< 1 Wafalme 16 >

1 Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani dhidi ya Baasha, kusema:
Forsothe the word of the Lord was maad to Hieu, sone of Anany, ayens Baasa, and seide,
2 “Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao.
For that that Y reiside thee fro dust, and settide thee duyk on Israel, my puple; sotheli thou yedist in the weie of Jeroboam, and madist my puple Israel to do synne, that thou schuldist terre me to ire, in the synnes of hem; lo!
3 Basi nitamwangamiza Baasha pamoja na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwanawe Nebati.
Y schal kitte awey the hyndrere thingis of Baasa, and the hyndrere thingis of `his hows, and Y schal make thin hows as the hows of Jeroboam, sone of Nabath.
4 Mbwa watawala watu wa Baasha watakaofia mjini na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.”
Doggis schulen ete that man of Baasa, that schal be deed in citee, and briddis of the eyr schulen ete that man of Baasa, that schal die in the feeld.
5 Kwa matukio mengine ya utawala wa Baasha, aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Sotheli the residue of wordis of Baasa, and what euer thingis he dide, and hise batels, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kynges of Israel?
6 Baasha akalala na baba zake naye akazikwa huko Tirsa. Naye Ela mwanawe akawa mfalme baada yake.
Therfor Baasa slepte with hise fadris, and he was biried in Thersa; and Hela, his sone, regnede for hym.
7 Zaidi ya hayo, neno la Bwana likamjia Baasha pamoja na nyumba yake kupitia kwa nabii Yehu mwana wa Hanani, kwa sababu ya maovu yote aliyokuwa ametenda machoni pa Bwana, akamkasirisha kwa mambo aliyotenda, na kuwa kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu aliiangamiza.
Forsothe whanne the word of the Lord was maad in the hond of Hieu, sone of Anany, ayens Baasa, and ayens his hows, and ayens al yuel which he dide bifor the Lord, to terre hym to ire in the werkis of hise hondis, that he schulde be as the hows of Jeroboam, for this cause he killide hym, that is, Hieu, the prophete, the sone of Anany.
8 Katika mwaka wa ishirini na sita wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala huko Tirsa kwa miaka miwili.
In the sixe and twentithe yeer of Aza, kyng of Juda, Hela, the sone of Baasa, regnyde on Israel, in Thersa, twei yeer.
9 Zimri, mmoja wa maafisa wake, aliyekuwa na amri juu ya nusu ya magari yake ya vita, akafanya hila mbaya dhidi ya Ela. Wakati huo Ela alikuwa Tirsa, akilewa katika nyumba ya Arsa, mtu aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme huko Tirsa.
And Zamry, `his seruaunt, duyk of the half part of knyytis, rebellide ayens hym; sotheli Hela was in Thersa, and drank, and was drunkun in the hows of Arsa, prefect of Thersa.
10 Zimri akaingia, akampiga na kumuua katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda. Kisha Zimri akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Therfor Zamri felde in, and smoot, and killide hym, in the seuene and twentithe yeer of Asa, kyng of Juda; and regnede for hym.
11 Mara tu alipoanza kutawala na kuketi juu ya kiti cha ufalme, aliua jamaa yote ya Baasha. Hakumwacha mwanaume hata mmoja, akiwa ni ndugu au rafiki.
And whanne he hadde regned, and hadde setun on his trone, he smoot al the hows of Baasa, and he lefte not therof a pissere to the wal, and hise kynnesmen, and frendis.
12 Hivyo Zimri akaangamiza jamaa yote ya Baasha, kulingana na neno la Bwana lililonenwa dhidi ya Baasha kupitia nabii Yehu:
And Zamri dide awey al the hows of Baasa, bi the word of the Lord, which he spak to Baasa, in the hond of Hieu, the prophete, for alle the synnes of Baasa,
13 kwa sababu ya dhambi zote Baasha na mwanawe Ela walizokuwa wametenda na wakasababisha Israeli kuzitenda, basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
and for the synnes of Hela, his sone, whiche synneden, and maden Israel to do synne, and wraththiden the Lord God of Israel in her vanytees.
14 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ela, na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Sotheli the residue of the wordis of Hela, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
15 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala huko Tirsa siku saba. Jeshi lilikuwa limepiga kambi karibu na Gibethoni, mji wa Wafilisti.
In the seuene and twentithe yeer of Aza, kyng of Juda, Zamri regnede seuene daies in Tharsa; forsothe the oost bisegide Gebethon, the citee of Philisteis.
16 Wakati Waisraeli waliokuwa kambini waliposikia kuwa Zimri alikuwa amefanya hila mbaya dhidi ya mfalme na kumuua, wakamtangaza Omri, jemadari wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli siku iyo hiyo huko kambini.
And whanne it hadde herd, that Zamri hadde rebellid, and hadde slayn the kyng, al Israel made Amry kyng to hem, that was prince of the chyualrye, on Israel, in that dai, in `the castels.
17 Ndipo Omri na Waisraeli wote pamoja naye wakaondoka Gibethoni na kuizingira Tirsa.
Therfor Amry stiede, and al Israel with hym, fro Gebethon, and bisegide Thersa.
18 Wakati Zimri alipoona kuwa mji umechukuliwa, alikwenda ndani ya ngome ya jumba la kifalme na kulichoma moto jumba la kifalme na kujiteketeza ndani yake. Kwa hiyo akafa,
Sothely Zamri siy, that the citee schulde be ouercomun, and he entride in to the palis, and brente hym silf with the kyngis hows;
19 kwa sababu ya dhambi alizofanya, akitenda maovu machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Yeroboamu na katika dhambi alizofanya na kusababisha Israeli kuzifanya.
and he was deed in hise synnes whiche he synnede, doynge yuel bifor the Lord, and goynge in the weie of Jeroboam, and in hise synnes, bi whiche he made Israel to do synne.
20 Kwa matukio mengine ya utawala wa Zimri, na uasi alioutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Sotheli the residue of wordis of Zamri, and of his tresouns, and tyrauntrie, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
21 Ndipo watu wa Israeli wakagawanyika katika makundi mawili, nusu wakamuunga mkono Tibni mwana wa Ginathi ili awe mfalme na nusu nyingine wakamuunga mkono Omri.
Thanne the puple of Israel was departid in to twei partis; the half part of the puple suede Thebny, sone of Geneth, to make hym kyng, and the half part suede Amry.
22 Lakini wafuasi wa Omri wakajionyesha wenye nguvu kuliko wale wa Tibni mwana wa Ginathi. Hivyo Tibni akafa na Omri akawa mfalme.
Sotheli the puple that was with Amry, hadde maystry ouer the puple that suede Thebny, the sone of Geneth; and Thebny was deed, and Amri regnede.
23 Katika mwaka wa thelathini na moja wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili, sita kati ya hiyo katika Tirsa.
In the oon and thrittithe yeer of Aza, kyng of Juda, Amri regnede on Israel, twelue yeer; in Thersa he regnede sixe yeer.
24 Alinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha na akajenga mji juu ya hicho kilima, akiuita Samaria, kutokana na Shemeri, jina la mmiliki wa kwanza wa kilima hicho.
And he bouyte of Soomeer, for twei talentis of siluer, the hil of Samarie, and `bildide that hil; and he clepide the name of the citee, which he hadde bildid, bi the name of Soomer, lord of the hil of Samarie.
25 Lakini Omri akatenda maovu machoni pa Bwana na kutenda dhambi kuliko wote waliomtangulia.
Forsothe Amry dide yuel in the siyt of the Lord, and wrouyte weiwardli, ouer alle men that weren bifor hym.
26 Akaenenda katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake, ambazo alisababisha Israeli kutenda, hivyo basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
And he yede in al the weie of Jeroboam, sone of Nabath, and in hise synnes, bi whiche he made Israel to do synne, that he schulde terre to ire, in his vanytees, the Lord God of Israel.
27 Kwa matukio mengine ya utawala wa Omri, yale aliyofanya na vitu alivyovifanikisha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Forsothe the residue of wordis of Amry, and hise batels, which he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
28 Omri akalala pamoja na baba zake na akazikwa huko Samaria. Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.
And Amry slepte with hise fadris, and was biried in Samarie; and Achab, his sone, regnede for hym.
29 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili.
Forsothe Achab, the sone of Amry, regnede on Israel, in the `eiyte and thrittithe yeer of Asa, kyng of Juda; and Achab, sone of Amry, regnede on Israel, in Samarie, two and twenti yeer.
30 Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa Bwana kuliko yeyote aliyewatangulia.
And Achab, sone of Amry, dide yuel in the siyte of the Lord, ouer alle men that weren bifor hym;
31 Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu.
and it suffiside not to hym that he yede in the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, ferthermore and he weddide a wijf, Jezabel, the douyter of Methaal, kyng of Sydoneis; and he yede, and seruyde Baal, and worschipide hym.
32 Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria.
And he settide an auter to Baal in the temple of Baal, which he hadde bildid in Samarie, and he plauntide a wode;
33 Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.
and Achab addide in his werk, and terride to ire the Lord God of Israel, more thanne alle kyngis of Israel that weren bifor hym.
34 Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la Bwana alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.
Forsothe in hise daies Ahiel of Bethel bildide Jerico; in Abiram, his firste sone, he foundide it, in Segub, his laste sone, he settide yatis therof, bi the word of the Lord, which he hadde spoke in the hond of Josue, sone of Nun.

< 1 Wafalme 16 >