< 1 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
Jeroboam in Israel chunga ahung vaihomna kum somle get lhin kum in, Abijah in Judahhte chung’ah vaihom in ahung pang in ahi.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
Aman Jerusalem ah kum thum vai ana hom in. Anu chu Absalom chanu Maacah ahi.
3 Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
Aman jong, ama masanga leng vaihom hobang bangin, thilse jeng ana bol in, apului David kitah bang in a Pakai a Pathen ah ana kitah joupon ahi.
4 Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
Ahin David jal’a, Pakai Pathen in achilhahte aban banna thaomeivah banga vah dinga vaihomna mun ahin ban losah ahin, achapa Abijah jong chu ama nunga Jerusalema vai ahin hop sah ahi.
5 Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
Ajeh chu David in a Pakai mit mu’a apha jeng ana bol’a, Pakai thupeh hoitah’a ahinkho lhumkeiya ana jui lhung kei ahin, Hit mi Uriah chung’a ana kipal bou chu ahi.
6 Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
Hiche Abijah leh Jeroboam vaihom sung hin aki kah lhon ah gal kisattona ana um mat chat jingin ahi.
7 Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
Abijah vaihom sunga thilsoh dangho Judahh lengte thusim kijih na Lekhabu a aum soh kei jin ahi. Abijah le Jeroboam kikah a gal ana umjing in ahi.
8 Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
Abijah athi phat in David khopia ana kivui jin ahi. Hijou chun achapa Asa chu leng ahung chang in ahi.
9 Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
Jeroboam in Israel chung’a vai ana hom na kum somni ahung lhin hin, Judahh chung’a Asa in vai ahin hom pan in ahi.
10 naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
Aman Jerusalema kum somli le khat vai ana hom in ahi. Api chu Abshalom chanu Maacah ahi.
11 Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
Asa hin apului David bang in Pakai mit un alung lhaina ngen ana bol lin ahi.
12 Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
Aman gamsunga numei pasal kijoh ho doiphung ho jouse chu anapaidoh in chuleh apu apaten ana hou’u doiho jong sumang gam’in ahi.
13 Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
Aman api Maacah jeng jong Lengnu nu ahina akonin ana haisah in ahi, ajeh chu aman thet umtah Asherah doi ana kisem jeh ahi. Aman kidah umtah adoi hochu asat lhan Kidron phaicham lamah aga hal lhan ahi.
14 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
Aman doiphung ho jouse chu ana suhmanglou vang'in, aman ahinkho lhung keijin kitah tah’in Pakai anajui lhung keijin ahi.
15 Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Apaleh aman, sana le dangka chuleh thildang dangho ahin ana kat dohsa lhon hochu Pakai Houin ana polut'in ahi.
16 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
Judahh lengpa Asa leh Israel lengpa Baasha teni kikah in gal anaum jingin ahi.
17 Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
Israel leng Baasha in Judahh gam ahinsat in, Judahhte leng Asa gamsunga mi alut le apot aumthei louna dingin Ramah chu kulpi aget khumin ahi.
18 Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
Asa in hiche lethuh na in, Pakai Houin sungle Leng inpia sum kholna a sana dangka ho jouse chu alahdoh in, hichu Hezion tupa Benhadad, Tabrimon chapa Syria Lengpa chu aga pehsah in thu hicheng jong athot in ahi.
19 “Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
“Napa le kapa kikah a kinoptona anaum bang bang chun, tunjong nang le kei kikah ajong kinoptona nei hite. Ven keiman sana le dangka kipa thilpeh, ka hinthot in ahi. Israel Lengpa Baasha toh kinoptona naneilhon chu sukeh in, chutileh aman keima ei dalha in tin ei suboi ta ponte,” ati.
20 Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
Asa Lengpa tepna chu Benhadad in jong ana noppeh in, Israel khopi ho nokhum dingin asepaite asoltan ahi. Hitichun amahon Ijon, Dan, Abel-beth-maacah chuleh Kinnereth pumpi leh Naphtali gam pumpi ana banjo gam tauvin ahi.
21 Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
Israel Lengpa Baasha chun thilsoh hochu ajahdoh phat in, Ramah khopi chu kulpi akaikhum na a kon chun aki nungle in Tirzah langa achetan ahi.
22 Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
Hichun Asa lengpa Judahh gamsung a mijousen Baasha in Ramah a umkhum kulpi semna a amanchah songle thingho chu lhoh mang dingin thu apen ahi. Asa in hiche hochu Benjamin gamsunga um Giba khopi leh Mizpah khopi pal getkhum na in amang tan ahi.
23 Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
Asa vaihomna sunga thilsohho leh atha neina dungjuija ana toh le thilbol ho chuleh khopi ana tundoh minho chu Judahh Lengte thusim kijih lutna Lekhabua chun aum in ahi. Ateh lang in akeng ahung natan ahi.
24 Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
Asa athi phat in ama chu apu apate toh David khopiah anavui tauvin ahi. Hijeh chun Asa chapa Jehosaphat chun Leng mun ahin lotan ahi.
25 Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
Judahh mite lah a Asa lengpan vai ahom akum ni channa in Jeroboam chapa Nadab chun Israelte lah’a vai ana hom in ahi. Aman Israelte lah a kumni vai ahom in ahi.
26 Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
Aman Pakai mitmu’n thilse jeng ana bol’in, apa natoh nung anajuijin, Jeroboam in Israel te ana chonset sah chu anache jompi in ahi.
27 Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
Hijouchun, Issachar phunga kona Ahijah chapa Baasha chun Nadab chu thading ana gon, aman asepaite toh Gibbethon kiti Philistina khopia chu ana nokhum got laitah in ana that tan ahi.
28 Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
Asa lengpan Judahh mite lah a vai ana hopna kum thum channa in Baasha in Nadab ana that in Israelte leng in anapang in ahi.
29 Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
Aman Jeroboam chilhahte abonchan ana that gamin, leng insunga mite chu khatcha ana hinghoi pon ahi. Hichehi Pakaiyin Shiloh’a, Ahijah Themgaopa mangcha a Jeroboam chung chang thu ana sei chu aguilhun na ahi tai.
30 kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
Hitobang thilsoh hi Jeroboam in Pakai Israel Pathen chu asuh lunghang jeh leh, ama chonset na chungchon na Israel mipite chu ana chonset sah jeh ahi.
31 Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Nadab in avaihom sunga thilsoh holeh aman ana toh thilho Israel lengte thusim kijihna lekhabu a aum in ahi.
32 Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
Judahh lengpa Asa leh Israel lengpa Baasha kikah a kidouna anaum jingin ahi.
33 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
Judahh gam’a Asa lengpan vai ahom kum thum channa in Ahijah chapa Baasha in Israel gam pumpia vai ana hom in ahi. Baasha in Tirzah a kum somni le li vai ana hom in ahi.
34 Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.
Ahin, amahon Jeroboam chonna dungjuijin Pakai mitmu’n thilse jeng ana bollin, Jeroboam min Israelte ana chonset sah chu aman jong ana che jom pin ahi.

< 1 Wafalme 15 >