< 1 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
Léta pak osmnáctého království Jeroboáma syna Nebatova, kraloval Abiam nad Judou.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
Tři léta kraloval v Jeruzalémě. A jméno matky jeho bylo Maacha, dcera Abissalomova.
3 Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
Ten chodil ve všech hříších otce svého, kteréž páchal před oblíčejem jeho; a nebylo srdce jeho celé při Hospodinu Bohu jeho, jako srdce Davida otce jeho.
4 Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
A však pro Davida dal jemu Hospodin Bůh jeho svíci v Jeruzalémě, vzbudiv syna jeho po něm, a utvrdiv Jeruzalém,
5 Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
Proto že David činil to, což bylo dobrého před Hospodinem, a neuchýlil se od žádné věci z těch, kteréž jemu byl přikázal, po všecky dny života svého, kromě skutku při Uriášovi Hetejském.
6 Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
A byl boj mezi Roboámem a Jeroboámem po všecky dny života jeho.
7 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
Jiné pak věci Abiamovy, a všecko což činil, popsáno jest v knize o králích Judských, ano i o boji mezi Abiamem a Jeroboámem.
8 Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
A když usnul Abiam s otci svými, pochovali ho v městě Davidově. I kraloval Aza syn jeho místo něho.
9 Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
A tak léta dvadcátého Jeroboáma, krále Izraelského, kraloval Aza nad Judou.
10 naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
Jedno a čtyřidceti let kraloval v Jeruzalémě. A jméno matky jeho bylo Maacha, dcera Abissalomova.
11 Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
I činil Aza, což dobrého bylo před Hospodinem, jako David otec jeho.
12 Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
Nebo ohyzdné sodomáře vyplénil z země, a odjal všecky modly, kterýchž nadělali otcové jeho.
13 Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
Nadto i Maachu matku svou ssadil, aby nebyla královnou; nebo byla udělala hroznou modlu v háji. Protož podťal Aza modlu tu ohyzdnou, a spálil při potoku Cedron.
14 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
A ačkoli výsosti nebyly zkaženy, a však srdce Azovo bylo celé při Bohu po všecky dny jeho.
15 Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Vnesl také ty věci, kteréž posvěceny byly od otce jeho, i ty věci, kterýchž sám posvětil, do domu Hospodinova, stříbro a zlato i nádoby.
16 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
Pročež byla válka mezi Azou a Bázou, králem Izraelským, po všecky dny jejich.
17 Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
Nebo Báza král Izraelský vytáhl proti Judovi, a stavěl Ráma, aby nedal žádnému vyjíti ani jíti k Azovi králi Judskému.
18 Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
Ale vzav Aza všecko stříbro i zlato, kteréž pozůstalo v pokladích domu Hospodinova, a v pokladích domu královského, dal je v ruce služebníků svých, a poslal je král Aza k Benadadovi synu Tabremmon, syna Hezion, králi Syrskému, kterýž bydlil v Damašku, řka:
19 “Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
Smlouva jest mezi mnou a mezi tebou, mezi otcem mým a mezi otcem tvým. Aj, teď posílám tobě dar, stříbro a zlato; jdi, zruš smlouvu svou s Bázou králem Izraelským, ať odtrhne ode mne.
20 Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
I uposlechl Benadad krále Azy, a poslav knížata s vojsky svými proti městům Izraelským, dobyl Jon a Dan, též Abelbetmaachy, i všeho Ceneretu, a vší země Neftalím.
21 Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
To když uslyšel Báza, přestal stavěti Ráma, a zůstal v Tersa.
22 Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
Tedy král Aza provolal po všem Judstvu, žádného nevyměňuje. I pobrali to kamení z Ráma, i dříví jeho, z něhož stavěl Báza, a vystavěl z toho král Aza Gabaa Beniaminovo a Masfa.
23 Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
Jiné pak všecky věci Azovy, i všecka síla jeho a cokoli dělal, i jaká města vystavěl, zapsáno jest v knize o králích Judských. Jen že v věku starosti své byl nemocný na nohy.
24 Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
I usnul Aza s otci svými, a pochován jest s nimi v městě Davida otce svého. A kraloval místo něho Jozafat syn jeho.
25 Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
Nádab pak syn Jeroboámův, počal kralovati nad Izraelem léta druhého Azy, krále Judského, a kraloval nad Izraelem dvě létě.
26 Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
A činil to, což zlého jest před očima Hospodinovýma, chodě po cestě otce svého, v hříších jeho, jimiž k hřešení přivodil lid Izraelský.
27 Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
I činil mu úklady Báza syn Achiášův z domu Izachar, a porazil ho Báza u Gebbeton, kteréž bylo Filistinských. Nádab zajisté a všickni Izraelští oblehli byli Gebbeton.
28 Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
A tak zabil ho Báza léta třetího Azy, krále Judského, a kraloval místo něho.
29 Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
I stalo se, když počal kralovati, že zahubil všecken dům Jeroboámův, a nepozůstavil žádné duše z Jeroboáma, až je i vyhladil vedlé řeči Hospodinovy, kterouž byl mluvil skrze služebníka svého Achiáše Silonského,
30 kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
Pro hříchy Jeroboámovy, jimiž hřešil, a jimiž k hřešení přivodil lid Izraelský, pro dráždění jeho, kterýmž dráždil Hospodina Boha Izraelského.
31 Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Jiné pak věci Nádabovy a všecko, což činil, zapsáno jest v knize o králích Izraelských.
32 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
Byla tedy válka mezi Azou, a mezi Bázou králem Izraelským, po všecky dny jejich.
33 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
Léta třetího Azy, krále Judského, kraloval Báza syn Achiášův nade vším Izraelem v Tersa za čtyřmecítma let.
34 Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.
A činil to, což zlého jest před Hospodinem, chodě po cestě Jeroboámově a v hříších jeho, jimiž k hřešení přivodil Izraele.

< 1 Wafalme 15 >