< 1 Wafalme 14 >

1 Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
At the time that he became sick Abijah [the] son of Jeroboam.
2 naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
And he said Jeroboam to wife his arise please and you will disguise yourself and not people will know that (you *Q(K)*) [are] [the] wife of Jeroboam and you will go Shiloh there! [is] there Ahijah the prophet he he spoke on me to king over the people this.
3 Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
And you will take in hand your ten bread[s] and cakes and a jar of honey and you will go to him he he will tell to you what? will it happen to the lad.
4 Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
And she did thus [the] wife of Jeroboam and she arose and she went Shiloh and she went [the] house of Ahijah and Ahijah not he was able to see for they were fixed eyes his from old age his.
5 Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
And Yahweh he had said to Ahijah here! [the] wife of Jeroboam [is] about to come to seek a word from with you concerning son her for [is] sick he like this and like this you will speak to her and it may be when comes she and she [will be] acted as a stranger.
6 Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
And it was when heard Ahijah [the] sound of feet her coming in the entrance and he said come O wife of Jeroboam why? this [are] you acting as a stranger and I [have been] sent to you hard.
7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
Go say to Jeroboam thus he says Yahweh [the] God of Israel because that I raised up you from among the people and I made you a ruler over people my Israel.
8 Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
And I tore away the kingdom from [the] house of David and I gave it to you and not you have been like servant my David who he kept commandments my and who he walked after me with all heart his to do only the right in view my.
9 Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
And you have done evil to act more than all [those] who they were before you and you have gone and you have made for yourself gods other and molten images to provoke to anger me and me you have cast behind back your.
10 “‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
Therefore here I [am] about to bring calamity to [the] house of Jeroboam and I will cut off to Jeroboam [one who] urinates on a wall shut up and freed in Israel and I will sweep away behind [the] house of Jeroboam just as someone sweeps away dung until is complete it.
11 Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
The [one who] dies of Jeroboam in the city they will devour the dogs and the [one who] dies in the open country they will devour [the] bird[s] of the heavens for Yahweh he has spoken.
12 “Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
And you arise go to house your when go feet your the city towards and he will die the child.
13 Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
And they will mourn for him all Israel and they will bury him for this [one] to only him he will go of Jeroboam into a grave because it was found in him something good to Yahweh [the] God of Israel in [the] house of Jeroboam.
14 “Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
And he will raise up Yahweh for himself a king over Israel who he will cut off [the] house of Jeroboam this the day and what? also now.
15 Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
And he will strike down Yahweh Israel just as it sways reed in the water and he will pluck up Israel from on the ground good this which he gave to ancestors their and he will scatter them from [the] other side of the River because that they have made Asherah poles their provoking to anger Yahweh.
16 Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
So he may give up Israel on account of [the] sins of Jeroboam which he has sinned and which he has caused to sin Israel.
17 Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
And she arose [the] wife of Jeroboam and she went and she came Tirzah towards she [was] coming at [the] threshold of the house and the lad he died.
18 Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
And they buried him and they mourned for him all Israel according to [the] word of Yahweh which he spoke by [the] hand of servant his Ahijah the prophet.
19 Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
And [the] rest of [the] matters of Jeroboam which he waged war and which he reigned there they [are] written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Israel.
20 Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
And the days which he reigned Jeroboam [were] twenty and two year[s] and he lay down with ancestors his and he became king Nadab son his in place of him.
21 Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
And Rehoboam [the] son of Solomon he reigned in Judah [was] a son of forty and one year[s] Rehoboam when became king he and seven-teen year[s] - he reigned in Jerusalem the city where he had chosen Yahweh to put name his there from all [the] tribes of Israel and [the] name of mother his [was] Naamah the Ammonite [woman].
22 Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
And it did Judah the evil in [the] eyes of Yahweh and they made jealous him more than all that they had done ancestors their by sins their which they sinned.
23 Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
And they built also they for themselves high places and sacred pillars and Asherah poles on every hill high and under every tree luxuriant.
24 Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
And also cult prostitute[s] he was in the land they did according to all the abominations of the nations which he had dispossessed Yahweh from before [the] people of Israel.
25 Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
And it was in the year fifth of the king Rehoboam he came up (Shishak *Q(K)*) [the] king of Egypt on Jerusalem.
26 Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
And he took [the] treasures of [the] house of Yahweh and [the] treasures of [the] house of the king and everything he took and he took all [the] shields of gold which he had made Solomon.
27 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
And he made the king Rehoboam in place of them shields of bronze and he entrusted [them] on [the] hand of [the] commanders of the runners who guarded [the] entrance of [the] house of the king.
28 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
And it was as often as went the king [the] house of Yahweh they carried them the runners and they returned them to [the] guardroom of the runners.
29 Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Rehoboam and all that he did ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
30 Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
And war it was between Rehoboam and between Jeroboam all the days.
31 Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.
And he lay down Rehoboam with ancestors his and he was buried with ancestors his in [the] city of David and [the] name of mother his [was] Naamah the Ammonite [woman] and he became king Abijam son his in place of him.

< 1 Wafalme 14 >