< 1 Wafalme 13 >
1 Kwa neno la Bwana, mtu wa Mungu alifika Betheli kutoka Yuda wakati Yeroboamu alipokuwa amesimama kando ya madhabahu ili kutoa sadaka.
Et voilà qu’un homme de Dieu vint avec les paroles du Seigneur, de Juda à Béthel, Jéroboam étant près de l’autel et jetant de l’encens.
2 Akapiga kelele dhidi ya madhabahu kwa neno la Bwana: “Ee madhabahu, madhabahu! Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika nyumba ya Daudi. Juu yako atawatoa dhabihu makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu wale ambao wanatoa sadaka hapa sasa, nayo mifupa ya wanadamu itachomwa juu yako.’”
Et il s’écria contre l’autel, avec les paroles du Seigneur, et il dit: Autel, autel, le Seigneur dit ceci: Voilà qu’un fils naîtra dans la maison de David, du nom de Josias, et il immolera sur toi les prêtres des hauts lieux, qui maintenant brûlent sur toi de l’encens, et il brûlera sur toi des os d’hommes.
3 Siku iyo hiyo, mtu wa Mungu akatoa ishara: “Hii ndiyo ishara Bwana aliyotangaza: Madhabahu haya yatapasuka na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.”
Et il donna en ce jour-là ce signe, disant: Ceci sera le signe que le Seigneur a parlé: Voilà que l’autel sera brisé, et que sera répandue la cendre qui est sur lui.
4 Mfalme Yeroboamu aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, alipopiga kelele dhidi ya madhabahu huko Betheli, akanyoosha mkono wake kutoka madhabahuni na kusema, “Mkamate!” Lakini mkono aliokuwa ameunyoosha kumwelekea yule mtu ukasinyaa na kubaki hapo hapo, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha.
Or lorsque le roi eut entendu la parole que l’homme de Dieu avait dite en criant contre l’autel à Béthel, il étendit sa main de dessus l’autel, disant: Saisissez-le. Et sa main qu’il avait étendue contre le prophète se sécha, et il ne put pas la retirer à lui.
5 Pia, madhabahu yalipasuka na majivu yakamwagika sawasawa na ishara iliyotolewa na mtu wa Mungu kwa neno la Bwana.
L’autel aussi se brisa, et la cendre se répandit de l’autel, selon le signe que l’homme de Dieu avait prédit avec les paroles du Seigneur.
6 Kisha mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “Niombee kwa Bwana Mungu wako ili mkono wangu upate kupona.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwombea kwa Bwana, nao mkono wa mfalme ukapona na kuwa kama ulivyokuwa hapo kwanza.
Alors le roi dit à l’homme de Dieu: Implore la face du Seigneur ton Dieu, et prie pour moi, afin que ma main me soit rendue. Et l’homme de Dieu pria la face du Seigneur, et la main du roi revint à lui, et elle devint comme elle était auparavant.
7 Mfalme akamwambia yule mtu wa Mungu, “Twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
Or le roi dit à l’homme de Dieu: Viens avec moi en ma maison pour dîner, et je te donnerai des présents.
8 Lakini yule mtu wa Mungu akamjibu mfalme, “Hata kama ungenipa nusu ya mali zako, nisingekwenda pamoja na wewe, wala nisingekula mkate au kunywa maji hapa.
Et l’homme de Dieu répondit au roi: Quand vous me donneriez la moitié de votre maison, je n’irai point avec vous, et je ne mangerai point de pain ni ne boirai point d’eau en ce lieu;
9 Kwa kuwa niliagizwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate wala usinywe maji au kurudi kwa njia uliyojia.’”
Car c’est ainsi qu’il m’a été commandé avec les paroles du Seigneur, qui a donné cet ordre: Tu ne mangeras point de pain, tu ne boiras point d’eau, et tu ne retourneras point par la voie par laquelle tu es venu.
10 Kwa hiyo akafuata njia nyingine na hakurudi kupitia njia ile ambayo alikuwa ameijia Betheli.
Il s’en alla donc par une autre voie, et il ne retourna pas par le chemin par lequel il était venu à Béthel.
11 Basi kulikuwepo na nabii fulani mzee aliyekuwa anaishi Betheli, ambaye wanawe walikuja kumwambia yote ambayo mtu wa Mungu alikuwa ameyafanya pale siku ile. Pia wakamwambia baba yao yale aliyomwambia mfalme.
Or un certain vieux prophète habitait à Béthel, et ses fils vinrent vers lui, et lui racontèrent toutes les œuvres qu’avait faites l’homme de Dieu ce jour-là à Béthel; et les paroles qu’il avait dites au roi, ils les racontèrent à leur père.
12 Baba yao akawauliza, “Ameelekea njia gani?” Nao wanawe wakamwonyesha ile njia yule mtu wa Mungu kutoka Yuda aliyopita.
Et leur père leur dit: Par quelle voie s’en est-il allé? Ses fils lui montrèrent la voie par laquelle s’en était allé l’homme de Dieu qui était venu de Juda.
13 Hivyo akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda.” Walipokwisha kumtandikia punda, akampanda
Et il dit à ses fils: Préparez-moi l’âne. Et lorsque ceux-ci l’eurent préparé, il monta dessus.
14 na kumfuatilia yule mtu wa Mungu. Akamkuta ameketi chini ya mwaloni na akamuuliza, “Je, wewe ndiwe mtu wa Mungu kutoka Yuda?” Akamjibu, “Mimi ndiye.”
Et il s’en alla après l’homme de Dieu, et il le trouva assis sous le térébinthe, et il lui dit: Es-tu l’homme de Dieu qui es venu de Juda? Celui-ci répondit; Je le suis.
15 Basi nabii akamwambia, “Karibu nyumbani pamoja na mimi ule.”
Viens, dit-il, avec moi en ma maison pour manger du pain.
16 Yule mtu wa Mungu akasema, “Siwezi kurudi na kwenda nawe, wala siwezi kula mkate au kunywa maji pamoja nawe mahali hapa.
L’homme de Dieu lui répondit: Je ne puis retourner ni aller avec toi, et je ne mangerai point de pain et ne boirai point d’eau en ce lieu;
17 Nimeambiwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate au kunywa maji huko au kurudia njia uliyojia.’”
Parce que le Seigneur m’a parlé avec les paroles du Seigneur, disant: tu ne mangeras point de pain et ne boiras point d’eau là, et tu ne retourneras point par la voie par laquelle tu seras allé.
18 Yule nabii mzee akajibu, “Mimi pia ni nabii, kama wewe. Naye malaika alisema nami kwa neno la Bwana: ‘Mrudishe aje katika nyumba yako ili apate kula mkate na kunywa maji.’” (Lakini alikuwa akimwambia uongo.)
Cet homme lui répondit: Moi aussi, je suis prophète, semblable à toi, et un ange m’a parlé avec les paroles du Seigneur, disant: Ramène-le avec toi en ta maison, afin qu’il mange du pain et qu’il boive de l’eau. Il le trompa,
19 Hivyo mtu wa Mungu akarudi pamoja naye na akala na kunywa katika nyumba yake.
Et le ramena avec lui: il mangea donc du pain en sa maison, et il but de l’eau.
20 Wakati walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia yule nabii mzee aliyemrudisha huyo mtu wa Mungu.
Et, lorsqu’ils étaient assis à table, la parole du Seigneur fut adressée au prophète qui l’avait ramené,
21 Akampazia sauti yule mtu wa Mungu aliyekuwa ametoka Yuda, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Umeasi neno la Bwana na hukushika amri uliyopewa na Bwana Mungu wako,
Et il cria à l’homme de Dieu qui était venu de Juda, disant: Voici ce que dit le Seigneur: Parce que tu n’as pas été obéissant à la parole du Seigneur, et que tu n’as point gardé le commandement que t’a prescrit le Seigneur ton Dieu,
22 bali ulirudi na ukala mkate na kunywa maji mahali ambapo alikuambia usile wala usinywe. Kwa hiyo maiti yako haitazikwa katika kaburi la baba zako.’”
Et que tu es retourné, et que tu as mangé du pain et bu de l’eau dans le lieu dans lequel je t’ai ordonné de ne point manger de pain et de ne point boire d’eau, ton cadavre ne sera pas porté dans le sépulcre de tes pères.
23 Wakati huyo mtu wa Mungu alipomaliza kula na kunywa, nabii aliyekuwa amemrudisha akamtandikia punda wake.
Lors donc qu’il eut mangé et bu, le vieux prophète sella son âne pour le prophète qu’il avait ramené.
24 Alipokuwa akienda akakutana na simba njiani, akamuua na maiti yake ikabwagwa barabarani, yule punda wake na simba wakiwa wamesimama karibu yake.
Et lorsque celui-ci s’en fut allé, un lion le rencontra et le tua, et son cadavre était étendu dans le chemin: l’âne se tenait auprès de lui, et le lion se tenait auprès du cadavre.
25 Baadhi ya watu waliopita pale waliona maiti imebwagwa pale chini, simba akiwa amesimama kando ya maiti, wakaenda na kutoa habari katika mji ambao nabii mzee aliishi.
Et voilà que des hommes qui passaient virent son cadavre étendu sur la voie, et le lion qui se tenait auprès du cadavre. Et ils vinrent, et le publièrent dans la ville dans laquelle ce vieux prophète demeurait.
26 Yule nabii aliyekuwa amemrudisha kutoka safari yake aliposikia habari hii akasema, “Ni yule mtu wa Mungu ambaye aliasi neno la Bwana. Bwana amemtoa kwa simba, ambaye amemrarua na kumuua, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limemwonya.”
Ce qu’ayant appris, ce prophète qui l’avait détourné de sa voie, dit: C’est l’homme de Dieu qui a été désobéissant à la parole du Seigneur, et le Seigneur l’a livré au lion, qui l’a brisé et l’a tué, selon la parole que le Seigneur lui avait dite.
27 Nabii akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda,” nao wakafanya hivyo.
Et il dit à ses fils: Sellez-moi l’âne. Lorsque ceux-ci l’eurent sellé,
28 Kisha akatoka akaenda akakuta maiti imebwagwa chini barabarani, punda na simba wakiwa wamesimama kando yake. Simba hakuwa amekula ile maiti wala kumrarua punda.
Et que lui s’en fut allé, il trouva le cadavre étendu sur la voie, et l’âne et le lion qui se tenaient auprès du cadavre: le lion ne mangea pas du cadavre et ne fit pas de mal à l’âne.
29 Basi yule nabii mzee akachukua maiti ya mtu wa Mungu, akailaza juu ya punda na akairudisha katika mji wake, ili amwombolezee na kumzika.
Le prophète prit donc le cadavre de l’homme de Dieu, le mit sur l’âne, et le ramena dans la ville du vieux prophète, pour le pleurer.
30 Kisha akailaza ile maiti katika kaburi lake huyo nabii mzee, nao wakaomboleza juu yake na kusema, “Ee ndugu yangu!”
Et il mit son cadavre dans son sépulcre; et ils le pleurèrent, disant: Hélas! hélas! mon frère!
31 Baada ya kumzika, akawaambia wanawe, “Wakati nitakapokufa, mnizike kwenye kaburi alimozikwa huyu mtu wa Mungu; lazeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.
Et lorsqu’ils l’eurent pleuré, il dit à ses fils: Lorsque je serai mort, ensevelissez-moi dans le sépulcre dans lequel l’homme de Dieu est enseveli; mettez mes os auprès de ses os.
32 Kwa maana ujumbe alioutangaza kwa neno la Bwana dhidi ya madhabahu huko Betheli na dhidi ya madhabahu yote katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Samaria, hakika yatatokea kweli.”
Car certainement il arrivera ce qu’il a prédit avec les paroles du Seigneur, contre l’autel qui est à Béthel, et contre tous les temples des hauts lieux qui sont dans les villes de Samarie.
33 Hata baada ya haya, Yeroboamu hakubadili njia zake mbaya, lakini mara nyingine tena akaweka makuhani kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu kutoka watu wa aina zote. Yeyote aliyetaka kuwa kuhani alimweka wakfu kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu.
Après cela, Jéroboam ne revint point de ses voies très mauvaises; mais au contraire, il fit des derniers du peuple des prêtres des hauts lieux: à quiconque le voulait il remplissait sa main, et celui-ci devenait prêtre des hauts lieux.
34 Hii ilikuwa ndiyo dhambi ya nyumba ya Yeroboamu ambayo iliisababishia kuanguka na kuangamia kwake hadi kutoweka kwenye uso wa dunia.
Et c’est pour ce motif que pécha la maison de Jéroboam, et qu’elle fut détruite et exterminée de la surface de la terre.