< 1 Wafalme 12 >

1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
Roboam se rendit à Sichem, car tout Israël était venu à Sichem pour le faire roi.
2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
Lorsque Jéroboam, fils de Nebath, en eut connaissance (car il était encore en Égypte, où il s'était enfui de la présence du roi Salomon, et Jéroboam vivait en Égypte;
3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
et on l'envoya chercher), Jéroboam et toute l'assemblée d'Israël vinrent et parlèrent à Roboam, en disant:
4 “Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
« Ton père a rendu notre joug difficile. Maintenant donc, allège le dur service de ton père et le lourd joug qu'il nous a imposé, et nous te servirons. »
5 Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
Il leur dit: « Partez pour trois jours, puis revenez vers moi. » Alors les gens sont partis.
6 Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
Le roi Roboam consulta les vieillards qui s'étaient présentés devant Salomon, son père, de son vivant, et dit: « Quel conseil me donnez-vous pour répondre à ces gens? »
7 Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
Ils répondirent: « Si tu veux être aujourd'hui le serviteur de ce peuple, si tu le sers et si tu lui réponds par de bonnes paroles, alors ils seront tes serviteurs pour toujours. »
8 Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
Mais il abandonna le conseil des vieillards qu'ils lui avaient donné, et tint conseil avec les jeunes gens qui avaient grandi avec lui, et qui se tenaient devant lui.
9 Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
Il leur dit: « Quel conseil donnez-vous, pour que nous répondions à ces gens qui m'ont parlé en disant: « Allègez le joug que votre père a mis sur nous? »".
10 Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
Les jeunes gens qui avaient grandi avec lui lui dirent: « Dis à ces gens qui t'ont parlé en disant: « Ton père a rendu notre joug lourd, mais allège-le pour nous », dis-leur: « Mon petit doigt est plus gros que la taille de mon père.
11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
Mon père vous a chargé d'un joug lourd, mais moi, je vais ajouter à votre joug. Mon père vous a châtiés avec des fouets, mais moi, je vous châtierai avec des scorpions.'"
12 Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
Jéroboam et tout le peuple se présentèrent à Roboam le troisième jour, comme le roi le leur avait demandé, en disant: « Revenez me voir le troisième jour. »
13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
Le roi répondit durement au peuple, abandonna le conseil des vieillards qu'ils lui avaient donné,
14 akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
et leur parla selon le conseil des jeunes gens, en disant: « Mon père a rendu votre joug pesant, mais moi, j'ajouterai à votre joug. Mon père vous a châtiés avec des fouets, mais moi je vous châtierai avec des scorpions. »
15 Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
Et le roi n'écouta pas le peuple, car c'était une chose provoquée par l'Éternel, afin d'affermir sa parole, que l'Éternel avait dite par Achija de Silo à Jéroboam, fils de Nebath.
16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
Lorsque tout Israël vit que le roi ne les écoutait pas, le peuple prit la parole et dit au roi: « Quelle part avons-nous en David? Nous n'avons pas d'héritage dans le fils de Jessé. À tes tentes, Israël! Occupe-toi maintenant de ta propre maison, David. » Et Israël s'en alla vers ses tentes.
17 Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
Mais quant aux enfants d'Israël qui habitaient dans les villes de Juda, Roboam régnait sur eux.
18 Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
Alors le roi Roboam envoya Adoram, qui était à la tête des hommes soumis au travail forcé, et tout Israël le lapida à mort. Le roi Roboam se hâta de monter sur son char, pour fuir à Jérusalem.
19 Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
Ainsi Israël s'est rebellé contre la maison de David jusqu'à ce jour.
20 Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
Lorsque tout Israël apprit que Jéroboam était de retour, ils l'envoyèrent appeler à l'assemblée et l'établirent roi sur tout Israël. Il n'y eut personne qui suivit la maison de David, sauf la tribu de Juda seulement.
21 Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
Lorsque Roboam fut arrivé à Jérusalem, il rassembla toute la maison de Juda et la tribu de Benjamin, cent quatre-vingt mille hommes d'élite qui étaient des guerriers, pour combattre la maison d'Israël, afin de ramener la royauté à Roboam, fils de Salomon.
22 Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
Mais la parole de Dieu fut adressée à Shemaya, homme de Dieu, en ces termes:
23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
« Parle à Roboam, fils de Salomon, roi de Juda, à toute la maison de Juda et de Benjamin, et au reste du peuple, et dis-lui:
24 ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
« Yahvé dit: Vous ne monterez pas et vous ne combattrez pas contre vos frères, les enfants d'Israël. Chacun retournera dans sa maison, car cette chose vient de moi. »" Ils écoutèrent donc la parole de Yahvé, s'en retournèrent et poursuivirent leur chemin, selon la parole de Yahvé.
25 Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
Jéroboam bâtit Sichem dans la montagne d'Ephraïm, et il y habita; puis il sortit de là et bâtit Penuel.
26 Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
Jéroboam disait en son cœur: « Maintenant le royaume va revenir à la maison de David.
27 Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
Si ce peuple monte pour offrir des sacrifices dans la maison de l'Éternel à Jérusalem, le cœur de ce peuple se tournera de nouveau vers son seigneur, vers Roboam, roi de Juda; il me tuera et reviendra à Roboam, roi de Juda. »
28 Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
Le roi tint conseil et fit deux veaux d'or, et il leur dit: « C'est trop pour vous de monter à Jérusalem. Regardez et contemplez vos dieux, Israël, qui vous ont fait monter du pays d'Égypte! »
29 Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
Il plaça l'un à Béthel, et l'autre à Dan.
30 Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
Cela devint un péché, car le peuple alla jusqu'à Dan pour se prosterner devant celui qui était là.
31 Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
Il fit des maisons de hauts lieux et établit des prêtres parmi tout le peuple, qui n'étaient pas des fils de Lévi.
32 Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
Jéroboam institua une fête au huitième mois, le quinzième jour du mois, comme la fête qui a lieu en Juda, et il monta à l'autel. Il le fit à Béthel, en sacrifiant aux veaux qu'il avait faits, et il plaça à Béthel les prêtres des hauts lieux qu'il avait faits.
33 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.
Il monta à l'autel qu'il avait fait à Béthel, le quinzième jour du huitième mois, au mois qu'il avait choisi de son propre cœur; il donna une fête aux enfants d'Israël, et il monta à l'autel pour brûler des parfums.

< 1 Wafalme 12 >