< 1 Wafalme 14 >
1 Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
Dans le même temps Abia, fils de Jéroboam, était malade.
2 naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
Et Jéroboam dit à sa femme: Lève-toi donc et te travestis, de sorte qu'on ne se doute pas que tu es la femme de Jéroboam, et va-t'en à Silo! Voici, là est Ahia, le prophète, qui m'a annoncé que je deviendrais le roi de ce peuple.
3 Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
Et prends dans ta main dix pains et des gâteaux et une cruche de miel, et entre chez lui: il te révélera ce qui arrivera à l'enfant.
4 Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
Et ainsi fit la femme de Jéroboam, et s'étant levée elle se rendit à Silo chez Ahia. Or Ahia avait perdu la vue, car l'âge rendait ses yeux obtus.
5 Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
Et l'Éternel avait dit à Ahia: Voici que la femme de Jéroboam vient pour requérir de toi un avis touchant son fils, parce qu'il est malade: tu lui parleras de telle et telle manière, et quand elle paraîtra, elle ne voudra pas être reconnue.
6 Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
Et lorsque Ahia entendit le bruit de ses pas, comme elle entrait dans la porte, il dit: Entre, femme de Jéroboam! pourquoi donc ne veux-tu pas être connue? Pour moi, j'ai pour toi un message sévère.
7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
Va, dis à Jéroboam: Ainsi parle l'Éternel, Dieu d'Israël: Parce que je t'ai élevé du sein du peuple, et établi prince de mon peuple d'Israël,
8 Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
et que j'ai détaché le royaume de la maison de David et te l'ai donné, mais que tu n'as pas imité mon serviteur David qui a gardé mes commandements et m'a suivi de tout son cœur pour ne faire que ce qui est droit à mes yeux,
9 Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
et parce que tu as fait pis que tous tes prédécesseurs, et que tu t'en es allé et t'es fait d'autres dieux et des images de fonte pour me provoquer et que tu m'as jeté en arrière de toi;
10 “‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
cela étant, voici je vais amener la calamité sur la maison de Jéroboam et j'arracherai à Jéroboam ceux qui pissent à la muraille, le mineur et l'émancipé en Israël, et je balaierai après la maison de Jéroboam comme on balaie les ordures, à fond.
11 Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
Ceux qui mourront à Jéroboam dans la ville, seront mangés par les chiens, et ceux qui mourront dans la campagne, seront mangés par les oiseaux du ciel; car l'Éternel a parlé.
12 “Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
Quant à toi, lève-toi et regagne ta maison! comme tu mettras le pied dans la ville, l'enfant mourra.
13 Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
Et tout Israël célébrera son deuil et lui donnera la sépulture, car seul de ceux de Jéroboam il recevra la sépulture, parce qu'il s'est trouvé en lui pour l'Éternel, Dieu d'Israël, quelque chose de bon dans la maison de Jéroboam.
14 “Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
Et l'Éternel se suscitera un roi dans Israël qui extirpera la maison de Jéroboam, née aujourd'hui et à naître encore.
15 Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
Et l'Éternel frappera Israël [à le faire branler] comme branle le jonc dans les eaux, et arrachera Israël de ce sol excellent qu'il avait donné à leurs pères, et les dispersera par delà le Fleuve, parce qu'ils se sont fait des Astartés, provoquant l'Éternel.
16 Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
Et il livrera Israël pour les péchés de Jéroboam, dont il s'est rendu coupable et où il a entraîné Israël.
17 Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
Et la femme de Jéroboam se leva et partit, et gagna Thirtsa; comme elle atteignit le seuil de la maison, l'enfant mourut.
18 Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
Et tout Israël lui donna la sépulture et célébra son deuil, selon la parole de l'Éternel qu'il avait dite par l'organe de son serviteur Ahia, le prophète.
19 Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Le reste des actes de Jéroboam, ses guerres et son règne sont d'ailleurs consignés dans le livre des annales des rois d'Israël.
20 Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et la durée du règne de Jéroboam fut de vingt-deux ans, et il reposa à côté de ses pères, et Nadab, son fils, régna en sa place.
21 Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
Et Roboam, fils de Salomon, régna sur Juda. Roboam, à son avènement, avait quarante-un ans, et il régna dix-sept ans à Jérusalem, la ville que l'Éternel avait choisie pour y placer son Nom, de préférence à toutes les Tribus d'Israël. Or le nom de sa mère était Naama, l'Ammonite.
22 Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
Et Juda fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, et ils L'irritèrent plus que tout ce qu'avaient fait leurs pères par les péchés dont ils s'étaient rendus coupables.
23 Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
Et ils se bâtirent, eux aussi, des tertres et des colonnes et des Astartés et des Aschères sur toute colline éminente et sous tout arbre verdoyant.
24 Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
Il y avait aussi des prostitués dans le pays; ils imitèrent toutes les infamies des nations que l'Éternel avait chassées devant les enfants d'Israël.
25 Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
Et la cinquième année du règne de Roboam, il arriva que Sisac, roi d'Egypte, s'avança contre Jérusalem.
26 Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
Et il enleva les Trésors du Temple de l'Éternel et les trésors du palais royal, et il enleva tout et enleva tous les boucliers d'or qu'avait faits Salomon.
27 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
Et pour les remplacer le roi Roboam fit des boucliers d'airain et il les commit aux soins des chefs des coureurs qui gardaient la porte du palais du Roi.
28 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
Et toutes les fois que le Roi venait au temple de l'Éternel, les coureurs les portaient; puis ils les rapportaient dans la salle des coureurs.
29 Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Or le reste des actes de Roboam et tout ce qu'il fit, est d'ailleurs consigné dans le livre des annales des rois de Juda.
30 Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
Et il y eut toujours guerre entre Roboam et Jéroboam.
31 Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Roboam reposa à côté de ses pères et reçut la sépulture avec ses pères dans la ville de David. Or le nom de sa mère était Naama, l'Ammonite. Et Abiam, son fils, régna en sa place.