< 1 Wafalme 13 >
1 Kwa neno la Bwana, mtu wa Mungu alifika Betheli kutoka Yuda wakati Yeroboamu alipokuwa amesimama kando ya madhabahu ili kutoa sadaka.
Glej, iz Juda je prišel Božji mož po Gospodovi besedi do Betela in Jerobeám je stal pri oltarju, da zažge kadilo.
2 Akapiga kelele dhidi ya madhabahu kwa neno la Bwana: “Ee madhabahu, madhabahu! Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika nyumba ya Daudi. Juu yako atawatoa dhabihu makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu wale ambao wanatoa sadaka hapa sasa, nayo mifupa ya wanadamu itachomwa juu yako.’”
Zaklical je zoper oltar v Gospodovi besedi in rekel: »Oh oltar, oltar, tako govori Gospod: ›Glej, otrok bo rojen Davidovi hiši, po imenu Jošíja in na tebi bo daroval duhovnike visokih krajev, ki zažigajo kadilo na tebi in človeške kosti bodo žgane na tebi.‹«
3 Siku iyo hiyo, mtu wa Mungu akatoa ishara: “Hii ndiyo ishara Bwana aliyotangaza: Madhabahu haya yatapasuka na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.”
In isti dan je dal znamenje, rekoč: »To je znamenje, ki ga je Gospod govoril: ›Glej, oltar bo razpočen in pepel, ki je na njem, se bo izsul.‹«
4 Mfalme Yeroboamu aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, alipopiga kelele dhidi ya madhabahu huko Betheli, akanyoosha mkono wake kutoka madhabahuni na kusema, “Mkamate!” Lakini mkono aliokuwa ameunyoosha kumwelekea yule mtu ukasinyaa na kubaki hapo hapo, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha.
Pripetilo se je, da ko je kralj Jerobeám slišal izjavo Božjega moža, ki je zaklical proti oltarju v Betelu, da je svojo roko iztegnil od oltarja, rekoč: »Primite ga.« Njegova roka, ki jo je iztegnil proti njemu, pa se je posušila, tako da je ni mogel povleči nazaj k sebi.
5 Pia, madhabahu yalipasuka na majivu yakamwagika sawasawa na ishara iliyotolewa na mtu wa Mungu kwa neno la Bwana.
Tudi oltar je bil razpočen in pepel razsut z oltarja, glede na znamenje, ki ga je Božji mož dal po Gospodovi besedi.
6 Kisha mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “Niombee kwa Bwana Mungu wako ili mkono wangu upate kupona.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwombea kwa Bwana, nao mkono wa mfalme ukapona na kuwa kama ulivyokuwa hapo kwanza.
Kralj je Božjemu možu odgovoril in rekel: »Prosi sedaj obličje Gospoda, svojega Boga in moli zame, da bo moja roka lahko ponovno povrnjena k meni.« Božji mož je rotil Gospoda in kraljeva roka je bila ponovno povrnjena k njemu in postala, kakor je bila ta poprej.
7 Mfalme akamwambia yule mtu wa Mungu, “Twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
Kralj je Božjemu možu rekel: »Pridi z menoj domov, osveži se in dal ti bom nagrado.«
8 Lakini yule mtu wa Mungu akamjibu mfalme, “Hata kama ungenipa nusu ya mali zako, nisingekwenda pamoja na wewe, wala nisingekula mkate au kunywa maji hapa.
Božji mož je kralju odgovoril: »Če mi daš polovico svoje hiše, ne bom šel s teboj niti na tem kraju ne bom jedel kruha niti pil vode.«
9 Kwa kuwa niliagizwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate wala usinywe maji au kurudi kwa njia uliyojia.’”
Kajti tako mi je bilo naročeno po Gospodovi besedi, rekoč: »Ne jej kruha, niti ne pij vode, niti se ne obračaj ponovno po isti poti, po kateri si prišel.«
10 Kwa hiyo akafuata njia nyingine na hakurudi kupitia njia ile ambayo alikuwa ameijia Betheli.
Tako je odšel po drugi poti in se ni vrnil po poti, po kateri je prišel v Betel.
11 Basi kulikuwepo na nabii fulani mzee aliyekuwa anaishi Betheli, ambaye wanawe walikuja kumwambia yote ambayo mtu wa Mungu alikuwa ameyafanya pale siku ile. Pia wakamwambia baba yao yale aliyomwambia mfalme.
Torej v Betelu je prebival star prerok. Njegovi sinovi so prišli in mu povedali vsa dela, ki jih je tisti dan Božji mož storil v Betelu. Tudi besede, ki jih je govoril kralju, so povedali svojemu očetu.
12 Baba yao akawauliza, “Ameelekea njia gani?” Nao wanawe wakamwonyesha ile njia yule mtu wa Mungu kutoka Yuda aliyopita.
Njihov oče jim je rekel: »Po kateri poti je odšel?« Kajti njegovi sinovi so videli po kateri poti je odšel Božji mož, ki je prišel iz Juda.
13 Hivyo akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda.” Walipokwisha kumtandikia punda, akampanda
Svojim sinovom je rekel: »Osedlajte mi osla.« Tako so mu osedlali osla, in jahal je na njem
14 na kumfuatilia yule mtu wa Mungu. Akamkuta ameketi chini ya mwaloni na akamuuliza, “Je, wewe ndiwe mtu wa Mungu kutoka Yuda?” Akamjibu, “Mimi ndiye.”
in odšel za Božjim možem in ga našel sedeti pod hrastom. Rekel mu je: » Ali si ti Božji mož, ki je prišel iz Juda?« Ta je rekel: »Jaz sem.«
15 Basi nabii akamwambia, “Karibu nyumbani pamoja na mimi ule.”
Potem mu je rekel: »Pridi z menoj domov in jej kruh.«
16 Yule mtu wa Mungu akasema, “Siwezi kurudi na kwenda nawe, wala siwezi kula mkate au kunywa maji pamoja nawe mahali hapa.
Ta pa je rekel: »Ne smem se vrniti s teboj, niti vstopiti s teboj, niti na tem kraju ne bom jedel kruha niti pil vode,
17 Nimeambiwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate au kunywa maji huko au kurudia njia uliyojia.’”
kajti po Gospodovi besedi mi je bilo rečeno: ›Ti tam ne boš jedel niti kruha niti pil vode niti se ne boš ponovno obrnil, da bi šel po poti, po kateri si prišel.‹«
18 Yule nabii mzee akajibu, “Mimi pia ni nabii, kama wewe. Naye malaika alisema nami kwa neno la Bwana: ‘Mrudishe aje katika nyumba yako ili apate kula mkate na kunywa maji.’” (Lakini alikuwa akimwambia uongo.)
Rekel mu je: »Tudi jaz sem prerok, kot si ti in angel mi je po Gospodovi besedi govoril, rekoč: ›Privedi ga s seboj nazaj v svojo hišo, da bo lahko jedel kruh in pil vodo.‹« Toda lagal mu je.
19 Hivyo mtu wa Mungu akarudi pamoja naye na akala na kunywa katika nyumba yake.
Tako je z njim odšel nazaj in v njegovi hiši jedel kruh in pil vodo.
20 Wakati walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia yule nabii mzee aliyemrudisha huyo mtu wa Mungu.
Pripetilo se je, ko sta sedela pri mizi, da je Gospodova beseda prišla preroku, ki ga je privedel nazaj
21 Akampazia sauti yule mtu wa Mungu aliyekuwa ametoka Yuda, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Umeasi neno la Bwana na hukushika amri uliyopewa na Bwana Mungu wako,
in Božjemu možu, ki je prišel iz Juda, je zaklical, rekoč: »Tako govori Gospod: ›Ker nisi ubogal Gospodovih ust in se nisi držal Gospodove zapovedi, ki ti jo je Gospod, tvoj Bog, zapovedal,
22 bali ulirudi na ukala mkate na kunywa maji mahali ambapo alikuambia usile wala usinywe. Kwa hiyo maiti yako haitazikwa katika kaburi la baba zako.’”
temveč si prišel nazaj in si na tem kraju jedel kruh in pil vodo, o čemer ti je Gospod rekel: ›Ne jej kruha in ne pij nobene vode, ‹ tvoje truplo ne bo prišlo v mavzolej tvojih očetov.‹«
23 Wakati huyo mtu wa Mungu alipomaliza kula na kunywa, nabii aliyekuwa amemrudisha akamtandikia punda wake.
Pripetilo se je, ko je pojedel kruh in potem ko je popil, da je zanj osedlal osla, namreč za preroka, ki ga je privedel nazaj.
24 Alipokuwa akienda akakutana na simba njiani, akamuua na maiti yake ikabwagwa barabarani, yule punda wake na simba wakiwa wamesimama karibu yake.
Ko je ta odšel, ga je na poti srečal lev in ga usmrtil. Njegovo truplo je bilo vrženo na pot in poleg njega je stal osel, [in] tudi lev je stal poleg trupla.
25 Baadhi ya watu waliopita pale waliona maiti imebwagwa pale chini, simba akiwa amesimama kando ya maiti, wakaenda na kutoa habari katika mji ambao nabii mzee aliishi.
Glej, ljudje so hodili mimo in videli truplo, vrženo na pot in leva, stoječega poleg trupla in prišli so in to povedali v mestu, kjer je živel stari prerok.
26 Yule nabii aliyekuwa amemrudisha kutoka safari yake aliposikia habari hii akasema, “Ni yule mtu wa Mungu ambaye aliasi neno la Bwana. Bwana amemtoa kwa simba, ambaye amemrarua na kumuua, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limemwonya.”
Ko je prerok, ki ga je privedel nazaj iz poti, slišal o tem, je rekel: »To je Božji mož, ki je bil neposlušen Gospodovi besedi. Zato ga je Gospod izročil levu, ki ga je raztrgal in umoril glede na Gospodovo besedo, ki mu jo je govoril.«
27 Nabii akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda,” nao wakafanya hivyo.
Svojim sinovom je spregovoril, rekoč: »Osedlajte mi osla.« In osedlali so mu.
28 Kisha akatoka akaenda akakuta maiti imebwagwa chini barabarani, punda na simba wakiwa wamesimama kando yake. Simba hakuwa amekula ile maiti wala kumrarua punda.
Odšel je in na poti našel njegovo truplo ter osla in leva stati poleg trupla. Lev ni pojedel trupla niti raztrgal osla.
29 Basi yule nabii mzee akachukua maiti ya mtu wa Mungu, akailaza juu ya punda na akairudisha katika mji wake, ili amwombolezee na kumzika.
Prerok je pobral truplo Božjega moža, ga položil na osla in ga privedel nazaj, in stari prerok je prišel v mesto, da žaluje in da ga pokoplje.
30 Kisha akailaza ile maiti katika kaburi lake huyo nabii mzee, nao wakaomboleza juu yake na kusema, “Ee ndugu yangu!”
Njegovo truplo je položil v svoj grob in žalovali so nad njim, rekoč: »Ojoj, moj brat!«
31 Baada ya kumzika, akawaambia wanawe, “Wakati nitakapokufa, mnizike kwenye kaburi alimozikwa huyu mtu wa Mungu; lazeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.
Pripetilo se je, potem ko ga je pokopal, da je govoril svojim sinovom, rekoč: »Ko umrem, potem me pokopljite v mavzoleju, v katerem je pokopan Božji mož. Moje kosti položite poleg njegovih kosti,
32 Kwa maana ujumbe alioutangaza kwa neno la Bwana dhidi ya madhabahu huko Betheli na dhidi ya madhabahu yote katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Samaria, hakika yatatokea kweli.”
kajti beseda, ki jo je klical po Gospodovi besedi zoper oltar v Betelu in zoper vse hiše visokih krajev, ki so v mestih Samarije, se bo zagotovo zgodila.«
33 Hata baada ya haya, Yeroboamu hakubadili njia zake mbaya, lakini mara nyingine tena akaweka makuhani kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu kutoka watu wa aina zote. Yeyote aliyetaka kuwa kuhani alimweka wakfu kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu.
Po tej stvari se Jerobeám ni odvrnil iz svoje zle poti, temveč je ponovno naredil najnižje izmed ljudi za duhovnike na visokih krajih. Kogarkoli je hotel, je uméstil in ta je postal eden izmed duhovnikov visokih krajev.
34 Hii ilikuwa ndiyo dhambi ya nyumba ya Yeroboamu ambayo iliisababishia kuanguka na kuangamia kwake hadi kutoweka kwenye uso wa dunia.
Ta stvar je postala greh Jerobeámovi hiši, celo, da jo odseka in da jo uniči iz obličja zemlje.