< 1 Wafalme 11 >
1 Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
Tedy król Salomon rozmiłował się niewiast obcych wiele: nie tylko córki Faraonowej, ale i Moabitczanek, Ammonitczanek, Edomczanek, Sydończanek, Hetejczanek.
2 Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
Z tych narodów, o których powiedział Pan synom Izraelskim: Nie wchodźcie do nich, i one niech nie wchodzą do was; albowiem nakłoniłyby serce wasze za bogi swymi. Do tych przylgnął Salomon miłością.
3 Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
Tak iż miał żon królowych siedm set, a założnic trzy sta; i odwróciły żony jego serce jego.
4 Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
I stało się, gdy już był Salomon stary, że żony jego nakłoniły serce jego za bogi cudzymi, tak iż nie było serce jego zupełne z Panem, Bogiem jego, jako serce Dawida, ojca jego.
5 Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
Ale udał się Salomon za Astarotą, boginią Sydońską, i za Molochem, obrzydliwością Ammonitów.
6 Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
I uczynił Salomon, co się nie podobało Panu, ani chodził doskonale za Panem, jako Dawid, ojciec jego.
7 Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
Tedy zbudował Salomon kaplicę Chamosowi, obrzydliwości Moabskiej, na górze przeciw Jeruzalemowi i Molochowi, obrzydliwości synów Ammonowych.
8 Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
I tak uczynił wszystkim żonom swym cudzoziemkom, które kadziły, i ofiarowały bogom swoim.
9 Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
I rozgniewał się Pan na Salomona, że się odwróciło serce jego od Pana, Boga Izraelskiego, który się mu był ukazał po dwa kroć.
10 Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
I zakazał mu tego, aby nie chodził za bogi cudzymi; wszakże nie strzegł tego, co Pan przykazał.
11 Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
Przetoż rzekł Pan do Salomona: Ponieważeś się tego dopuścił, nie strzegąc przymierza mego, ani wyroków moich, którem ci przykazał, pewnie oderwę królestwo od ciebie, a dam je słudze twojemu,
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
Wszakże za dni twoich nie uczynię tego dla Dawida, ojca twego; ale z ręki syna twego oderwę je.
13 Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
Lecz wszystkiego królestwa nie oderwę; pokolenie jedno dam synowi twemu dla Dawida, sługi mego, i dla Jeruzalemu, którem obrał.
14 Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
Przetoż wzbudził Pan przeciwnika Salomonowi, Adada Edomczyka z nasienia królewskiego, który był w Edom.
15 Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
Albowiem stało się, gdy Dawid był w Edom, a Joab, hetman wojska, wyjechał, aby pochował pobite, i pobił wszystkie mężczyzny w Edom;
16 Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
(Bo tam sześć miesięcy mieszkał Joab ze wszystkimi Izraelczykami, aż wytracił wszystkie mężczyzny w Edom.)
17 Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
Tedy uciekł Adad sam, i niektórzy mężowie Edomscy z sług ojca jego z nim, aby szli do Egiptu; a Adad był chłopcem nie wielkim.
18 Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
Którzy wyszedłszy z Madyjan przyszli do Faran, a wziąwszy z sobą niektóre męże z Faran weszli do Egiptu, do Faraona króla Egipskiego, który mu dał dom, i żywność mu naznaczył, dał mu też i ziemię.
19 Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
I znalazł Adad wielką łaskę w oczach Faraonowych, tak, iż mu dał za żonę siostrę żony swej, siostrę królowej Tafnes.
20 Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
I porodziła mu siostra Tafnes Gienubata, syna jego, którego odchowała Tafnes w domu Faraonowym. I był Gienubat w domu Faraonowym między syny Faraonowymi.
21 Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
A gdy usłyszał Adad w Egipcie, iż zasnął Dawid z ojcy swymi, a iż umarł Joab, hetman wojska, tedy rzekł Adad do Faraona: Puść mię, że pójdę do ziemi mojej.
22 Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
Któremu odpowiedział Farao: Czegoż ci niedostawa u mnie, że chcesz iść do ziemi twojej? A on rzekł: Niczego; a wszakże puść mię.
23 Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
Wzbudził także Bóg nań przeciwnika, Rezona, syna Elijadowego, który był uciekł od Adarezera, króla Soby, Pana swego.
24 Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
A zebrawszy do siebie męże, był książęciem roty, gdy je Dawid mordował; przetoż odszedłszy do Damaszku, mieszkali w nim, a królowali nad Damaszkiem.
25 Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
I był przeciwnikiem Izraelowi po wszystkie dni Salomonowe, a to oprócz szkód, które mu czynił Adad; bo się brzydził Izraelem, gdy królował w Syryi.
26 Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
Jeroboam też, syn Nabata Efratejczyka z Saredy, (a imię matki jego Serwa, która była wdową, ) sługa Salomonowy, podniósł przeciwko królowi rękę.
27 Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
A tać była przyczyna, dla której podniósł rękę swą przeciwko królowi, że Salomon zbudowawszy Mello, zaprawił dziurę w mieście Dawida, ojca swego.
28 Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
A Jeroboam był mąż mocny i możny. Przetoż widząc Salomon młodzieńca, że był sprawny, postanowił go nad podatkami wszystkiemi domu Józefowego.
29 Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
I stało się tegoż czasu, gdy Jeroboam wyszedł z Jeruzalemu, że go znalazł na drodze Achyjasz Sylonitczyk, prorok, będąc odziany płaszczem nowym; a tylko sami dwaj byli na polu.
30 naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
Tedy wziąwszy Achyjasz płaszcz nowy, który miał na sobie, rozdarł go na dwanaście sztuk.
31 Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
I rzekł do Jeroboama: Weźmij sobie dziesięć sztuk; bo tak mówi Pan, Bóg Izraelski: Oto Ja oderwę królestwo z rąk Salomonowych, a dam tobie dziesięć pokoleń.
32 Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
Jedno tylko pokolenie zostanie mu dla sługi mego Dawida, i dla miasta Jeruzalem, którem obrał ze wszystkich pokoleń Izraelskich;
33 Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
Przeto, że mię opuścili, a kłaniali się Astarocie, bogini Sydońskiej, i Chamosowi, bogu Moabskiemu, i Molochowi, bogu synów Ammonowych, a nie chodzili drogami mojemi, aby czynili to, co się mnie podoba, ani też strzegli wyroków moich, i sądów mo ich, jako Dawid, ojciec jego.
34 “‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
Wszakże nie odejmę wszystkiego królestwa z ręki jego, owszem zostawię go książęciem po wszystkie dni żywota jego dla Dawida, sługi mego, któregom obrał, który strzegł rozkazania mego i wyroków moich.
35 Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
Ale wziąwszy królestwo z ręki syna jego, dam tobie z niego dziesięć pokoleń:
36 Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
A synowi jego dam pokolenie jedno, aby została pochodnia Dawidowi, słudze memu, po wszystkie dni przedemną w mieście Jeruzalemie, którem sobie obrał, aby tam przebywało imię moje;
37 Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
A ciebie wezmę, abyś królował nad wszystkiem, czego żąda dusza twoja, a będziesz królem nad Izraelem.
38 Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
Przetoż jeźli będziesz słuchał wszystkiego, coć przykażę, a będziesz chodził drogami mojemi, czyniąc to, co dobrego jest w oczach moich, strzegąc wyroków moich, i przykazań moich, jako czynił Dawid, sługa mój: tedy będę z tobą, a zbudujęć dom mocny, jakom zbudował Dawidowi, i podam ci Izraela;
39 Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
I trapić będę nasienie Dawidowe dla tego; a wszakże nie po wszystkie dni.
40 Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
Przetoż Salomon chciał zabić Jaroboama; ale wstawszy Jeroboam uciekł do Egiptu, do Sesaka, króla Egipskiego, i był w Egipcie aż do śmierci Salomonowej.
41 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
A inne sprawy Salomonowe, którekolwiek czynił, i mądrość jego, izali nie są wypisane w księgach spraw Salomonowych?
42 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
A dni, których królował Salomon w Jeruzalemie nad wszystkim Izraelem, było czterdzieści lat.
43 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
I zasnął Salomon z ojcy swymi, a pogrzebiony jest w mieście Dawida, ojca swego; i królował Roboam, syn jego, miasto niego.