< 1 Wafalme 14 >

1 Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
Ob tistem času je Jerobeámov sin Abíja zbolel.
2 naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
Jerobeám je rekel svoji ženi: »Vstani, prosim te in se preobleci, da te ne bodo spoznali, da si Jerobeámova žena in pojdi v Šilo. Glej, tam je prerok Ahíja, ki mi je povedal, da naj bi bil jaz kralj nad tem ljudstvom.
3 Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
S seboj vzemi deset hlebov, kolačke in vrč medu in pojdi k njemu. Povedal ti bo, kaj bo z otrokom.«
4 Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
Jerobeámova žena je tako storila, vstala, odšla v Šilo in prišla k Ahijevi hiši. Toda Ahíja je ni mogel videti, kajti njegove oči so zaradi starosti otemnele.
5 Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
Gospod je rekel Ahiju: »Glej, prihaja Jerobeámova žena, da od tebe prosi stvar za svojega sina, kajti on je bolan. Tako in tako ji boš rekel, kajti tako bo, ko bo vstopila, da se bo pretvarjala, da je druga ženska.«
6 Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
To je bilo tako, da ko je Ahíja zaslišal glas njenih stopal, ko je vstopila pri vratih, je rekel: »Vstopi, ti Jerobeámova žena; zakaj se pretvarjaš, da si druga? Kajti k tebi sem poslan s težkimi novicami.
7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
Pojdi, povej Jerobeámu: ›Tako govori Gospod, Izraelov Bog: ›Ker sem te povišal izmed ljudstva in te naredil princa nad svojim ljudstvom Izraelom
8 Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
in kraljestvo odtrgal od Davidove hiše in ga dal tebi; pa vendar ti nisi bil kakor moj služabnik David, ki je ohranjal moje zapovedi in ki mi je sledil z vsem svojim srcem, da počne samo to, kar je bilo pravilno v mojih očeh,
9 Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
temveč si storil zlo bolj kot vsi, ki so bili pred teboj, kajti odšel si in si naredil druge bogove in ulite podobe, da me dražiš do jeze in si me vrgel za svoj hrbet.
10 “‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
Zato glej, jaz bom nad Jerobeámovo hišo privedel zlo in od Jerobeáma bom iztrebil tistega, ki lula proti zidu in tistega, ki je zaprt in je ostal v Izraelu in odvzel bom preostanek Jerobeámove hiše, kakor človek odvaža gnoj, dokler ta ves ne izgine.
11 Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
Tistega, ki bo od Jerobeámovih umrl v mestu, bodo žrli psi. Tistega pa, ki umre na polju, bo žrla perjad neba, kajti Gospod je to govoril.
12 “Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
Vstani torej, pojdi k svoji lastni hiši in ko tvoja stopala vstopijo v mesto, bo otrok umrl.
13 Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
Ves Izrael bo žaloval za njim in ga pokopal, kajti on bo edini izmed Jerobeámovih prišel do groba, ker se je v Jerobeámovi hiši v njem našla neka dobra stvar do Gospoda, Izraelovega Boga.
14 “Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
Poleg tega si bo Gospod dvignil kralja nad Izraelom, ki bo tisti dan iztrebil Jerobeámovo hišo. Toda kaj? Celo sedaj.
15 Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
Kajti Gospod bo udaril Izraela, kakor se trst maje v vodi in Izraela bo izkoreninil iz te dobre dežele, ki jo je dal njihovim očetom in razkropil jih bo preko reke, ker so si naredili svoje ašere, izzivajoč Gospoda do jeze.
16 Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
Izraela se bo odrekel zaradi grehov Jerobeáma, ki je storil greh in ki je Izraela pripravil, da greši.‹«
17 Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
Jerobeámova žena je vstala, odšla in prišla v Tirco in ko je prišla k pragu vrat, je otrok umrl
18 Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
in pokopali so ga in ves Izrael je žaloval za njim, glede na Gospodovo besedo, ki jo je govoril po roki svojega služabnika, preroka Ahíja.
19 Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Ostala Jerobeámova dela, kako se je vojskoval in kako je kraljeval, glej, ta so zapisana v kroniški knjigi Izraelovih kraljev.
20 Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Dni, ko je Jerobeám kraljeval, je bilo dvaindvajset let in zaspal je s svojimi očeti in namesto njega je zakraljeval njegov sin Nadáb.
21 Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
Salomonov sin Rehabám je kraljeval v Judu. Rehabám je bil star enainštirideset let, ko je začel kraljevati in v Jeruzalemu je kraljeval sedemnajst let, mestu, ki ga je Gospod izbral izmed vseh Izraelovih rodov, da tam postavi svoje ime. Ime njegove matere je bilo Amónka Naáma.
22 Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
Juda je počel zlo v Gospodovih očeh in s svojimi grehi, ki so jih zagrešili, so ga dražili do ljubosumnosti, nad vsem, kar so počeli njihovi očetje.
23 Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
Kajti zgradili so si tudi visoke kraje, podobe in ašere na vsakem visokem hribu in pod vsakim zelenim drevesom.
24 Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
V deželi so bili tudi posvečeni vlačugarji in ti so počeli glede na vse ogabnosti narodov, ki jih je Gospod pregnal pred Izraelovimi otroki.
25 Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
Pripetilo se je v petem letu kralja Rehabáma, da je egiptovski kralj Šišák prišel gor nad Jeruzalem.
26 Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
Odnesel je zaklade Gospodove hiše in zaklade kraljeve hiše, celo vse je odnesel. Odnesel je vse zlate ščite, ki jih je Salomon naredil.
27 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
Kralj Rehabám je namesto njih naredil bronaste ščite in jih predal v roke vodje straže, ki je varoval vrata kraljeve hiše.
28 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
To je bilo tako, kadar je kralj odšel v Gospodovo hišo, da jih je straža nosila in jih [potem] ponovno odnesla v stražarnico.
29 Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Torej preostala izmed Rehabámovih dejanj in vse, kar je storil, mar niso zapisana v kroniški knjigi Judovih kraljev?
30 Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
Med Rehabámom in Jerobeámom pa je bila vse njune dni vojna.
31 Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.
Rehabám je zaspal s svojimi očeti in bil s svojimi očeti pokopan v Davidovem mestu. Ime njegove matere je bilo Amónka Naáma. Namesto njega je zakraljeval njegov sin Abíjam.

< 1 Wafalme 14 >