< 1 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
C’Est dans la dix-huitième année du règne de Jéroboam, fils de Nebat, qu’Abiam devint roi de Juda.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
Il régna trois ans à Jérusalem. Sa mère se nommait Maakha, fille d’Abichalom.
3 Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
Il se rendit coupable de tous les péchés que son père avait commis avant lui, et son cœur n’appartint pas sans partage à l’Eternel, son Dieu, comme le cœur de son aïeul David.
4 Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
Car, c’est en faveur de David que l’Eternel, son Dieu, lui avait accordé un domaine en Jérusalem, voulant conserver son descendant après lui et assurer la durée de Jérusalem;
5 Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
parce que David avait fait ce qui est droit aux yeux de l’Eternel et n’avait contrevenu, toute sa vie, à aucune de ses prescriptions, à part l’affaire d’Urie, le Héthéen.
6 Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
Il y eut guerre entre Roboam et Jéroboam tout le temps de sa vie.
7 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
Pour le surplus des faits et gestes d’Abiam, ils sont mentionnés dans le livre des annales des rois de Juda, ainsi que la guerre entre Abiam et Jéroboam.
8 Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
Abiam reposa avec ses pères, et fut enseveli dans la Cité de David. Asa, son fils, lui succéda.
9 Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
C’Est dans la vingtième année du règne de Jéroboam sur Israël qu’Asa devint roi de Juda.
10 naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
Il régna quarante et un ans à Jérusalem. Le nom de sa mère était Maakha, fille d’Abichalom.
11 Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
Asa fit ce qui est agréable au Seigneur, à l’exemple de son aïeul David.
12 Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
Il fit disparaître du pays ceux qui se prostituaient, et il en éloigna toutes les impures idoles faites par ses pères.
13 Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
Il destitua même de la régence sa mère Maakha, qui avait consacré une image à Achéra; par l’ordre d’Asa, cette image fut abattue et brûlée dans la vallée de Cédron.
14 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
Toutefois, les hauts-lieux ne disparurent point; mais le cœur d’Asa resta fidèle à l’Eternel, son Dieu, toute sa vie.
15 Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Il fit porter dans la maison du Seigneur ce que son père et lui-même avaient consacré en fait d’argent, d’or et de vases précieux.
16 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
Il y eut guerre entre lui et Baasa, roi d’Israël, toute leur vie.
17 Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
Baasa, roi d’Israël, étant venu attaquer Juda, fortifia Rama pour ne pas laisser l’entrée libre à Asa, roi de Juda.
18 Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
Alors Asa prit tout l’argent et l’or qui restaient dans les trésors du temple, joints aux trésors de la maison du roi, les remit à ses serviteurs et les envoya à Ben-Hadad, fils de Tabrimmôn, fils de Hezyôn, roi de Syrie, résidant à Damas, avec ces paroles:
19 “Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
"Toi et moi soyons alliés, comme mon père fut allié du tien. Je t’envoie un cadeau d’argent et d’or, afin que tu rompes ton alliance avec Baasa, roi d’Israël, et qu’il se retire de chez moi."
20 Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
Ben-Hadad, accédant à la demande d’Asa, envoya ses généraux contre les villes d’Israël, et prit de vive force Iyyôn, Dan, Abel-Beth-Maakha, toute la région de Kinnerot avec tout le territoire de Nephtali.
21 Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
Lorsque Baasa en fut informé, il renonça à fortifier Rama et s’établit à Tirça.
22 Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
Le roi Asa convoqua alors tous les gens de Juda, sans dispenser personne; et ils enlevèrent les pierres et le bois employés par Baasa aux travaux de Rama; Asa s’en servit pour fortifier Ghéba-en-Benjamin et Miçpa.
23 Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
Pour le surplus de l’histoire d’Asa, ses exploits et ses travaux, et les villes qu’il a bâties, tous ces faits sont consignés dans le livre des annales des rois de Juda; il est à noter seulement que, dans sa vieillesse, il eut les pieds malades.
24 Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
Asa s’endormit avec ses pères et fut inhumé auprès d’eux dans la Cité de David, son aïeul. Josaphat, son fils, régna à sa place.
25 Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
Nadab, fils de Jéroboam, devint roi d’Israël la seconde année du règne d’Asa, roi de Juda, et régna deux ans sur Israël.
26 Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
Il fit ce qui déplaît à l’Eternel, imitant la conduite de son père et les péchés qu’il avait fait commettre à Israël.
27 Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
Baasa, fils d’Ahiyya, de la maison d’Issachar, conspira contre lui et le fit périr à Ghibetôn, ville des Philistins, tandis que Nadab et tout Israël assiégeaient cette ville.
28 Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
C’Est la troisième année du règne d’Asa, roi de Juda, que Baasa tua Nadab, à qui il succéda.
29 Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
Devenu roi, il extermina toute la famille de Jéroboam, n’en épargnant pas une âme, jusqu’à ce qu’il l’eût anéantie, ainsi que le Seigneur l’avait annoncé par l’organe de son serviteur Ahiyya, de Silo,
30 kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
à cause des péchés que Jéroboam avait commis et fait commettre à Israël, provoquant ainsi la colère du Seigneur, Dieu d’Israël.
31 Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Quant au reste de l’histoire et des actes de Nadab, ils sont consignés dans le livre des annales des rois d’Israël.
32 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
Il y eut guerre entre Asa et Baasa, toute leur vie.
33 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
C’Est dans la troisième année d’Asa, roi de Juda, que Baasa, fils d’Ahiyya, devint roi de tout Israël; il résida à Tirça et régna vingt-quatre ans.
34 Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.
Il fit ce qui déplaît au Seigneur, imitant la conduite de Jéroboam et les péchés qu’il avait fait commettre à Israël.

< 1 Wafalme 15 >