< 1 Wafalme 12 >

1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
And Rehobo'am went to Shechem; for all Israel were come to Shechem to make him king.
2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
And it came to pass, when Jerobo'am the son of Nebat, heard of it, (but he was yet in Egypt, whither he was fled from the presence of king Solomon, and Jerobo'am dwelt in Egypt;
3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
And they had sent and called him; ) that Jerobo'am and all the congregation of Israel came, and spoke unto Rehobo'am, saying,
4 “Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
Thy father made our yoke hard; but do thou now make lighter the hard service of thy father, and his heavy yoke which he put upon us, and we will serve thee.
5 Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
And he said unto them, Go away yet for three days, and then return to me. And the people went away.
6 Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
Then consulted king Rehobo'am with the old men, that had stood before Solomon his father while he yet lived, and said, How do ye advise that I should give an answer to this people?
7 Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
And they spoke unto him, saying, If thou wilt this day be a servant unto this people, and wilt serve them, and be attentive to them, and speak to them good words; then will they be servants unto thee for all times.
8 Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
But he forsook the counsel of the old men, which they had given him, and consulted with the young men that were grown up with him, those who stood before him:
9 Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
And he said unto them, What do you counsel how we should give an answer to this people, who have spoken to me, saying, Make lighter the yoke which thy father did put upon us?
10 Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
Then spoke unto him the young men that were grown up with him, saying, Thus must thou say unto this people that have spoken unto thee, saying, Thy father made our yoke heavy, but do thou make it lighter unto us: thus must thou speak unto them, My little finger is thicker than my father's loins.
11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
And now, if my father hath burdened you with a heavy yoke, I will even add to your yoke; if my father hath chastised you with whips, then will I chastise you with scorpion-thorns.
12 Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
When now Jerobo'am and all the people came to Rehobo'am on the third day, as the king had spoken, saying, Return to me on the third day.
13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
The king answered the people harshly, and forsook the old men's counsel that they had advised him;
14 akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
And he spoke to them after the counsel of the young men, saying, My father made your yoke heavy, and I will even add to your yoke; my father chastised you with whips, but I will chastise you with scorpion-thorns.
15 Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
Thus the king hearkened not unto the people; for it was so brought about from the Lord, in order that he might fulfill his word, which the Lord had spoken by means of Achiyah the Shilonite unto Jerobo'am the son of Nebat.
16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
So when all Israel saw that the king hearkened not unto them, the people gave the king an answer saying, What portion have we in David? nor have we an inheritance in the son of Jesse; to your tents, O Israel: now see to thy own house, David. So did Israel go away unto their tents.
17 Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
But as for the children of Israel who dwelt in the cities of Judah, over them did Rehobo'am reign.
18 Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
Then sent king Rehobo'am Adoram, who was over the tribute; but all Israel stoned him with stones, that he died. Therefore king Rehobo'am made speed with all his might to get up into his chariot, to flee to Jerusalem.
19 Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
So did Israel rebel against the house of David unto this day.
20 Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
And it came to pass, when all Israel heard that Jerobo'am was returned, that they sent and called him unto the congregation, and made him king over all Israel: there was none that followed the house of David, save the tribe of Judah alone.
21 Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
And when Rehobo'am was come to Jerusalem, he assembled all the house of Judah, with the tribe of Benjamin, a hundred and eighty thousand chosen men, warriors, to fight against the house of Israel, to bring back the kingdom to Rehobo'am the son of Solomon.
22 Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
But the word of God came unto Shema'yah the man of God, saying,
23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
Say unto Rehobo'am, the son of Solomon, the king of Judah, and unto all the house of Judah and Benjamin, and to the remnant of the people, saying,
24 ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
Thus hath said the Lord, Ye shall not go up, nor fight with your brethren the children of Israel: return every man to his house; for from me hath this thing been brought about. And they hearkened to the word of the Lord, and returned to go home, according to the word of the Lord.
25 Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
And Jerobo'am built Shechem in the mountain of Ephraim, and dwelt therein; and he went out from there and built Penuel.
26 Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
And Jerobo'am said in his heart, Now may the kingdom return to the house of David:
27 Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
If this people go up to prepare sacrifices in the house of the Lord at Jerusalem, then may the heart of this people turn again unto their Lord, even unto Rehobo'am the king of Judah, and they might kill me, and return to Rehobo'am the king of Judah.
28 Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
Whereupon the king took counsel, and he made two calves of gold, and said unto the people, You have been long enough going up to Jerusalem: behold, here are thy gods, O Israel, which have brought thee up out of the land of Egypt.
29 Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
And he placed the one in Beth-el, and the other put he in Dan.
30 Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
And this thing became a sin; and the people went before the one, as far as Dan.
31 Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
And he made a house of the high-places, and made priests of the lowest of the people, who were not of the sons of Levi.
32 Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
And Jerobo'am made a feast in the eighth month, on the fifteenth day of the month, like unto the feast that is in Judah, and he offered upon the altar; so did he in Beth-el, sacrificing unto the calves that he had made: and he stationed at Beth-el the priests of the high-places whom he had made.
33 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.
So he offered upon the altar which he had made in Beth-el on the fifteenth day of the eighth month, in the month which he had falsely devised of his own heart; and he ordained a feast unto the children of Israel, and he went up to the altar, to burn incense.

< 1 Wafalme 12 >