kuizunguka madhabahu na hata kujaza lile handaki.
L'eau coulait autour de l'autel; il remplit aussi d'eau la tranchée.
36 Wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea mbele na kuomba, akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Abrahamu, na Isaki na Israeli, ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu katika Israeli na ya kwamba mimi ni mtumishi wako na nimefanya mambo haya yote kwa neno lako.
Au moment de l'offrande du soir, le prophète Élie s'approcha et dit: « Yahvé, Dieu d'Abraham, d'Isaac et d'Israël, que l'on sache aujourd'hui que tu es Dieu en Israël et que je suis ton serviteur, et que j'ai fait toutes ces choses selon ta parole.
37 Unijibu mimi, Ee Bwana, nijibu mimi, ili watu hawa wajue kwamba wewe, Ee Bwana, ndiwe Mungu, na kwamba unaigeuza mioyo yao ikurudie tena.”
Écoute-moi, Yahvé, écoute-moi, afin que ce peuple sache que toi, Yahvé, tu es Dieu, et que tu as ramené son cœur à la raison. »
38 Kisha moto wa Bwana ukashuka na kuiteketeza ile dhabihu, zile kuni, yale mawe, ule udongo, na pia kuramba yale maji yaliyokuwa ndani ya handaki.
Le feu de l'Éternel tomba et consuma l'holocauste, le bois, les pierres et la poussière, et il lécha l'eau qui était dans le fossé.
39 Wakati watu wote walipoona hili, wakaanguka kifudifudi na kulia, “Bwana: yeye ndiye Mungu! Bwana: yeye ndiye Mungu!”
Quand tout le peuple vit cela, il tomba sur sa face. Ils disaient: « Yahvé, c'est Dieu! Yahvé, c'est Dieu! »
40 Kisha Eliya akawaamuru, “Wakamateni hao manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja atoroke!” Wakawakamata, naye Eliya akawaleta mpaka Bonde la Kishoni na kuwachinja huko.
Élie leur dit: « Saisissez les prophètes de Baal! Ne laissez pas un seul d'entre eux s'échapper! » Ils s'en emparèrent, et Élie les fit descendre au torrent de Kishon, où il les tua.
41 Eliya akamwambia Ahabu, “Nenda, ukale na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.”
Élie dit à Achab: « Lève-toi, mange et bois, car on entend le bruit d'une pluie abondante. »
42 Hivyo Ahabu akaondoka ili kula na kunywa. Lakini Eliya akapanda kileleni mwa Karmeli, akasujudu na akaweka kichwa chake katikati ya magoti yake.
Et Achab monta pour manger et pour boire. Élie monta au sommet du Carmel; il se prosterna par terre et mit son visage entre ses genoux.
43 Akamwambia mtumishi wake, “Nenda ukatazame kuelekea bahari.” Akaenda na kutazama. Akasema, “Hakuna kitu chochote huko.” Mara saba Eliya akasema, “Nenda tena.”
Il dit à son serviteur: « Monte maintenant et regarde vers la mer. » Il est monté et a regardé, puis a dit: « Il n'y a rien. » Il a dit sept fois: « Vas-y encore ».
44 Mara ya saba, mtumishi akaleta taarifa, “Wingu dogo kama mkono wa mwanadamu linainuka kutoka baharini.” Hivyo Eliya akasema, “Nenda ukamwambie Ahabu, ‘Tandika gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.’”
La septième fois, il dit: « Voici qu'un petit nuage, semblable à la main d'un homme, s'élève de la mer. » Il dit: « Monte, dis à Achab: « Prépare-toi et descends, pour que la pluie ne t'arrête pas. »"
45 Wakati ule ule anga likawa jeusi kwa mawingu, upepo ukainuka na mvua kubwa ikanyesha, naye Ahabu akaenda zake Yezreeli.
En peu de temps, le ciel s'obscurcit de nuages et de vent, et il y eut une grande pluie. Achab monta à cheval et se rendit à Jizreel.
46 Nguvu za Bwana zikamjia Eliya, naye akajikaza viuno, akakimbia mbele ya Ahabu njia yote hadi maingilio ya Yezreeli.
La main de Yahvé était sur Elie; il mit son manteau dans sa ceinture et courut devant Achab jusqu'à l'entrée de Jizreel.

< 1 Wafalme 18 >