< 1 Wafalme 16 >

1 Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani dhidi ya Baasha, kusema:
Then the word of the Lord came to Jehu, the son of Hanani, against Baasha, saying:
2 “Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao.
“Even though I exalted you from the dust, and I set you as ruler over my people Israel, still you have walked in the way of Jeroboam, and you have caused my people Israel to sin, so that you have provoked me by their sins.
3 Basi nitamwangamiza Baasha pamoja na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwanawe Nebati.
Behold, I will cut down the posterity of Baasha, and the posterity of his house. And I will make your house like the house of Jeroboam, the son of Nebat.
4 Mbwa watawala watu wa Baasha watakaofia mjini na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.”
Whoever will have died of Baasha in the city, the dogs will consume him. And whoever will have died of him in the countryside, the birds of the air will consume him.”
5 Kwa matukio mengine ya utawala wa Baasha, aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Now the rest of the words of Baasha, and whatever he did, and his battles, were these not written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
6 Baasha akalala na baba zake naye akazikwa huko Tirsa. Naye Ela mwanawe akawa mfalme baada yake.
Then Baasha slept with his fathers, and he was buried at Tirzah. And Elah, his son, reigned in his place.
7 Zaidi ya hayo, neno la Bwana likamjia Baasha pamoja na nyumba yake kupitia kwa nabii Yehu mwana wa Hanani, kwa sababu ya maovu yote aliyokuwa ametenda machoni pa Bwana, akamkasirisha kwa mambo aliyotenda, na kuwa kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu aliiangamiza.
And when the word of the Lord had arrived by the hand of the prophet Jehu, the son of Hanani, against Baasha, and against his house, and against every evil that he had done before the Lord, so that he provoked him by the works of his hands, so that he became like the house of Jeroboam: for this reason, he killed him, that is, the prophet Jehu, the son of Hanani.
8 Katika mwaka wa ishirini na sita wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala huko Tirsa kwa miaka miwili.
In the twenty-sixth year of Asa, the king of Judah, Elah, the son of Baasha, reigned over Israel, at Tirzah, for two years.
9 Zimri, mmoja wa maafisa wake, aliyekuwa na amri juu ya nusu ya magari yake ya vita, akafanya hila mbaya dhidi ya Ela. Wakati huo Ela alikuwa Tirsa, akilewa katika nyumba ya Arsa, mtu aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme huko Tirsa.
And his servant Zimri, the commander of one half part of the horsemen, rebelled against him. Now Elah was drinking at Tirzah, and he became inebriated in the house of Arza, the prefect of Tirzah.
10 Zimri akaingia, akampiga na kumuua katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda. Kisha Zimri akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Then Zimri, rushing in, struck him and killed him, in the twenty-seventh year of Asa, the king of Judah. And he reigned in his place.
11 Mara tu alipoanza kutawala na kuketi juu ya kiti cha ufalme, aliua jamaa yote ya Baasha. Hakumwacha mwanaume hata mmoja, akiwa ni ndugu au rafiki.
And when he had reigned and had sat upon his throne, he struck down the entire house of Baasha. And he did not leave behind of them anything that urinates against a wall, among both close relatives and his friends.
12 Hivyo Zimri akaangamiza jamaa yote ya Baasha, kulingana na neno la Bwana lililonenwa dhidi ya Baasha kupitia nabii Yehu:
And so, Zimri destroyed the entire house of Baasha, in accord with the word of the Lord, which he had spoken to Baasha, by the hand the prophet of Jehu,
13 kwa sababu ya dhambi zote Baasha na mwanawe Ela walizokuwa wametenda na wakasababisha Israeli kuzitenda, basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
because of all the sins of Baasha, and the sins of Elah, his son, who sinned and caused Israel to sin, provoking the Lord, the God of Israel, with their vanities.
14 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ela, na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
But the rest of the words of Elah, and all that he did, were these not written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
15 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala huko Tirsa siku saba. Jeshi lilikuwa limepiga kambi karibu na Gibethoni, mji wa Wafilisti.
In the twenty-seventh year of Asa, the king of Judah, Zimri reigned for seven days in Tirzah. For the army was besieging Gibbethon, a city of the Philistines.
16 Wakati Waisraeli waliokuwa kambini waliposikia kuwa Zimri alikuwa amefanya hila mbaya dhidi ya mfalme na kumuua, wakamtangaza Omri, jemadari wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli siku iyo hiyo huko kambini.
And when they had heard that Zimri had rebelled, and that he had killed the king, all of Israel made Omri as a king for themselves; he was the leader of the military over Israel in the encampment in that day.
17 Ndipo Omri na Waisraeli wote pamoja naye wakaondoka Gibethoni na kuizingira Tirsa.
Therefore, Omri ascended, and all of Israel with him, from Gibbethon, and they besieged Tirzah.
18 Wakati Zimri alipoona kuwa mji umechukuliwa, alikwenda ndani ya ngome ya jumba la kifalme na kulichoma moto jumba la kifalme na kujiteketeza ndani yake. Kwa hiyo akafa,
Then Zimri, seeing that the city was about to be taken, entered the palace, and he set fire to himself along with the royal house. And he died
19 kwa sababu ya dhambi alizofanya, akitenda maovu machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Yeroboamu na katika dhambi alizofanya na kusababisha Israeli kuzifanya.
in his sins, which he had sinned, doing evil before the Lord, and walking in the way of Jeroboam, and in his sin, by which he caused Israel to sin.
20 Kwa matukio mengine ya utawala wa Zimri, na uasi alioutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
But the rest of the words of Zimri, and of his treachery and tyranny, were these not written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
21 Ndipo watu wa Israeli wakagawanyika katika makundi mawili, nusu wakamuunga mkono Tibni mwana wa Ginathi ili awe mfalme na nusu nyingine wakamuunga mkono Omri.
Then the people of Israel were divided into two parts: one half part of the people followed Tibni, the son of Ginath, having appointed him as king, and one half part followed Omri.
22 Lakini wafuasi wa Omri wakajionyesha wenye nguvu kuliko wale wa Tibni mwana wa Ginathi. Hivyo Tibni akafa na Omri akawa mfalme.
But the people who were with Omri prevailed over the people who were following Tibni, the son of Ginath. And Tibni died, and Omri reigned.
23 Katika mwaka wa thelathini na moja wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili, sita kati ya hiyo katika Tirsa.
In the thirty-first year of Asa, the king of Judah, Omri reigned over Israel for twelve years; he reigned for six years at Tirzah.
24 Alinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha na akajenga mji juu ya hicho kilima, akiuita Samaria, kutokana na Shemeri, jina la mmiliki wa kwanza wa kilima hicho.
And he bought the mount of Samaria from Shemer for two talents of silver. And he built upon it, and he called the name of the city that he had built, Samaria, after the name of Shemer, the owner of the mount.
25 Lakini Omri akatenda maovu machoni pa Bwana na kutenda dhambi kuliko wote waliomtangulia.
But Omri did evil in the sight of the Lord, and he wrought wickedness, beyond all who had been before him.
26 Akaenenda katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake, ambazo alisababisha Israeli kutenda, hivyo basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
And he walked in all the ways of Jeroboam, the son of Nebat, and in his sins, by which he had caused Israel to sin, so that he provoked the Lord, the God of Israel, by their vanities.
27 Kwa matukio mengine ya utawala wa Omri, yale aliyofanya na vitu alivyovifanikisha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Now the rest of the words of Omri, and his battles that he carried out, were these not written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
28 Omri akalala pamoja na baba zake na akazikwa huko Samaria. Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.
And Omri slept with his fathers, and he was buried in Samaria. And Ahab, his son, reigned in his place.
29 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili.
Truly, Ahab, the son of Omri, reigned over Israel in the thirty-eighth year of Asa, the king of Judah. And Ahab, the son of Omri, reigned over Israel at Samaria for twenty-two years.
30 Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa Bwana kuliko yeyote aliyewatangulia.
And Ahab, the son of Omri, did evil in the sight of the Lord, beyond all who had been before him.
31 Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu.
And it was not enough for him to walk in the sins of Jeroboam, the son of Nebat. In addition, he took as a wife Jezebel, the daughter of Eth-baal, the king of the Sidonians. And he went astray, and he served Baal, and adored him.
32 Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria.
And he set up an altar for Baal, in the temple of Baal, which he had built at Samaria.
33 Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.
And he planted a sacred grove. And Ahab added to his works, provoking the Lord, the God of Israel, beyond all the kings of Israel who had been before him.
34 Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la Bwana alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.
In his days, Hiel from Bethel built up Jericho. With Abiram, his firstborn, he founded it, and with Segub, his youngest son, he set up its gates, in accord with the word of the Lord, which he had spoken by the hand of Joshua, the son of Nun.

< 1 Wafalme 16 >