< 1 Wafalme 14 >
1 Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
En ce temps-là, Abija, fils de Jéroboam, tomba malade.
2 naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
Jéroboam dit à sa femme: « Lève-toi, je t'en prie, et déguise-toi, afin qu'on ne te reconnaisse pas comme la femme de Jéroboam. Va à Silo. Voici, le prophète Achija y est, qui a dit que je serais roi de ce peuple.
3 Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
Prends avec toi dix pains, des gâteaux et un pot de miel, et va le voir. Il te dira ce qu'il adviendra de l'enfant. »
4 Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
La femme de Jéroboam fit ainsi; elle se leva, alla à Silo, et arriva à la maison d'Achija. Or Achija ne pouvait pas voir, car ses yeux étaient fixes à cause de son âge.
5 Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
Yahvé dit à Achija: « Voici que la femme de Jéroboam vient te demander des nouvelles de son fils, car il est malade. Dis-lui telle et telle chose, car il se peut que, lorsqu'elle entrera, elle se fasse passer pour une autre femme. »
6 Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
Et lorsque Achija entendit le bruit de ses pieds lorsqu'elle franchit la porte, il dit: « Entre, femme de Jéroboam! Pourquoi te fais-tu passer pour une autre? Car je suis envoyé vers toi avec une lourde nouvelle.
7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
Va dire à Jéroboam: « Yahvé, le Dieu d'Israël, dit: « Parce que je t'ai élevé du milieu du peuple, que je t'ai établi prince de mon peuple d'Israël,
8 Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
que j'ai arraché le royaume à la maison de David et que je te l'ai donné; et pourtant tu n'as pas été comme mon serviteur David, qui a gardé mes commandements et qui m'a suivi de tout son cœur, pour ne faire que ce qui était juste à mes yeux,
9 Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
mais tu as fait le mal par-dessus tous ceux qui étaient avant toi, et tu es allé te faire d'autres dieux, des images en fonte, pour m'irriter,
10 “‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
C'est pourquoi voici, je vais faire venir le malheur sur la maison de Jéroboam, j'exterminerai de Jéroboam tous ceux qui urinent sur un mur, ceux qui sont enfermés et ceux qui sont en liberté en Israël, et je balaierai la maison de Jéroboam, comme on balaie du fumier jusqu'à ce qu'il ait disparu.
11 Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
Les chiens mangeront celui qui appartient à Jéroboam et qui meurt dans la ville, et les oiseaux du ciel mangeront celui qui meurt dans les champs, car Yahvé a parlé ».
12 “Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
Lève-toi donc, et va dans ta maison. Quand tes pieds entreront dans la ville, l'enfant mourra.
13 Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
Tout Israël le pleurera et l'enterrera; car c'est le seul de Jéroboam qui sera mis au tombeau, parce qu'on a trouvé en lui quelque chose de bon pour l'Éternel, le Dieu d'Israël, dans la maison de Jéroboam.
14 “Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
Et Yahvé se suscitera sur Israël un roi qui exterminera la maison de Jéroboam. C'est le jour! Quoi? Dès maintenant.
15 Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
Car l'Éternel frappera Israël, comme un roseau qu'on secoue dans l'eau; il déracinera Israël de ce bon pays qu'il a donné à ses pères, et il le dispersera au delà du fleuve, parce qu'il a fait ses mâts d'Ashéra, en irritant l'Éternel.
16 Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
Il livrera Israël à cause des péchés de Jéroboam, qu'il a commis et par lesquels il a fait pécher Israël. »
17 Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
La femme de Jéroboam se leva et partit, et elle vint à Thirtsa. Comme elle arrivait sur le seuil de la maison, l'enfant mourut.
18 Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
Tout Israël l'enterra et prit le deuil, selon la parole de l'Éternel, qu'il avait prononcée par son serviteur Achija, le prophète.
19 Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Le reste des actions de Jéroboam, comment il a combattu et comment il a régné, cela est écrit dans le livre des Chroniques des rois d'Israël.
20 Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Le temps que Jéroboam régna fut de vingt-deux ans; puis il se coucha avec ses pères, et Nadab, son fils, régna à sa place.
21 Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
Roboam, fils de Salomon, régna en Juda. Roboam avait quarante et un ans lorsqu'il devint roi, et il régna dix-sept ans à Jérusalem, la ville que Yahvé avait choisie parmi toutes les tribus d'Israël, pour y mettre son nom. Le nom de sa mère était Naama, l'Ammonite.
22 Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
Juda fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, et ils excitèrent sa jalousie par les péchés qu'ils commirent, par-dessus tout ce qu'avaient fait leurs pères.
23 Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
Ils se construisirent des hauts lieux, des colonnes sacrées et des mâts d'Ashéra, sur toute colline élevée et sous tout arbre vert.
24 Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
Il y avait aussi des sodomites dans le pays. Ils faisaient toutes les abominations des nations que Yahvé avait chassées devant les enfants d'Israël.
25 Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
La cinquième année du roi Roboam, Shishak, roi d'Égypte, monta contre Jérusalem.
26 Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
Il emporta les trésors de la maison de l'Éternel et les trésors de la maison du roi. Il emporta même tout, y compris tous les boucliers d'or que Salomon avait faits.
27 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
Le roi Roboam fit à leur place des boucliers d'airain et les confia aux mains des chefs de garde qui gardaient la porte de la maison du roi.
28 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
Chaque fois que le roi entrait dans la maison de Yahvé, les gardes les portaient et les ramenaient dans la salle des gardes.
29 Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Le reste des actes de Roboam, et tout ce qu'il a fait, n'est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
30 Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
Il y eut une guerre continuelle entre Roboam et Jéroboam.
31 Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.
Roboam se coucha avec ses pères, et il fut enterré avec ses pères dans la ville de David. Le nom de sa mère était Naama, l'Ammonite. Son fils Abijam régna à sa place.