< 1 Wafalme 12 >
1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
Rehabám je odšel v Sihem, kajti ves Izrael je prišel v Sihem, da ga postavijo za kralja.
2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
Pripetilo se je, ko je Nebátov sin Jerobeám, ki je bil še v Egiptu, slišal o tem (kajti pobegnil je izpred prisotnosti kralja Salomona in je Jerobeám prebival v Egiptu),
3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
da so poslali in ga poklicali. Jerobeám in vsa Izraelova skupnost pa je prišla in spregovorila Rehabámu, rekoč:
4 “Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
»Tvoj oče je naš jarem naredil boleč. Sedaj torej olajšaj bolečo službo svojega očeta in njegov težek jarem, ki ga je položil na nas in mi ti bomo služili.«
5 Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
Rekel jim je: »Odidite še za tri dni, potem ponovno pridite k meni.« In ljudstvo je odšlo.
6 Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
Kralj Rehabám se je posvetoval s starci, ki so stali pred njegovim očetom Salomonom, medtem ko je še živel in rekel: »Kako svetujete, da lahko odgovorim temu ljudstvu?«
7 Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
Odgovorili so mu, rekoč: »Če hočeš biti ta dan služabnik temu ljudstvu in jim hočeš služiti in jim odgovoriti in jim govoriti dobre besede, potem bodo tvoji služabniki na veke.«
8 Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
Toda zapustil je nasvet starcev, ki so mu ga dali in se posvetoval z mladeniči, ki so odrasli z njim in ki so stali pred njim
9 Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
in jim rekel: »Kakšen nasvet dajete vi, da lahko odgovorimo temu ljudstvu, ki mi je govorilo, rekoč: ›Naredi jarem, ki ga je tvoj oče položil nad nas, lažji?‹«
10 Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
Mladeniči, ki so zrasli z njim, so mu govorili, rekoč: »Tako boš govoril temu ljudstvu, ki ti je govorilo, rekoč: ›Tvoj oče je naš jarem naredil težek, toda ti nam ga olajšaj; ‹ tako jim boš rekel: ›Moj mali prst bo debelejši kakor očetova ledja.
11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
Kakor vam je moj oče naložil težek jarem, bom sedaj dodal vašemu jarmu. Moj oče vas je kaznoval z biči, toda jaz vas bom kaznoval s škorpijoni.‹«
12 Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
Tako je Jerobeám in vse ljudstvo tretji dan prišlo k Rehabámu, kakor je kralj določil, rekoč: »Ponovno pridite k meni tretji dan.«
13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
Kralj je ljudstvu surovo odgovoril in zapustil nasvet starcev, ki so mu ga dali.
14 akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
Spregovoril jim je glede na nasvet mladeničev, rekoč: »Moj oče je vaš jarem naredil težek, jaz pa bom vašemu jarmu dodal. Moj oče vas je kaznoval tudi z biči, toda jaz vas bom kaznoval s škorpijoni.«
15 Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
Zatorej kralj ni prisluhnil ljudstvu, kajti stvar je bila od Gospoda, da je lahko izpolnil svojo besedo, ki jo je Gospod po Šilčanu Ahíju govoril Nebátovemu sinu Jerobeámu.
16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
Torej ko je ves Izrael videl, da jim kralj ni prisluhnil, je ljudstvo odgovorilo kralju, rekoč: »Kakšen delež imamo v Davidu? Niti nimamo dediščine v Jesejevem sinu. K svojim šotorom, oh Izrael. Sedaj poglej k svoji lastni hiši, David.« Tako je Izrael odšel v svoje šotore.
17 Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
Toda kar se tiče Izraelovih otrok, ki so prebivali v Judovih mestih, je nad njimi kraljeval Rehabám.
18 Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
Potem je kralj Rehabám poslal Adoráma, ki je bil nad davkom in ves Izrael ga je kamnal s kamni, da je umrl. Zato je kralj Rehabám pohitel, da se spravi k svojemu bojnemu vozu, da pobegne v Jeruzalem.
19 Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
Tako se je Izrael uprl zoper Davidovo hišo do današnjega dne.
20 Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
Pripetilo se je, ko je ves Izrael slišal, da je Jerobeám ponovno prišel, da so poslali in ga poklicali k skupnosti in ga postavili za kralja nad vsem Izraelom. Tam ni bilo nikogar, ki je sledil Davidovi hiši, razen samo Judovega rodu.
21 Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
Ko je Rehabám prišel v Jeruzalem, je zbral vso Judovo hišo, z Benjaminovim rodom, sto osemdeset tisoč izbranih mož, ki so bili bojevniki, da se bojujejo zoper Izraelovo hišo, da kraljestvo ponovno privedejo k Salomonovemu sinu Rehabámu.
22 Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
Toda beseda od Boga je prišla k Šemajáju, Božjemu možu, rekoč:
23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
»Govori Salomonovemu sinu Rehabámu, Judovemu kralju in vsej Judovi in Benjaminovi hiši in preostanku ljudstva, rekoč:
24 ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
›Tako govori Gospod: ›Ne boste šli gor niti se ne boste borili zoper vaše brate, Izraelove otroke. Vsak mož naj se vrne k svoji hiši, kajti ta stvar je od mene.‹« Prisluhnili so torej Gospodovi besedi in se vrnili, da odidejo, glede na Gospodovo besedo.
25 Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
Potem je Jerobeám na gori Efrájim zgradil Sihem in tam prebival in odšel od tam ter zgradil Penuél.
26 Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
Jerobeám je v svojem srcu rekel: »Sedaj se bo kraljestvo vrnilo k Davidovi hiši.
27 Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
Če gre to ljudstvo gor, da opravi klavno daritev v Gospodovi hiši, v Jeruzalemu, potem se bo srce tega ljudstva ponovno obrnilo k njihovemu gospodu, k Judovemu kralju Rehabámu, mene pa bodo ubili in ponovno odšli k Judovemu kralju Rehabámu.«
28 Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
Nakar se je kralj posvetoval in naredil dve teleti iz zlata ter jim rekel: »To je za vas preveč, da greste gor v Jeruzalem. Poglejte svoje bogove, oh Izrael, ki so te privedli gor iz egiptovske dežele.«
29 Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
Eno je postavil v Betelu, drugo pa v Danu.
30 Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
Ta stvar je postala greh, kajti ljudstvo je odšlo, da bi oboževalo pred enim, celó k Danu.
31 Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
Naredil je hišo visokih krajev in iz najnižjih izmed ljudstva naredil duhovnike, ki niso bili izmed Lévijevih sinov.
32 Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
Jerobeám je odredil praznovanje v osmem mesecu, na petnajsti dan meseca, podobno prazniku, ki je v Judu in daroval na oltarju. Tako je storil v Betelu, žrtvoval je teletoma, ki ju je naredil in v Betelu je postavil duhovnike visokih krajev, ki jih je naredil.
33 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.
Tako je daroval na oltarju, ki ga je naredil v Betelu, na petnajsti dan osmega meseca, celó v mesecu, ki ga je zasnoval iz svojega lastnega srca in odredil praznovanje Izraelovim otrokom in daroval na oltarju in zažgal kadilo.