< 1 Wafalme 12 >
1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
Then Rehoboam went to Shechem. For in that place, all of Israel had gathered to appoint him as king.
2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
Yet truly, Jeroboam, the son of Nebat, while he was still in Egypt as a fugitive from the face of king Solomon, hearing of his death, returned from Egypt.
3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
And they sent and called him. Therefore, Jeroboam went, with the entire multitude of Israel, and they spoke to Rehoboam, saying:
4 “Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
“Your father imposed a very harsh yoke upon us. And so, you should now take away a little from the very harsh rule of your father and from his very grievous yoke, which he imposed upon us, and we will serve you.”
5 Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
And he said to them, “Go away, until the third day, and then return to me.” And when the people had gone away,
6 Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
king Rehoboam took counsel with the elders who had assisted before his father Solomon while he was still living. And he said, “What counsel do you give to me, so that I may respond to this people?”
7 Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
They said to him, “If today you will obey and serve this people, and yield to their petition, and if you will speak lenient words to them, they will be your servants for all days.”
8 Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
But he abandoned the counsel of the old men, which they had given to him. And he consulted the young men who had been raised with him, and who were assisting him.
9 Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
And he said to them: “What counsel do you give to me, so that I may respond to this people, who have said to me: ‘Make light the yoke that your father imposed on us?’”
10 Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
And the young men who had been raised with him, said: “You shall speak in this way to this people, who have spoken to you, saying: ‘Your father weighed down our yoke. You should relieve us.’ You shall say this to them: ‘My little finger is thicker than the back of my father.
11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
And now, my father placed a heavy yoke upon you, but I will add more upon your yoke. My father cut you with whips, but I will beat you with scorpions.’”
12 Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
Therefore, Jeroboam and all the people went to Rehoboam on the third day, just as the king had spoken, saying, “Return to me on the third day.”
13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
And the king responded to the people harshly, leaving behind the counsel of the elders that they had given to him.
14 akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
And he spoke to them according to the counsel of the young men, saying: “My father weighed down your yoke, but I will add more to your yoke. My father cut you with whips, but I will beat you with scorpions.”
15 Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
And the king did not acquiesce to the people. For the Lord had turned him away, so that he might raise up his word, which he had spoken by the hand of Ahijah, the Shilonite, to Jeroboam, the son of Nebat.
16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
And so the people, seeing that the king had not been willing to listen to them, responded to him, saying: “What part do we have in David? Or what inheritance do we have in the son of Jesse? Go to your own tents, O Israel. Now David, see to your own house.” And Israel went away to their own tents.
17 Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
But over all the sons of Israel who were living in the cities of Judah, Rehoboam reigned.
18 Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
Then king Rehoboam sent Adoram, who was over the tribute. And all of Israel stoned him, and he died. Therefore, king Rehoboam hurrying, climbed into the chariot, and fled to Jerusalem.
19 Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
And Israel drew away from the house of David, even to the present day.
20 Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
And it happened that, when all of Israel had heard that Jeroboam had returned, gathering an assembly, they sent and called him, and they appointed him as king over all of Israel. And no one followed the house of David, except the tribe of Judah alone.
21 Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
Then Rehoboam went to Jerusalem, and he gathered together the entire house of Judah, and the tribe of Benjamin, one hundred and eighty thousand elect men of war, so that they might fight against the house of Israel, and might bring the kingdom back to Rehoboam, the son of Solomon.
22 Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
But the word of the Lord came to Shemaiah, the man of God, saying:
23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
“Speak to Rehoboam, the son of Solomon, the king of Judah, and to all the house of Judah, and to Benjamin, and to the rest of the people, saying:
24 ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
‘Thus says the Lord: You shall not go up, and you shall not make war against your brothers, the sons of Israel. Let each man return to his own house. For this word came from me.’” And they listened to the word of the Lord, and they returned from the journey, as the Lord had instructed them.
25 Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
Then Jeroboam built up Shechem, on mount Ephraim, and he lived there. And departing from there, he built up Penuel.
26 Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
And Jeroboam said in his heart: “Now the kingdom will return to the house of David,
27 Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
if this people ascend to offer sacrifices in the house of the Lord at Jerusalem. And the heart of this people will be converted to their lord Rehoboam, the king of Judah, and they will put me to death, and return to him.”
28 Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
And devising a plan, he made two golden calves. And he said to them: “No longer choose to ascend to Jerusalem. Behold, these are your gods, O Israel, who led you away from the land of Egypt!”
29 Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
And he stationed one in Bethel, and the other in Dan.
30 Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
And this word became an occasion of sin. For the people went to adore the calf, even to Dan.
31 Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
And he made shrines on the high places, and he made priests out of the lowest people, who were not of the sons of Levi.
32 Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
And he appointed a solemn day in the eighth month, on the fifteenth day of the month, in imitation of the solemnity that was celebrated in Judah. And ascending to the altar, he acted similarly in Bethel, so that he immolated to the calves, which he had made. And in Bethel, he appointed priests of the high places, which he had made.
33 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.
And he ascended to the altar, which he had raised up in Bethel, on the fifteenth day of the eighth month, the day that he had decided in his own heart. And he made a solemnity to the sons of Israel, and he ascended to the altar, so that he might burn incense.