< 1 Wafalme 12 >

1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
[分裂近因]勒哈貝罕去了舍根,因為全以色列集合在舍根,要立他為王。
2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
乃巴特的兒子雅洛貝罕,為躲避撒羅滿王,曾逃往埃及,現在聽說撒羅滿已死,便從挨家埃及回來了。
3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
有人派人請了他回來,他便和以色列全會眾前來,對勒哈貝罕說:「
4 “Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
你的父親使我們的負擔繁重,現在,你得減輕你父親加給我們的苦役和重軛,我們纔肯服事你。」
5 Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
他回答他們說:「你們暫時回去,三天以後再來見我。」人民就都走了。
6 Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
勒哈貝罕便同那些在他父親撒羅滿生時,作臣僕的老年人商議說:「依你們的意見,我該怎樣答覆這些民眾﹖」
7 Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
他們回答說:「如果你今天願意作這民眾的僕人,服事他們,答應他們,對他們說好話,他們必會常常服事你。」
8 Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
但是,君王竟拒絕了老年人給他出的主意,反去同那些與他一起長大,侍立在他面前的少年商議,
9 Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
問他們說:「這些人民對我說:請你將你父親加於我們的重軛減輕些。依你們的意見我該怎樣答覆他們﹖」
10 Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
這些與他一起長大的少年人答說:「這些人民對你說:你父親使我們負擔繁重,請你給我們減輕些! 你要回答他們,對他們這樣說:我的小指比我父親的腰還粗!
11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
我父親曾加重了你們的重擔,我更要加重你們的重擔;我父親用皮鞭責打你們,我卻要用鐵刺鞭責打你們! 」
12 Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
雅洛貝罕和全體人民照君王所說:「你們第三天再來見我」的話,第三天就來見勒哈貝罕。
13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
君王嚴厲答覆了人民,拋棄了老年人給他出的主意,
14 akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
卻依照少年人的主張,對民眾說:「我的父親加重了你們的重擔,我更要加重,我父親用皮鞭責打你們,我反要用鐵刺鞭責打你們。」
15 Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
君王始終不肯聽從民眾。這一轉變原是出於上主,為實現他自己的話,就是上主藉史羅人阿希雅對乃巴特的兒子雅洛貝罕所說的話。政治分裂
16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
全以色列人見君王不肯依他們,便回覆君王說﹕「我們與達味有什麼分子﹖我們與葉瑟的兒子毫無關係! 以色列! 回到你的帳幕去啊! 達味啊! 現在你只顧你的本家罷! 」以色列人於是都回了自己的帳幕,
17 Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
只有那些住在猶大城市的以色列子民,仍屬勒哈貝罕統治。
18 Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
勒哈貝罕王派遣監管勞役的阿多蘭,去見以色列,以色列人卻用石頭將它砸死,勒哈貝罕急忙上車,逃回了耶路撒冷。
19 Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
這樣,以色列便與達味家分離了,直到現在。
20 Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
那時,全以色列人聽說雅洛貝罕已經回來,便派人邀請它前來赴會,立他為王,統治全以色列;從此跟隨達味家的,只有猷大支派。
21 Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
勒哈貝罕一回到耶路撒冷,即刻召集猶大全家和本雅明支派所有十八萬善戰的精兵,要去攻打以色列家,想把王國奪回,再歸屬撒羅滿的兒子勒哈貝罕;
22 Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
但是,天主有話傳於天主的人舍瑪雅說﹕「
23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
你去告訴撒羅滿的兒子,猶大王勒哈貝罕,猶大全家和本雅明以及其餘的人民說﹕
24 ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
上主這樣說﹕你們不要前去,攻打你們的兄弟以色列人,你們各自回家去罷! 因為這事原出於我。」他們便聽從了上主的話,依照上主的話回去了。宗教分裂
25 Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
雅洛貝罕在厄弗辣因山地修築了舍根,住在那裏;又從那裏出來,修築了培奴耳。
26 Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
雅洛貝罕心中思量﹕「這王國遲早要歸於達味王室;
27 Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
如果這人民上耶路撒冷,在上主殿內獻祭,他們的心難免不歸向他們的主上猶大勒哈貝罕,把我打死,再歸屬於猶大王勒哈貝罕。」
28 Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
因此,雅洛貝罕王拿定了主意,製造了兩隻金牛犢,對人民說﹕,「你們不需要再上耶路撒冷去了;以色列! 看,這就是領你們由埃及地上來的天主! 」
29 Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
他將一隻供在貝特耳,一隻供在丹。
30 Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
這使以色列陷於罪惡,因為民眾竟遠至丹去敬拜另一隻。
31 Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
雅貝洛罕又在高丘建立了神殿,將不屬於肋末子孫的平民立為司祭;
32 Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
規定八月十五日舉行慶節,像在猶大所舉行的慶節一樣,親自上壇獻祭。他也如此在貝特耳向他所製造的牛犢獻了祭,並在貝特耳為他建造的高丘神壇,委派了司祭。
33 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.
在他隨意選定的八月十五日,他親自上了他在貝特耳所築的祭壇,為以色列子民舉行慶節,上壇焚香獻祭。

< 1 Wafalme 12 >