< 1 Wafalme 14 >
1 Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
Tegoż czasu rozniemógł się Abijas, syn Jeroboama.
2 naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
I rzekł Jeroboam do żony swej: Wstań teraz, a odmień się, aby nie poznano, żeś ty żoną Jeroboamową, a idź do Sylo; oto tam jest Achyjasz prorok, który mi powiedział, żem miał zostać królem nad tym ludem.
3 Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
A wziąwszy z sobą dziesięcioro chleba, i placków, i faskę miodu, idź do niego; on ci oznajmi, co się stanie dziecięciu.
4 Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
I uczyniła tak żona Jeroboamowa, a wstawszy poszła do Sylo, i weszła do domu Achyjaszowego; ale Achyjasz nie mógł już widzieć, bo mu były zaszły oczy dla starości jego.
5 Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
A Pan rzekł do Achyjasza: Oto żona Jeroboamowa wchodzi, aby się od ciebie czego wywiedziała o synu swym, przeto że choruje; ale tak a tak rzeczesz jej, a stanie się, gdy będzie wchodziła, zmyśli się być inszą.
6 Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
Przetoż gdy usłyszał Achyjasz tupanie nóg jej, wchodzącej we drzwi, rzekł: Wnijdź żono Jeroboamowa; przecz się zmyślasz być inszą? Jam bowiem srogim posłem do ciebie.
7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
Idź, powiedz Jeroboamowi: Tak mówi Pan, Bóg Izraelski: Ponieważem cię wywyższył z pośrodku ludu, a postanowiłem cię książęciem nad ludem moim Izraelskim;
8 Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
I oderwałem królestwo od domu Dawidowego, a dałem je tobie, tyś jednak nie był jako sługa mój Dawid, który strzegł rozkazania mego, i który chodził za mną całem sercem swojem, to tylko czyniąc, co jest dobrego w oczach moich;
9 Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
Aleś czynił złe nad wszystkie, którzy byli przed tobą; albowiem odszedłszy, poczyniłeś sobie bogi cudze, i lane, abyś mię pobudził do gniewu, a mnieś zarzucił w tył sobie:
10 “‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
Przetoż oto Ja przywiodę złe na dom Jeroboamowy, i wytracę z Jeroboama aż do najmniejszego szczenięcia, więźnia, i opuszczonego w Izraelu, i wymiotę ostatki domu Jeroboamowego, jako wymiatają gnój, aż do czysta.
11 Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
Tego, który z domu Jeroboamowego umrze w mieście, zjedzą psy, a który umrze na polu, zjedzą ptaki powietrzne, ponieważ Pan wyrzekł.
12 “Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
A ty wstawszy idź do domu twego a gdy wchodzić będziesz do miasta, tedy umrze dziecię.
13 Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
I będzie go płakał wszystek Izrael, i pochowają go; bo ten sam z domu Jeroboamowego wnijdzie do grobu, przeto iż się znalazło o nim samym słowo dobre od Pana, Boga Izraelskiego w domu Jeroboamowym.
14 “Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
Wszakże postanowi sobie Pan króla nad Izraelem, który wykorzeni dom Jeroboamowy dnia tego; a co mówię, wzbudzi? I owszem już wzbudził.
15 Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
I uderzy Pan Izraela, i zachwieje nim, jako się chwieje trzcina na wodach, a wykorzeni Izraela z ziemi tej dobrej, którą dał ojcom ich, i rozproszy je za rzekę, przeto iż sobie poczynili gaje, wzruszając Pana ku gniewu.
16 Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
A tak wyda Izraela dla grzechu Jeroboamowego, który grzeszył, i który do grzechu przywiódł Izraela.
17 Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
Tedy wstała żona Jeroboamowa, i poszła, a przyszła do Tersa; a gdy wstępowała na próg domu, umarło dziecię.
18 Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
I pochowali je, a płakał go wszystek Izrael według słowa Pańskiego, które opowiedział przez sługę swego Achyjasza proroka.
19 Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
A inne sprawy Jeroboamowe, jako walczył, i jako królował, oto spisane są w kronikach o królach Izraelskich.
20 Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
A dni, których królował Jeroboam, było dwadzieścia i dwa lat, i zasnął z ojcy swymi, a Nadab, syn jego, królował miasto niego.
21 Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
Roboam też, syn Salomona, królował w Judzie. A było Roboamowi czterdzieści lat i jeden, gdy począł królować, a siedmnaście lat królował w mieście Jeruzalemie, które Pan obrał ze wszystkich pokoleń Izraelskich, aby tam przebywało imię jego. A imię matki jego było Naama, Ammonitka.
22 Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
I czynił Juda złe przed Panem, a wzruszyli go ku gniewu grzechami swemi, któremi grzeszyli nad wszystko, co czynili ojcowie ich.
23 Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
Albowiem i oni pobudowali sobie wyżyny, i słupy, i gaje na każdym pagórku wysokim, i pod każdem drzewem zielonem.
24 Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
Byli też i Sodomczycy w onej ziemi, sprawujący się według wszystkich obrzydliwości poganów, które wyrzucił Pan od obliczności synów Izraelskich.
25 Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
I stało się roku piątego królowania Roboama, że wyciągnął Sesak, król Egipski, przeciw Jeruzalemowi.
26 Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
I pobrał skarby domu Pańskiego, i skarby domu królewskiego, wszystko to pobrał; wziął też wszystkie tarcze złote, które był sprawił Salomon;
27 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
Miasto których król Roboam sprawił tarcze miedziane, i poruczył je przełożonym nad piechotą, którzy strzegli drzwi domu królewskiego.
28 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
A gdy wchodził król do domu Pańskiego, brała je piechota, i zasię odnosiła do komor swoich.
29 Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
A inne sprawy Roboamowe, i wszystko co czynił, azaż nie są napisane w kronikach o królach Judzkich?
30 Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
I była wojna między Roboamem i między Jeroboamem po wszystkie dni.
31 Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.
I zasnął Roboam z ojcy swymi, a pochowany jest z nimi w mieście Dawidowem; a imię matki jego było Naama, Ammonitka. I królował Abijam, syn jego, miasto niego.