< 1 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
And in the eighteenth yeere of King Ieroboam the sonne of Nebat, reigned Abiiam ouer Iudah.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
Three yeere reigned hee in Ierusalem, and his mothers name was Maachah the daughter of Abishalom.
3 Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
And hee walked in all the sinnes of his father, which hee had done before him: and his heart was not perfit with the Lord his God as the heart of Dauid his father.
4 Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
But for Dauids sake did the Lord his God giue him a light in Ierusalem, and set vp his sonne after him, and established Ierusalem,
5 Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
Because Dauid did that which was right in the sight of the Lord, and turned from nothing that he commanded him, all the dayes of his life, saue onely in the matter of Vriah the Hittite.
6 Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
And there was warre betweene Rehoboam and Ieroboam as long as he liued.
7 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
The rest also of the actes of Abiiam, and all that he did, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Iudah? there was also warre betweene Abiiam, and Ieroboam.
8 Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Abiiam slept with his fathers, and they buried him in the citie of Dauid: and Asa his sonne reigned in his steade.
9 Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
And in the twentie yeere of Ieroboam King of Israel reigned Asa ouer Iudah.
10 naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
He reigned in Ierusalem one and fourtie yeere, and his mothers name was Maachah the daughter of Abishalom.
11 Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
And Asa did right in the eyes of the Lord, as did Dauid his father.
12 Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
And he tooke away the Sodomites out of the lande, and put away all the idoles that his fathers had made.
13 Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
And he put downe Maachah his mother also from her estate, because shee had made an idole in a groue: and Asa destroyed her idoles, and burnt them by the brooke Kidron.
14 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
But they put not downe the hie places. Neuertheles Asas heart was vpright with the Lord all his dayes.
15 Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Also he brought in the holy vessels of his father, and the things that he had dedicated vnto ye house of the Lord, siluer, and golde, and vessels.
16 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
And there was warre betweene Asa and Baasha King of Israel all their dayes.
17 Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
Then Baasha king of Israel went vp against Iudah, and buylt Ramah, so that he woulde let none go out or in to Asa King of Iudah.
18 Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
Then Asa tooke all the siluer and the gold that was left in the treasures of the house of the Lord, and the treasures of the kings house, and deliuered them into the handes of his seruantes, and King Asa sent them to Ben-hadad the sonne of Tabrimon, the sonne of Hezion king of Aram that dwelt at Damascus, saying,
19 “Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
There is a couenant betweene me and thee, and betweene my father and thy father: behold, I haue sent vnto thee a present of siluer and golde: come, breake thy couenant with Baasha King of Israel, that he may depart from me.
20 Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
So Ben-hadad hearkened vnto King Asa, and sent the captaines of the hosts, which he had, against the cities of Israel, and smote lion, and Dan, and Abel-beth-maachah, and all Cinneroth, with all the land of Naphtali.
21 Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
And when Baasha heard thereof, hee left buylding of Ramah, and dwelt in Tirzah.
22 Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
Then king Asa assembled al Iudah, none excepted. and they tooke the stones of Ramah, and the timber thereof, wherewith Baasha had buylt, and King Asa built with them Geba of Beniamin and Mizpah.
23 Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
And the rest of all the actes of Asa, and all his might, and all that he did, and the cities which he buylt, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Iudah? but in his olde age he was diseased in his feete.
24 Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Asa slept with his fathers, and was buried with his fathers in the citie of Dauid his father. And Iehoshaphat his sonne reigned in his steade.
25 Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
And Nadab the sonne of Ieroboam began to reigne ouer Israel the second yere of Asa King of Iudah, and reigned ouer Israel two yeere.
26 Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
And he did euill in the sight of the Lord, walking in the way of his father, and in his sinne wherewith he made Israel to sinne.
27 Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
And Baasha the sonne of Ahijah of ye house of Issachar conspired against him, and Baasha slue him at Gibbethon, which belonged to the Philistims: for Nadab and all Israel layde siege to Gibbethon.
28 Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Euen in the third yeere of Asa King of Iudah did Baasha slay him, and reigned in his steade.
29 Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
And when he was King, he smote all the house of Ieroboam, he left none aliue to Ieroboam, vntill hee had destroyed him, according to the word of the Lord which he spake by his seruant Ahijah the Shilonite,
30 kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
Because of the sinnes of Ieroboam which he committed, and wherewith he made Israel to sinne, by his prouocation, wherewith he prouoked the Lord God of Israel.
31 Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
And the residue of the actes of Nadab, and all that he did, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Israel?
32 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
And there was warre betweene Asa and Baasha King of Israel, all their dayes.
33 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
In the thirde yeere of Asa King of Iudah, began Baasha the sonne of Ahijah to reigne ouer all Israel in Tirzah, and reigned foure and twentie yeeres.
34 Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.
And he did euill in the sight of the Lord, walking in the way of Ieroboam, and in his sinne, wherewith he made Israel to sinne.

< 1 Wafalme 15 >