< 1 Wafalme 13 >
1 Kwa neno la Bwana, mtu wa Mungu alifika Betheli kutoka Yuda wakati Yeroboamu alipokuwa amesimama kando ya madhabahu ili kutoa sadaka.
And there! - a man of God he came from Judah by [the] word of Yahweh to Beth-el and Jeroboam [was] standing at the altar to make smoke.
2 Akapiga kelele dhidi ya madhabahu kwa neno la Bwana: “Ee madhabahu, madhabahu! Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika nyumba ya Daudi. Juu yako atawatoa dhabihu makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu wale ambao wanatoa sadaka hapa sasa, nayo mifupa ya wanadamu itachomwa juu yako.’”
And he called out on the altar by [the] word of Yahweh and he said O altar altar thus he says Yahweh here! a son [is] about to be born to [the] house of David [will be] Josiah name his and he will sacrifice on you [the] priests of the high places who make smoke on you and bones of humankind people will burn on you.
3 Siku iyo hiyo, mtu wa Mungu akatoa ishara: “Hii ndiyo ishara Bwana aliyotangaza: Madhabahu haya yatapasuka na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.”
And he gave on the day that a sign saying this [is] the sign which he has spoken Yahweh here! the altar [is] about to be torn apart and it will be poured out the fatty ash which [is] on it.
4 Mfalme Yeroboamu aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, alipopiga kelele dhidi ya madhabahu huko Betheli, akanyoosha mkono wake kutoka madhabahuni na kusema, “Mkamate!” Lakini mkono aliokuwa ameunyoosha kumwelekea yule mtu ukasinyaa na kubaki hapo hapo, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha.
And it was when heard the king [the] word of [the] man of God which he called out on the altar at Beth-el and he stretched out Jeroboam hand his from at the altar saying - seize him and it dried up hand his which he had stretched out on him and not he was able to bring back it to himself.
5 Pia, madhabahu yalipasuka na majivu yakamwagika sawasawa na ishara iliyotolewa na mtu wa Mungu kwa neno la Bwana.
And the altar it was torn apart and it was poured out the fatty ash from the altar according to the sign which he had given [the] man of God by [the] word of Yahweh.
6 Kisha mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “Niombee kwa Bwana Mungu wako ili mkono wangu upate kupona.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwombea kwa Bwana, nao mkono wa mfalme ukapona na kuwa kama ulivyokuwa hapo kwanza.
And he answered the king and he said - to [the] man of God entreat please [the] face of Yahweh God your and pray for me so may it come back hand my to me and he entreated [the] man of God [the] face of Yahweh and it came back [the] hand of the king to him and it was as at the former [time].
7 Mfalme akamwambia yule mtu wa Mungu, “Twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
And he spoke the king to [the] man of God come! with me the house towards and sustain! so let me give to you a gift.
8 Lakini yule mtu wa Mungu akamjibu mfalme, “Hata kama ungenipa nusu ya mali zako, nisingekwenda pamoja na wewe, wala nisingekula mkate au kunywa maji hapa.
And he said [the] man of God to the king if you will give to me half of household your not I will go with you and not I will eat bread and not I will drink water in the place this.
9 Kwa kuwa niliagizwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate wala usinywe maji au kurudi kwa njia uliyojia.’”
For thus - he commanded me by [the] word of Yahweh saying not you must eat bread and not you must drink water and not you must return by the way which you went.
10 Kwa hiyo akafuata njia nyingine na hakurudi kupitia njia ile ambayo alikuwa ameijia Betheli.
And he went by a way another and not he returned by the way which he had come by it to Beth-el.
11 Basi kulikuwepo na nabii fulani mzee aliyekuwa anaishi Betheli, ambaye wanawe walikuja kumwambia yote ambayo mtu wa Mungu alikuwa ameyafanya pale siku ile. Pia wakamwambia baba yao yale aliyomwambia mfalme.
And a prophet one old [was] dwelling in Beth-el and he came son his and he recounted to him every deed which he had done [the] man of God - this day in Beth-el the words which he had spoken to the king and they recounted them to father their.
12 Baba yao akawauliza, “Ameelekea njia gani?” Nao wanawe wakamwonyesha ile njia yule mtu wa Mungu kutoka Yuda aliyopita.
And he spoke to them father their where? this [is] the way [which] he went and they had seen sons his the way which he had gone [the] man of God who he had come from Judah.
13 Hivyo akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda.” Walipokwisha kumtandikia punda, akampanda
And he said to sons his saddle for me the donkey and they saddled for him the donkey and he rode on it.
14 na kumfuatilia yule mtu wa Mungu. Akamkuta ameketi chini ya mwaloni na akamuuliza, “Je, wewe ndiwe mtu wa Mungu kutoka Yuda?” Akamjibu, “Mimi ndiye.”
And he went after [the] man of God and he found him sitting under the oak and he said to him ¿ [are] you [the] man of God who you came from Judah and he said I [am].
15 Basi nabii akamwambia, “Karibu nyumbani pamoja na mimi ule.”
And he said to him come with me the house towards and eat bread.
16 Yule mtu wa Mungu akasema, “Siwezi kurudi na kwenda nawe, wala siwezi kula mkate au kunywa maji pamoja nawe mahali hapa.
And he said not I am able to turn back with you and to go with you and not I will eat bread and not I will drink with you water in the place this.
17 Nimeambiwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate au kunywa maji huko au kurudia njia uliyojia.’”
For a word [was] to me by [the] word of Yahweh not you must eat bread and not you must drink there water not you must return to go by the way which you went by it.
18 Yule nabii mzee akajibu, “Mimi pia ni nabii, kama wewe. Naye malaika alisema nami kwa neno la Bwana: ‘Mrudishe aje katika nyumba yako ili apate kula mkate na kunywa maji.’” (Lakini alikuwa akimwambia uongo.)
And he said to him also I [am] a prophet like you and an angel it has spoken to me by [the] word of Yahweh saying bring back him with you to house your so he may eat bread so he may drink water he lied to him.
19 Hivyo mtu wa Mungu akarudi pamoja naye na akala na kunywa katika nyumba yake.
And he went back with him and he ate bread in house his and he drank water.
20 Wakati walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia yule nabii mzee aliyemrudisha huyo mtu wa Mungu.
And it was they [were] sitting to the table. And it came [the] word of Yahweh to the prophet who he had brought back him.
21 Akampazia sauti yule mtu wa Mungu aliyekuwa ametoka Yuda, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Umeasi neno la Bwana na hukushika amri uliyopewa na Bwana Mungu wako,
And he called out to [the] man of God who he had come from Judah saying thus he says Yahweh because for you have been disobedient to [the] mouth of Yahweh and not you have kept the command which he commanded you Yahweh God your.
22 bali ulirudi na ukala mkate na kunywa maji mahali ambapo alikuambia usile wala usinywe. Kwa hiyo maiti yako haitazikwa katika kaburi la baba zako.’”
And you went back and you ate bread and you drank water in the place which he spoke to you may not you eat bread and may not you drink water not it will go corpse your to [the] grave of ancestors your.
23 Wakati huyo mtu wa Mungu alipomaliza kula na kunywa, nabii aliyekuwa amemrudisha akamtandikia punda wake.
And it was after ate he bread and after drank he and he saddled for him the donkey for the prophet whom he had brought back him.
24 Alipokuwa akienda akakutana na simba njiani, akamuua na maiti yake ikabwagwa barabarani, yule punda wake na simba wakiwa wamesimama karibu yake.
And he went and it met him a lion on the way and it killed him and it was corpse his thrown down in the road and the donkey [was] standing beside it and the lion [was] standing beside the corpse.
25 Baadhi ya watu waliopita pale waliona maiti imebwagwa pale chini, simba akiwa amesimama kando ya maiti, wakaenda na kutoa habari katika mji ambao nabii mzee aliishi.
And there! men [were] passing by and they saw the corpse thrown down in the road and the lion standing beside the corpse and they went and they spoke in the city which the prophet old [was] dwelling in it.
26 Yule nabii aliyekuwa amemrudisha kutoka safari yake aliposikia habari hii akasema, “Ni yule mtu wa Mungu ambaye aliasi neno la Bwana. Bwana amemtoa kwa simba, ambaye amemrarua na kumuua, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limemwonya.”
And he heard the prophet who he had brought back him from the way and he said [is] [the] man of God that who he was disobedient to [the] mouth of Yahweh and he has given him Yahweh to the lion and it has mauled him and it has killed him according to [the] word of Yahweh which he spoke to him.
27 Nabii akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda,” nao wakafanya hivyo.
And he spoke to sons his saying saddle for me the donkey and they saddled [it].
28 Kisha akatoka akaenda akakuta maiti imebwagwa chini barabarani, punda na simba wakiwa wamesimama kando yake. Simba hakuwa amekula ile maiti wala kumrarua punda.
And he went and he found corpse his thrown down in the road and [the] donkey and the lion [were] standing beside the corpse not it had eaten the lion the corpse and not it had mauled the donkey.
29 Basi yule nabii mzee akachukua maiti ya mtu wa Mungu, akailaza juu ya punda na akairudisha katika mji wake, ili amwombolezee na kumzika.
And he picked up the prophet [the] corpse of [the] man of God and he placed him to the donkey and he brought back him and he came to [the] city of the prophet old to mourn and to bury him.
30 Kisha akailaza ile maiti katika kaburi lake huyo nabii mzee, nao wakaomboleza juu yake na kusema, “Ee ndugu yangu!”
And he placed corpse his in own grave his and people mourned on him alas! O brother my.
31 Baada ya kumzika, akawaambia wanawe, “Wakati nitakapokufa, mnizike kwenye kaburi alimozikwa huyu mtu wa Mungu; lazeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.
And it was after buried he him and he said to sons his saying at death my and you will bury me in the grave which [the] man of God [is] buried in it beside bones his place bones my.
32 Kwa maana ujumbe alioutangaza kwa neno la Bwana dhidi ya madhabahu huko Betheli na dhidi ya madhabahu yote katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Samaria, hakika yatatokea kweli.”
For certainly it will happen the word which he called out by [the] word of Yahweh on the altar which [is] in Beth-el and on all [the] houses of the high places which [are] in [the] cities of Samaria.
33 Hata baada ya haya, Yeroboamu hakubadili njia zake mbaya, lakini mara nyingine tena akaweka makuhani kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu kutoka watu wa aina zote. Yeyote aliyetaka kuwa kuhani alimweka wakfu kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu.
After the matter this not he turned back Jeroboam from way his evil and he returned and he appointed from [the] ends of the people priests of high places the [one] desiring he filled hand his and he may be priests of high places.
34 Hii ilikuwa ndiyo dhambi ya nyumba ya Yeroboamu ambayo iliisababishia kuanguka na kuangamia kwake hadi kutoweka kwenye uso wa dunia.
And it became by the matter this [the] sin of [the] house of Jeroboam and to annihilate [it] and to destroy [it] from on [the] surface of the ground.